WANA CCM KINONDONI CHAGUENI EMMENUEL TAMILA MAJENE KWA MAENDELEO YA JIMBO NA CCM

July 29, 2015
 

-- Mroki Mroki C.E.O MD Digital Company & FK Blog General Secretary PPAT Professional Photojournalist & BLOGGER P.O.BOX 110097, Mob: +255 755 373999 /+255 717 002303, Email: mrokim@gmail.com. Blog: www.mrokim.blogspot.com DAR ES SALAAM, TANZANIA

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAMUAGA BALOZI WA INDIA ALIYEMALIZA MUDA WA KAZI NCHINI

July 29, 2015


Balozi wa India nchini Tanzania anayemaliza muda wake wa kazi, Mhe.Debnath Shaw akitoa hotuba yake ya kuaga mbele ya wageni waalikwa wakiwemo  baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakiongozwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya wakati wa hafla ya chakula cha mchana iliyofanyika katika Hoteli ya New Afrika Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Julai, 2015.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (kushoto) pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hapa nchini ambaye pia ni mkuu wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, Mhe.Juma Halfan Mpango wakifuatilia hotuba ya Mhe.Debnath Shaw (hayupo pichani).
Balozi wa China hapa nchini, Mhe.LU Youqing (kulia) pamoja na Afisa  Mambo ya Nje, Bi.Eliet Magogo (katikati) pamoja na mmoja wa wageni waalikwa wakisikiliza hotuba.

Mabalozi pamoja na Maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje wakifurahia hotuba ya Balozi huyo wa India hapa nchini.
Balozi Yahya kwa pamoja na  Balozi Shaw wakitakiana afya njema
 Mshereheshaji akiendelea kusherehesha wakati wa hafla hiyo.
Balozi Yahya akiwaongoza Balozi  Shaw (kulia) na Balozi  Mpango kupata chakula wakati wa hafla fupi ya chakula cha mchan akumuaga Balozi Shaw.
 Balozi Yahya akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Shaw na Balozi Mpango
 Picha ya Pamoja.
 Balozi Simba akibadilishana mawazo na Balozi Debnath Shaw mara baada ya hafla hiyo.
Balozi Simba akiagana na Balozi Juma Mpango baada ya hafla hiyo Picha na Reuben Mchome

Shirika la Umoja wa Mataifa kukabiliana na biashara, YA matumizi za dawa za kulevya ZANZIBAR

July 29, 2015


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar
Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, akisalimiana na Muwakilishi wa Shirika la Umoja
wa Mataifa linalohusika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) Afrika Mashariki
Bw. Jose Castillo, walipokutana kwa ajili ya mazungumzo ofisini kwake
Migombani.
Muwakilishi wa Shirika la Umoja wa
Mataifa linalohusika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) Afrika Mashariki Bw.
Jose Castillo, akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Makamu wa Kwanza
wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, Ofisini kwake Migombani.
Muwakilishi wa Shirika la Umoja wa
Mataifa linalohusika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) Afrika Mashariki Bw.
Jose Castillo, akiagana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Fatma Abdulhabib Ferej, baada ya mazungumzo yaliyokuwa chini ya
Maalim Seif. Katikati ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Dkt. Omar Dadi Shajak.
 MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA ECG NA AL KAN KUTOKA MISRI, IKULU DAR ES SALAAM

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL, AKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA ECG NA AL KAN KUTOKA MISRI, IKULU DAR ES SALAAM

July 29, 2015
6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Wafanyabiashara wa ECG na Al Kan kutoka nchini Misri, wakati walipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Julai 29, 2015 kwa mazungumzo.
Picha na OMR
D
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyabiashara wa ECG AL Kan kutoka nchini Misri, baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam,leo Julai, 29, 2015.
JESHI LA POLISI LANOLEWA JUU YA HAKI ZA BINADAMU KIPINDI CHA UCHAGUZI

JESHI LA POLISI LANOLEWA JUU YA HAKI ZA BINADAMU KIPINDI CHA UCHAGUZI

July 29, 2015


mail.google.comJ
aji Mstaafu Thomas Mihayo alipokuwa akitoa Mada katika Semina ya Siku mbili kwa Maafisa wa Jeshi la Polisi iliyoandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini ili kulijengea uwezo Jeshi la Polisi katika kulinda haki za binadamu kipindi cha uchaguzi. Semina hiyo imefanyika  huko Ukumbi wa Hotel ya Grand mjini Zanzibar.
…………………………………………………..
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Jeshi la Polisi nchini limeshauriwa kuzisoma kwa kina na kuzielewa vyema Sheria na kanuni za Uchaguzi kabla ya kuzitekeleza.
Kufanya hivyo kutalipelekea Jeshi hilo kuepuka lawama na kufanya wajibu wao kikamilifu ili kuufanya Uchaguzi unaokuja uwe katika hali ya uhuru, haki na amani.
Wito huo umetolewa na Jaji Mstaafu Thomas Mihayo alipokuwa akitoa Mada katika Warsha ya Siku mbili kwa Maafisa wa Jeshi la Polisi iliyoandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini huko Ukumbi wa Hotel ya Grand mjini Zanzibar.
Amesema Jeshi hilo linawajibu wa kuhakikisha Sheria za nchi zinafuatwa lakini jambo la msingi ni kuzielewa Sheria hizo kabla ya kuzitekeleza.
Jaji Mihayo amesema inashangaza kuona kuwa Tanzania inaelekea katika kipindi cha uchaguzi Mkuu wakati Maafisa na Makamanda hawazielewi vyema Sheria na kanuni za Uchaguzi unaokuja.
Hivyo amewaomba Maafisa Wawaelimishe Makamanda wenzao juu ya Sheria na kanuni za uchaguzi ili wakati utakapofika watende haki na Wajibu wao bila ya upendeleo.
“Polisi kazi yenu nikuhakikisha Sheria zinafuatwa lakini zitafutwa vipi wakati wenyewe hamzijui..Jambo la msingu ni kuzisoma na kuzielewa kwanza ndio mufanye juhudi za kutekelezwa” alisema Mihayo.
Amefahamisha kuwa Jeshi hilo linapaswa kufuata Sheria za nchi bila kufuata matakwa ya Watawala na kwamba Watawala hao watabadilika kulingana na uchaguzi lakini Wananchi wataendelea kuwepo.
“Jeshi la Pilisi linawajibika kwa Wananchi na si Viongozi wa Serikali hivyo nakuombeni mzijue Sheria na muwe wakwanza kuzitekeleza” Alishauri Jaji Mihayo.
Kwa upande wake Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Makame ameshukuru Mtandao wa Watetezi wa haki za Binadamu kwa kuendesha Semina hiyo katika kipindi muafaka cha harakati za uchaguzi mkuu.
Amesema kila mtu ni mlinzi wa haki za binadamu katika kila sehemu anayofanyia kazi nakwamba jambo muhimu ni kuhakikisha Haki zinalindwa hasa ikizingatiwa kuwa suala la haki za binadamu ni lakimataifa.
Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini Harusi Mpatani ameliomba Jeshi hilo kuhakikisha linawalinda Wananchi wote ikiwemo Watetezi wa haki za binadamu.
Semina hiyo ya siku mbili iliyoandaliwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini ni mwendelezo wa kulijengea uwezo Jeshi la Polisi katika kulinda haki za binadamu ili kuufanya uchaguzi unaokuja uwe huru,haki na Salama.
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA UONGOZI WA SUMATRA, TRA, TABOA, RC-DSM NA WAZIRI WA FEDHA IKULU KWA MAZUNGUMZO.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA UONGOZI WA SUMATRA, TRA, TABOA, RC-DSM NA WAZIRI WA FEDHA IKULU KWA MAZUNGUMZO.

July 29, 2015

2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA) TRA, SUMATRA, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Waziri wa Fedha, wakati  walipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Julai 29, 2015.
Picha na OMR
3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa SUMATRA, TRA, na Wamiliki wa Mabasi Tanzania TABOA, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, na Waziri wa Fedha, baada ya kumalizika kwa mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwa Makamu Ikulu jijini Dar es Salaam,leo Julai, 29, 2015.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA AUSTRALIA NA GAVANA MKUU WA NCHI HIYO

July 29, 2015

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na Waziri Mkuu wa Australia Mhe. Tonny Abbot alipowasili asubuhi ya tarehe 28 Julai 2015 katika makao Makuu ya kiongozi huyo jijini Sydney.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo rasmi na Waziri Mkuu wa Australia Mhe. Tonny Abbot asubuhi ya tarehe 28 Julai 2015 katika makao Makuu ya kiongozi huyo jijini Sydney.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la lililoandaliwa kwa heshima yake huku akipigiwa mizinga 21 alipowasili asubuhi ya tarehe 28 Julai 2015 katika makao Makuu ya kiongozi huyo jijini Sydney.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiutambulisha ujumbe wake kwa Waziri Mkuu wa Australia Mhe. Tonny Abbot alipowasili asubuhi ya tarehe 28 Julai, 2015 katika makao Makuu ya kiongozi huyo jijini Sydney.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka sahihi katika kitabu cha wageni alipowasili kwenye jumba la serikali jijini Sydney tarehe 28 Julai 2015 na kukutana na kufanya mazungumzo na Gavana Mkuu wa Australia Mheshimiwa Peter Cosgrove aliyesimama nyuma yake pamoja na Mama Salma Kikwete na Mke wa Gavana huyo Mama Cosgrove.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea wakati wa chakula cha mchana kwenye jumba la serikali jijini Sydney tarehe 28 Julai 2015 baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Gavana Mkuu wa Australia Mheshimiwa Peter Cosgrove. PICHA NA IKULU
 RAIS KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA CHUO KIKUU CHA NEWCASTLE, AUSTRALIA

RAIS KIKWETE ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA YA CHUO KIKUU CHA NEWCASTLE, AUSTRALIA

July 29, 2015
KI1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mstahiki Meya wa jiji la Newcastle Mhe. Nuatali Nelmes na viongozi wa chuo kabla ya kuanza kwa msafara wa kwenda jukwaa kuu kutunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa Sheria (Doctor of Laws honorific causa) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Newcastle Bwana Paul Jeans chuoni hapo nchini Australia leo tarehe 29.7.2015 katika ukumbi wa chuo hicho.
KI2
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya kumbukumbu na Mstahiki Meya wa jiji la Newcastle Mhe. Nuatali Nelmes kabla ya kuanza kwa msafara wa kwenda jukwaa kuu kutunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa Sheria (Doctor of Laws honorific causa) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Newcastle Bwana Paul Jeans chuoni hapo nchini Australia leo tarehe 29.7.2015 katika ukumbi wa chuo hicho.
KI3
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Mstahiki Meya wa jiji la Newcastle Mhe. Nuatali Nelmes na viongozi wa chuo wakipata maelezo kabla ya kuanza kwa msafara wa kwenda jukwaa kuu kutunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa Sheria (Doctor of Laws honorific causa) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Newcastle Bwana Paul Jeans chuoni hapo nchini Australia leo tarehe 29.7.2015 katika ukumbi wa chuo hicho.
KI4
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika msafara wa kwenda jukwaa kuu kutunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa Sheria (Doctor of Laws honorific causa) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Newcastle Bwana Paul Jeans chuoni hapo nchini Australia leo tarehe 29.7.2015 katika ukumbi wa chuo hicho.
KI6
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na viogozi wa chuo jukwaa kuu wakisimama wakati nyimbo za Taifa za Tanzania na Australia zikipigwa wakati wa kuanza kwa sherehe za kutunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa Sheria (Doctor of Laws honorific causa) na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Newcastle Bwana Paul Jeans chuoni hapo nchini Australia leo tarehe 29.7.2015 katika ukumbi wa chuo hicho.
KI7
Wasanii wa kabila la Wakakulang wakicheza ngoma za asili yao katika kunogesha sherehe za kihistorua ambapo Rais Kikwete amekuwa ni Mkuu wa Nchi wa kwanza kupokea digrii hiyo ya heshima kutoka katika Chuo hicho.
PICHA NA IKULU

Jaji Mutungi Ajiandikisha Katika Daftari la Kudumu La Wapigakura

July 29, 2015
 Mhe. Jaji Francis S.K. Mutungi akiwa na kitambulisho chake mara baada ya kujiandikisha mapema Leo katika kituo cha Shule ya Msingi Bunge Jijini Dar es salaam.


  Mwandikishaji Msaidizi Bi. Maida Ally Yusufu akimsainisha Jaji Mutungi fomu ambazo zimebeba taarifa zake kwa ajili ya kujiandikisha Leo katika kituo cha

 Alama za vidole zikichukuliwa na Mwandikishaji Bw. Ernest Moses Selelya mara baada ya kukamilisha taratibu za ujazaji wa fomu ya utambulisho.
Mhe.Jaji Francis Mutungi akipokea kitambulisho cha mpiga kura kutoka kwa Mwandikishaji Bw.Ernest Moses Selelya.