March 13, 2014

ASKARI MWENYE BIDII HATIMAYE AMEJISHINDIA MILLION MBILI

 Kwa wale wapitao Mwai Kibaki Road zamani Old Bagamoyo Road watakuwa wanamjua Askari huyu ambaye amekuwa akijituma vilivyo pale darajani Mlalakuwa, Kawe. Askari huyu alikuwa akimbii mvua, yuko mapema asubuhi, yuko usiku na achoki, labda tu kama ana weakness zake mchana kama vile kwenda kuganga njaa sehemu nyingine kama ilivyo desturi ya askari wengine wa usalama barabarani.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova(wa tatu toka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Askari wa usalama barabarani, Moses Alphage (wa pili kushoto) aliyeibu ka kidedea kwenye program ya kuhamasisha na kupongeza utendaji kazi wa askari wa usalam barabarani jijini Dar es salaam iliyonedeshwa na kituo hicho cha Redio na kujishindia Sh 2 Milioni. Wa kwanza kushoto ni Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania Albert Maneno na kulia ni mtangazaji wa Clouds Said Mohamed maarufu Bonge.
 Mfanyakazi wa Idara ya Masoko wa Kampuni ya Vodacom Albert Maneno (wa tatu kushoto) akiongea kabla ya kukabidhi Sh. 2 milioni kwa askari wa kikosi cha Usalama Barabarani Moses Alphage (wa kwanza kushoto) aliyeibuka kidedea katika program ya kuibua hamasa ya kazi kwa askari hao jijini Dar es Salaam iliyoendeshwa na kituo cha Redio Clouds FM. Fedha hizo zimetolewa na wafanyakazi wa Vodacom pamoja na wananchi mbalimbali walioguswa na programu hiyo. Wa kwanza kulia ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Suleiman Kova.
March 13, 2014

Kura 487 zampa Sitta Uenyekiti Bunge Maalum la Katiba

1122 
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Bw. Edward Lowasa na Anna Tibaijuka wakimpongeza Mwenyekiti Mpya wa Bunge maalum la Katiba Bw. Samwel Sitta Mara baada ya Kutangazwa Kuwa Mshindi wa Nafasi hiyo kwa Idadi ya Kura 487 dhidi ya Hashim Rungwe aliyepata kura 69 na kura zilizoharibika  ni 7 DSC04961 
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba na aliyekuwa Mgombe katika nafasi ya Uenyekiti Bw. Hashim Rungwe akinadi Sera zake kwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kabla ya zoezi la Upigaji kura kwa nafasi hiyo jana Mjini Dodoma.
March 13, 2014

MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA AFYA NA MAZINGRA WAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAA MACHI 12,2014

????????  
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Enjinia Bashir Mrindoko (katikati), akikata utepe kuzindua rasmi Uzinduzi wa maji safi na salama Afya na Mazingra (wakwanza kushoto), Balozi wa Ubelgiji Nchini Tanzania Koenraad Adam, na anaefuatia mwenye shati la bluu Mwakilishi wa Jumuia ya Umoja wa Ulaya (EU), Eric Beaume (wakwanza kulia), Mkurugenzi Mkuu Wizara ya Maendeleo Ubelgiji, Peter Moors.
March 13, 2014

CTI WATEMBELEA KIWANDA CHA BIA CHA TBL DAR

 Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Bw. Steve Kilindo (wa tatu kushoto), akiwaelekeza jambo wadau kutoka  Shirikisho la wenye viwanda Tanzania (CTI), waliofanya ziara maalumu kiwandani hapo juzi, kuangalia jinsi kampuni hiyo ilivyofanikiwa na kuzalisha na kulinda mazingira (wa nne kushoto) ni Mkurugenzi wa Sera na Ushawishi, Bw. Hussein Kamote mkuu wa msafara na Meneja Uendelezaji Biashara, Bw Hassan Chamshama (wa sita). (Na Mpigapicha Wetu)
Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bi. Doris Malulu (aliyesimama), akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Shirikisho la wenye viwanda Tanzania (CTI), Bi Lilian Manga, baada ya wadau kutoka shirikisho hilo kufanya ziara kiwandani hapo kuangalia jinsi TBL ilivyofanikiwa kuzalisha vinywaji bora bila kuharibu mazingira.
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Bw. Steve Kilindo (kulia), akizungumza na wadau kutoka  Shirikisho la wenye Viwanda Tanzania (CTI), waliofanya ziara maalumu juzi kiwandani hapo kuangalia jinsi kampuni hiyo ilivyofanikiwa kuzalisha vinywaji na kulinda mazingira. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Bi. Lilian Manga, Mkurugenzi wa Machapisho na Habari, Bw. Thomas Kimbunga, Bw. Jesper Friis na Meneja Uendelezaji Biashara, Bw Hassan Chamshama. (Na Mpigapicha Wetu)
 Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Bw. Steve Kilindo (kulia), akizungumza na wadau kutoka  Shirikisho la wenye Viwanda Tanzania (CTI), waliofanya ziara maalumu juzi kiwandani hapo kuangalia jinsi kampuni hiyo ilivyofanikiwa kuzalisha vinywaji na kulinda mazingira. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Bi. Lilian Manga, Mkurugenzi wa Machapisho na Habari, Bw. Thomas Kimbunga, Bw. Jesper Friis na Meneja Uendelezaji Biashara, Bw Hassan Chamshama. (Na Mpigapicha Wetu)
March 13, 2014

Samia Suluhu arudisha Fomu ya kuwania nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bunge Maalum la Katiba

Kina Mama wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wakimsindikiza Mjumbe wa Bunge Hilo na Mgombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Bi. Samia Suluhu Hassan(Aliyenyanyua fomu)kurudisha fomu kwa Katibu wa Bunge Mapema Leo asubuhi Mjini Dodoma.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Thomas Kashilila akitoa maelekezo kwa wapambe wa mgombea Nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba kabla ya kupokea Fomu hizo Mapema Leo asubuhi Mjini Dodoma.
March 13, 2014

SERIKALI YATOA UFAFANUZI KUHUSU VITAMBULISHO KWA WAANDISHI BUNGE MAALUM LA KATIBA

1 (6) 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kuhusu utoaji wa Vitambulisho vya Waandishi wa Habari kwenye shughuli za Bunge Maalum la Katiba.
2 (4) 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene akizungumza na wabahabari (hawapo pichani) kuhusu utoaji wa Vitambulisho vya Waandishi wa Habari kwenye shughuli za Bunge Maalum la Katiba.Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Vyombo vya Habari cha Idara hiyo, Vicent Tiganya.
Picha zote na Georgina Misama-MAELEZO
………………………………………………………………………………..
Na Frank Mvungi-MAELEZO
SERIKALI imetoa ufafanuzi juu ya vitambulisho vya waandishi wa habari ( Press card) wakati wa Bunge Maalum la katiba na kusema kuwa ndicho kigezo pekee kitakachowezesha  waandishi wa habari kutimiza majukumu yao vyema katika kipindi  chote cha bunge hilo.
March 13, 2014

TFDA YATEKETEZA VIPODOZI VISIVYOFAA VYENYE THAMANI YA SH. MILIONI 188

1 (5) 
Afisa Uhusiano wa Mamalaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudensia Simwanza akizungumza na wanahaabari (hawapo pichani) kuhusu vipodozi vilivyopigwa marufuku na mamlaka hiyo.Kulia ni Afisa Habari wa Idara ya Habari(MAELEZO) Frank Mvungi.
Picha na Husssein Makame-MAELEZO.
2 (3)  
Afisa Uhusiano wa Mamalaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudensia Simwanza, akionesha moja ya vipodozi vilivyopigwa marufuku na mamalaka hiyo kinachotumiwa na wanawake kukuza makalio.3 (3) Baadhi ya vipodozi vilivyopigwa marufuku na Mamalaka ya Chakula na Dawa (TFDA).4 (3) 
Baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Afisa Uhusiano wa Mamalaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudensia Simwanza (hawapo pichani).
Picha na Hussein Makame-MAELEZO.
Frank Mvungi-Maelezo
MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA) imeteketeza vipodozi visivyofaa kwa matumizi ya binadamu vyenye thamani ya takribani Shilingi Milioni 188 katika kipindi cha mwaka 2012/2013.
Hayo yamesemwa na Afisa Uhusiano wa mamlaka hiyo, Gaudensia Simwanza wakati akizunguza na wanahabari kwenye mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
March 13, 2014

RAIS KIKWETE APOKEA RIPOTI YA MGAWANYIKO WA WATU KWA UMRI NA JINSI LEO IKULU, DAR ES SALAAM

s1 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa ambaye pamoja na Kamishna wa Sensa Hajjat Amina Mrisho baada ya kupokea Ripoti ya Mgawanyo wa Watu kwa Umri na Jinsia kwa data za sensa ya watu na makazi mwaka 2012 leo Machi 13, 2014   Ikulu jijini Dar es salaam
March 13, 2014

WASIKIE `LIVE` SIMBA WAKIZUNGUMZIA TABIA YA TIMU ZA LIGI KUU KUKAMIA MECHI NA KUHARIBU UBORA WA SOKA!!

loga maelezo 
Kocha wa Simba SC, Mcroatia, Dravko Logarusic akitoa maelekezo kwavijana wake
Na Baraka Mpenja wa Fullshangwe, Dar es salaam
0712461976 au 0764302956
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamelaumu timu zinazoingia kwa kukamia wapinzani wao katika mitanange ya lala salama ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014.
Akizungumza na mtandao huu, afisa habari wa Simba Asha Muhaji amesema hali ya kukamiana uwanjani inaharibu ubora wa mpira katika mechi mbalimbali.
“Kuna wakati unaweza kushangaa, mchezaji fulani akawa na kazi ya kumkaba kwa nguvu mshambuliaji wenu. Mfano Amissi Tambwe kwa Simba, badala ya kucheza mpira kwa ufanisi, yeye anacheza kimabavu na kumjeruhi mwenzake. Sasa mpira kama huu hauna maana”. Alisema Asha.