WAZIRI MKUCHIKA AELEZA SABABU ZA TANZANIA
Add caption |
WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais anayeshuhulikia Utawala Bora, Kaptein mstaafu, George Mkuchika amesema migogoro ya ardhi, mauaji ya maalbino na vikongwe, wanachi kujichukulia sheria mikononi, rushwa pamoja na ujangili zinadaiwa kuwa moja ya sababu zinazochangia kuporomoka kwa Tanzania katika viwango vya utawala bora duniani.
Mkuchika aliyasema hayo alipokuwa akizungumza katika
kikao cha 30 cha kamati ya ushauri wa mkoa wa Kilimanjaro (RCC) kikao
ambacho ni cha kwanza kwa mwaka 2014 na maalum kwa ajili ya kujadili
vipauumbele vya Bajeti ya Mkoa huo kwa mwaka 2014/2015.
Kaptein Mkuchika alisema kutokana na taarifa zilizotolewa hivi karibuni, Tanzania inashika nafasi ya pili kwa utawala bora nyuma ya Rwanda kwa nchi za ukanda wa Afrika mashariki nyuma ya Rwanda, 17 katika ukanda wa Afrika na 102 kati ya nchi 176 duniani ambapo kwa mujibu wa taarifa hizo Tanzania imeshuka kiwango katika ukanda wa Afrika katika kipindi cha miaka miwili.
Alisema katika taarifa hizo, Tanzania ilikuwa ikishika nafasi ya 10 miaka miwili iliyopita na kuongeza kuwa kuporomoka huko kunatokana na kukithiri kwa ukiukwaji wa haki za binadamu, mauaji ya albino na vikongwe, mapigano ya wakulima na wafugaji, Ujangili, ambapo zaidi ya watu kumi walikufa mkoani Manyara.
Kaptein Mkuchika alisema kutokana na taarifa zilizotolewa hivi karibuni, Tanzania inashika nafasi ya pili kwa utawala bora nyuma ya Rwanda kwa nchi za ukanda wa Afrika mashariki nyuma ya Rwanda, 17 katika ukanda wa Afrika na 102 kati ya nchi 176 duniani ambapo kwa mujibu wa taarifa hizo Tanzania imeshuka kiwango katika ukanda wa Afrika katika kipindi cha miaka miwili.
Alisema katika taarifa hizo, Tanzania ilikuwa ikishika nafasi ya 10 miaka miwili iliyopita na kuongeza kuwa kuporomoka huko kunatokana na kukithiri kwa ukiukwaji wa haki za binadamu, mauaji ya albino na vikongwe, mapigano ya wakulima na wafugaji, Ujangili, ambapo zaidi ya watu kumi walikufa mkoani Manyara.