CHAMA HAKITAMBEBA MTU AMBAE YEYE MWENYEWE HAKUJIBEBA -HAPI

September 08, 2024

 


AKIWA katika mkutano na viongozi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo uliofanyika katika ukumbi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA) Mkoani Pwani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania Jumuiya ya CCM, Ndugu. Ally Salum Hapi *(MNEC) ametuma salamu kwa viongozi wasio wajibika katika nafasi zao walizoaminiwa na wananchi huku akisema Chama cha Mapinduzi hakitambeba mtu katika uchaguzi unaokuja.

"Chama chetu kina utaratibu mzuri sana katika chaguzi muda unapofika na kila muda wa uchaguzi ndiyo maana tunasisitiza suala la kupata wagombea bora tutakao wauza kwa urahisi ambae anakubalika na wananchi na siyo anayekubalika kwenye mifuko ya watu wachache, kiongozi ambaye anazijua shida za wananchi na uchaguzi wa serikali za mitaa ndiyo msingi wa uchaguzi mkuu" alisema Hapi

Kuhusu viongozi wasiowajibika kwenye nafasi zao Hapi alitumia mkutano huo kukumbusha kuwa katika kipindi kilichosalia kuelekea uchaguzi Mkuu mwaka ujao ni muhimu kwa kila kiongozi aliyechaguliwa na wananchi kujitathimini iwapo anafaa kurejea katika nafasi yake kwenye uchaguzi ujao, iwapo wananchi watamuunga mkono kutokana na kazi zake.


"Waheshimiwa madiwani naomba mchape kazi muda ndiyo huu chama hakitambeba mtu ambaye hakujibeba yeye mwenyewe kwa utendaji kazi wake, wala hakitambeba mtu anayejisemea mwenyewe ambae hakisemei chama, hamsemei Mbunge wala hamsemei Rais wa CCM ninachoomba mtambue ni kuwa unafika kwenye uchaguzi huchaguliwi wewe kwa sababu ni bingwa wa fitna au wewe ni bingwa wa kumsema vibaya mwenzio au wewe ni bingwa wa kujisemea wewe mwenyewe tu bali matendo yako na namna ulivyoshughulika na matatizo ya wananchi pamoja na kazi unazozifanya kwa hiyo tupeleke wagombea wanaokubalika wenye sifa na wanaojua uongozi na wanajua kuishi na watu, kila mwenye sifa nendeni mkawahamasishe wagombee"alisema


Katika Hatua nyingine Hapi aliwanyooshea kidole na kuwaonya watu wanaojihusisha na udalali kwenye uchaguzi kwa kujifanya wao ndiyo kila kitu juu ya ushindi wa wagombea kwa kuwa wanajua namna ya kuzungumza na wananchi hali hiyo imekuwa mzigo mkubwa kwa viongozi walioko madarakani na kusababisha washindwe kufanya kazi kwa ufasaha.


"Lakini wapo watu hapa ni madalali wa uchaguzi ambao wametengeneza upepo kwa mtu yeyote anayetaka kugombea nafasi hiyo lazima amuone yeye na akiamini ushindi wa mgombea upo kwenye mikono yake, katika kipindi hiki jiepusheni na madalali wa siasa katika uchaguzi" alisema Hapi




Imetolewa na Idara ya Oganaizesheni ya Jumuiya ya Wazazi Taifa





Share this

Related Posts

Previous
Next Post »