RC TANGA AONGOZA MAPOKEZI YA COASTAL UNION "MABINGWA WA KOMBE LA UHAI"

December 03, 2013
Na Oscar Assenga, Tanga.
MKUU wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa jana aliwaongoza wakazi wa mkoa katika mapokezi ya kuipokea timu ya Vijana ya Coastal Union ambao ni mabingwa wapya wa Mashindano ya Kombe Uhai Cup baada ya kuifunga Yanga kwenye mechi ya Fainali.

Maandalizi ya mapokezi hayo yalianza majira ya saa nane mchana kwa shamrashamra za aina yake huku barabara iliyokua ikielekea kwenye uwanja wa Mkwakwani ilifurika umati mkubwa wa mashabiki wake.

AFRIKA KUSINI KUTUA ALHAMISI KUIVAA TANZANITE

December 03, 2013
Release No. 203
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Desemba 3, 2013


Kikosi cha Afrika Kusini kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia kwa wasichana wenye umri chini ya miaka 20 dhidi ya Tanzania (Tanzanite) kinatua nchini Alhamisi (Desemba 5 mwaka huu).

Afrika Kusini ambayo itafikia hoteli ya Sapphire itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) itatua saa 8 kamili mchana kwa ndege ya South Africa Airways.

Mechi hiyo itachezeshwa na refa Nabikko Ssemambo kutoka Uganda wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Gebreyohanis Trhas kutoka Ethiopia. Waamuzi wengine ambao pia wanatoka Uganda ni Nakitto Nkumbi na Irene Namubiru.