Na Amina Omari,Tanga
Kiwanda cha kutengeneza mikate cha (TANGA MODERN BAKERY
)kimekua cha pili kufungiwa shirika la viwango Tanzania TBS katika
kipindi kisichozidi wiki moja mkoani Tanga baada ya kubainika kuwa
kinazalisha mikate bila kufuata taratibu za viwango bora vya uzalishaji.
Akizungumza katika oparesheni hiyo, Afisa Uhusiano wa TBS Rhoida Andusamile
alisema wamezuia uzalishaji katika kiwanda hicho baada ya kubaini kuwa
wamiliki wakiwanda hicho wamekua wakitengeneza mikate ambayo
inatengenezwa bila kufuata taratibu za shirika la viwango nchini.
Alisema mikate ni bidhaa ambayo ipo katika viwango vya lazima vya ubora hivyo kiwanda hicho kwa muda mrefu kimekuwa kinazalisha bidhaa bila kuwa na nembo ya ubora ya kutoka TBS.
“Niwajibu wetu kuhakikisha kila mzalishaji nchini
anazalisha bidhaa zenye ubora kwa lengo la kuwakinga walaji na madhara
ya kiafya hivyo tumekuwa tukiendesha ukaguzi wa mara kwa mara katika
bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini lengo ikiwa ni kumlinda
mlaji”Andusamile.
Nae mkaguzi washirika hilo Deusdedit Paschal alisema bakery hiyo ilitakiwa kabla haijaanza uzalishaji wapeleke sampuli za mikate TBS kwa ajili ya kuangalia ubora pamoja na ukaguzi kufanyika lakini yote hayo hayakufanyika.
Alisema
kwa miaka 16 kiwango hicho kimekuwa kizalisha mikate hiyo pamoja na
bidhaa nyingine kama keki bila ya ya kuwa na mikataba na TBS wala nembo
ya ubora pamoja na ukaguzi.
Kwa upande wake Meneja
wa kiwanda hicho Hilal Salim alikiri kuendesha uzalishaji bila kuwa na
nembo ya kuthibitisha ubora wa bidhaa yake ,hata hivyo alliomba TBS
kutokifungia kiwanda hicho kwani wananchi wengi wataathirika na ukosefu
wa bidhaa zake
Hata
hivyo baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho walisema kufungiwa kwa
kiwanda hicho kutawathiri kiuchumi kwani walikuwa wanatagemea ajira hiyo
kuendesha familia zao.
Mei
22 mwaka huu shirika la viwango nchini TBS lilifungia kiwanda cha
kutengeneza maji cha Al Hayaa kutoka na kuendeleza uzalishaji wa bidhaa
hiyo bila kuwa na leseni ya ubora.
|
RCL KUENDELEA KUTIMUA VUMBI LEO
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Raundi
ya pili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) inaendelea leo (Mei 26 mwaka huu)
kwa mechi sita za kwanza zitakazochezwa katika miji sita tofauti.
Abajalo
ya Dar es Salaam na Kariakoo ya Lindi zitaumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
Karume, Dar es Salaam wakati Machava FC ya Kilimanjaro itakuwa mwenyeji wa
Mpwapwa Stars ya Dodoma kwenye Uwanja wa Ushirika mjini Moshi.
Nayo
Stand United FC ya Shinyanga itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye
Uwanja wa Namfua mjini Singida huku Polisi Jamii ya Bunda mkoani Mara ikimenyana
na Biharamulo FC ya Kagera kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.
Mjini
Kigoma kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika ni kati ya wenyeji Saigon FC na Katavi
Warriors ya Katavi wakati Njombe Mji itaikaribisha Kimondo SC ya Mbeya kwenye Uwanja
wa Sabasaba mjini Njombe.
Timu
zitakazofuzu kucheza raundi ya tatu zitacheza mechi za kwanza kati ya Juni 8 na
9 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakuwa kati ya Juni 15 na 16 mwaka huu.
Mwisho.
TAIFA STARS KWENDA ADDIS ABABA LEO
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kuondoka leo (Mei 26 mwaka huu) usiku kwenda Addis Ababa, Ethiopia ambapo itaweka kambi na kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya kwenda Morocco.
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kuondoka leo (Mei 26 mwaka huu) usiku kwenda Addis Ababa, Ethiopia ambapo itaweka kambi na kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya kwenda Morocco.
Stars
inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka saa 5 usiku kwa
ndege ya EgyptAir ikiwa na kikosi cha wachezaji 21 chini ya nahodha wake
kipa Juma Kaseja.
Timu
hiyo ikiwa Ethiopia, Juni 2 mwaka huu itacheza mechi ya kirafiki dhidi
ya Sudan ambapo siku inayofuata itaondoka kwenda Marrakech, Morocco kwa
kupitia Cairo, Misri. Mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya
wenyeji Morocco itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech.
Mbali
ya nahodha Kaseja, wachezaji wengine wanaoondoka katika kikosi hicho
ambacho kina wiki sasa tangu kingie kambini jijini Dar es Salaam ni
Mwadini Ally na Ally Mustafa ambao wote ni makipa.
Wengine
ni Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Aggrey Morris, Haroub Nadir, Mwinyi
Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum
Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya,
Athuman Idd na Haruni Chanongo.
Wachezaji
Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wako na timu yao ya TP Mazembe
ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo watajiunga moja kwa moja na Stars
jijini Marrakech, Juni 4 mwaka huu wakitokea Maputo, Msumbiji mara baada
ya mechi yao ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Liga Muculumana ya huko.
Katika
msafara huo wa Ethiopia benchi la ufundi la Stars linaundwa na Kim
Poulsen (Kocha Mkuu), Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi),Juma Pondamali
(Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja wa timu), Dk. Mwanandi
Mwankemwa (Daktari), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred
Chimela (Mtunza vifaa).
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Redd's Miss Tanga, kutembelea vivutio vya utalii June 17.
Na Oscar Assenga,Tanga.
WAREMBO wanaowania umalkia wa Mkoa wa Tanga “Redd’s Miss Tanga 2013”wanatarajiwa
kutembelea katika vivutio vya utalii na maeneo ya kihistori yaliyopo mkoani
hapa June 17 mwaka huu lengo likiwa ni kujifunza utalii wa ndani ili kuweza
kupata fuksa nzuri ya kuweza kuutangaza kwa wageni na wenyeji.
Shindano hilo linatarajiwa
kufanyika 22 kwenye Uwanja wa Mkwakwani mkoani hapa ambapo litapambwa na
wasanii nguli wa muziki wa dansi hapa nchini na bongo fleva ili kuweza kuwapa
burudani wakazi wa mkoa huu ambao watajitokeza kushuhudia kinyang’anyiro hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa, Mkurugezi wa Kampuni ya DATK Intertaimeint, Asha Kigundula, alisema kuwa warembo hao tayari wameanza mazoezi kwenye Ukumbi wa Lavida uliopo jijini Tanga ambapo wameweza kuwateka wadau wa tasnia hiyo ambao wamekuwa wakijitokeza kila siku kushuhudia mazoezi hayo.
“Ninachoweza kusema shindano la mwaka huu litakuwa la aina yake kutokana na kusheheni warembo bomba wenye mvuto na hivyo kuonyesha kutakuwa na mchuano mkali miongoni mwao “Alisema Kigundula
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa, Mkurugezi wa Kampuni ya DATK Intertaimeint, Asha Kigundula, alisema kuwa warembo hao tayari wameanza mazoezi kwenye Ukumbi wa Lavida uliopo jijini Tanga ambapo wameweza kuwateka wadau wa tasnia hiyo ambao wamekuwa wakijitokeza kila siku kushuhudia mazoezi hayo.
“Ninachoweza kusema shindano la mwaka huu litakuwa la aina yake kutokana na kusheheni warembo bomba wenye mvuto na hivyo kuonyesha kutakuwa na mchuano mkali miongoni mwao “Alisema Kigundula
Shindano hilo litaanza saa 2,
usiku na kueleza kuwa maandalizi ya shindano hilo yanaendelea vizuri na jumla
ya warembo 14 watashindania taji hilo. Kigundula alisema kuwa mpaka juzi
warembo 10 wamejitokeza na kuanza mazoezi yanayosimamiwa na warembo hao ni Miss
Tanga 2012 Teresia Kimolo na Mariam Bandawe.
Warembo hao ni Hawa Ramadhan (18),Hazina Mbaga (19)Like Abdulraman (19), Jack Emannuel (18),Waida Mmbwambo(20), Tatu Hussein(19), Mwanahamis Mashaka(20), Neema Abdallah (18), Winfrida Gutram (21)Lulu Mbonea (19) na Aisha Rashid (21).
"Kila kitu kinaendelea vizuri, ikiwa na warembo kuendelea kujiandikisha kushiriki shindano la mwaka huu, ambalo nina hakika litakuwa la aina yake"alisema Kigundula
Alisema kwamba shindano la mwaka huu litaandika historia mpya ya urembo mkoani humo kwa kuwa Kampuni DATK imejipanga, hivyo mashabiki wa mashindano ya urembo wa jijini hapo kwa ujumla wakae mkao wa kupata raha.
Redd's, Miss Tanga, imedhaminiwa na CXC Africa,Executive Solutions,Busta General Supply, Mkwabi Interprises,Lusindic Investment LTD, Lavida Pub,Jambo Leo,Staa Spoti,Five Brothers Cloud's Media Group, pamoja na Blog Michuzi Media Group,Bongostaz.com, Saluti5,Kajuna, JaneJohn, na Kidevu na Assengaoscar.blogspot.com.
Mwisho.
Warembo hao ni Hawa Ramadhan (18),Hazina Mbaga (19)Like Abdulraman (19), Jack Emannuel (18),Waida Mmbwambo(20), Tatu Hussein(19), Mwanahamis Mashaka(20), Neema Abdallah (18), Winfrida Gutram (21)Lulu Mbonea (19) na Aisha Rashid (21).
"Kila kitu kinaendelea vizuri, ikiwa na warembo kuendelea kujiandikisha kushiriki shindano la mwaka huu, ambalo nina hakika litakuwa la aina yake"alisema Kigundula
Alisema kwamba shindano la mwaka huu litaandika historia mpya ya urembo mkoani humo kwa kuwa Kampuni DATK imejipanga, hivyo mashabiki wa mashindano ya urembo wa jijini hapo kwa ujumla wakae mkao wa kupata raha.
Redd's, Miss Tanga, imedhaminiwa na CXC Africa,Executive Solutions,Busta General Supply, Mkwabi Interprises,Lusindic Investment LTD, Lavida Pub,Jambo Leo,Staa Spoti,Five Brothers Cloud's Media Group, pamoja na Blog Michuzi Media Group,Bongostaz.com, Saluti5,Kajuna, JaneJohn, na Kidevu na Assengaoscar.blogspot.com.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)