Wasanii 400 wa Afrika kutikisa tamasha la Sauti za Busara 2017 Zanzibar

January 25, 2017
Mkurugenzi wa tamasha la Sauti za Busara Bw.Yusuf Mahmoud akionesho moja ya kitabu chenye mambo lukuki yahuso tamasha hilo pamoja la habari mbalimbali za wasanii watakaotumbuiza kwenye tamasha hilo la aina yake kwa wakazi wa Zanzibar na wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali za nchi na nje.

Mwanamuziki mkongwe mwenye makazi yake ya kimuziki nchini Japan Fresh Jumbe akizungumza na waandishi wa habari mapema kuhusu ushirika wake pamoja na bendi yake nzima katika tamasha la sauti za busara.

Mwenyekiti wa Tamasha la  Sauti za Busara Bw. Simai M. Said wa pili kutoka kushoto akiwa anaongea na waandishi wa habari juu ya Tamasha la 14 la sauti za busara.

Mkurugenzi wa Tamasha la 14 la Sauti za Busara, Bw. Yusuf Mahmoud (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam huku akitaja baadhi ya wanamuziki ambao watatumbuiza 'Live' katika Tamasha hilo. 

JUMLA ya wasanii 400 wa Ki-Afrika toka takribani makundi 40 wanatarajia kutumbuiza katika Tamasha la Sauti za Busara 2017. Tamasha hilo litakaloanza kufanyika tarehe 9-12 ya mwezi Februari 2017 litafanyika Mji Mkongwe, Zanzibar.

Akizungumza Mkurugenzi wa Tamasha la Sauti za Busara, Bw. Yusuf Mahmoud alisema Tamasha litakutanisha wanamuziki kutoka sehemu mbali mbali ambapo wanamuziki wa Tanzania watashirikiana na wa Morrocco, kutakua na mwanya wa kufahamiana zaidi kupitia vikao vya Movers and Shakers, na hafla itakayofanyika usiku wa wapendanao baada ya tamasha.

Muziki unalateta watu pamoja kutoka sehemu mbalimbali. Duniani na ujumbe mkubwa kwa Dunia ni kuwa muziki unakuza umoja na urafiki hata kwenye mipaka ya sehemu mbalimbali. Alisema Tamasha la 14 la Sauti za Busara kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa tamasha hilo, lenye kauli mbiu ya ‘AfricaUnited’ mwaka huu tamasha litakua na majukwaa matatu yatakayotumiwa na wasanii wote kimataifa/nyumbani.

Watu mbali mbali wenye rangi tofauti, umri tofauti kwa mara nyingine tena wataunganishwa na tamasha kusheherekea muziki wa ki-Afrika. Matarajio ya mahudhurio ni makubwa kutoka Tanzania na nje ya Nchi kufatia kujaa kwa sehemu za malazi Mji Mkongwe kwa wiki ya tamasha. Wasanii wote watatumbuiza ‘live’ muziki wa Ki-Afrika kila siku kuanzia saa 10:30 jioni mpaka saa 7:00 usiku.

Lengo la tamasha ni kuhakikisha kila mmoja anamudu kiingilio hivyo kwa watanzania ni Sh 6,000 kwa siku na Sh20,000 kwa siku nne za tamasha. Tamasha hili ambalo kwa asilimia 100 huwa live kitu ambacho kinalifanya tamasha hili liwe la kipekee huwapakipaumbele wanamuziki chipukizi kutambulisha kazi zao zenye kutambulisha uhalisia wa utamaduni.

 Tamasha la Sauti za Busara hukutanisha wataalamu wa muziki wa kimataifa na kutoa nafasi kw amuziki wa Afrika Mashariki kufwakifikia watu mbalimbali dunia nzima kupitia jukwaa la Sauti za wanamuziki wa nyumbani amabao hutumbuiza tamashani hupata mialiko kushiriki matamasha mbali mbali Barani Ulaya na Afrika. 

"...Ndani ya siku hizo nne jumla ya wasanii 400 wa ki-Afrika (makundi 40) yatatumbuiza tamasha Sauti za Busara 2017. Tamasha litaanza na gwaride kutoka maeneo ya Kisonge (karibu na Michenzani) kuanzia saa 9:00 jioni Alhamis tarehe 9/2. Tamasha litakutanisha wanamuziki kutoka sehemu mbali mbali ambapo wanamuziki wa Tanzania watashirikiana na wa Morrocco, kutakua na mwanya wa kufahamiana zaidi kupitia vikao vya Movers and Shakers, na hafla itakayofanyika usiku wa wapendanao baada ya tamasha. Muziki unalateta watu pamoja kutoka sehemu mbalimbali. Duniani na ujumbe mkubwa kwa Dunia ni kuwa muziki unakuza umoja na urafiki hata kwenye mipaka ya sehemu mbalimbali," alisema Mkurugenzi wa Tamasha la Sauti za Busara, Bw.Yusuf Mahmoud.

 Kati ya makundi 40 nusu yanatoka Tanzania. Makundi hayo ni Afrijam Band, CAC Fusion, Chibite Zawose Family, Cocodo African Music Band, Jagwa Music, Matona's G Clef Band, Mswanu Gogo Vibes, Rajab Suleiman & Kithara, Tausi Women's Taarab, Usambara Sanaa Group, Wahapahapa Band, Ze Spirits Band.

Tuna hakika makundi kama haya yatawakilisha vema matamasha ya nje endapo yatapata nafasi, Makundi mengine ni pamoja na Batimbo Percussion Magique (Burundi), Bob Maghrib (Morocco), Buganda Music Ensemble (Uganda), Grace Barbe (Seychelles), H_art the Band (Kenya), Imena Cultural Troupe (Rwanda), Isau Meneses (Mozambique), Karyna Gomes (Guine Bissau), Kyekyeku (Ghana), Loryzine (Reunion), Madalitso Band (Malawi), Pat Thomas & Kwashibu Area Band (Ghana), Rocky Dawuni (Ghana), Roland Tchakounté (Cameroon), Sahra Halgan Trio (Somaliland), Sami Dan and Zewd Band (Ethiopia), Sarabi (Kenya), Simba & Milton Gulli (Mozambique).

 Shukrani zetu za dhati na za kipekee tunazifikisha kwa Hotel ya Golden Tulip kwa kuhakikisha kikao hiki kinafanikiwa. Pia tunawashukuru ninyi wote mliohundhuria kikao hiki na kuhakikisha mnafikisha taarifa zetu kwa wananchi. Wadhamini wa tamasha hili ni pamoja na Africalia, Chuchu FM Radio, Zanlink and Coastal Aviation Embassy of Germany, Ethiopian Airlines, Ikala Zanzibar Stone Town Lodge, Memories of Zanzibar, Mozeti, Music In Africa, Norwegian Embassy, Pro Helvetia, Swiss Agency for Development & Cooperation (SDC), Tifu TV, na wengine wengi.

 Kwa mawasiliano zaidi tembelea tovuti yetu www.busaramusic.org. -- ___________________________________________________________________________________ Joachim Mushi, Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mhariri Mkuu wa Thehabari.com. Mail address:- mushi@thehabari.com/ jomushi79@yahoo.com/ info@thehabari.com Mobile:- 0717 030066 / 0756 469470 Web:- www.thehabari.com http://joemushi.blogspot.com

WAKUU WA WILAYA WATEMBELEA SHAMBA LA JARIBIO LA MAHINDI LA KITUO CHA MAKUTUPORA MKOANI DODOMA

January 25, 2017
 Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine (kushoto), akizungumza na wakuu wa wilaya za Dodoma na maofisa watendaji na wenyeviti wa serikali za mitaa na wadau wa kilimo  alipotembelea shamba la Jaribio la Mahindi yaliyoboreshwa kwa kutumia Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) chini ya Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (WEMA) katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha  Makutupora mkoani Dodoma leo.
 Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Dodoma wakiwa kwenye mkutano na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine (hayupo pichani), walipotembelea Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Makutupora mkoani Dodoma leo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deogratius Ndejembi, Bahi, Elizabeth Kitundu, Mpwapwa Jabir Shekimweri na Mshauri wa Kilimo Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Aziza Mumba.
 Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, Hussein Mansour akizungumza (kushoto), akiwaelekeza jambo Wakuu wa Wilaya wa Mkoa wa Dodoma walipotembelea shamba la Jaribio la Mahindi yaliyoboreshwa kwa kutumia Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) chini ya Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (WEMA) katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha  Makutupora mkoani Dodoma leo. Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Elizabeth Kitundu, Kongwa, Deogratius Ndejembi, Mpwapwa, Jabir Shekimweri na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine Kamuzora.

 Wanahabari, watafiti wa kilimo, wenyeviti wa serikali za mitaa na watendaji wakiwa kwenye mkutano kabla ya kutembea shamba hilo la jaribio la mahindi.
  Wanahabari, watafiti wa kilimo, wenyeviti wa serikali za mitaa na watendaji wakiwa nje ya lango kuu la kuingia katika shamba hilo wakisubiri kupewa taratibu za kuingia.
 Mshauri wa Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (Wema), Dk.Alois Kullaya (kulia), akitoa maelezo kabla ya kuingia kwenye shamba hilo la jaribio la mahindi.
Mtafiti wa Kituo hicho,Ismail Ngolinda (kulia), akitoa maelekezo kuhusu shamba hilo.
Mshauri wa Jukwaa la Bioteknolojia Tanzania (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange (kushoto), akizungumza na viongozi mbalimbali baada ya kutembelea shamba hilo. Kutoka kulia ni  Mshauri wa Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (Wema), Dk.Alois Kullaya, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine, Kaimu Mkurugenzi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira, Richard Muyungi, Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, Hussein Mansour na Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Kilimo Kanda ya Kati Dodoma, Dk. Leon Mroso.

 Mshauri wa Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (Wema), Dk.Alois Kullaya, akielekeza kuhusu mahindi hayo ya jaribio hilo.
Picha ya Pamoja.


Na Dotto Mwaibale, Dodoma

KATIBU Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine Kamuzora amesema utafiti wa kilimo ni muhimu ili kuongeza chakula nchini.

Kamuzora alitoa kauli hiyo alipotembelea shamba la Jaribio la Mahindi yaliyoboreshwa kwa kutumia Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) chini ya Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (WEMA) katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha  Makutupora mkoani Dodoma leo.

Alisema bila ya kuwepo kwa utafiti wa kilimo hatuwezi kufikia ufanisi wa kupata chakula kingi hivyo matokeo mazuri ya utafiti ni muhimu kwa maendeleo ya kilimo.

Alisema majaribio ya kisayansi ni muhimu na ni mkombozi kwa mkulima hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya tabia nchi na ukame.

Katika hatua nyingine Kamuzora aliwataka wakuu wa wilaya na watendaji na wenyeviti wa serikali za mitaa wa mkoa wa Dodoma waliotembelea shamba hilo kuwa mabalozi kwa wananchi wao kwa kile walichokiona kwenye shamba hilo la majaribio. 

Aliomba kuwepo na subira wakati utafiti huo ukiendelea na kusubiri kuthibitishwa na vyombo vyenye dhamana na kama wataona unafaa basi utatumika.

" Utafiti haufanywi kwa siku moja na kuanza kutumika una mlolongo mrefu ili kutoa nafasi kwa vyombo husika kuona kama upo salama na kuruhusu kutumika" alisema Kamuzora
Alisema vyombo vyenye dhamana vikiridhika vitatoa kibali cha kuanza utumiaji wa teknolojia hii mpya licha ya nchi nyingine za wenzetu kuanza kuitumia,” alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deogratius Ndejembi alisema ni muhimu sasa kuharakisha matumizi ya teknolojia hiyo badala ya kupoteza muda mwingi ukizingatia kuwa hivi sasa nchi inakabiliwa na ukame hasa katika wilaya yake.

"Kazi inayofanywa na watafiti wetu ni nzuri ila nawashauri wafanye utafiti utakaosaidia katika kipindi hiki cha  mabadiliko ya tabia nchi yaliyopo maeneo mbalimbali.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwawa Jabir Shekimweri alisema utafiti huo umeonesha mafanikio makubwa hasa pale unapoyaangalia mahindi yaliyotumia mbegu iliyotokana na teknolojia hiyo kuwa ni bora na makubwa wakati yale yaliyotumia mbegu za kienyeji kuwa dhaifu.

"Nisema kuwa mbegu za utafiti huu zitakapoanza kutumika zitasaidia sana wakulima hasa wa wilaya yangu ambayo inakabiliwa na ukame katika baadhi ya maeneo" alisema Shekimweri.

Recycling of waste, discovering of gas should foster progress in Tanzania

January 25, 2017
 United Nations Environment Programme, Executive Director, Erik Solheim (right) speaks to reporters at the news conference held in Dar es Salaam on his official visit to Tanzania on Global environmental agenda, on his right, UN Resident Coordinator, Alvaro Rodriguez.
United Nations Environment Programme (UNEP), National Coordination Officer, Ms Clara Makenya (right) when she stressed a point to reporters during the press conference held in Dar es Salaam on the official visit to UN Environment Head Erik Solheim to Tanzania. Second left is UNEP, Executive Director, Erik Solheim, far left, UN Resident Coordinator, Alvaro Rodriguez. 

TANZANIA should adapt recycling waste policy, increasing uses of gas instead of charcoal for cooking as a long term solution on ensuring sustainable environmental protection to tape the pressing challenge of climate change.
Speaking to reporters in Dar es Salaam on his first visit to the country, UN Environment Programme (UNEP), Executive Director, Erik Solheim said that UNEP is the leading global environment authority that sets the global environment agenda.

“The discovering of gas reserved in Tanzania should be use as stepping stone to employment, business opportunity and as a tool to alleviate poverty,” he noted.

He commended that the efforts taken by the government through local municipalities for setting an area in the outskirt of city center Pugu Dampo as a permanently place for cabbage without destructing the environment of the Dar es Salaam city.

Solheim added that the UN environment works with a wide range of partners, including United Nations entities, international organizations, national governments, non-governmental organizations, the private sector and civil society.

He added hope that “other leaders will be inspired to pick up the baton and ensure that Africa’s rich natural resources can be conserved, and thus serve as the foundation for a sustainable future and food security for all on the continent.”
He said that the government should also adding some efforts in banning the uses of plastics bags as the magnitude of it increases the environmental degradation that pose a huge threat to the country’s social and economic development.

“We also hailed efforts taken by the high commissioners here in Tanzania such as China and former two former Presidents Hon. Mwinyi and Hon. Mkapa for participating in the recently anti-poaching marching,” he stressed.

 On her part, UNEP, National Coordination Officer, Ms Clara Makenya said that the visit of the UNEP boss emphasized much on the reduction of uses of charcoal for cooking as the cultural fuel the cutting of trees across the country.
“We had an opportunity to meet civil society, NGOs and academicians on the pressing issues of climate change and food security as a scorching agenda in many years to come,” she added.

UNEP, boss has been following with keen interest and commends the efforts by the President of the United Republic of Tanzania, Dr John Magufuli in the fight of corruption and bring about to an end of poaching and the illegal wildlife trade.
UN environment views the shift to Dodoma as an opportunity to bring about positive change and development not just to the central part of Tanzania, but also the whole country. The sustainability of this anticipated growth can be reinforced with the integration of environmental consideration.

In cooperation with partners, UNEP supports cities across the world in addressing environment impacts and integrating the environment into the long term strategic planning. It has been the case with the programs that UN environment has had in the country, such as the poverty and environment initiative
Africa Environment Day, marked annually on 3 March, focuses on last year on ‘Combating Desertification in Africa: Enhancing Agriculture and Food Security.’
The continent has lost 65 per cent of its agricultural land since 1950 due to land degradation, according to figures cited by UNEP. Up to 12 per cent of its agricultural gross domestic product (GDP) is lost due to deteriorating conditions and 135 million people are at risk of having to move from their land by 2020 due to desertification.
Geofrey Adroph BLOGGER P.O.BOX 24793, Mob: +255 755 274953 /+255 713 363965, Email: pamojapure@gmail.com. Blog: http://www.pamoja.co.tz/ DAR ES SALAAM, TANZANIA

Wateja Tigo Pesa kupata 5.82bn/-gawio la 11 la faida la robo mwaka

January 25, 2017


Mkuu wa Kitengo cha fedha cha Fedha TigoPesa Christopher Kimaro (kushoto) akiongea na waandishi wa habari(hawapo picha) wakati wa kutangaza gawio kwa wateja wa Tigo Pesa jijini Dar Es Salaam jana. Kulia ni Mkuu wa Huduma za Fedha kwa Simu, Ruan Swanepoel .


Mkuu wa Huduma za Fedha kwa Simu, Ruan Swanepoel akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari katika mkutano wa waandishi wa habari 

Dar es Salaam, Januari 23, 2017 - Kampuni inayoongoza kwa maisha ya kidijitali Tigo Tanzania imetangaza gawio jingine la malipo ya faida ya robo mwaka la shilingi bilioni 5.82 ambalo kampuni inagawa  kwa wateja  wote wanaotumia huduma ya pesa kwa kupitia simu. Gawio hilo ni kipindi cha robo ya nne ya mwaka  uliyoishia Desemba 31 2016.
Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkuu wa Huduma za Fedha kwa Simu, Ruan Swanepoel alisema  kampuni hiyo kwa ujumla  imeshawalipa wateja wake wanaotumia huduma za fedha kwa njia ya simu  jumla ya shilingi bilioni 58.10 sawa na dola za Marekani milioni 26.3 kama malipo ya robo mwaka tangu kuanzishwa malipo hayo ya riba na Tigo Julai 2014.
Swanepoel alisema kuwa katika robo ya kwanza ya mwaka riba iliyotolewa kama gawio ilipanda  hadi asilimia 11 ikiwa ni matokeo mazuri ya viwango vilivyopokelewa katika mfuko wa fedha  uliowekwa katika benki mbalimbali za biashara nchini Tanzania.
“Riba hii ni malipo kwa wateja binafsi, mawakala wa reja reja, mawakala wakubwa na wabia wengine wa kibiashara wa Tigo ambao kila mmoja anapokea malipo kulingana na thamani ya fedha zilizohofadhiwa katika pochi ya kielektroniki ya Tigo Pesa,” Swanepoel alifafanua.
Swanepoel aliongeza, “Tunayo furaha sana kuwatangazia  ongezeko hili la gawio la riba kwa mara ya 11 mfululizo,  hali inayoleta nafuu kwa mamilioni ya watumiaji wa Tigo Pesa kwa kuwasaidia kukabiliana na majukumu mbalimbali ya kifedha. Hii inaonesha jinsi tulivyojikita katika  kutoa huduma ya fedha inayowafikia wateja wetu na nchi kwa ujumla  kupitia huduma yetu ya Tigo Pesa.”
  
Alibainisha kuongezeka kwa faida kuwa ni kutokana na kuboreshwa kwa mazingira ya soko na kasi ya kuongezeka kwa idadi ya watumiaji wa Tigo Pesa kama kichocheo kikubwa katika ongezeko kubwa la gawio la riba hususani kwa upande wa wafanya biashara. Tigo Pesa hivi sasa ina mtandao mkubwa wa wafanya biashara zaidi ya 55,000 wanaowezesha malipo ya miamala  nchini kote.
Kama ilivyokuwa awali kwa mujibu wa Swanepoel malipo kwa wateja  yanakokotolewa kwa kuzingatia wastani wa salio la kila siku  linalokuwa katika pochi ya kielektroniki ya simu na kwamba mgawanyo wa gawio hili la faida  ni kulingana na waraka wa Benki Kuu uliotolewa Februari 2014.

Tigo Pesa inakuwa ni huduma ya kwanza ya fedha kwa njia ya simu  duniani  ambayo mwaka 2014 iligawa gawio la hisa  lililozalishwa  kutoka katika akaunti ya dhamana ya pesa katika simu  katika mfumo wa gawio wa robo mwaka kwa wateja wake.

SBL yawapatia Watanzania milioni mbili maji ya uhakika, salama

January 25, 2017
 Mkurugenzi wa Mahusiano wa SBL, John Wanyancha akitoa ufafanuzi  kwa  waandishi wa habari kuhusu mradi wa maji ulioweza kuwafikia watanzania milioni 2 katika programu ya hisani ya kusaidia jamii inayoendeshwa na kampuni hiyo  inayolenga kuboresha maisha katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema jana  katika hoteli ya Morena Mkoani Dodoma.


Waandishi wa habari wa mkoani Dodoma wakichukua matukio wakati wa mkutano uliofanyika mapema jana katika hoteli ya Morena mkoani Dodoma.

Moja ya mradi wa maji uliodhamiwa na kampuni ya Serengeti Breweries Limited  uliozinduliwa mapema Novemba mwaka jana katika Kijiji cha Makanya wilayani Same katika  programu ya hisani ya kusaidia jamii inayoendeshwa na kampuni hiyo  inayolenga kuboresha maisha.




Dodoma, Januari 24, 2017- Kampuni ya Bia ya Serengeti imewapatia Watanzania zaidi ya  milioni mbili kote nchini maji safi na salama bure katika kipindi cha miaka sita iliyopita  kupitia programu ya hisani ya kusaidia jamii inayoendeshwa na kampuni hiyo  inayolenga kuboresha maisha.

 Kupitia programu yake inayofahamika kama Maji kwa Uhai, SBL imechimba visima vya kisasa 16 katika mikoa minane na kuwezesha jamii  katika maeneo hayo  kupata maji ya uhakika na salama.

Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari mjini Dodoma leo, Mkurugenzi wa Mahusiano wa SBL, John Wanyancha  alisema kwamba kampuni hiyo ya bia  imejikita katika kupunguza uhaba wa maji katika maeneo ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakitaabika kutokana na uhaba wa bidhaa hiyo.

 “SBL  ina sera iliyojikita katika ustawi wa jamii yetu ambapo Maji ya Maisha  ikiwa ni moja ya maeneo manne ya kipaumbele ambayo kampuni yetu  imeyafafanua katika malengo yake ya kutoa msaada kijamii kwa jamii inamofanya shughuli zake, alisema Wanyancha akifafanua  maeneo mengine ya kipaumbele kama Kutoa Stadi za Maisha, Mazingira Endelevu na Kuhamasisha Unywaji wa Kistaarabu.

Wanyancha aliongeza kwamba kwa kutoa huduma ya maji ya uhakika katika jamii, SBL imewawezesha watu kutumia muda mwingi zaidi katika uzalishaji  kuliko kusafiri umbali mrefu  kutafuta maji.

Aliongeza, “licha ya kuboresha afya za wakazi wa maeneo hayo, upatikanaji wa maji safi na salama ndani ya jamii  unahakikisha kuwa watoto hususani watoto wa kike  wanaosoma shule  wanapata muda  mzuri wa  kuhudhuria  shuleni kwa uhuru zaidi bila usumbufu”.

Mkurugenzi huyo wa Mahusiano  alieleza kwamba mpango wa Maji ya Maisha kwa mwaka 2017 ni  kuanzisha miradi zaidi katika maeneo ya Ngare Nairobi, wilayani Siha, Chang’ombe B wilayani Temeke (Dar es Salaam) na Karatu na Likamba katika mkoa wa Arusha ambapo miradi yote itawanufaisha  wakazi zaidi ya 300,000.