February 05, 2014

IGP MANGU APANGUA KIKOSI CHAKE, ABADILI MAKAMANDA

Na Mwandishi Wetu 

MKUU wa Jeshi la Polisi Tanzania, Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu ameanza kufanya mabadiliko ya baadhi ya makamanda wa mikoa, wakuu wa upelelezi wa mikoa, wakuu wa usalama barabarani wa mikoa pamoja na watendaji wengine wa vikosi na vitengo mbalimbali ndani ya Jeshi hilo. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso-SSP; miongoni mwa makamanda wa mikoa waliofanyiwa mabadiliko ni pamoja na aliyekuwa Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma Kamishna msaidizi mwandamizi (SACP) Deusdedit Nsimeki anayekwenda kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Kamishna msaidizi (ACP) Akili Mpwapwa sasa anakuwa Kamanda wa Polisi Ruvuma. 
Taarifa hiyo imeeleza aliyekuwa Ofisa Mnadhimu Mkoa wa Lindi, Kamishna Msaidizi (ACP) Renatha Mzinga anakuwa Kamanda wa Mkoa wa Lindi, aliyekuwa Ofisa Mnadhimu Mkoa wa Dodoma Kamishna Msaidizi (ACP) Suzan Kaganda amehamishwa kuwa Kamanda Mkoa wa Tabora huku aliyekuwa Kamanda wa Polisi Tabora (ACP), Peter Ouma amehamishiwa Polisi Makao Makuu. 

9 KANEMBWA WATAKIWA KUWASILISHA UTETEZI

February 05, 2014
Release No. 020
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Februari 6, 2014

9 KANEMBWA WATAKIWA KUWASILISHA UTETEZI
Wachezaji tisa wa Kanembwa JKT pamoja na timu yao wanaolalamikiwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kumpiga mwamuzi Peter Mujaya wanatakiwa kujitetea mbele ya Kamati ya Nidhamu itakayokutana Jumapili (Februari 9 mwaka huu).

Utetezi huo unaweza kuwa wa mdomo kwa walalamikiwa kufika wenyewe mbele ya kamati itakayokutana saa 4 kamili asubuhi au kuuwasilisha kwa njia ya maandishi.

Kamati ilikutana jana Jumatano (Februari 5 mwaka huu) kusikiliza malalamiko dhidi ya wachezaji hao na timu yao kwa tukio hilo lililotokea Novemba 2 mwaka jana kwenye mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) dhidi ya Stand United FC iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Wachezaji hao ni Abdallah Mgonja, Bariki Abdul, Philipo Ndonde, Mbeke Mbeke, Mkuba Clement, Mrisho Mussa, Nteze Raymond, Ntilakigwa Hussein na Uhuru Mwambungu. Mlalamikiwa mwingine ambaye naye anatakiwa kujitetea ni timu ya Kanembwa JKT.

Ikiwa chini ya Mwenyekiti wake Tarimba Abbas, Kamati hiyo baada ya kusikiliza malalamiko dhidi ya wahusika na kupokea ushahidi wa aina mbalimbali kutoka kwa mlalamikaji imesema ili iweze kutenda haki katika shauri hilo ni lazima walalamikiwa wapate fursa ya kusikilizwa.

Katika hatua nyingine, Kamati hiyo iliyokutana kwa mara ya kwanza tangu ilipoundwa imesema imesikitishwa na vitendo vya fujo ndani ya mpira wa miguu, na kuwataka watu wasijihusishe na aina yoyote ya fujo.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MGAMBO SHOOTING,RUVU SHOOTING HAKUNA MBABE ZATOKA SULUHU PACHA.

February 05, 2014
WACHEZAJI WA MGAMBO NA RUVU SHOOTING WAKISALIMIANA KABLA YA KUANZA MECHI YAO LEO KWENYE UWANJA WA MKWAKWANI



February 05, 2014
BARAZA LA SANAA ZANZIBAR LATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA SUALA LA UTAMADUNI 
Na Masanja Mabula -Pemba .05/02/2014.

Afisa utamaduni Mkoa wa Kaskazini Pemba Hamad Said Mgau amelitaka Baraza la Sanaa Zanzibar  kusimamia vyema suala la utamaduni  ili kudhibiti upotoshaji wa utamaduni wa asili unaofanywa na baadhi ya wanii hapa nchini .

Amesema kuwa utamaduni wa asili visiwani hapa ikiwemo ngoma ya Msewe imekuwa ikipotoshwa na baadhi ya watu kwa makusudi , hivyo ni vyema kwa Baraza kuwa makini katika kusimamia na kulinda asili ya utamaduni huo .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Wete , Mgau amesema kuwa endapo Baraza halitakuwa makini kuwadhibiti watu wanaochafua utamaduni huo , basi vizazi vijavyo vitarithi utamaduni usiolingana na maadili .

"Tunashughudia baadhi ya wanii wanapotosha kabisa uhalisia wa ngoma ya msewe , hivyo ni vyema Baraza la Sanaa kuwa makini na watu wa aina hiiambao wamekusudia kuharibu uahalisia wa sanaa hiyo " alifahamisha Mgau .

Aidha amefahamisha kwamba utamaduni wa asili umekuwa ni kivutoa kwa watalii , na kuongeza kwamba kitendo cha kupotoshwa kunaweza kuleta athari kwa Taifa ikiwa udhibiti wake hautapewa kiupambele .

Hata hivyo ameeleza kwamba Upotoshaji wa Ngoma ya Msewe zaidi umakuwa ukifanywa na wanii nje ya Kisiwa Cha Pemba , na kusema kuwa wnaotaka kuiga kucheza ngoma hiyo ni lazima wafuate taratibu zake .
February 05, 2014

TANAPA YAKABIDHI MADARASA MAWILI KATIKA SHULE YA SEKONDARI NKOARISAMBU-ARUMERU

Mwenyekiti wa kamati ya ardhi,maliasili na mazingira ,Mh James Lembeli akiongoza ujumbe wake kusalimiana na wanachi wa kata ya Nkoarisambu katika wilaya ya Meru mkoani Arusha ambako kamati hiyo ilitembelea shule ya sekondari Nkoarisambu kuzindua majengo mawili ya madarasa.
Naibu waziri wa ardhi,maliasili na mazingira,Mahamud Mgimwa akiteta jambo na Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki Joshua Nassar kabla ya uzinduzi wa madarasa yaliyojengwa kwa mchango wa wananchi na TANAPA.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Nkoarisambu iliyopo wilayani Meru mkoani Arusha ambayo imejengewa madarasa mawili kwa ushirikiano wa wananchi na TANAPA.
Mwenyekiti wa kamati ya ardhi,maliasili na mazingira,Mh James Lembeli akijaribu kubadilishana mawazo na naibu waziri wa maliasili na utalii,Mahamud Mgimwa pamoja na mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki Mh Joshua Nassar.

RC GALLAWA AFANYA ZIARA WILAYA YA TANGA

February 05, 2014
MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKIFUNGUA JENGO LA MAABARA YA SHULE YA SEKONDARI PONGWE WAKATI AKIWA KWENYE ZIARA YAKE YA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO KATIKA WILAYA YA TANGA.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa akifungua jengo la maabara kwenye shule ya sekondari Pongwe juzi akiwa kwenye ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye wilaya ya Tanga anayeshuhudia wa kwanza ni Meya wa Jiji la Tanga,Omari Guledi.
Kaimu Meneja wa Tanesco Mkoa wa Tanga,Joackim Luheta
kushoto akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku
Gallawa wa pili kulia jinsi ya kituo cha kupozea umeme Kange jinsi
kinavyofanya kazi wakati wa ziara yake ya kukagua shughulia mbalimbali
za maendeleo kwenye wilaya ya Tanga.
Kaimu Meneja wa Tanesco Mkoa wa Tanga,Joackim Luheta kushoto akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Luteni Mstaafu Chiku Gallawa  wa Tatu kushoto jinsi ya kituo hicho cha kupozea umeme Kange jijini Tanga kinavyofanya kazi wanaoshuhudia ni kushoto ni Meya wa Jiji la Tanga Omari Guledi na Mkuu wa wilaya ya Tanga,Halima Dendego.
MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA KATIKATI AKISISITIZA JAMBO KWA KAIMU MENEJA WA TANESCO MKOA WA TANGA,JOACKIM LUHETA KUHUSU KITUO HICHO WA KWANZA KUSHOTO NI MKUU WA WILAYA YA TANGA,HALIMA DENDEGO.
HAPO MKUU WA MKOA WA TANGA,LUTENI MSTAAFU CHIKU GALLAWA AKISAINI KITAMBU CHA WAGENI MARA BAADA YA KUWASILI KWENYE KITUO HICHO CHA KUPOZEA UMEME KANGE JIJINI TANGA.