Mfumuko wa bei za  Bidhaa masoko mbalimbali jijini Tanga wapanda

Mfumuko wa bei za Bidhaa masoko mbalimbali jijini Tanga wapanda

July 17, 2013
Na Mwandishi Wetu,Tanga.

MFUMKO wa bei ya kiungo (Nazi) na vyakula kama Ndizi ya mkono wa Tembo jijini Tanga, umepanda maradufu katika masoko mbalimbali hususani katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Uchunguzi uliofanywa na Blog hii katika baadhi ya masoko ya Ngamiani, Mgandini na soko la Makorora  unaonyesha kwamba wafanyabiashara wengi wamepandisha bei za nafaka hususan nazi na ndizi ya mkono wa Tembo.
Bei hizo zimeonekana kupanda haraka kwa kipindi cha mwezi huu mtukufu wa ramadhani ambapo awali bei ya ndizi ya mkono wa Tembo kikonyo kimoja kilikuwa Sh300 hadi 400, lakini sasa imefika sh800 kwa kila kikonyo kimoja, nazi ilikuwa kati ya Sh300 hadi Sh400 na sasa imepanda na kufikia Sh700 hadi Sh1000 kwa kila moja.
Wakizungumza suala la kupanda kwa bei ya Nazi na ndizi ya mkono wa Tembo baadhi ya wafanyabiashara hao wamesema licha ya kuwa huu ni mwezi mtukufu wa ramadhani, lakini kinachochangia pia ni kutokana na halisi ya usafiri na miundombinu ya barabara ambako bidhaa hizo zinakotoka.
“Nikweli kuwa kipindi hiki cha mwezi huu mtukufu wa ramadhani watu wengi wa dhehebu la dini ya kiislamu wanashirki kufunga na hata wengine pesa wanazonunulia futari zinawashinda kutokana na kipato wanachopata hakitoshelezi lakini siyo sisi wafanyabiashara ndiyo tunajipandishia bei hapana bali hata huko tunakokwenda kununua wakulima nao wametupandishia bei,” amesema mfanyabiashara wa Nazi na Ndizi ya mkono wa Tembo aliyejitambulisha kwa jina la Josephat.
Aidha wamesema kuwa bei hiyo ya Ndizi ya mkono wa Tembo na kiungo hicho (Nazi) inaweza kupanda maradufu tena kutokana na hali ngumu ya usafirishaji kutokana na kutopatikana kutoka kwa wakulima mashambani.
                                              (Mwisho).

Ushindi tulioupata Arusha ni ishara ya Kukubalika.

July 17, 2013
Na Mwandishi Wetu,Tanga.
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya Tanga kimesema ushindi walioupata kwenye kata nne za Mkoa wa Arusha katika uchaguzi mdogo wa udiwani mkoani Arusha uliofanyika hivi karibuni ni ishara tosha kuwa chama hicho kinakubalika na wananchi wa mkoa huo.
 
Uchaguzi huo ulifanyika hivi karibuni kwenye kata za Kaloleni,Themi,Kimandulu na Elirahi ambapo chama hicho kiliweza kuchukua nafasi hizo kwa ushindi wa kushindo na kuwabwaga wapinzani wao.
 
Akizungumza na Blog hii, Katibu wa Chama hicho wilaya ya Tanga,Khalid Rashid amesema kuwa licha ya chama hicho kukubalika mkoani humo lakini pia ni ishara tosha kuwa katika ujazo mkuu ujao wa mwaka 2015 vyama vyengine visahau kuchukua nafasi kwenye ukanda wa kaskazini ambapo ndio ngome ya chama hicho.
 
Rashid amewapongeza wananchi wa Arusha  kwa kazi kubwa ya kukiamini chama hicho pamoja na kukupa ridhaa ya kuwaongoza kwani nafasi hiyo inaonyesha ushirikiano ma umoja baina ya viongozi wa kanda na Taifa ilivyoweza kutengeneza mazingira mazuri kuhakikisha wanapata ushindi kwenye uchaguzi huo.
 
Ameongeza kuwa wanaimani kuwa kwa siku zijazo Meya wa Jiji la Arusha atapatikana kupitia chama hicho kutokana na wingi wa idadi ya madiwani waliopo kwenye baraza la madiwani ambapo alisisitiza mshikamano wao ndio ulioleta matokeo mazuri kwa chama hicho.
 
Aidha amesema katika wilaya ya Tanga chama hicho walifanya mikutano sana ya kuhamasisha wananchi kujiunga na chama hicho lengo lilikuwa ni kutengeneza chadema msingi kwa kila mtaa,vijiji na vitongoji ambapo mikutano hiyo waliifanya kwenye kata 7 ambazo ni Mabawa,Msambweni,Duga, Makorora, Central, Chumbageni na Nguvumali lengo likiwa ni kutembelea kata zote 24 za halmashauri ya Jiji la Tanga.
 
Amesema mikutano hiyo ilikuwa na malengo matatu ya kuzungumzia suala la chadema ni msingi na kuzungumzia kuhusu bajeti ya halmashauri ya Jiji la Tanga ikiwemo kupinga kauli ya waziri mkuu ambayo aliitoa bungeni ya sasa hivi watu watakaoleta vurugu wapigwe tu ambapo chama hicho kinaona kitendo hicho serikali haikutenda haki kwa wananchi.
 
Mwisho.