MAFUNZO YAANZA VEMA LIGI KUU ZANZIBAR

September 18, 2014
Na Ameir Khalid, ZANZIBAR
TIMU ya Mafunzo imepata ushindi mwembanba wa bao 1-0 dhidi ya Mtende Rangers katika mechi ya Ligi Kuu Zanzibar uwanja wa Amaan jioni hii.
Mchezaji Sadik Habib ndiye aliyepeleka kilio kwa wakulima hao wa viazi kutoka Mkoa wa Kusini Unguja, akipachika bao hilo mnamo dakika ya 60 ya mchezo akiunganisha mpira wa krosi uliopigwa na mwenzake Ali Juma.
Katika mchezo huo uliopigwa uwanja wa Amaan, timu hizo zilionesha soka la ushindani na kushambuliana kwa zamu, lakini hadi mapumziko milango ilibaki kuwa migumu kufunguka.
Wachezaji wa Mafunzo wakishangilia ushindi wao

Mafunzo iliyoongozwa na Hemed Suleiman ‘Moroko’ kocha wa zamani wa Zanzibar Heroes na Coastal Union, ilicheza kwa kujiamini na kupeleka mashambulizi mengi lakini washambuliaji wake Sadik Habibu na Rashid Abdalla walishindwa kutumia vyema nafasi nyingi walizozipata.
Moroko amepewa jukumu la kuinoa Mafunzo kwa muda kutokana na kocha mkuu wa timu hiyo Mohammed Shaaban ‘Kachumbari’, kulazimika kutokukaa benchi kwa kukosa Leseni C kama agizo la Shirikisho la Soka Afrika linavyoelekeza.
Na katika uwanja wa Gombani Pemba,  wanagenzi wa ligi hiyo Shaba FC, wametoka sare ya 1-1 na maafande wa 1-1 dhidi ya JKU.
Mchezaji Is-hak Othman aliifungia JKU dakika ya 18 kabla Suleiman Ali kuisawazishia Shaba dakika ya 65.
Kesho na Jumamosi ni mapumziko na Jumapili ligi hiyo itaingia mzunguko wa pili kwa mchezo kati ya Shaba na Polisi uwanja wa Gombani, na Miembeni na Chuoni watakipiga uwanja wa Amaan.

MWENYEKITI WA CHADEMA,FREEMAN MBOWE AFIKA MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI KWA MAHOJIANO LEO

September 18, 2014


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe akiwasili kwenye makao makuu ya Jeshi la Polisi nchini,Mapema leo asubuhi tayari kwa kwenda kuhojiwa juu kauli aliyoitoa kwenye Mkutano Mkuu wa chama hicho hivi katibuni,kuwa watafanya maandamano nchini nzima bila kikomo.
 Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),John Mnyika akizungumza na waandishi wa habari waliokuwepo kwenye eneo la makao makuu ya Jeshi la Polisi,juu ya kile kilichokuwa kikiendelea kwenye mahojiani katika ya Mwenyekiti wa Chama hicho na Jeshi la Polisi.Picha na Othman Michuzi.
 Makamu Mwenyekiti wa Chadema,Prof. Abdallah Safari na Wakili wa Chama,Wakili Mabele Marando wakiwasili kwenye Makao Makuu wa Jeshi la Polisi mapema leo.
 Baadhi ya Wachama na Wafuafi wa Chadema wakishangilia wakati Mwenyekiti wao akiwasili kwenye Makao Makuu ya Jeshi la Palisi leo.

Kamishna wa Polisi,CP Paul Chagonja akitoa akiwataka wanachana na wafuasi wa Chadema kuondoka kwenye eneo hilo kwani hakuna sababu ya kufanya fujo.
 Ulinzi mlali katika eneo hilo.
 Amri ikipita ya kuwataka wanachadema kuondoka eneo hilo.
 Askari akiwataka wanachadema kuondoka.

Huyu alikuwa akikaidi amri ya Jeshi la Polisi ilibidi aondolewe kwa nguvu.
 Ulinzi Mkali.
Baadhi ya wanachama wa Chadema wakiondolea ndani la eneo la Makao Makuu wa Chadema.

RAIS KIKWETE AWASILI MAREKANI KUHUDHURIA MKUTANO WA 69 WA UMOJA WA MATAIFA

September 18, 2014


Rais Kikwete akiagana na viongozi mbalimbali waliofika kumuaga katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam Septemba 15, 2014. Kushoto ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali
Rais Kikwete akiagana na viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama waliofika kumuaga katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam Septemba 15, 2014. Kulia ni Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali
Rais Kikwete akisindikizwa na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali wakati alipokuwa anaondoka katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kuelekea Marekani Septemba 15, 2014. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili New York, Marekani. Kulia Mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Tuvako Manongi akifuatiwa na Mama  Upendo Manongi Septemba 16, 2014
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakilakiwa na maofisa mbalimbali wa Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa baada ya kuwasili New York, Marekani, Septemba 16, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakilakiwa na maofisa mbalimbali wa Tanzania  baada ya kuwasili New York, Marekani, Septemba 16, 2014.  PICHA NA IKULU

*WAREMBO WA SHINDANO LA MISS TANZANIA 2014 WATEMBELEA HIFADHI YA MIKUMI

September 18, 2014

 Warembo wanaotarajia kushiriki katika shindano la Miss Tanzania 2014 wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili katika hifadhi ya taifa Mikumi jana ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani nchini. 
 Kaimu Mhifadhi Utalii katika Hifadhi ya Mikumi mkoani Morogoro, Apaikunda Mungure, akiwagawia vipeperushi warembo wa shindano la Miss Tanzania 2014 walio tembelea hifadhi hiyo jana ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani. Vipeperushi hivyo vina taarifa mbalimbali za hifadhi hiyo ya taifa. 
 Kaimu Mhifadhi Utalii katika Hifadhi ya Mikumi mkoani Morogoro, Apaikunda Mungure akiendelea kugawa vipeperushi kwa warembo hao. 
 Mwongoza watalii katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi mkoani Morogoro, Benina Mwananzila  akiwapa maelezo  warembo wa Miss Tanzania 2014 juu ya bwawa la viboko na mamba lililopo katika hifadhi hiyo wakati warembo hao walipo tembelea hifadhi hiyo jana ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani nchini. 

Warembo wa Redd’s Miss Tanzania 2014 wakiwa katika Camp ya Mbuyu iliyopo katika hifadhi ya taifa Mikumi jana walipotembelea hifadhi hiyo ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani nchini. 
Picha na Mpigapicha wetu.