SERIKALI YATENGA BILIONI 50 KUBORESHA KILIMO CHA ZAO KOROSHO NCHINI-NAIBU WAZIRI MAVUNDE

August 18, 2023

 



NAIBU Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde akizungumza wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Wadau wa Korosho nchini kilichofanyika Jijini Tanga ambapo alisema uboreshaji huo unakwenda sambamba na kuongeza bajeti kwenye sekta ya Kilimo.


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, ya Viwanda,. Biashara, Kilimo na Mifugo Mariam Ditopile akziungumza wakati wa mkutano huo


Mwenyekiti wa Bodi ya korosho Tanzania, Jenerali Mstaafu Aloyce Mwanjile akizungumza wakati wa mkutano


MKUU wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akizungumza wakati wa mkutano huo
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Pesa Angelica Pesha akizungumza akielezea namna wakulima watakavyonufaika kupokea malipo yao kupitia line zao za simu kwenye akaunti ya Tigo Pesa wakati wa mkutano huo
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Pesa Angelica Pesha akizungumza akielezea namna wakulima watakavyonufaika kupokea malipo yao kupitia line zao za simu kwenye akaunti ya Tigo Pesa wakati wa mkutano huo
Mkurugenzi Mkuu wa Tigo Pesa Angelica Pesha kushoto akiwa na washiriki wengine wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye mkutano wa wadau wa Korosho Jijini Tanga
Sehemu ya Wakuu wa Mikoa wakifuatilia mkutano huo
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania (TSB) Saady Kambona katikati akiwa kwenye kikao hicho


Na Oscar Assenga, TANGA

NAIBU Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde amesema Serikali imetenga bajeti ya Sh.Bilioni 50 kwa mwaka wa Fedha 2023/2024 kwa ajili ya kuboresha kilimo cha zao la korosho nchini.

Mavunde aliyasema hayo leo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Wadau wa Korosho nchini kilichofanyika Jijini Tanga ambapo alisema uboreshaji huo unakwenda sambamba na kuongeza bajeti kwenye sekta ya Kilimo.

Alisema hiyo itakuwa kwa ajili ya kulipia pembejeo zinazotolewa kwa wakulima ikiwemo pamoja na kugawa miche bora ya mikorosho kwa wakulima ikiwemo kuhuisha kanzidata ya wakulima wa Korosho.

Aidha alisema kanzidata hiyo ya wakulima wa korosho kwa kupima mashamba ikiwemo kuchukua GPS Codines kuhesabu idadi ya mikorosho kwa kutumia mfumo wa satellite, kupiga picha wakulima na kuchukua namba za vidole.

“Lakini pia kumpatia mkulima namba maalumu ya utambulisho ambayo ataitumia kupata pembejeo na kuuza korosh zake katika msimu unaokuja watahakikisha ile namba maaliumu ya mkulima ambayo anaitumia kama utambulishio wa kupata pembenejo ndio itakayotumika kuuzia korosho zake”Alisema

Mavunde alisema hiyo itawasaidia kupata takwimu sahahi za wakulima huku akiiagiza kwenye bodi ya Korosho nao wasimamizi wa usajili wa wakulima katika ngazi ya wilaya lazima sasa maelekezo washuke mpaka ngazi ya kata ili zoezi hilo liende kwa haraka zaidi ili waweze kuwasajili wakulima.

Hata hivyo alisema bado wanafikiria mpango wa kuongeza idadi ya wasimamizi kupitia usajili huo ambao utawasaidia kupata nafasi kujua aina ya wakulima walionao na ukubwa wa mashamba yao ikiwemo pembejeo wanazopokea na miche walionao.
“Hii itawasaidia sana kwenye takwimu zao kama serikali katika kuwahudumia wakulima lakini la tatu tutaendelea kuvutia na kuhamasisha uwekezaji mkubwa kwenye ubanguaji na usindikaji wa korosho “Alisema

Hata hivyo alisema tayari wamekwisha kutenga eneo la kutosha kwa ajili hiyo katika kijiji cha Maranje Kata ya Mtiniko Halmashauri ya Mji wa Nanyamba Mkoani Mtwara lenye ukubwa wa Ekari 1375 zimetengwa na zitatumika kujenga kongani ya viwanda

Katika hatua nyengine, Naibu Waziri Mavunde alisema kwa kulifanya zao hilo liendelee kuwa na mchango mkubwa kwenye uchumi wa Taifa.

“Ukiangalia takwimu za dunia biashara ya kirosho kwa msimu uliopita ni Trilioni 17.8 duniani na inadiriwa ilifanyika na ifikapo mwaka 2028 biashara ya korosho itakuwa ni zaidi ya Trilioni 21.8 duniani hivyo inawaambie kwamba mfanye uwekezaji mzuri kuanza kwenye tafiti na kuwawezesha wakulima kulima kwa tija ipo fursa kubwa dunia kwa zao hilo”Alisema Naibu Waziri Mavunde

Awali akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya korosho Tanzania, Jenerali Mstaafu Aloyce Mwanjile amesema kuwa katika msimu wa mwaka 2022/23 jumla ya korosho ghafi zaidi ya tani laki moja 176.6 ziliweza kukusanywa na kuingiza zaidi ya Sh bilioni 328.

Alisema kati ya hizo tani zaidi ya laki 168 zilisafirishwa nje ya nchi na zilizobaki ziliendelea kubanguliwa ndani ya nchi na kwa msimu wa 2023/2024 bodi imepanda kuendelea kushirikiana na wadau wa korosho nchini kutekeleza mipango mbalimbali ya kuongeza uzalishaji,ubanguaji na ufanisi wa masoko nchini.

Aidha alisema kwamba bodi kwa kushirikiana na wizara wameendelea kufanya mazungumzo na wawekezaji ambao watafungulia Industry Park Maranja wilaya ya Nanyamba Mkoani Mtwara eneo ambapo kikifanikiwa watakwenda kuwa na ubanguaji wa tani zaidi ya laki mbili nchini jambo ambalo kwao wanaliona kama sahihi kwenye kuongeza thamani kwenye mnyororo wa zao la Korosho.

Naye kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba akitoa salamu za mkoa kwenye mkutano huo alisema mkoa huo unatekeleza ilani ya CCM ya Mwaka 2020 ili kuweza kuongeza uzalishaji wa Korosho kufikia tani 700,000 itakapofika mwaka 2025/2026.

Alisema mkoa umepanga kuzalisha tani 10,000 ili kuweza kuchangia kwenye tani laki saba zilizopangwa kitaifa na wamejiwekea mipango mbalimbali ikiwemo ufufuaji wa mashamba pori ambapo mashamba pori 3382 yaliibuliwa na jumla ya ekari 328 zimekwisha kufufuliwa.

BENKI YA CRDB YAMTANGAZA MSHINDI WA TATU WA TOYOTA CROWN KATIKA KAMPENI YA BENKI NI SIMBAKING

August 18, 2023

 

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd (wa pili kulia), akimkabidhi Robert Masala kadi ya gari aina ya Toyota Crown baada ya kushinda katika kampeni ya Benki ni SimBanking katika hafla iliyofanyika nyumbani kwa mshindi, Goba jijini Dar es Salaam Agosti 17, 2023. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Meneja wa CRDB Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Donath Shirima na Balozi wa Benki ya CRDB Stephane Aziz Ki.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd (katikati), akimkabidhi namba ya gari aina ya Toyota Crown mteja wa benki hiyo, Robert Masala (wa pili kulia) baada ya kuibuka mshindi wa kampeni ya Benki ni SimBanking katika hafla ilifyoanyika nyumbani kwa mshindi huyo Goba jijini Dar es Salaam Agosti 17, 2023. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Meneja wa CRDB Tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Donath Shirima, Balozi wa Benki ya CRDB, Stephane Aziz Ki na kulia ni Meneja Mwandamizi wa Huduma Mbadala za Kibenki, Mangire Kibanda.

=========   =========   =========

Benki ya CRDB imemkabidhi Robert Masala, mkazi wa Goba jijini Dar es Salaam gari jipya aina ya Toyota Crown baada ya kuibuka mshindi katika awamu ya tatu ya kampeni ya Benki ni Simbanking.

Masala aliyeibuka kidedea kwa mwezi Julai anaungana na Jared Awando Ojweke aliyekuwa mshindi wa shinda gari Juni na Mayani Yahaya Hassan aliyekuwa wa kwanza mapema Mei.

Akieleza namna anavyoitumia huduma za SimBanking, Masala amesema amekuwa mteja wa Benki ya CRDB tangu mwaka 2005 na huduma hiyo imekuwa ikimrahisishia kufanya miamala hasa ya biashara zake kwa urahisi na kwa wakati.

“Mimi ni mwajiriwa hapa Dar lakini nina biashara Mwanza ambako ndio nyumbani. Simbanking huwa inanisaidia sana kwenye usimamizi wa mapato na matumizi ya biashara. Kati ya mwezi Mei na Juni nilikuwa na miradi naikamilisha hivyo nilitumia sana Simbanking nje ya utaratibu wa kawaida. Nadhani hii imechangia kwa namna au nyingine mimi kushinda gari hili,” amesema Masala.

Tangu alipofungua akaunti ya Benki ya CRDB, Masala ambaye ni baba wa watoto wawili anasema amekuwa akitumia huduma za Simbanking tangu tangu mwanzoni ilipokuwa ikitumia teknolojia ya USSD pekee kwa kubofya *150*03# mpaka ilipoanzishwa programu ya kidijitali ya SimBanking App ambayo amesema ni rahisi na ina ufanisi mkubwa.

Kwa waajiriwa wenzake, Masala amewashauri kuitumia Benki ya CRDB pamoja na Simbanking ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kushinda zawadi kemkem zinazotolewa kila mwezi kuanzia fedha taslimu, simu za mkononi hata gari hasa Toyota Crown linalotolewa kila mwezi na Vanguard atakalokabidhiwa mshindi wa jumla.


Kama ilivyokuwa kwa washindi waliomtangulia, Masele naye amekabidhiwa gari hilo lenyye thamani ya TSZ 20 milioni likiwa limekatiwa bima kubwa na kujaziwa mafuta “full tank.”

Akimkabidhi zawadi hiyo, Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Badru Idd amesema kwa hali ilivyo sasa hivi ni ngumu kuuepuka uchumi wa kidijiti hivyo Watanzania hawapaswi kubaki nyuma watumia huduma za Simbanking, jukwaa bora zaidi nchini na linaloongoza kwa kutumiwa kati ya programu za benki zilizopo.

“Leo tunamtangaza Robert Masala aliyeibuka mshindi wa gari kwenye droo iliyochezeshwa tarehe 3 mwezi huu. Yeye ni ni mshindi wa tatu kuondoka na gari baada ya Jared Awando Ojweke wa hapa Dar es Salaam na Mayani Yahaya Hassan wa mkoani Dodoma kushinda miezi miwili iliyopita. Simbanking ni ya kila mtu, unaweza kumaliza mahitaji yako ukiwa mahali popote,” amesema Idd.

Ikiwa benki kiongozi nchini, meneja huyo amesema Benki ya CRDB inahakikisha wakati wote inaboresha huduma zake ili kukidhi mahitaji ya wateja ikitambua kwamba matarajio yao yanabadilika kila siku.

Hivi karibuni Benki ya CRDB ilizindua SimBanking App mpya ikiwa ni sehemu ya jitihada za benki katika kuboresha huduma na kuleta mapinduzi katika sekta ya fedha nchini.

SimBanking mpya imetengenezwa kwa muunganiko wa teknolojia za kisasa na za hali ya juu ikiwamo akili mnemba (Artificial intelligence), jambo linaloifanya kuwa na uwezo mkubwa katika utambuzi wa tabia na mahitaji ya mteja pindi anapotumia.
Mshindi wa gari aina ya Toyota Crown wa kampeni ya Benki ni Simbanking ya Benki ya CRDB, Robert Masala akiwa na mkewe, Esther Itule baada ya kukabidhiwa gari hilo na Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Badru Idd. 


--