WAZIRI MPINA AWAKAANGA VIONGOZI WANAOHUJUMU WAFUGAJI, AMSIFU DC GODWIN GONDWE KUSIMAMIA KIKAMILIFU SEKTA YA MIFUGO

December 26, 2017
 WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina wa pili kulia akitazama mifugo ya ngombe aina ya Borani waliyopo kwenye ranchi ya mzeri wilayani Handeni mkoani Tanga wakati wa ziara yake wa kwanza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Handeni,Godwin Gondwe
  Mkuu wa wilaya ya Handeni,Godwin Gondwe kushoto akimuleza jambo  WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina kulia ambaye alifanya ziara ya kikazi wilayani humo
 WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akisisitiza jambo wakati akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kumaliza ziara yake kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Handeni,Godwin Gondwe
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina wa pili kutoka kushoto akiwa na Mkuu wa wilaya ya Handeni Godwin Gondwe wakati alipoitembelea ranchi ya mzeri wilayani humo
NA MWANDISHI MAALUM, HANDENI
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amechukizwa na tabia ya baadhi  watendaji wa Serikali katika Hifadhi za Misitu, Mapori ya Akiba na Serikali za Mitaa kukamata mifugo kiholela na kutoza faini zisizo na misingi ya kisheria huku akisifu utendaji kazi ya wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga, Godwin Gondwe katika usimamizi wenye weledi wa sheria za mifugo nchini.
Mpina ametoa kauli hiyo akiwa wilayani Handeni ambapo alitumia fursa hiyo kupiga marufuku ukamataji mifugo kiholela huku akimtaja Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Gondwe kama kielelezo cha kuwa kiongozi wa kwanza kitaifa anayezifahamu vizuri na kuzisimamia kikamilifu sheria za mifugo na kuleta tija katika ukuaji wa sekta hiyo ikiwemo kuanzisha kijiji cha wafugaji,kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi na utoaji huduma bora za mifugo wakati wote.
Akizungumzia tatizo hilo la ukamataji holela wa mifugo nchini, Waziri Mpina amesema kama sekta hiyo isingekuwa inazalisha mazao ya mifugo na Serikali kuamua kuagiza kutoka nje ya nchi basi ingezilazimu kutumia kiasi cha sh. Trilioni 17.8 huku kaya milioni 4.49 za  kilimo nchini zinajishughulisha na ufugaji mifugo aina mbalimbali.
“Watendaji wa Serikali waliofanya hujuma na dhuluma kwa wafugaji hawatabaki salama, tutawafuatilia na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria”alisema.
Amesema  Sheria ya misitu na. 14 ya mwaka 2002 kifungu cha 26 kinazuia mifugo kuingia kwenye hifadhi za misitu ya kitaifa au iliyo chini ya Mamlaka za Serikali za Mitaa ambapo pamoja na wafugaji kuvunja sheria hiyo bado wanahitaji kutendewa inavyostahili kwa mujibu wa sheria za nchi ili kuweka ulinganifu wa watanzania wote mbele ya sheria za nchi.
Waziri Mpina amebainisha kuwa kumekuwa na mazoea mbalimbali ya ukamataji holela wa mifugo yanayoendelea nchini ambayo yanatekelezwa bila kuzingatia sheria ya ustawi wa Wanyama (Animal welfare Act No.19 of 2008) na Kanuni zake za mwaka 2010 kifungu cha 7 na 8 na Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Na 17 ya mwaka 2003 (Animal Disease Act No.17 of 2003) hivyo mifugo imekuwa ikishikiliwa kama kidhibiti kwa muda mrefu na mingine kufa kutokana na magonjwa na ukosefu huduma ikiwemo matibabu,chanjo na kuogeshwa ili kuepuka magonjwa ndorobo na kupe.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe amesema wao kama Serikali ya wilaya katika sheria ndogo yao ikiwa kundi la mifugo litaingia kwenye maeneo yasiyoruhusiwa wameweka faini isiyozidi sh 300,000 kwa kundi la ng’ombe ambapo alisema pamoja na pongezi za Waziri Mpina bado wataendelea kubuni mbinu mbalimbali za kuboresha sekta ya ufugaji ikiwemo uimarishaji wa majosho, malisho na uzuiaji uuzaji nyama kiholela barabarani.

KAMPUNI YA MSAMA PROMOTIONS YAVIPIGA JEKI VITUO VYA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU

December 26, 2017
 
 Mkurugenzi wa Msama Promotions,Bwa Alex Msama akishiriki kushusha vifurushi vya mchele,ambavyo baadae alivitoe kwa vituo vya watoto waishia katika mazingira Magumu,makabidhiano ya msaada huo yalifanyika kwenye ofisi zake Kinondoni jijini Dar.
 Mkurugenzi wa Msama Promotions,Bwa.Alex Msama akikabidhi zawadi ya vyakula kwa ajili ya sikukuu za Krisimasi na Mwaka Mpya kwa mlezi wa kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu cha Mwandaliwa-Boko jijini Dar,Bi.Halima Mpeta. 
Kampuni ya Msama Promotions imetoa msaada wa vyakula mbalimbali  kwa baadhi ya vituo vya watoto waishio katika mazingira magumu,vilivyopo jijini Dar Es Salaam.

Akizungumza na Wanahabari wakati wa makabidhiano ya msaada huo,Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions,Alex Msama alisema kuwa kama ilivyo ada ya kampuni yake,kila ifikapo mwishoni mwa mwaka hutoa sadaka kwa vituo mbalimbali vya watoto waishio katika mazingira Magumu.

"Nimeamua kufanya hivi pia kuwakumbuka wototo wetu wanaoishi katika mazingira magumu,na wao washerehekee sikukuu kwa furaha kama wenzao,kwa hiyo nimetoa unga,mchele,mafuta,viywaji mbalimbali na vingine ili watoto hao nao kwa pamoja wafurahie msimu wa siku kuu",alisema Msama.

Nae mlezi wa kituo cha kulelea watoto waishio katika mazingira magumu cha Mwandaliwa-Boko jijini Dar,Bi.Halima Mpeta ameishukuru Kampuni ya Msama Promotions na Uongozi wake kwa kuwakumbuka katika msimu huu,wamemshukuru na kumuombea Heri zaidi afanikiwe katika mambo yake ili azidi kuwakumbuka na kuwasaidia wasiojiweza katika maeneo mbalimbali.

 Mkurugenzi wa Msama Promotion Alex Msama akimkabidhi msaada wa vyakula mmoja wa Viongozi wa kituo hicho cha watoto waishia katika mazingira Magumu cha Maunga,Kinondoni jijini Dar Es Salaamu.
Mwakilishi wa kituo cha TOVICHIDO,Bi Honoratha Michael akipokea msaada wa vyakula kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions,Alex Msama ,hafla hiyo fupi ilifanyika ofisini kwake Kinondoni Jiini Dar
-- Ahmad Issa Michuzi Editorial Director P.O BOX 9033, DAR ES SALAAM. issamichuzi.blogspot.com www.michuzijr.blogspot.com othmanmichuzi.blogspot.com Phone:0713 422 313/ 0783 422 313 Tanzania- East Africa.

WANANCHI JIJINI DAR ES SALAAM WAIPONGEZA KAMPUNI YA ABACUS PHARMA (A) LTD

December 26, 2017
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu (kulia), Daktari Bingwa wa Magonjwa ya homoni na Kisukari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Faraja Chiwanga  na Dk. Mohamed Mohamed wa ugonjwa wa Kisukari katika hospitali hiyo wakikata keki maalumu iliyotengenezwa kwa bidhaa za Sugar Free zisizo na sukari wakati wa uzinduzi  wa bidhaa hizo katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

 Muonekano wa keki hiyo iliyotengenezwa kwa bidhaa hizo zisizo na sukari.
 Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu, akizungumza bidhaa hizo. (Kwa maelezo zaidi kuhusu bidhaa hizo piga simu namba 0784834010)
Hii ndiyo timu ya maofisa masoko wa kampuni hiyo.

Na Dotto Mwaibale

WANANCHI jijini Dar es Salaam na vitongoji vyake wameipongeza  Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD kwa kuwaletea bidhaa za Sugar Free ambazo zinasaidia kupunguza  matumizi makubwa ya sukari kwenye vyakula.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam walisema kampuni hiyo haina budi kupongezwa kwa kuzileta bidhaa hizo katika soko la Tanzania ili kukabiliana na changamoto ya matumizi kupitia vyakula.

"Hivi sasa kila pembe ya nchi yetu kumekuwa na changamoto ya ugonjwa wa kisukari ambao kwa kiasi kikubwa unatokana na mfumo wa ulaji na unywaji wa vyakula vyenye sukari kupita kiasi kwa bidhaa hizi mpya zinazosambazwa na Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD hakika itasaidia sana" alisema Frank Erasto mkazi wa Temeke jijini Dar es Salaam.

Erasto alisema yeye ni mihongoni mwa waathirika wa ugonjwa wa kisukari lakini tangu bidhaa hizo ziingie katika soko la Tanzania amekuwa akitumia bidhaa hizo ili asiongeze sukari mwilini mwake baada ya kupata matibabu.

Mkazi wa Mbezi Beach jijini Dar es Salaam aliyejitambulisha kwa jina moaja la Reuben alisema familia yake imeanza kutumia bidhaa hizo ambazo hazina gharama kubwa.

"Familia yangu na marafiki zangu tumeanza kutumia bidhaa hizi za Sugar Free kusema kweli ni nzuri na zina radha kama ile zilizopo kwenye chakula halisi" alisema Reuben.


Mkazi wa Kariakoo Happyness Kimaro alisema kwake anaona bidhaa hizo ni mkombozi kwani ameanza kuzitumia baada ya kuathiriwa na ugonjwa wa kisukari na hapendi kuongeza sukari mwilini mwake.

"Sisi wagonjwa wa kisukari tumekuwa na changamoto kubwa ya ulaji wa vyakula mara tunaambiwa tusile hiki na kile tule vyakula ambavyo havina sukari ambavyo havina ladha sasa kwa kuletewa bidhaa hizi tunasema ni nafuu kwetu" alisema Kimaro.

Akizungumza bidhaa hizo, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Abacus Pharma (A) LTD, Ramesh Babu alisema bidhaa hizo zimesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matumizi makubwa ya sukari katika vyakula. 


Alisema bidhaa hizo zimetengenezwa mahususi ili kukabiliana na ongezeko la sukari mwilini na hivi sasa zinapatikana kwa bei ya chini katika soko la nchi za Tanzania, Uganda, Kenya, Rwanda na Burundi na kuwa bei hizo zipo kuanzia shilingi,4200, 4,500, 5,700, 8,850 na za bei ya juu ni shilingi 13,000 na kuwa zinategemea bidhaa husika.

"Bidhaa hizi zipo za aina mbili za sugar free gold  ambazo hutumika katika chai, uji, na vinywaji baridi tu  na sugar free natura hutumika katika baking, kupikia vyakula vinavyohitaji sukari katika upishi na pia hutumika katika chai, uji na vinywaji baridi na matumizi yake ni rahisi sana," alisema Babu.

Alisema kwa Tanzania bidhaa hizo zimeanza kuchukua soko kubwa baada ya wananchi kuona umuhimu wake na hivyo wanategemea muitikio utaendelea kuwa mkubwa.

Aliongeza kuwa, lengo kubwa la kampuni hiyo kusambaza bidhaa hizo ni kusaidia jamii kuelewa matumizi ya bidhaa hizo ambazo hazina sukari ingawa zina ladha ya sukari kama ile ya kawaida  na kwamba bidhaa hizo zimethibitishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO).


Akizungumza katika uzinduzi wa bidhaa hizo, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya homoni na Kisukari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Faraja Chiwanga alisema ugonjwa wa kisukari ni changamoto kubwa kwani Tanzania ni nchi ya tano Barani Afrika kwa kuwa na wagonjwa wengi.


Alisema hali hiyo inatokana na watu wengi hasa vijijini kutojijua mapema kama wameathiriwa na ugonjwa huo ambapo baadhi yao huanza kugundua baada ya kupata upofu, kukatwa miguu na kadhalika. 


Aliongeza kuwa, matibabu ya mgonjwa mmoja wa kisukari yanafikia asilimia 25 ya pato la familia fedha ambazo ni nyingi jambo linalowafanya wauguzaji kukata tamaa ya kumtibu mgonjwa na kuamua fedha hizo kuzielekeza katika matumizi mengine.


Dk.Chiwanga alitoa mwito kwa kusema ni vizuri kuzuia kupata kisukari kuliko kutibu.

Akizungumzia bidhaa za sugar free alisema hazitibu ugonjwa wa kisukari isipo kuwa zinamsaidia mgonjwa au mtu mwenye kisukari anapokula vyakula vingine visivyo na sukari kupata radha ile ile.

Alisema mtu mwenye ugonjwa wa kisukari hatakiwi kabisa kuvuta sigara ingawa vitu vingine kama vinywaji na pombe anatakiwa kutumia kwa uangalifu.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII JAPHET HASUNGA AWAONYA WANANCHI WA KISARAWE KUVAMIA HIFADHI

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII JAPHET HASUNGA AWAONYA WANANCHI WA KISARAWE KUVAMIA HIFADHI

December 26, 2017

1
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa tatu kulia) akiwa na baadhi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Huduma za Misitu  Tanzania (TFS),  kutoka makao makuu  Dar es Salaam  akiangalia vitalu vya miche ya miti  wakati   alipowatembelea wanakijiji wa Maguruwe wanaopakana na msitu wa Hifadhi wa  Kazimzumbwi waliojitolea kuotesha miche ya miti  kwa ajili ya kupanda   kwenye  eneo la msitu huo uliokuwa umevamiwa takriban theluthi tatu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 1993 hadi 2014.
2
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa kwanza kulia) akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Misitu wa Wilaya ya Kisarawe, Mathew Mwanuo   ( wa kwanza  kushoto)  wakati  alipofanya ziara mwishoni mwa wiki ya kutembelea  kilichokuwa  Kiwanda  cha Caoline, kilichopo katika  msitu wa hifadhi Pugu wilayani Kisarawe mkoani Pwani .
3
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akiwa na baadhi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Huduma za Misitu  Tanzania (TFS),  kutoka makao makuu jijini Dar es Salaam  wakioneshwa  ramani ya Msitu wa Hifadhi Kazimzumbwi na Kaimu Meneja wa Misitu wa Wilaya ya Kisarawe, Mathew Mwanuo (  wa tatu kushoto) kuhusiana na“eneo la msitu huo lilivyokuwa limevamiwa takriban theluthi tatu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 1993 hadi 2014.
4
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Kisarawe, Viongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wakiwemo  watumishi   wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara mwishoni mwa wiki  ya kutembelea  msitu wa Hifadhi wa Kazimzumbwi na Pugu wilayani Kisarawe mkoani Pwani.
5
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati)  akizungumza na wanakijiji wa Maguruwe  wanaopakana na msitu wa Hifadhi wa  Kazimzumbwi waliojitolea kuotesha miche ya miti kwa ajili ya kupanda   kwenye  eneo la msitu huo uliokuwa umevamiwa takriban theluthi tatu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 1993 hadi 2014 wakati Naibu Waziri huyo alipofanya  ziara mwishoni mwa wiki katika msitu huo.
6
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akisaini kitabu cha wageni alipotembelea  eneo kilichokuwa Kiwanda  cha Caoline, kilichopo  katika  msitu wa hifadhi Pugu wilayani Kisarawe mkoani Pwani wakati Naibu Waziri huyo alipofanya ziara mwishoni mwa wiki  katika msitu wa Hifadhi wa Kazimzumbwi na Pugu.
8
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akipatiwa maelezo na Mkurugenzi wa Rasilimali za Misitu na Nyuki wa   Wakala wa Huduma za Misitu  Tanzania (TFS), Zawadi Mbwambo  ( wa kwanza  kushoto)  wakati  alipofanya ziara jana ya   kutembelea  kilichokuwa  Kiwanda  cha Caoline, kilichopo katika  msitu wa hifadhi Pugu wilayani Kisarawe mkoani Pwani
9
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa kwanza kushoto) akioneshwa eneo la msitu Kazimzumbwi na Kaimu Meneja wa Misitu wa Wilaya ya Kisarawe, Mathew Mwanuo   lilivyokuwa limevamiwa takriban theluthi tatu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 1993 hadi 2014 wakati Naibu Waziri huyo alipofanya  ziara mwishoni mwa wiki katika msitu huo
Picha na Lusungu Helela-MNRT
……………………
NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga amewataka wananchi wanaozunguka hifadhi za misitu katika wilaya ya Kisarawe kuzingatia mipaka iliyowekwa pamoja na matumizi ya ardhi ili kuepuka migogoro inayoweza kujitokeza baina ya wananchi na serikali.
Hasunga alisema jana kwenye ziara aliyoifanya alipotembelea Kiwanda cha Caoline, pamoja na msitu wa hifadhi Kazimzumbwi na Pugu.
Alisema serikali haitakubali kuona maeneo ya hifadhi yanavamiwa ovyo na wananchi ama mifugo kuachiliwa bila utaratibu maalum.
“Kuna umuhimu mkubwa wa kukuza sekta ya utalii. Wataalii wengi wanapenda kuona misitu. Hii ni sehemu ya utalii,” alisema.
Aliwataka Kisarawe kuangalia vivutio walivyonavyo ili kuboresha katika maeneo hayo kwa ajili ya kuvutia utalii.
Kwa upande wake Kaimu Meneja Misitu Kisarawe, Mathew Mwanuo alisema wilaya hiyo ina misitu minne ya hifadhi ya serikali Kuu ambayo ni Ruvu Kusini, Masanganya, Pugu na Kazimzumbwi.
Alisema msitu wa Kazimzumbwi umekuwa ukivamiwa mara kwa mara na watu kutoka maeneo mbalimbali hasa jijini Dar es Salaam.
“Msitu huu ulikuwa umevamiwa takriban theluthi tatu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 1993 hadi 2014. Hata hivyo wavamizi hao waliendelea kuvamia kwa nyakati tofauti hadi mwaka huu,” alisema.
Alisema walianza kuwaondoa mwishoni mwa Agosti mwaka huu, Kamati ya Ulinzi na Usalam ya wilaya ya Kisarawe kwa kushirikiana na maofis wa Wakala wa Huduma za misitu Tanzania walianza kutembelea eneo la msitu kuangalia uvamizi na uharibifu uliofanyika katika Msitu wa Hifadhi wa Kazimzumbwi ikiwa ni pamoja na kuona ukubwa wa uharibifu na namna ya kutekeleza zoezi.

TANESCO YAFURAHISHWA NA HATUA ZA SERIKALI KULINDA VYANZO VYA MAJI YA KUFUA UMEME

December 26, 2017

  NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
INAELEZWA kuwa umeme wa maji, (Hydro power) ndio umeme wenye bei nafuu zaidi ukilinganisha na umeme unaotokana na vyanzo vingine.
Kwa mujibu wa Naibu Mkurugenzi wa TANESCO anayeshughulikia uzalishaji (Power Generation), Mhandisi Abdallah Ikwasa, matumizi ya juu ya umeme nchini kwa sasa ni Megawati 1,060, kati ya hizo, TANESCO kwa kutumia mitambo yake, huzalisha Megawati zaidi ya 1,000, na kati ya hizo, Megawati 381 zinatokana na umeme unaozalishwa kutokana na maji, (Hydro powere) kutoka vituo vinne vya umeme wa maji vya Kidatu, Mtera, New Pangani Falls, Hale na Nyumba ya Mungu.
Hata hivyo katika siku za karibuni shughuli za kibinadamu zimekuwa zikiongezeka kwenye vyanzo vya maji yanayoelekea kwenye vituo vya kufua umeme, na hivyo kutishia shuhghuli za uzalishaji umeme kwenye vituo hivyo.
Mhandisi Ikwasa alitoa mfano Mto Pangani ambapo yapo maeno ambayo shughuli za kilimo zinaendelea karibu na mto, na madhara yatokanayo na shughuli hizo hupelekea kingo za mto kuwa dhaifu na wakati wa mvua maji yanachukua udongo na kuingiza kwenye mto na hivyo kina cha mto kinakuwa kifupi.
“Sasa kipindi ambacho mvua zinanyesha unatarajia maji mengi yatiririke kwenye mto lakini kwa sababu kina kimepungua mto hauwezi kubeba yale maji na badala yake maji yanasambaa na kusababisha mafuriko na mbaya zaidi hayafiki kwenye mabwawa kwa kiwango kinachohitajika.” Alisema Mhandisi Ikwasa.
Alisema TANESCO kama wadau wakubwa wa maji wamekuwa wakishirikiana na mamlaka zinazosimamia mabonde, ili kuelimisha watumiaji wengine wa  maji.
“Tunataka kuhakikisha kwamba, kunakuwepo na matumizi endelevu ya maji, tunatambua wananchi wanahitaji maji kwa kilimo na sisi tunayahitaji kwa uzalishaji umeme kwa hivyo yakitumika vizuri yanaweza kufanya kazi zote.” Alisema.
Mhandisi Ikwasa aliipongeza Serikali kwa juhudi kubwa inazochukua kuhakikisha vyanzo vya maji vinalindwa.
“Makamu wa Rais aliunda kikosi kazi cha kuhakikisha vyanzo vya maji vinatunzwa na juhudi hizo zimeanza kuzaa matunda.” Alisema.
Ili kuhakikisha wananchi wanajenga dhana ya umiliki wa miundombinu ya TANESCO, Shirika limekuwa likishirikiana na wananchi katika shughuli mbalimbali za kijamii kama vile kusaidia kutoa huduma za afya, elimu ya awali na usafiri katika maeneo yanayozunguka vituo vya kuzalisha umeme.

“Tunataka wananchi wafahamu kuwa pamoja na kwamba kazi yetu ni kuzalisha umeme, lakini tunataka tuwe sehemu ya maisha yao, kwa kusaidia mambo ya kijamii kama vile kutoa elimu bure ya awali, zahanati, na usafiri wa basi unaosaidia wananchi kusafiri kuelekea kwenye shughuli zao, tunadhani kwa ushirikiano huu, wananchi watakuwa wakwanza kulinda miundombinu yetu na pia kuhakikisha mazingira yanatunzwa kwenye vyanzo vya maji.” Alisema Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji.
Ili kuhakikisha ujumbe huo pia unawafikia wananchi wote kupitia vyombo vya habari, wahariri wa vyombo vya habari walipata fursa ya kutembelea vituo vya kufua umeme wa maji vya Hale, New Pangani na Nyumba ya Mungu, vilivyoko mikoa ya Tanga na Kilimanjaro, kituo cha Mtera kilichoko mkoani Iringa na Kidatu mkoani Morogoro ili hatimaye watoe elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira ya vyanzo vya mito ambayo maji yake ndio huelekea kwenye vituo vya kufua umeme.

 Meneja wa kituo cha kufua umeme wa maji cha Kidatu, Mhandisi Anthony Mbushi, (kushoto), akizungumza kuhusu jinsi mageti ya kuruhusu maji kwenye mabwawa kwenda kwenye mitambo ya kufua umeme yanavyofanya kazi. Kulia ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, anayeshughulikia uzalishaji umeme. Mhandsisi Abdallah Ikwasa.
 Wananchi wa Kidatu, wakisub iri usafiri wa basi la Shirika la Umeme TANESCO, kuwapeleka kwenye mnada ili kuuza mazao yao. Usafiri huo hutolewa bure na Shirika katika mpango wake wa Corporate Social Responsibility (CSR) ili kujenga uhusiano mwema.
 Moja ya mashine za kufua umeme wa maji, (turbine), kituo cha Hale.
 Wasimamizi wa kituo cha kudhibiti mfumo wa umeme cha Mtera.
 Bwawa la New Pangani Water Falls.
 Kaimu Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, akizungumza jambo.
Mhandisi Mahenda S.Mahenda, Meneja vituo vya kufua umeme vya Pangani Hydro Systems, akifafanua jambo.
-- Khalfan Said Photojournalist K-VIS MEDIA P.o.box 77807 Dar es Salaam, Tanzania Mobile: +255-784-646-453/+255-653-813-033 Blog: khalfansaid.blogspot.com