JAFFO ATAKA DODOMA IWE (FRUITS CITY) MJI WA MATUNDA

JAFFO ATAKA DODOMA IWE (FRUITS CITY) MJI WA MATUNDA

April 20, 2018


Na Mahmoud Ahmad Dodoma

Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi Suleiman Jaffo amewataka watendaji waliochini yake kuhakikisha wanahimiza wananchi kupanda miti ya matunda ndani ya mkoa wa Dodoma sanjari na Halmashauri ya manispaa ya Dodoma ili mji huo uwe mji wa matunda(Fruits City).

Kauli hiyo ameitoa mwanzo mwa wiki kwenye Chuo cha Serikali za mitaa Hombolo wakati akiongea na wanafunzi na wafanyakazi wa chuo hicho wakati akizindua mnara uliopewa jina la Magufuli Square kuenzi utendaji wa mh.Rais.

Amesema kuwa anataka kuona upatikana wa matunda kwenye mji wa Dodoma kuanzia kwenye Bara bara zote za mji huo wanapanda mitii ya matunda ili kuweza kuwa na mji wenye urahisi wa upaitikanaji wa matunda.

“Nataka mtu akiwa nahamu na matunda wakati anatembea anaweza kuyapata popote ndani ya mji huu tena kwa urahisi kuliko kutembea umbali mrefu kutafuta ukwaju au maembe” alisisitiza Jaffo.

Akizungumzia mnara huo aliozindua mh. Jaffo alisema kuwa lengo lake ni kuhamasisha watumishi wa umma kujua wajibu wao katika utumishi wao na kujitathmini katika uwajibikaji wao wakutoa huduma bora kwa wananchi

Amesema kufanyakazi kwa bidii ndio msingi katika maisha yao ya utumishi na kujali hali za wananchi wanyonge wa taifa hili kama alivyo mh. Raisi dkta John Magufuli yeye amejipambanua katika kuwajali wanyonge wa nchi hii na sisi tujitazame kama tumefanana naye katika majukumu yetu ya kila siku.

Akautaka uongozi wa chuo hicho na wanafunzi kuanza kuishi kwa mitazamo ya kuwatumikia wananchi wanyonge kwa maslahi mapana ya kuweka mbele uzalendo kwa nchi yao ilikulipeleka taifa mbele kwenye mafanikio sahihi ya uchumi wa kati.

Amekizungumzia kikundi cha ngoma kilichotumbuiza katika Hafla hiyo kwa kuutaka uongozi wa chuo hicho kuweka mikakati ya kukisaidia kuweza kuwa na miradi ya kuwainua katika kufikia kuweza kurekodi Albamu yao na kuwa na mradi wa kuku ili kuwa mfano na Alama ya chuo hicho
RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI KUTOKA UMOJA NA AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA WAGENI KUTOKA UMOJA NA AFRIKA (AU) NA MISRI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

April 20, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Kamishna wa Amani na Usalama wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Balozi Smail Chergui Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab kabla ya kuanza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Misri ambaye kwasasa ni Mshauri wa Rais wa Misri Injinia Ibrahim Mahlab Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

WAZIRI DKT. KALEMANI AWASHA UMEME KWA MARA YA KWANZA KATIKA KIJIJI CHA LUMWAGO

April 20, 2018

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani,mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliam,Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi pamoja na mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya Mufindi wakiwa nafungua na kuwasha umeme kwa mara ya kwanza katika kijiji cha Lumwago kata ya Upendo wilayani Mufindi mkoani Iringa.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi wakishangilia baada ya kuona kweli umeme umewaka katika kijiji cha Lumwago
Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi akiwa Kwenye furaha ya ajabu baada ya kuona wananchi wake wamefanikiwa kupata umeme katika eneo hilo ambazo minasekana linakuwa kwa kasi kubwa

Mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi akiongea mbele ya wapiga kura wake wa jimbo hilo

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani akiwaonyesha wananchi wa jimbo la Mafinga Mjini kifaa cha Umeme Tayari (UMETA).

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewasha umeme kwa mara ya kwanza katika Kata ya Upendo mtaa wa Lumwago uliyopo wilayani Mufindi, Mkoa wa Iringa.

Uzinduzi huo uliofanyika mbele ya mamia ya wananchi wa mtaa wa Lumwago ambao walikuwa na furaha baada ya kuona umeme huo umewaka kwa mara ya kwanza

Waziri Kalemani alifanya uzinduzi huo akiwa katika ziara ya kazi mkoani Iringa wakati wa kukagua miradi ya umeme inayotekelezwa na REA awamu ya tatu.

Awali, akiongea na wananchi Dkt. Kalemani alisema kuwa wananchi zaidi ya 200 wataanza kupata umeme kufuatia tukio la kurasimishwa kuwashwa kwa nishati hiyo Lumwago.

“Tunatoa kipaumbele chetu kwa sasa kwani ni kuhakikisha kwamba wananchi wengi wanapata umeme na huduma hiyo inakuwa ya uhakika,” alisema Dkt. Kalemani

Akifafanua zaidi, alisema kuwa, Serikali imeanzisha harakati za kufanya ukaguzi kwenye utekelezaji wa Miradi yote ya umeme mkoani humo.

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwataka viongozi wa Halmashauri mbalimbali za vijiji kote nchini, kuhakikisha wanajiandaa kwa ajili ya kuunganishiwa umeme katika taasisi zote za umma zikiwemo Shule, Vituo vya Afya, Miradi ya Maji, Masoko na nyinginezo.

Vilevile, alikumbushia umuhimu wa kila mmoja kuhakikisha baada ya kuunganishiwa umeme katika eneo lake anakumbuka kulipa bili za huduma hiyo muhimu.

“Usipolipa,Serikali itakukatia umeme hivyo kurudisha nyuma maendeleo yako,” alisisitiza.

Jambo jingine ambalo Waziri Kalemani alisisitiza ni kwa wakandarasi kuhakikisha wanawagawia bure wateja 200 wa kwanza watakaojitokeza kuunganishiwa umeme wa REA, kifaa cha Umeme Tayari (UMETA) kama ilivyoelekezwa na Serikali na siyo vinginevyo.

Hapo awali,mbunge wa jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi pamoja na kupongeza jitihada ambazo Wizara ya nishati imekuwa ikifanya nchi nzima katika kuhakikisha huduma ya umeme inapatikana katika maeneo mbalimbali, pia alimwomba Waziri Kalemani kulipa upendeleo jimbo hilo kwa kuwa ndio kitovu cha uchimi wa viwanda mkoani Iringa.

“Mheshimiwa nikuombe utusaidia kwenye vijiji vilivyobaki katika jimbo langu kwasasababu wananchi wangu niwachapakazi na wapenda maendeleo” alisema Chumi

Chumi aliwamwambia waziri kuwa jimbo la Mafinga Mjini ni moja kati ya maeneo ambayo yanaviwanda vingi ambavyo vinasaidia kukuza uchumi wa nchi pamoja na kuongeza ajira kwa watanzania wanaoishi katika jimbo hilo.

“Hapa tunazaidi ya viwanda arobain vya mazao ya miti na tunaviwanda vingine vingi na viwanda vyote hivi vinatumia nisharti ya umeme hivyo naomba nitoe rai kuwa mji wa mafinga unahitaji sana huduma ya nishati hii kwa kiasi kikubwa” alisema Chumi

DC SHINYANGA AKUTANA NA WANANCHI KIJIJI CHA NYAMBUI KUTATUA MGOGORO UJENZI WA MNADA TINDE

April 20, 2018
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amekutana na wakazi wa kijiji cha Nyambui kilichopo katika kata ya Tinde halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kutatua mgogoro wa eneo la ujenzi wa mradi wa mnada utakaotumika badala ya ule uliopo hivi sasa.


Mkuu huyo wa wilaya amefika katika kijiji hicho kutatua mgogoro huo leo Ijumaa Aprili 20,2018 akiwa ameambatana na maafisa mbalimbali wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.

Akizungumza wakati wa kikao hicho,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro aliiagiza halmashauri kupima eneo hilo na kuboresha miundo mbinu ya mnada mpya huku akisisitiza wananchi wazawa kupewa kipaumbele katika maeneo ya biashara.

“Niiagize halmashauri kuwa sasa tunapokwenda kuuboresha huu mnada,ni lazima kwanza tuwape kipaumbele wazawa wa eneo hili kwa sababu walikuwepo tangu mwanzoni,wakaiachia serikali kwa ajili ya maendeleo, tukishamaliza basi maeneo yanayobaki tutawapa wageni watakaokuja kufanya biashara hapa bahati nzuri majina yenu tunayo hivyo kazi itakuwa rahisi’,alieleza Matiro.

“Tunataka tufanye mnada hapa na mnada huu unatupa pesa kama halmashauri,hivyo miundo mbinu kama choo,maji,ofisi lazima viwekwe kwenye utaratibu kabla mnada huu mpya haujaanza na tutakuja kukagua ili tuone kama yale tuliyoagiza yanafanyika? kazi ya kwanza inayotakiwa hapa ni kupima eneo na kuweka mpango kazi”,aliongeza.

Baadhi ya wananchi wa kijiji hicho wanadai kutolipwa fidia ya ardhi na nyumba wakati wa ujenzi wa barabara ya Tinde – Kahama uliokuwa unasimamiwa na Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) ambao baada ya kukamilisha ujenzi walikabidhi eneo hilo kwenye halmashauri ambayo iliamua eneo hilo litumike kwa ajili ya ujenzi wa mnada mpya.

Hata hivyo inaelezwa kuwa baada ya wananchi kuona halmashauri hailiendelezi eneo hilo huku mnada uliopo ukiendelea kuwa mchafu waliamua kuvamia eneo la ujenzi wa mnada huku wengine wakidai hawajalipwa fidia kupisha eneo hilo hivyo kukwamisha ujenzi huo.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Thomas Tukay alisema jumla ya wananchi 67 wa kijiji cha Nyambui walilipwa shilingi milioni 30.4 kwa ajili ya fidia ya majengo na ardhi wakati wa ujenzi wa barabara ya Tinde – Kahama mwaka 2004 hivyo wanaodai hawajalipwa ni waongo.

Aliongeza kuwa halmashauri hiyo iliamua kuanzisha mradi wa mnada mpya katika kitongoji cha Mwandu ili mnada wa mwanzo uliopo katika kitongoji cha Ngaka uhamie hapo Mwandu na kule Ngaka iwe sehemu ya kituo cha mabasi na malori.

Mwenyekiti wa kijiji hicho,Richard Mpanga alisema wananchi wapo tayari kushirikiana na serikali endapo itaweka miundombinu rafiki katika mnada huo mpya.

“Ule mnada wa kwanza ambao ni wa siku nyingi ni mchafu,hata vyoo hakuna watu wanajisaidia ovyo kwenye mlima ulipo jirani, ukiletwa hapa wananchi wanaweza kupata magonjwa,hivyo halmashauri itengeneze kwanza miundo mbinu ndiyo mnada uhamie hapa”,alisema.

Nao wakazi wa eneo hilo waliitupia lawama halmashauri kwa kutosimamia kikamilifu mnada uliopo huku wakidai baadhi ya viongozi wa halmashauri kutokuwa waadilifu na kukwamisha mradi huo.


ANGALIA PICHA HAPA CHINI


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nyambui kata ya Tinde halmashauri ya wilaya ya Shinyanga leo Aprili 20,2018 - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wakazi wa Nyambui na kuwataka kushirikiana na serikali katika miradi ya maendeleo - Kulia ni mwenyekiti wa kijiji cha Nyambui Richard Mpanga ,Kushoto ni Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Ngasa Mboje

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wakazi wa Nyambui ili kutatua mgogoro wa eneo la ujenzi wa mnada

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akisisitiza jambo. Kushoto ni diwani wa kata ya Tinde Japhar Kanolo
Mkuu wa Idara ya Ardhi na Maliasili wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, Thomas Tukay akifafanua jambo wakati wa kikao hicho

Mwenyekiti wa kijiji cha Nyambui Richard Mpanga akifafanua kuhusu mgogoro wa eneo la mradi wa mnada na changamoto za mnada uliopo sasa.

Katibu tawala wilaya ya Shinyanga, Boniface Chambi akizungumza katika kikao hicho
Diwani wa kata ya Tinde Japhar Kanolo akielezea kuhusu mgogoro wa eneo la mnada
Mkazi wa kijiji cha Nyambui aliyejulikana kwa jina la Mohammed akichangia hoja wakati wa kikoa hicho cha utatuzi wa kikao

Mkazi wa kijiji cha Nyambui Katale Kadama akielezea kuhusu mgogoro wa eneo la mnada na jinsi la kuutatua

Mkazi wa Nyambui,Walesi Kiabo Kilatu akichangia hoja wakati wa kikao hicho

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wakati wa Nyambui akitatua mgogoro wa eneo la ujenzi wa mnada.

Kushoto ni diwani wa kata ya Tinde Japhar Kanolo akimweleza jambo mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akijadiliana na baadhi ya wananchi wa Nyambui kuhusu mgogoro wa eneo la mradi wa mnada.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akiendelea kuzungumza na wakazi wa Nyambui. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

LIGI KUU YA WANAWAKE YA SERENGETI PREMIUM LITE HATUA YA NANE BORA KUENDELEA WIKIENDI,SERENGETI YAGAWA MAVAZI RASMI KWA TIMU

April 20, 2018
Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Premium Lite Hatua ya Nane Bora inatarajia kuendelea Wikiendi hii.

Jumamosi Aprili 21,2018 zitachezwa mechi Tatu na mchezo mmoja utachezwa Jumapili Aprili 22,2018.

Jumamosi Kwenye Uwanja wa Karume Evergreen watawakaribisha Alliance ,Wakati kwenye Uwanja wa Mbweni JKT Quenns watakuwa wenyeji wa Simba Queens nayo Kigoma Sisterz ikiwa Uwanja wa Tanganyika kuwaalika Baobab.

Mchezo wa Panama dhidi ya Mlandizi Queens wenyewe utachezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Samora Iringa.

Ligi hiyo ilisimama kupisha maandalizi ya timu ya Taifa ya Wanawake iliyokuwa na mchezo wa kufuzu fainali za Africa kwa Wanawake dhidi ya Zambia.

Katika hatua nyingine Wadhamini wa Ligi hiyo ya Wanawake kampuni ya Bia ya Serengeti kupitia Bia yake ya Serengeti Premium Lite,imekabidhi mavazi rasmi kwa timu zote.

Meneja Masoko wa Serengeti Anitha Msangi amesema Serengeti inaamini kuwa kuidhamini Ligi Kuu ya Wanawake wanachangia kuleta maendeleo ya Mpira wa Wanawake.

Amesema Mashabiki wanayo nafasi kubwa katika maendeleo ya Mpira wa Wanawake na kuwataka waweze kujitokeza kuunga mkono Ligi Kuu ya Wanawake pamoja na kuziunga mkono timu za Wanawake.

BENKI YA KILIMO TANZANIA KUFUNGUA OFISI ZA KIKANDA KWA AWAMU

April 20, 2018



Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma

Serikali imeeleza kuwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) inatekeleza Mpango wa Miaka Mitano (2017- 2021), wa kusogeza huduma karibu na wateja kwa kuanzisha ofisi za Kikanda katika Kanda ya Kaskazini, Kusini, Kati, Ziwa, Nyanda za Juu Kusini na Zanzibar kwa awamu.

Hayo yameelezwa Bungeni Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakati akijibu maswali ya msingi ya Mbunge wa Viti Maalumu Mhe. Jacqueline Msongozi (CCM), aliyetaka kujua lini Serikali itapeleka Benki ya Kilimo katika Mkoa wa Ruvuma ili wananchi waweze kukopeshwa.

Aidha, Mhe. Msongozi alitaka kufahamu utayari wa Serikali kupunguza riba ya mikopo wanayokopeshwa Wakulima katika Benki hiyo.

Akijibu maswali hayo, Dkt. Ashatu Kijaji alisema kuwa hadi kufikia Juni 30, 2018 Ofisi ya Kanda ya Kati, Dodoma, itakuwa imefunguliwa ambayo pia itakuwa ni Makao Mkauu ya Benki hiyo.

“Baada ya ufunguzi wa ofisi ya Kanda ya Kati kukamilika Benki Itafanya uchambuzi wa fursa zilizopo Kikanda na hivyo kuchukua hatua na taratibu za kufungua ofisi nyingine kulingana na upatikanaji wa rasilimali fedha”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa Benki hiyo inatoa mikopo kwa kutumia mfumo wa makundi, kundi la kwanza wakulima wadogo wadogo kwa riba ya asilimia 8- 12, kundi la pili la miradi mikubwa ya kilimo kwa asilimia 12 – 16 kwa mwaka na kundi la mwisho ni mikopo ya ushirika ambapo riba yake inaendana na hali ya soko la matumizi ya mkopo. Kuhusu kupunguza riba kwa wakopaji, Dkt. Kijaji alibainisha kuwa majadiliano ya kiwango cha riba yanaweza kufanyika kulingana na historia ya mkopaji.

SERIKALI YAANZISHA MPANGO WA KUTOA MAFUNZO KWA VIJANAKUKIDHI MAHITAJI YA VIWANDA VYA NGUO

April 20, 2018


Mhe. Charles J. Mwijage (Mb), Waziri wa viwanda, biashara na uwekezaji, akizungumza wakati akifungua mkutano wa wadau wa sekta ya pamba na mavazi katika halfa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hazina- Mjini Dodoma leo 20 Aprili, 2018. Picha Zote Na Mathias Canal, NFRA

Baadhi ya wakuu wa mikoa inoyozalisha Pamba kwa wingi wakifatilia mkutano wa wadau wa sekta ya pamba na mavazi katika halfa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hazina- Mjini Dodoma leo 20 Aprili, 2018.
Mgeni-Rasmi Waziri wa viwanda, biashara na uwekezaji, Mhe. Charles J. Mwijage (Mb), akisisitiza jambo wakati akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa sekta ya pamba na mavazi katika halfa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hazina- Mjini Dodoma leo 20 Aprili, 2018.
Naibu waziri wa Kilimo, Mhe. Dkt Mary Mwanjelwa akijadiliana na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Antony Mtaka wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya pamba na mavazi katika halfa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hazina- Mjini Dodoma leo 20 Aprili, 2018.

Waziri wa kilimo, Mhe. Dkt Charles Tizebawakati akifatilia kwa makini mkutano wa wadau wa sekta ya pamba na mavazi katika halfa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hazina- Mjini Dodoma leo 20 Aprili, 2018.

Baadhi ya wadau wa sekta ya pamba wakifatilia kwa makini mkutano wa wadau wa sekta ya pamba na mavazi katika halfa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hazina- Mjini Dodoma leo 20 Aprili, 2018.

Na Mathias Canal, Dodoma

Serikali kwa kushirikiana na viwanda vya nguo na mavazi imeanzisha mpango maalum wa kutoa mafunzo ya ushonaji kwa vijana kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya viwanda vya nguo.

Upatikanaji wa ujuzi wa aina hiyo utapunguza gharama kwa wawekezaji na kuongeza ufanisi katika uzalishaji. Vilevile, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kupitia msaada wa Gatsby Africa, kimeendelea kutoa mafunzo ya Shahada ya Teknolojia ya Nguo (Textile Degree) ambapo, mwaka 2016/2017, Chuo kilitoa wahitimu 44 ikilinganishwa na wahitimu 13 kwa mwaka 2015/2016. Lengo ni kuhakikisha kuwa kuna wataalam wa kutosha wa fani ya ubunifu na uzalishaji mavazi nchini.

Hayo yamebainishwa na Mhe. Charles J. Mwijage (Mb), Waziri wa viwanda, biashara na uwekezaji, wakati akifungua mkutano wa wadau wa sekta ya pamba na mavazi katika halfa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Hazina- Mjini Dodoma leo 20 Aprili, 2018

Alisema kuwa Tanzania ni moja ya nchi zinazozalisha pamba kwa kiasi kikubwa barani Afrika, ikiwa na zaidi ya wakulima 500,000 wanaolima pamba katika eneo linalokadiriwa kufikia hekta 412,000 katika mikoa 13 nchini. Sekta ya nguo na mavazi ni moja ya sekta za Kipaumbele katika kusukuma gurudumu la maendeleo nchini na inahusisha mnyororo mrefu wa uongezaji thamani kuanzia kuchambua pamba (ginneries); kusokota nyuzi (spinning); kuseketa vitambaa (weaving); kufuma vitambaa (knitting), kuchapa na kutia rangi (processing) na kushona mavazi (garments).

Aliongezaa kuwa Sekta hii ni moja ya sekta muhimu katika kutekeleza dhamira ya Serikali ya kuanzisha viwanda vinavyoajiri watu wengi kwa wakati mmoja. Sekta hii itawezesha kupunguza uingizaji wa nguo kutoka nje na kuongeza matumizi ya pamba inayolimwa nchini pamoja na malighafi nyingine zinazopatikana nchini kama vile magadi na gesi asilia.

Hata hivyo, Serikali imeendelea kuzishawishi taasisi za Umma kwa kuanzia majeshi na hospitali ili wanunue nguo na mavazi yanayozalishwa na viwanda vya ndani. Lengo ni kuhakikisha kuwa utaratibu wa makusudi unawekwa kwa Taasisi za umma kutumia bidhaa zinazozalishwa na viwanda vyetu hapa nchini. Kwa mfano uvaaji wa fulana aina ya Polo Shirt kwa wafanyakazi wote katika siku moja ya wiki, na pia wanafunzi wote shule za msingi na sekondari kuvaa sare hizo. Inakadiriwa kuwa kuna jumla ya wanafunzi milioni 15 na wafanyakazi wa sekta zote za umma wanafika 25,000.

Mhe Mwijage alisema kuwa Utengenezaji wa fulana moja ya polo unakadiriwa kutumia wastani wa gramu 300 za pamba, sketi moja inakadiriwa kutumia gramu 600 za pamba, kaptula moja inakadiriwa kutumia gramu 600 za pamba. Hivyo jumla ya gramu 900 za pamba zitahitajika kutengeneza sare kwa mwanafunzi mmoja awe wa kike au wa kiume.

Kama ikikadiriwa kila mwanafunzi atavaa wastani wa sare (sketi & shati au kaptula na shati) mbili tu kwa mwaka gramu 1800 (sawa na kilo 1.8) za pamba zitahitajika kwa mwanafunzi mmoja, hivyo wastani wa kilo 27,000,000 (sawa na tani 27,000) zitahitajika kwa mwaka. Endapo mahitaji yaliyokusudiwa yakipitishwa tunategemea kwamba viwanda vya ndani vitakuwa na uwezo wa kutumia asilimia 17 ya pamba yote inayozalishwa nchini kwa mwaka. Hii itahamasisha uzalishaji wa pamba, kuongeza ajira na kuongeza kipato.

“Serikali inakamilisha taratibu za kuidhinisha ‘’ Blue Print’’ ambayo imeainisha maeneo ya kufanyia maboresho ya Kisera na Kisheria ili kuhamasisha uwekezaji katika Sekta mbalimbali za uchumi ikiwemo sekta ya pamba nguo na mavazi” Alikaririwa Mhe Mwijage

Pia,aliwashukuru Wadau wa sekta ndogo ya pamba, nguo na Mavazi kwa kazi kubwa wanayofanya katika uzalishaji, biashara na wadau wengine kwa michango yao katika kuendeleza sekta hii.

Mkutano huo umehusisha Wizari ya Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara wa Fedha na Mipango, Wizara ya Kilimo; Waheshimiwa Wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge za Viwanda, Biashara na Mazingira; Bajeti; Kilimo, Mifugo na Maji; na Uwekezaji Mitaji ya Umma, Wakuu wa Mikoa; Makatibu Wakuu, Wawakilishi wa Sekta Binafsi, Maafisa wa Serikali na Taasisi za Serikali.

MAADHIMISHO SIKU YA MALARIA DUNIA,KITAIFA KUFANYIKA KASULU MKOANI KIGOMA

April 20, 2018
Tanzania inatarajia kuungana na nchi zingine duniani kwenye kuadhimisha siku ya Malaria Duniani ambayo ufanyika April 25 kila mwaka.

Maadhimisho hayo ya kitaifa yatafanyika wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma huku Waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii akitarajiwa kuzindua ripoti ya hali ya Malaria nchini.

Akiongea jijini Dar es Salaam leo, Waziri Nyoni ambaye ni Mkurugenzi wa Miradi kutoka VectorWorks alisema kutakuwa na shamra shamra mbali mbali kuanzia tarehe 22 April kabla ya kufikia kilele cha maadhimisho hayo.

VectorWorks ni mradi wa miaka mitano wa kupamba na malaria hapa nchini umefadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria na kuratibiwa na John Hopkins Center for Communications.

‘Sisi kazi yetu ni kuhakikisha hali ya ugonjwa wa malaria inapungua. Kwa sababu hiyo, tumekuwa na zoezi endelevu la kugawa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu kwa kila kaya hapa nchini. Vile vile, tunatumia vituo vya afya kuwafikia walengwa wakuu ambao ni akinamama waoenda kliniki na watoto wenye umri chini ya mwaka mmoja, alisema Nyoni.

Akina mama wanaonza kliniki ni lazima wapatiwe chandarua chenye dawa ya muda mrefu bure. Hii njia bora ya kujikinga na mbu waenezao malaria. Vile vile tunafanya kazi kwa kushirikiani na Serikali kupitia Wizara ya Afya kitengo cha kupamba na Malaria nchini ambao wamekuwa wakipuliza dawa yenye viatilifu kwenye maeneo yenye masalia ya mbu.

Tumepiga hatua kubwa kupunguza malaria hapa Tanzania kwa hivyo natoa wito wangu kwa kila Mtanzania kuhakikisha analala kwenye chandarua kwenye dawa ya muda mrefu, aliongeza Nyoni.

Kauli mbiu ya mwaka huu ni mimi natokomeza malaria, wewe je?

-- Ahmad Issa Michuzi Editorial Director P.O BOX 9033, DAR ES SALAAM. issamichuzi.blogspot.com www.michuzijr.blogspot.com othmanmichuzi.blogspot.com Phone:0713 422 313/ 0783 422 313 Tanzania- East Africa.

MAFURIKO JANGWANI KUPATIWA UFUMBUZI

April 20, 2018

Baadhi ya Mawaziri wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika(SADC) wakiwa kwenye majadiliano ya pamoja ambapo walizungumzia vipaumbele vinne, ikiwemo kuendeleza sekta ya viwanda pamoja na kukuza umoja wa kikanda katika sekta ya fedha na uwekezaji, mjini Washington DC Marekani.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akisikiliza majadiliano katika mkutano wa SADC, ambapo alishauri katika utaratibu wa uandaaji wa bajeti ni vyema Mawaziri wa Fedha wakashirikishwa. Kushoto kwake ni Gavava wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Florens Luoga, mjini Washington DC Marekani.

Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia kwa makini majadiliano kati yake na Benki ya Dunia ya namna yakumaliza tatizo la mafuriko eneo la Jangwani jijini Dar es Salaam. Wapili kulia ni Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), kushoto kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Zanzibar Bw. Khamis Mussa Omar na wa kwanza kulia kwake ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Florens Luoga na wa pili kulia kwake ni Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Charles Kichere mjini, Washington DC Marekani.

Ujumbe wa Benki ya Dunia ukiongozwa na Mkurugenzi wa Benki ya Dunia kwa nchi za Tanzania, Somalia, Burundi na Malawi Bi. Bella Bird. (upande wa kulia mwenye scarf shingoni) wakijadiliana na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) namna ya kutatua changamoto za mafuriko eneo la Jangwani, mjini Washington DC Marekani.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Fedha na Mipango)
Na. WFM- Washington D.C

Benki ya Dunia (WB) imekubali kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kukabiliana na athari za mafuriko zinazosababishwa na mvua kubwa zinazonyesha kila mwaka katika Jiji la Dar es Salaam na kuleta madhara makubwa hususan katika eneo la Jangwani jijini humo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) wakati akizungumza na ujumbe wa Benki ya Dunia ulioongozwa na Mkurugenzi wa Benki hiyo kwa nchi za Tanzania, Somalia, Burundi na Malawi Bi. Bella Bird, katika mikutano ya kipupwe inayoendelea mjini Washngton DC.

Dkt. Mpango amesema kuwa Benki ya Dunia imekubali kusaidia kukabiliana na mafuriko katika bonde la mto Msimbazi hasa katika eneo la kutoka Magomeni Mapipa kwendaa Faya na tayari Benki hiyo imeanza zoezi la kutafiti eneo la Jangwani ili kuweza kuangalia namna nzuri ya kugharamia uboreshaji wa mifereji katika bonde la mto Msimbazi ili kumaliza kero hiyo kwa wananchi wa Dar es Salaam.

“Tumewaeleza Benki ya Dunia changamoto hii ambayo imekuwa inajirudia kila mara na kusababisha upotevu wa maisha ya watu, kusababisha kufungwa kwa barabara , watu kushindwa kwenda kazini na wanafunzi kushindwa kwenda shule, hivyo wameonesha nia ya kumaliza kero hii kwa wananchi “ Alisema Dkt. Mpango.

Amesema kuwa baada ya timu ya Benki ya Dunia kumaliza kufanya kazi yao kwa kushirikiana na Manispaa ya jiji la Dar es Salaam, Serikali inaamini njia ya kudumu itapatikana na kuondokana na tatizo hilo la mafuriko ya mara kwa mara katika eneo la Jangwani.