TANGA UWASA YATUMIA MILIONI 20 KUKARABATI MTANDAO WA MAJI TAKA USAGARA

September 04, 2023

 

Meneja wa Mazingira wa Tanga Uwasa Nasibu Ramadhani akikagua mtandao wa maji taka katika eneo la Usagara Jijini Tanga ambao wameufanyia ukarabati mkubwa
Meneja wa Mazingira Tanga Uwasa Nasibu Ramadhani akikagua mtandao wa maji taka katika eneo la Usagara Jijini Tanga ambao wameufanyia ukarabati mkubwa
Muonekano wa chemba zilizokarabatiwa
Muonekano wa chemba zilizokarabatiwa


Na Oscar Assenga, TANGA

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (Tanga Uwasa) imetumia milioni 20 kwa ajili ya kuukarabati mtandao wa maji taka wa zamani katika eneo la Usagara maarufu kama Bandari Chafu.

Akizungumza Meneja wa Mazingira wa Tanga Uwasa Nasibu Ramadhani alisema uamuzi wa kuukarabati mtandao huo wa maji taka waliufanya baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wakazi wa wa eneo hilo tokea 2018.



Alisema malalamiko hayo yalikuwa yanahusiana na miuondombiu ya maji taka eneo hilo kuwa chakavu na hivyo kuhatarisha afya zao na hivyo kuomba mtandao huo uliojengwa na TPA miaka ya nyuma na hivyo baada ya kubinafishwa nyumba hizo.



Alisema hivyo wanawaomba Tanga Uwasa iwarebishie mfumo huo ambapo awali ulikuwa baada ya kuona changamoto hizo waliamua watenge fedha Milioni 20 kwa ajili ya kuukarabati mtandao huo.



Alisema katika ukarabati wa mtandao huo ulihusisha ukarabati wa chemba kubwa ambazo zinapokea maji taka kutoka kwenye maeneo hayo na ukarabati wa chemba ndogo ndogo ambazo zinaunganisha bomba na bomba na maeneo yenye bomba chakavu .



“Hayo ndio maeneo tuliyoyakarabati na tunatarajia kukarabati na mwaka huu tutakamilisha mpango huo wa ukarabati kukamilisha mfumo hiyo ili kuuwezesha kuishi muda mrefu hiyo itasaidia kuondokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokeza”Alisema



Hata hivyo alitoa wito kwa wakazi wa eneo hilo kuhakikisha miundombinu ya maji taka kuhakikisha hawaweki taka ngumu na wanaitunza ili iweze kukaa muda mrefu


PANGANI KUJA NA MKAKATI WA UFUMBUZI WA KUONGEZA KIWANGO CHA UFAULU WA WANAFUNZI

September 04, 2023

Mkazi wa Kijiji cha Kwakibuyu Ramadhan Mohammed akiwasilisha mada katika mafunzo ya kuwajengea ujuzi wa uhamasishaji jamii katika utetezi wa utatuzi wa changamoto za kielimu kwenye vijiji vya Mkaramo,Ubangaa,Mkwajuni,Kwakibuyu,Kipumbwi na Stahabu.mafunzo hayo yaliendeshwa na asasi ya Tree of Hope chini ya ufadhili wa Foundation for Civil Society (FCS)



Pangani Kujenga maelewano baina ya wazazi,wananchi,walimu ,viongozi na wanafunzi  imeelezwa kuwa ndiyo ufumbuzi wa kuongeza kiwango cha ufaulu wa  mitihani ya kitaifa kwa wanafunzi Wilayani Pangani.

Wajumbe wa kamati ya kuhamasisha uwajibikaji jamii na mamlaka zinazohusika kuboresha elimu katika vijiji vya Kipumbwi, Mkalamo,Ubangaa na Stahabu walisema hayo walipokuwa wakizungumza

Wajumbe hao ambao walikuwa wakizungumza baada ya  mafunzo elekezi ya utekelezaji wa mradi wa kujamasisha jamii na mamlaka zinazohusika kuboresha elimu katika jamii unaosimamiwa na asasi isiyo ya kiserikali  ya Tree Of Hope chini ya ufadhili wa Shirika la Foundation For Civil Society (FCS) walisema wanakwenda kutumia kila mbinu sahihi kuhakikisha maelewano yanajengeka kwa sababu wamebaini ndiyo kiini cha mafanikio.


Ali Ibrahim wa Kijiji cha Kwakibuyu ambacho wanafunzi wake wanasoma shule ya msingi Kipumbwi Wilayani hapa alisema badala ya kutupiana lawama ufaulu utapatikana kwa Kujenga maelewano na kuwa kitu kimoja katika kutekeleza majukumu.


"Ipo changamoto ya utoro,uhaba wa walimu na baadhi ya shule kukosa maji..kila changamoto ina njia zake wazazi wakichangia vyema vyakula wanafunzi watavutika na hawatatoroka,lakini uhaba wa walimu wazazi wakichangia kuwalipa posho walimu wastaafu ufaulu utaongezeka" alisema Ali.


Mratibu wa mradi huo kutoka Tree of Hope,Goodluck Malilo alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwapa mbinu wajumbe wa kamati hizo za utatizi wa changamoto za kielimu kwenye maeneo ya vijiji hivyo ili kuboresha elimu na kuinua kiwango cha ufaulu.


"Changamoto za kielimu katika vijiji vingi zunajulikana na kila mwananchi,

 mamlaka na walimu na uwepo wake siyo kwa sababu wenye mamlaka wameshindwa kuzitatua bali zimekosa utetezi na hili ndilo jukumu la wanakamati" alisema Malilo.


Mkuu wa Wilaya ya Pangani, Zainab Abdallah  alisema kamati hizo zinasaidia kuwezesha kila mmoja kuona uchungu na maendeleo ya elimu na kutimiza wajibu wake.