MBUNGE WA VITI MAALUMU CATHERINE MAGIGE AWAKUMBUKA WATOTO YATIMA NA WALE WAONAOISHI KATIKA MAHABUSU YA WATOTO ARUSHA

June 25, 2017
 Mbunge wa viti maalumu kupitia chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha Catherine Magige akimkabidhi mkurugenzi na watoto wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Faraja  orphance kilichopo jijini hapa,kituo hichi cha watoto yatima kina jumla ya watoto 200 na kati ya watoto hao watoto 30 wanaishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi.

wa pili kushoto  mbunge wa  viti maalumu akiwa anateta jambo na katibu wa UWT mkoa wa Arusha Fatuma Hassan ,wakwanza kulia ni katibu wa kanda ya kaskazini msikiti wa  Twariqatul  ndugu Abdi Ramathani


 mbunge wa viti maalumu akiwa anamkabidhi zawadi za iddi mkurugenzi wa kituo cha watoto yatima cha Samaritan villege Jospephat Mmnyi

 mbunge wa viti maalum akiwa pamoja na baadhi ya watoto wa kituo cha watoto yatima na wasiojiweza cha Faraja ,mkurugenzi wa kituo hicho pamoja na baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi mkoa wa Arusha
 mbunge wa viti maalumu akiwa amembeba moja ya mtoto aliotelekezwa na mama yake akiwa mdogo anaeishi katika kituo cha watoto yatima cha Faraja kilichopo jijini hapa wakati alipowapelekea zawadi ya iddi

 mbunge wa viti maalumu akimkabidhi msaada wa chakula mmoja wa kijana wa kito cha Zawiani wakati alipotembelea kutoa zawadi za  sikukuu ya iddi

“MBUNGE MUSSA AWATAKIA WANANCHI WA JIMBO LAKE KUONGEZA UZALISHAJI”

June 25, 2017



 MBUNGE wa Jimbo la Tanga (CUF) Alhaji Mussa Mbaruku amewataka wananchi heri ya sikukuu ya Eid El Fitri huku akiwataka kujiandaa na ujio wa fursa ya mradi wa bomba la mafuta ghafi kutoka hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga kwa kuongeza uzalishaji.

Alhaji Mussa aliyasea hayo wakati akizungumza na mtandano huu ambapo alisema mradi huo ni mkubwa ambao utahusisha watu wengi hivyo wananchi wanapaswa kujipanga ili kuweza kuendana na fursa hiyo muhimu kwa ajili ya kujiongezea kipato halisi.

Alisema lazima wakazi wa mkoa huo watambue kuwa wakati mradi huo ni mkubwa ambao unaweza kuchangia ukuaji wa kipato chao hivyo wajiandae kwa ajili ya shughuli mbalimbali ikiwemo mama ntilie waweze kuendesha shughuli zao kisasa.

“Mkoa wa Tanga hasa kwenye Jimbo langu la Tanga mjini kutatekelezwa mradi mkubwa wa mradi wa boma la mafuta ghafi kutoka hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga hiyo wananchi wangu wajiandae kwa kuongeza uwajibika na uzalishaji ambao utakuwa na tija kwao “Alisema.

“Lakini pia niwaambie wenzetu madereva wa tax, mafundi wajiandae kikamilifu kuona namna ya kuboresha huduma zao kwani ujio wa mradi huo utalifanya Jiji la Tanga kuwa na watu wengi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi ili kuweza kupata mafanikio “Alisema.

Aidha pia mbunge huyo aliwataka waumini ya dini ya kislaam kuendelea kutenda mema hata baada ya kumalizika mwezi mtukufu wa ramadhani ikiwemo kuwajali wengine.

Mbunge huyo pia aliwataka wananchi wa Jimbo hilo kuhakikisha wana sheherekea vema sikukuu ya Iddi Salama kwa kuwa makini hasa wakati watoto wao wanapokwenda kutembelea wawe na wasaidizi.

NYAMLANI AJITOA KUWANIA URAIS TFF

June 25, 2017


Makamu wa Rais wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani amejitoa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania urais wa shirikisho hilo unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu.

Nyamlani aliwasilisha barua TFF leo Jumapili Juni 25, mwaka huu ikiwa ni siku moja tu tangu Kamati ya Uchaguzi ipitishe jina lake kuwa miongoni mwa wagombea 10 wanaowania nafasi hiyo ya urais. Sababu aliyoeleza ni masuala binafsi.

Kwa msingi huo, wagombea wanaobaki kwenye kinyang’anyiro na kuhitajika kufika kwenye usaili kuanzia Juni 29, mwaka huu ni tisa wakiongozwa na Rais wa sasa, Jamal Malinzi anayetetea nafasi.

Mbali ya Malinzi wengine wanaowania nafasi hiyo ni Imani Madega, Wallace Karia, Fredrick Masolwa, Fredrick Mwakalebela, John Kijumbe, Shija Richard, Ally Mayay na Emmanuel Kimbe.

Waliojitokeza kuwania Makamu wa Rais na kurejesha fomu wako Mulamu Ng’hambi, Michael Wambura, Geofrey Nyange, Mtemi Ramadhani, Robert Selasela na Stephen Mwakibolwa.

Mbali ya nafasi za urais na makamu rais, Abdallah Mussa - aliyekuwa akiwania nafasi ya kugombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji TFF kutoka Kanda Na. 1 (Mikoa ya Kagera na Geita) aliondolewa kwa sababu ya kutoambatanisha kivuli cha cheti ya elimu ya sekondari.

Hivyo wagombea wa nafasi za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa kufuata Kanda 13 ni kama ifuatavyo:

NSSF YAKABIDHI HUNDI YA SHILINGI BILIONI 1.5 UPANUZI WA KIWANDA CHA CHAKI SIMIYU

June 25, 2017
Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama(kulia) akimkabidhi hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt.Fredrick Sagamiko.

Na Stella Kalinga, Simiyu

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umekabidhi hundi ya shilingi bilioni 1.5 kwa Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu, fedha ambazo ni mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha Chaki Wilayani humo na kuongeza uzalishaji.

Hundi hiyo imekabidhiwa kwa Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama kwa niaba ya Serikali na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius Kahyarara wilayani Maswa mkoani Simiyu.


Akizungumza wakati wa makabidhiano ya hundi hiyo Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius Kahyarara amepongeza Mkoa wa Simiyu kwa kutekeleza Sera ya Ujenzi wa Uchumi wa Viwanda kwa vitendo na kuwataka viongozi wa mkoa huo kutokatishwa tamaa.

Amesema NSSF kama Shirika la Umma linatekeleza sera na maelekezo ya Serikali na wametoa mkopo huo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ili wafanye upanuzi wa kiwanda cha chaki na kuongeza uzalshaji kwa kuwa suala la Viwanda ni la kipaumbele.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Prof.Godius Kahyarara(kushoto) akimkabidhi Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama hundi ya shilingi bilioni 1.5 zilizotolewa na NSSF kama mkopo kwa ajili ya upanuzi wa kiwanda cha chaki Maswa, (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka.

Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na watu wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama amesema kiwanda cha Chaki Maswa kimebeba ujumbe na dhana ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli ya kushikamanisha Uchumi wa Viwanda na Maendeleo ya watu kwa sababu kinatumia malighafi ya hapa nchini.

Aidha, amesema kiwanda hiki kitawanufaisha Watanzania hususani vijana wa Mkoa wa Simiyu ambao watafanya kazi moja moja katika kiwanda na wale wataohusika katika uchimbaji wa malighafi ambayo inapatikana maeneo mengine hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu Sera, Bunge,Kazi, Ajira,Vijana na wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akipokea taarifa ya Upembuzi yakinifu wa panuzi wa kiwanda cha chaki cha Maswa kutoka kwa mtalaam wa Taasisi ya Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF), Deodatus Sagamiko.

SHEAKH MKUU WA TANZANIA ,ABUBAKARY BIN ZUBERY ASHIRIKI FUTARI ILIYOANDALIWA NA BENKI YA AZANIA TAWI LA MOSHI

June 25, 2017
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakichukua Chakula wakati wa hafla fupi ya Futari iliyoandaliwa na Benki ya Azania na kufanyika ofisi za Bakwata mkoa wa Kilimanjaro.
Sheakh Mkuu wa Tanzania ,Mufti Abubakary Bin Zubery akishiriki hafla ya kupata Futari iliyoandaliwa na Benki ya Azania
Sheakh  Mkuu wa Tanzania Mufti Abubakary Zubery akiwa na Kaimu Mkurugenzi idara ya maendeleo ya Biashara wa Benki ya Azania, Jackson Lohay katika hafla ya Futari iliyoandaliwa na Benki hiyo.
Baadhi ya waumini wakishiriki Futari iliyoandaliwa na Benki ya Azania tawi la Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mghwira (Wa pili toka kushoto) akiwa na Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi,Hajira Mmambe (wa kwanza kushoto.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira akishiriki Futari iliyoandaliwa na Benki ya Azania tawi la Moshi
Kaimu Mkurugenzi idara ya maendeleo ya Biashara wa Benki ya Azania, Jackson Lohay akizungumza wakati wa halfa fupi ya Futari iliyoandaliwa kwa Waislamu wa mkoa wa Kilimanjaro na Benki hiyo .
Mwenyekiti wa Halmashari ya Bakwata Taifa ,Sheakh ,Alhaji Hamis Mataka akizungumza kwa niaba ya Sheakh Mkuu wa Tanzania ,Mufti Abubakary Bin Zubery wakati wa Futari iliyoandaliwa na Azania Bank tawi la Moshi.
Mwakilishi wa wateja wa Benki ya Azania Bank ,Ibrahim Shoo akizungumza kwa niaba ya wateja wa benki hiyo.
Sheakh Mkuu wa Tanzania ,Mufti Abubakary Bin Zubery akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongzi wa Dini ya Kiislamu mara baada ya kumalizika kwa hafla fupi ya Futari iliyoandaliwa na Benki ya Azania tawi la Moshi.
Wafanyakazi wa Benki ya Azania tawi la Moshi wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mghwira ,wengine ni Katibu tawala wa mkoa wa Kilimanjaro ,Mhandisi Aisha Amour.na Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi ,Hajira Mmambe.
Meneja wa Azania Bank tawi la Moshi,Hajira Mmambe akiagana na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mghwira mara baada a kumalizikwa kwa hafla ya Futari iliyoandaliwa na Benki hiyo katika viwanja vya ofisi ya Bakwata mjini Moshi.

Na Dixon Busagaga a Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.