MAJIMBO 214 KUNUFAIKA NA UGAWAJI WA VIFAA TIBA VYA SHILINGI BILIONI 14.9

January 05, 2024

 Na. WAF - Dar es Salaam 

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu leo Januari 5, 2023 amezindua usambazaji wa Vifaa Tiba (nje ya vilivyopangwa kununuliwa kwenye Bajeti ya 2023/24) vitakavyosambazwa katika majimbo yote 214 nchini Tanzania Bara.

Waziri Ummy amesema Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa fedha za nyongeza Tsh. Bilioni 14.9 mwezi November 2023 na kununuliwa vifaa hivyo ili kuendelea kuboresha huduma za Afya ya uzazi, mama na mtoto.

Miongoni mwa vifaa ambavyo Waziri Ummy amepokea ni pamoja na vitanda vya wagonjwa 3,080, vitanda vya kujifungulia 1,000, magodoro 5,500, mashuka 36,808, pamoja na meza za vutanda 306. 

“Tunategemea kupokea vifaa tiba vingine hivi karibuni ambavyo ni vitanda vya kujifungulia (4280), vitanda vya kufanyia uchunguzi (examination table) 4280, mkoba wa vifaa vya kujifungulia (delivery kit) 4280, kabati za vitanda (bed side lockers) 6420 na stendi ya dripu (6420).” Amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema takwimu zinaonesha asilimia 86 ya wanawake wajawazito Tanzania wanajifungulia katika Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali za Halmashauri, vifaa hivyo vitakwenda kusaidia kuboresha huduma za Afya ya uzazi, mama na mtoto.

Amesema, katika Kila jimbo litapata Vitanda 30, Magodoro 30, Mashuka 60, Bed side locker 30, Drip Stand 30, Meza ya kulia chakula 15, Vitanda vya kujifungulia 10, Delivery set 10 pamoja na Examination bed 10. 

“Waheshimiwa Wabunge watavikuta vifaa hivi kwenye vituo viwili katika kila jimbo ambapo Bohari ya Dawa (MSD) watashusha mzigo huu.” Amesema Waziri Ummy

Mwisho, Waziri Ummy amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Sekta ya Afya kutekeleza mikakati mbalimbali ya kuboresha huduma za afya ambapo imeweza kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

“Vifo vimepungua kutoka vifo 556 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2016 hadi vifo 104 kwa vizazi hai 100,000 ikiwa lengo la Dunia ni Tanzania kupunguza vifo vya wajawazito kufikia vifo 70 kila vizazi hai 100,000 ifikapo mwaka 2030.










TBS YAINGIA MAKUBALIANO NA JESHI LA POLISI KUKAGUA MAGARI YANAYOTUMIKA NCHINI

January 05, 2024

 NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limesaini Hati ya Makubaliano (MoU) na Jeshi la Polisi ili kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa TBS, Dkt. Athuman Ngenya amesema ushirikiano huo ni muhimu katika kutekeleza azma ya kuendelea kulinda Maisha ya watanzania kwa kuhakikisha kuwa ukaguzi wa magari wakati yanapotumika hapa nchini unaofanyika kwa mujibu wa Sheria ya Trafiki (yaani Road Traffic Act, Cap 168), unafanyika kwa kutumia mitambo ya kisasa ili kuthibitisha usalama wake.

"Kwa kuzingatia uwezo uliopo,TBS itatumia wataalam wake, viwango pamoja na mitambo ya kisasa katika kukagua na kupima magari yote yatakayoletwa na Jeshi la Polisi, Kitengo cha  Trafiki kwa ukaguzi kwa mujibu wa Sheria Usalama Barabarani Sura 168 ambayo inalazimu kufanyika ukaguzi wa vyombo vya moto ili kuhakikisha vinakidhi matakwa ya vigezo vya usalama kwa lengo la kulinda usalama wa abiria na watumiaji wengine wa barabara". Amesema 

Aidha amelihakikishia jeshi la polisi  kwamba TBS ni mshirika sahihi wa Jeshi la Polisi Tanzania, kwani ndiyo inayodhibiti ubora na usalama wa vyombo vya moto vinavyoingia nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi Haji amesema kupitia makubaliano hayo wanatarajia usalama barabarani kuimarika zaidi kwa watumiaji wa barabara.

"Tukiwa na Vyombo vya Moto salama tutakuwa na watumiaji salama wa barabara, tutakuwa na barabara salama na pia shughuli za uokozi zinaweza kuimarishwa na mwisho tutakuwa na tumeimarisha uongozi katika usalama barabarani". Amesema 

Amesema kuwa hatua hiyo ni utekelezaji wa Maelekezo ya Tume ya Haki Jinai inayosisitiza kushirikiana na wadau mbalimbali katika usimamizi wa sheria za usalama barabarani ili kuzuia uhalifu barabarani.

Pamoja na hayo amewataka wamiliki wa vyombo vya moto kuhakikisha wanatimiza wajibu wa kisheria wa kukagua vyombo vyao kama inavyoelekezwa katika sheria kwani jeshi la polisi litakuwa na muhari kwa watakaoshindwa kutii sheria bila shuruti.

Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi Haji wakisaini makubaliano (MoU) katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akibadilishana mikataba na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi Haji mara baada ya kusaini makubaliano (MoU) katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akibadilishana mikataba na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi Haji mara baada ya kusaini makubaliano (MoU) katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi Haji wakionesha mikataba mara baada ya kusaini makubaliano (MoU) katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini makubaliano (MoU) kati ya TBS na Jeshi la Polisi katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi Haji akizungumza kwenye hafla ya utiaji saini makubaliano (MoU) kati ya TBS na Jeshi la Polisi katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam

Baadhi ya Makamishna wa Polisi wakifuatilia hafla ya utiaji saini Makubaliano (MoU) kati ya Jeshi la Polisi na Shirika la Viwango Tanzania katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam
Baadhi ya Wakurugenzi na watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wakifuatilia hafla ya utiaji saini Makubaliano (MoU) kati ya Jeshi la Polisi na TBS katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi wakipata picha ya pamoja na Wakurugenzi na watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Makamishna wa Polisi katika hafla ya utiaji saini makubaliano (MoU) kati ya TBS na Jeshi la Polisi katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi wakipata picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani katika hafla ya utiaji saini makubaliano (MoU) kati ya TBS na Jeshi la Polisi katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi wakipata picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani katika hafla ya utiaji saini makubaliano (MoU) kati ya TBS na Jeshi la Polisi katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa  Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Kamishna wa Polisi Awadhi wakipata picha ya pamoja na baadhi ya Makamishna wa Jeshi la Polisi katika hafla ya utiaji saini makubaliano (MoU) kati ya TBS na Jeshi la Polisi katika kushirikiana katika ukaguzi wa Vyombo Vya Moto kwa kutumia Vifaa vya Kisasa vinavyomilikiwa na TBS. Hafla hiyo imefanyika leo Januari 5,2024 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

MHE. KAPINGA : TANOIL IMARISHENI UTENDAJI KAZI KULETA MATOKEO CHANYA

January 05, 2024


Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni Tanzu ya Mafuta ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wakati wa ziara yake ya kikazi katika kampuni hiyo Tarehe 05 Januari 2024 Jijini Dar es salaam.



Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga akitoa maelekezo kwa Bodi na Manejimenti ya Kampuni Tanzu ya Mafuta (TANOIL) wakati wa ziara yake ya kikazi Tarehe 05 Januari, 2024 Jijini Dar Es Salaam.




Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni Tanzu ya Mafuta (TANOIL), Patrick Mongela akieleza utendaji kazi wa Kampuni hiyo kwa Naibu Waziri Nishati Mhe. Judith Kapinga wakati wa ziara yake ya kikazi Tarehe 05 Januari, 2024 Jijini Dar Es Salaam.

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Kampuni Tanzu ya Mafuta(TANOIL), wakati wa ziara yake ya kikazi Tarehe 05 Januari, 2024 Jijini Dar Es Salaam.

Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Manejimenti ya Kampuni Tanzu ya Mafuta(TANOIL), wakati wa ziara yake ya kikazi, Tarehe 05 Januari, 2024 Jijini Dar Es Salaam.



Dar es Salaam,

Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni Tanzu ya Mafuta (TANOIL) ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na Menejimenti ya Kampuni hiyo wameaswa kuhakikisha kuwa wanaimarisha na kuleta matokeo chanya kiutendaji yanayofanywa na kampuni hiyo kwa watanzania na Taifa kwa jumla.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kampuni hiyo, Tarehe 5 Januari, 2024, Jijini Dar es Salaam.

Ameileza Bodi na Menejimenti kuwa wahakikishe TANOIL inatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia Malengo, Dhima na Azma ya kuanzishwa kwa Kampuni hiyo nchini.

Vilevile ameelekeza kuwa Viongozi hao watumie Mbinu zao, Taaluma na Uwezo Wao wote kuhakikisha kuwa Kampuni hiyo inatengeneza faida zaidi badala ya hasara kwa taifa na pia waepuke kuzalisha madeni.

Aidha ameelekeza TANOIL kushirikiana na TPDC, Mamlaka ya Uthibiti wa Huduma za Maji na Mafuta (EWURA) katika kutekeleza majukumu yao kwa kuwa yanashabihiana ili kuleta matokeo chanya ya kampuni hiyo katika kujiendesha.

TANZANIA YAPIGA HATUA KATIKA VIASHIRIA VYA AFYA YA MAMA NA MTOTO, TAKWIMU ZA VIFO ZASHUKA

January 05, 2024

 



Waziri wa Afya Mh. Ummy Mwalimu amesema taarifa za utafiti wa Demographia ya Afya ya Uzazi na Viashiria vya Malaria (TDHS/MIS) ya mwaka 2022 zinaonesha kuwa Tanzania imepiga hatua katika viashiria vingi vya afya ya mama na mtoto.

Ametoa mfano kuwa Vifo vitokanavyo na Uzazi vimeshuka kutoka 556 kwa kila vizazi hai 100,000 mwaka 2015/16 hadi 104 kwa kila vizazi hai 100,000 na vifo vya Watoto chini ya miaka mitano vimeshuka kutoka 67 kati ya vizazi hai 1000 mwaka 2015/16 hadi 43 kwa kila vizazi hai 1000. Hii ni sawa na kupunguza vifo vya kinamama wajawazito kutoka 11,000 hadi vifo 2,500 kwa mwaka.

Waziri Ummy Mwalimu ameyasema hayo Leo wakati usinduzi wa usambazaji wa vifaa vya uboreshaji wa huduma za mama na motto uliofanyika kwenye makao Makuu ya Bohari ya Dawa MSD jijini Dar es Salaam Leo Ijumaa Januari 5,2024.

Amesema hizi ni jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wadau wa afya katika kuhakikisha kuwa Nchi yetu inafikia malengo ya kitaifa na kimataifa kama vile malengo endelevu ya Milenia 2030 yanayotutaka kupunguza athari za vifo vitokanavyo na uzazi hadi kufikia vifo chini ya 70 katika kila vizazi 100,000 vifo vya Watoto chini ya 38 katika kila vizazi hai 1,000 pamoja na vya Watoto chini 12 katika vizazi hai 1,000.


Ummy Mwalimu ameongeza kuwa serikali imeendelea kuwekeza katika afya ya mama na mtoto kwa kujenga vituo vya huduma za upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni (CEmONC) kutoka vituo 340 mwaka 2021 hadi kufikia vituo 523 mwaka 2023. Maboresho ya upatikanaji huduma hizi katika vituo vya kutolea huduma za afya yamesogeza huduma hizo za upasuaji karibu na wananchi. zaidi ya asilimia 75 85 ya wananchi wanapata huduma za Afya ndani ya Kilometa 5 ndani ya maeneo wanayoishi.

Amesema hali kadhalika Serikali imeendelea kuwekeza katika Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto kwa kujenga Wodi za uangalizi maalumu (NCU za watoto wachanga) zinazohudumia watoto wachanga walio mahututi kwa mara mbili zaidi kutoka 99 mwaka 2021 hadi 189 mwaka 2023. Hizi ni hatau zinazochukuliwa na Serikali katika kutoa huduma bora za afya na kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa wakiwa chini ya kilo moja.
Sambamba na kuboresha huduma hizo Serikali imeendelea kununua na kusambaza vifaa tiba na dawa hivyo kuongeza wigo wa upatikanaji bidhaa za afya ya uzazi kutoka asilimia 82.5 mwaka 2022 hadi kufikia asilimia 88.2 mwaka 2023.

Aidha amesema Serikali imeendelea kuajiri na kupeleka watumishi wenye sifa katika Vituo vya kutolea huduma za afya nchi nzima kuajiri watumishi wa afya wapatao 28,759 hadi kufikia mwaka 2023.

Akizungumza kuhusu kuhusu Vitanda vua kutolea huduma za afya ya Uzazi, Serikali kwa kushirikiana na wafau amesema selikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa vifaatiba hivyo kwa ajili ya huduma za afya ya uzazi ambapo hali ya vitanda vya kutolea huduma kwenye vituo vya afya imeongezeka kutoka vitanda 84,162 (mwaka 2021) hadi vitanda 104,687 (mwaka 2023).

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ununuzi wa vifaa tiba hivi ambavyo vina thamani ya TZS 14,953,854,357 ambavyo ni vitanda vya wagonjwa (3080), vitanda vya kujifungilia (1000), magodoro (5500), mashuka (36808), meza za vitanda (overbed table) 306. Vifaa hivi vitasambazwa katika Majimbo yote 214 nchini Tanzania Bara.

Aidha wizard inategemea kupokea vifaa tiba vingine hivi karibuni ambavyo ni vitanda vya kujifungulia (4280), vitanda vya kufanyia uchunguzi (examination table) 4280, mkoba wa vifaa vya kujifungulia (delivery kit) 4280, kabati za vitanda (bed side lockers) 6420 na stendi ya dripu (6420).

Amesema wizara itagawa kila jimbo vifaa hivyo ambapo Kila jimbo litapata Vitanda 30; Magodoro 30; Mashuka 60; Bed side locker 30; Drip Stand 30; Meza ya kulia chakula 15; Vitanda vya kujifungulia 10; Delivery set 10 pamoja na Examination bed 10. Waheshimiwa Wabunge watavikuta vifaa hivi kwenye vituo viwili katika kila jimbo ambako MSD watashusha mzigo.

Waziri Ummy amesema ana imani kwamba, vifaa hivi vilivyotolewa leo vitachangia katika kuboresha zaidi huduma hizi za mama na mtoto. Aidha ametoa rai kwa Bohari ya dawa kuhakikisha vifaa tiba hivi vinasambazwa kwa wakati.
WAZIRI MAZRUI AZINDUA  BARABARA ZA KOMBENI, NYAMANZI NA DIMANI BICHI, DIMANI MAKETI NA VITONGOJI VYAKE

WAZIRI MAZRUI AZINDUA BARABARA ZA KOMBENI, NYAMANZI NA DIMANI BICHI, DIMANI MAKETI NA VITONGOJI VYAKE

January 05, 2024

 

Waziri wa Afya Zanzibar Mhe.Nassor Ahmed Mazrui akita utepe kuashiria uzinduzi wa barabara ya ndani ya Dimani-Sokoni-Dimani- Beach pamoja na barabara ya Kombeni -Nyamanzi zenye urefu wa kilomita 2.8  ikiwa ni shamrashamra za kutimiza miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

 

Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Nassor Ahmed Mazrui amesema ujenzi wa Barabara ya Kombeni, Nyamanzi na Dimani bichi, Dimani maketi na vitongoji vyake ni kichocheo Cha maendeleo na upatikanaji wa ajira kwa vijana wa maeneo hayo.

Ameyasema hayo huko Nyamazi Wilaya ya Magharibi B wakati wa uzinduzi wa Barabara hizo kufuatia shamrashamra za maadhimisho ya Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Amesema Wananchi wamaeneo hayo muda mrefu walikuwa na malalamiko ya Barabara lakini kutengezwa kwake kutaondosha changamoto walizokuwa wakizipata hasa Wanapokuwa na Watoto, Wagonjwa na Mizigo.

Amesema maeneo hayo yamo katika maeneo yanayokua kwa uekezaji na ujenzi wa majengo ya kisasa jambo ambalo litaufanya Mji huo kuwa Mji wa pili wa Zanzibar.

“Hapa zitatokea ajia kwani mkongo wa Mawasiliano Tehama unajengwa hapa, maonesho ya biashara yapo hapa, majengo mazuri yapo hapa huu utakuwa ni Mji wa Pili na utatoa fursa za ajira kwa Vijana wengi’, amesema Mazrui”

Aidha amesema kuwa ujenzi huo ni kuyaezi Mapinduzi yaliomkomboa Mnyonge kutoka katika makucha ya Wakoloni sambamba na kuwaletea maendeleo endelevu Wananchi wake.

Nae Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Shomari Omar Shomari akisoma Ripoti ya kitaalamu amesema Barabara hiyo ina urefu wa kilomita mbili nukta nana (2.8) inajengwa kwa kiwango Cha uwekaji wa tabaka lakemikali iliochanganywa na maji, uwekaji wa tabaka mbili za lami ya kokoto (chipsi) na uwekaji watabaka la lami na rojo.

Amesema Barabara hiyo inajengwa na Kampuni ya IRIS ASER kutoka Uturuki na ujenzi wake ulianza julai 17, 2022 na kukamilika Oktoba 5, 2023 ambayo magari yanayo takiwa kupita ni magari ya tani 10 na inaaminika kudumu kwa mda wa Miaka kumi.

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Idrissa Kitwana Mustafa amesema ujenzi huo utaondoa changamoto kwa Wananchi na Waekezaji na kuwa katika Mazingira mazuri.

Gharama za Ujenzi huo imechanganywa kwenye jumla ya Mradi wote wa Ujenzi wa Barabara za ndani kilomita 275.9 ambapo gharama zake zinakisiwa kuwa ni zaidi ya Dola za kimarekani Laki Nane.

PROF. NDALICHAKO ASISITIZA CMA KUJA NA MFUMO KIDIGITALI WA KURAHISISHA USULUHISHI NA UAMUZI

PROF. NDALICHAKO ASISITIZA CMA KUJA NA MFUMO KIDIGITALI WA KURAHISISHA USULUHISHI NA UAMUZI

January 05, 2024





Na; Mwandishi Wetu - Morogoro


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako ameitaka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) kuja na mfumo wa kidigitali ambao utarahisisha usuluhishi na utatuzi wa migogoro.


Prof. Ndalichako amesema hayo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha tathimini ya utendaji kazi wa tume hiyo na mafunzo kilichofanyika leo tarehe 4 Januari, 2024 mkoani Morogoro.


Ameeleza kuwa, mfumo huo utasaidia kufanya utatuzi wenye haki na kwa wakati na pia kupunguza mrundikano wa kesi.


Kwa upande mwengine amewataka watumishi wa ofisi hiyo kumuunga mkono Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya kazi kwa bidii na waledi ili kuimarisha uchumi wa wananchi pamoja na taifa kwa ujumla.


Pia, amewasisitiza kila mtumishi katika ofisi hiyo kushiriki katika mafunzo hayo kwa kuwa yanalenga kuleta maendeleo na mahusiano mazuri katika utendaji kazi wao.


Naye, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi, Dkt. Yose Mlyambina amesema Tume inatakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano na mahakama ili kuweza kupunguza mlundikano wa mashauri, kwani Uchumi utakua kwa kasi na uwekezaji utaongezeka ukichochewa na huduma bora za utoaji haki hususani haki kazi.


Kwa upande wa Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Usekerege Mpulla amesema kuwa CMA itahakikisha ina anzisha mfumo wa kidijitali ambao utawawezesha watumishi kufuatilia taarifa na kurahisisha upatikanaji wa taarifa hizo.


RAIS DKT MWINYI ASHUHUDIA KARAFUU ZA MAGENDO BANDARINI  WETE

RAIS DKT MWINYI ASHUHUDIA KARAFUU ZA MAGENDO BANDARINI WETE

January 05, 2024

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi ametembelea Bandari ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba katika ziara ya kushtukiza na kushuhudia karafuu za magendo tani 9.5 zenye thamani ya shilingi milioni 140 zilizotaka kusafirishwa kwa magendo na kukamatwa kwa ushirikiano wa Vyombo vya ulinzi na usalama Mkoa wa Kaskazini Pemba vikiwemo Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) na Kikosi cha Kuzuia Magendo (KMKM) tarehe 04 Januari 2024 , Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Aidha Rais Dkt.Mwinyi ameleeza kuwa Serikali imeamua asilimia 80 ya mauzo ya karafuu katika soko la dunia kumpatia mkulima wa karafuu na 20 kwa shirika la biashara Zanzibar (ZSTC) kutumika katika uendeshaji.

Vilevile Rais Dkt.Mwinyi amesema karafuu iliyokuwa bora inatoka Zanzibar kwa kuitunza vizuri na kuisafisha bei yake itaendelea kuimarika duniani.

Halikadhalika Rais Dkt.Mwinyi amewasihi wananchi wasifanye magendo kwa maana watapata hasara kulingana na sheria za nchi, pia amesema Serikali itaendelea kuongeza bei ya karafuu.

MAZUNGUMZO YA SIMU HUATHIRI USIKIVU

MAZUNGUMZO YA SIMU HUATHIRI USIKIVU

January 05, 2024





Na. Raymond Mtani BMH-DODOMA

Imeelezwa kuwa kuzungumza kwa njia ya simu kwa muda mrefu kinaweza kuwa chanzo mojawapo cha kupoteza usikivu.

Hayo yamesemwa na Leonard Tibihika, Mtaalamu wa Upimaji Usikivu wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) katika mahojiano maalumu kuhusu huduma za uchunguzi wa Usikivu Hospitalini hapo, leo Januari 5, 2024.

“isitafsirike vibaya, si kila anayeongea na simu anahatarisha usikivu, bali yule anayetumia muda mrefu kuongea na simu, kwa sababu mgandamizo wa sauti inayoingia sikioni ukiendelea kwa muda mrefu huathiri Ngoma ya Sikio” Alisema Tibihika.

Watu wengine waliyoko katika hatari ya kupoteza usikivu ni wale wanaofanya kazi katika mazingira ya kelele, alisema Mtalaamu huyo akitolea mfano, wafanyakazi wa viwandani na wanaokesha kwenye klabu za muziki, na wale wenye shughuli katika masoko.

“changamoto anayoweza kukutana nayo mtu anayepoteza usikivu ni kutogundua mapema kuwa usikivu wake hauko katika kiwango cha kawaida, akachukua hatua kwa sababu usikivu hupungua polepole wakati mwingine hadi ambiwe na wengine” Tibihika.

Kuchelewa kugundua kuwa usikivu unapotea, au kugundua na kutochukua hatua za kuchunguzwa ili kutibiwa husababisha watu wengi kufika Hospitali wakiwa katika hatua mbaya kiasi cha kuhatarisha kupoteza usikivu kabisa.

Taarifa za Vituo vya Udhibiti na Kukinga Magonjwa (CDCs) zinadokeza kuwa, Watoto na Vijana wadogo milioni 5.2 na watu wazima milioni 26 hupoteza uwezo wa kusikia kutokana na kuwa kwenye mazingira ya kelele.

Katika moja ya tafiti kuhusu kupoteza usikivu kwa matumizi makubwa ya simu uliyobandikwa katika tovuti ya Shirika la Afya Duniani (WHO), unathibitisha kuwa matumizi ya zaidi ya dakika 60 kila siku yanaweza kuathiri usikivu wa binadamu ndani ya miaka 5.

Tibihika, anatoa wito kwa watumiaji wa simu kwa muda mrefu, kuchukua hatua za kujikinga, pamoja na kuhakikisha wanafanyiwa uchunguzi wa usikivu angalau mara mbili ndani ya miezi 12.

Hospitali ya Benjamin Mkapa, ni miongoni mwa Hospitali tatu za serikali nchini zinazotoa huduma za uchunguzi wa usikivu kwa kufanya vipimo vya aina zote, asilimia kubwa ya wagonjwa wanaopoteza usikivu hubainika kuwa na tatizo la kupasuka Ngoma ya Sikio.