UJUE MTUNGI WA FAYA ULIOJAZWA NA ULIOTUPU/AMBAO GESI IMEKWISHA
Mtungi uliojaa kwa kuzima Moto |
Mtungi ulioactive kwaajili ya kuzima moto mshale wake utakuwa kwenye green (kijani). Ikiwa mshale utakuwa kulia mwa alama ya kijani mtungi huu umejazwa kupita kiasi na ni hatari.Imeandaliwa na RSA na Dj Sek Blog
Huu ni mtungi ambao hauna ujazo wowote na hauwezi kuzima moto kwa namna yoyote ile |
DJ SEK BLOG P.O.BOX Dar es salaam IT DEPARTMENT +255713966552,+255788462579 Web:www.dj-sek.blogspot.com
MWANAHARAKATI KHADIJA LIGANGA ANUIA KUKUSANYA PEDI KWA AJILI YA MABINTI WANAOSOMA.
Kutokana na Wasichana wengi walio
Mashuleni kulazimika kukosa Masomo yao katika Kipindi cha hedhi, Mwanaharakati
wa Kutetea haki za Wanawake na Wasichana nchini Khadija Liganga, amelazimika
kuanzisha kampeni ya kukusanya pedi 3,000 ndani ya mwezi huu ili kuwasaidia
wahitaji.
Akizungumza jana
katika Kipindi cha Passion Break Fast kinachorushwa na Radio Passion Fm ya
Jijini Mwanza, Liganga alibainisha kwamba ameamua kukusanya pedi hizo kutoka
kwa wadau mbalimbali ili kuziwasilisha katika Shule 10 za Msingi na Sekondari zilizo katika Mikoa ya
Mwanza na Mara hii ikiwa ni maalumu kwa ajili ya wasichana wanafunzi ambao
hawana uwezo wa kumudu kununua pedi hizo.
“Tarehe Moja
mwezi wa Kwanza mwaka huu, wanawake tulikutana Jijini Mwanza chini ya mpango
tuliouita Women Round Table kwa ajili ya kupanga mikakati mbalimbali ya
kimaendeleo kwa mwaka huu 2016. Moja ya mikakati niliyoipanga ni pamoja kuanzisha
mradi uitwao Binti Box ambao umelenga kusaidia uchangiaji na upatikanaji wa
pedi kwa ajili ya wanafunzi wenye uhitaji mashuleni pamoja na kuwapa elimu ya
namna ya kujiweka katika hali ya usafi wawapo katika kipindi cha hedhi”.
Alisema Liganga na kuongeza kuwa mpango huo utakuwa endelevu.
Kumekuwepo
na tatizo la wanafunzi wasichana katika maeneo mbalimbali nchini kukosa masomo
yao katika kipindi cha hedhi huku baadhi yao wakilazimika kuacha shule kutokana
na aibu wanayokumbana nayo wawapo shuleni hii ikiwa ni kutokana na kukosa elimu
ya kutosha pindi waingiapo katika kipindi cha hedhi.
Unaweza kuungana
na mwanaharaki huyo kwa kuchangia pedi ambapo anapatikana kwa nambari 0713 093 801
hiyo ikiwa ni kwa wale walio mbali na Jijini Mwanza ama waweza kutembelea ofisi
za Dida Vitenge Wear zilizopo Nganza Sekondari barabara ya kwenda Chuo Kikuu
cha SAUT jirani na ghorofa upande wa kushoto hapo.
Imeandaliwa na George Binagi-GB Pazzo wa Binagi Media Group
SERA YA ELIMU YATAJWA KUCHANGIA TATIZO LA UKOSEFU WA AJIRA KWA VIJANA
Katika kuadhimisha miaka 50 ya mahusiano na ushirikiano baina ya Uswisi na Tanzania, ubalozi wa Uswisi nchini umefanya mdahalo wa wazi kuhusu ajira kwa vijana ulioshirikisha wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi ili kubadilishana mawazo jinsi wao wanavyofanya ili kupambana na tatizo la ajira.
Mdahalo huo ambao ulifanyika katika hoteli ya Coral Beach, jijini Dar es Salaam ulijadili mambo mbalimbali ambayo yanasababisha kuwepo kwa ajira chache lakini pia uwezo wa vijana wa kuingia katika soko la ushindani la ajira.
Aidha mdahalo huo uliweza kujadili kuhusu changamoto iliyopo ya ajira kwa vijana na kuependekeza njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kukabiliana na tatizo hilo ambalo linaonekana kukua kwa jinsi siku zinavyokwenda.
Wakizungumza na Mo Dewji Blog baada ya kumalizika kwa mdahalo huo wadau mbalimbali ambalo walihudhuria walisema kuwa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana linaanzia katika aina ya sera ambazo serikali inazitumia katika sekta ya elimu kushindwa kufanya kazi katika soko la ajira la sasa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze alisema kuwa ili serikali kupunguza tatizo la ajira kwa vijana inatakiwa kuhakikisha inaimarisha uchumi wa nchi lakini ambao unatoa nafasi za ajira zaidi.
Alisema mbali na kuimarisha uchumi pia inatakiwa kuwatengenezea wananchi wake mazingira mazuri ambayo yatawashawishi kujiajiri bila kutegemea ajira ya serikali au makampuni binafsi ambayo kwa sasa ndiyo yanaonekana kutoa nafasi nyingi za ajira.
“Vijana wengi kwa sasa wakimaliza vyuo wanajiajiri na hata kama wanauza barabarani korosho huko nako ni kujiajiri … serikali inatakiwa kuimarisha uchumi wa nchi na sio kukuza tu lakini ukue na utoe fursa za ajira kwa wazawa,” alisema Eyakuze.
Aidha aliwataka vijana kuacha tabia ya kutegemea ajira za serikali na sekta binafsi kwani ushindani katika soko la ajira ni mkubwa na kama wanakuwa hawajajiandaa kwa kiasi kinachohitajika sasa katika soko la ajira basi inaweza kuwa ngumu kwao kupata nafasi.
Nae Amabalis Batamula kutoka Femina alisema sera ambazo zinatumika nchini hazitekelezwi kama zinavyopangwa na serikali na pia hazina faida kwa soko la ajira la sasa kutokana na kubadilika kwa jinsi miaka inavyozidi kwenda.
Alisema ni jambo la ajabu baadhi ya sera za elimu ni kuendelea kutumika hadi sasa licha ya soko la ajira kubadilika na hivyo kuhitaji sera mpya ambazo zinakwenda na wakati lakini pia kuwashauri vijana wanaohitimu kuacha kuishi kwa mazoea na badala yake wawe wakijiajiri ili kuepuka tatizo la ukosefu wa ajira.
Katika taarifa ambayo imetolewa na Shirika la Kazi Duniani (ILO), inaonyesha kuwa zaidi ya vijana 800,000 humaliza chuo kila mwaka na wanaokadiriwa kupata ajira rasmi ni 40,000 pekee hivyo kuonyesha ni jinsi gani kuna upungufu mkubwa wa ajira nchini.
Balozi wa Uswisi nchini, Florence Tinguely Mattli akitoa neno la ufunguzi katika mdahalo huru kuhusu ajira kwa vijana
Wachangia mada katika mdaharo huru kuhusu ajira kwa vijana Baadhi ya washiriki waliohudhuria mdahalo huo Mmoja wa washambuzi wa mada akielezea jambo katika mdahalo huru kuhusu ajira kwa vijana Washiriki wa mdahalo wakiwa katika makundi kujadili mada zilizotolewa[/caption]
Unaweza kusikiliza hapa baadhi ya washiriki waliozungumza na Mo Dewji Blog
ELIMU BORA ITOKANE NA WALIMU BORA - MELISA
Kushoto ni Afisa Elimu wa Shule za Msingi wilaya ya Arumeru Tumsifu Mushi akikabidhi tuzo za Walimu Bora kwa mshindi wa Kwanza Maganga Lorry wa shule ya msingi Mbaaseny ,katikati ni Mkurugenzi wa Shirika lisilokua la kiserikali la The Foundation for Tomorrow (TFFT) ,Melissa Queyquen akishuhudia tukio hilo lililoandaliwa na shirika lake .,jumla ya walimu 200 wameshiriki ambapo walimu 10 walipatia tuzo na zawadi mbalimbali.
Afisa Elimu wa Shule za Msingi wilaya ya Arumeru Tumsifu Mushi akizungumza katika utoaji wa tuzo za Walimu Bora ,,jumla ya walimu 200 wameshiriki ambapo walimu 10 walipatia tuzo na zawadi mbalimbali.Picha na Ferdinand Shayo
Kushoto ni Afisa Elimu wa Shule za Msingi wilaya ya Arumeru Tumsifu Mushi akikabidhi tuzo za Walimu Bora kwa mshindi wa 5 Mwalimu Clara Ernest wa shule ya Msingi Tuvaila ,
katikati ni Mkurugenzi wa Shirika lisilokua la kiserikali la The Foundation for Tomorrow (TFFT) ,Melissa Queyquen akishuhudia tukio hilo lililoandaliwa na shirika lake .,jumla ya walimu 200 wameshiriki ambapo walimu 10 walipatia tuzo na zawadi mbalimbali.
washindi wa tuzo za walimu bora wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Shirika lisilokua la kiserikali la The Foundation for Tommorrow (TFFT) ,Melissa Queyquen akishuhudia tukio hilo lililoandaliwa na shirika lake .,jumla ya walimu 200 wameshiriki ambapo walimu 10 walipatia tuzo na zawadi mbalimbali.
washindi wa tuzo za walimu bora wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Shirika lisilokua la kiserikali la The Foundation for Tommorrow (TFFT) ,Melissa Queyquen akishuhudia tukio hilo lililoandaliwa na shirika lake .,jumla ya walimu 200 wameshiriki ambapo walimu 10 walipatia tuzo na zawadi mbalimbali.
Mkurugenzi wa Shirika lisilokua la kiserikali la The Foundation for Tommorrow (TFFT) ,Melissa Queyquen akizungumza na walimu katika Halfa ya Utoaji tuzo za walimu bora kwa walimu wa shule za msingi wilaya ya Meru zilizofanyika jana ,jumla ya walimu 200 wameshiriki ambapo walimu 10 walipatia tuzo na zawadi mbalimbali.
washindi wa tuzo za walimu bora wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Shirika lisilokua la kiserikali la The Foundation for Tommorrow (TFFT) ,Melissa Queyquen akishuhudia tukio hilo lililoandaliwa na shirika lake .,jumla ya walimu 200 wameshiriki ambapo walimu 10 walipatia tuzo na zawadi mbalimbali.Picha na Ferdinand Shayo
Na Ferdinand Shayo wa Wazalendo 25 Blog ,Arusha.
Serikali
imetakiwa kuboresha mazingira bora ya walimu ili kukuza na kuboresha kiwango
cha elimu nchini kwani walimu ni kiungo muhimu katika elimu ambacho kinapaswa
kupewa kipaumbele kwenye kutimiza azma ya serikali kutoa elimu bora kwa
Watanzania.
Mkurugenzi
wa Shirika lisilokua la kiserikali la
The Foundation for Tomorrow (TFFT) ,Melissa
Queyquen ameyasema hayo jana wakati wa utoaji wa tuzo za walimu bora wa shule
za msingi za serikali kwa kutambua mchango wa walimu katika maendeleo ya elimu
nchini na ustawi bora wa jamii .
Melisa
alisema kuwa maendeleo ya taifa lolote lile yanategemea ubora wa elimu
waliyonayo watu wake hivyo ni vyema serikali inapofikiria kuboresha elimu
ifikirie kuboresha mazingira ya walimu kuanzia kitaaluma wanapoandaliwa kwenda
kufundisha ,vifaa vya kufindishia pamoja na stahiki zao.
“Bila Walimu Bora hakuna Elimu Bora ,Tumeamua
kuwatia moyo wa walimu kwa kutoa tuzo hizi na vyeti vya kutambua mchango wao
,washindi ni 10 mshindi wa kwanza amepatiwa cheti na shilingi la kitano,na
washindi wengine tumewapatia vyeti na fedha taslimu” Alisema Melisa
Afisa Elimu
wa Shule za Msingi Wilaya ya Meru Tumsifu Mushi
amewataka walimu kufanya kazi ya ualimu kwa moyo na kwa kujituma huku
wakitambua kuwa wana wajibu mkubwa wa kuandaa wataalamu watakaoisaidia jamii,taifa
na duni jukumu ambalo ni nyeti linapaswa kubebwa kwa uzito unaostahili.
Kwa upande
wao walimu waliopewa tuzo hizo Rose Salim wa shule ya Msingi Uraki na Ekaeli
Newasha wa Shule ya msingi Kimundo wamesema kuwa kundi la walimu limekua
likisahaulika mchango wake katika jamii hivyo tuzo hizo Zimeamsha ari na hamasa ya kufanya kazi kwa bidii.
“Kazi ya
ualimu unapaswa uwe unapenda watoto
unapenda kuwasaidia waweze kufika mbali kitaaluma ,binafsi nimefanya
kazi hii kwa miaka mingi na ninaipenda sana” Alisema Mwalimu Rose Salim
ASILIMIA 15 YA WANAWAKE NCHINI WAMEGUNDULIKA KUWA WAMEKEKETWA - DK. KIGWANGALA
Na Jumbe Ismaill, Singida
NAIBU
Waziri wa Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto amesema
asilimia 15 ya wanawake wamegundulika kuwa wamekeketwa na kwamba takwimu
hizo zinaonyesha pia kuwa ukeketaji huo umekithiri katika mikoa minane
hapa nchini.
Naibu
Waziri huyo,Dk.Hamisi Kigwangala ametoa takwimu hizo alipokuwa akifunga
kongamano la siku ya kupinga vitendo vya ukeketaji dhidi ya watoto wa
kike na wanawake lililofanyika mjini hapa.
Alifafanua
naibu waziri huyo kuwa takwimu hizo zinaonyesha kwamba ukeketaji huo
umekithiri katika mikoa ya Manyara,Dodoma,Arusha,Singida pamoja na mkoa
wa Mara na kwamba ukubwa wa tatizo hilo katika mikoa hiyo linatokana na
imani na mila potofu.
“Kwa
mujibu wa utafiti wa kidemografia na Afya Tanzania (Tanzania
Demographic and Health Survey) wa mwaka 2010 unaonyesha kuwa asilimia 15
ya wanawake wamekeketwa na kwamba takwimu hizo zinaonyesha ukeketaji
umekithiri katika mikoa ya Manyara asilimia 71”alisema.
Aliitaja
mikoa na asilimia zake kuwa ni mkoa wa Dodoma asilimia 64,Arusha
asilimia 59,Singida asilimia 51 na Mara asilimia 40 huku akiweka bayana
kuwa takwimu hizo zinaonyesha pia ukubwa wa tatizzo la ukeketaji katika
mikoa ya Dar-es-Salaam,Morogoro na Pwani kutokana na watu wa makabila
mbali mbali kuhamia katika mikoa hiyo.
“Serikali
inapinga,kulaani na kukemea tabia ya kuendelezwa kwa vitendo hivi vya
ukatili unaomdhalilisha mtoto wa kike kwani unamsababishia madhara
makubwa kiafya,kielimu, kisaikolojia na kimaendeleo”alisisitiza
Dk.Kigwangala.
Katika
kuhakikisha kuwa suala la udhalilishaji kwa wanawake na watoto wa kike
linazuiwa na kutokomezwa kabisa nchini,Dk.Kigwangala alibainisha kuwa
serikali imesaini na kuridhia mikataba ya kimataifa na kikanda,maazimio
na makubaliano mbali mbali yanayohusu haki na maendeleo ya watoto na
wanawake.
Hata
hivyo Naibu waziri huyo aliitaja baadhi ya mikataba hiyo kuwa ni pamoja
na mkataba wa kimataifa wa Haki za mtoto wa mwaka 1989,Mkataba wa
kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake wa mwaka 1989,mkataba wa
Afrika wa Haki za Binadamu na Haki za watu wa mwaka 1982 na itifaki yake
ya nyongeza inayohusu wanawake wa Afrika wa mwaka 2003 inayopinga mila
zenye kuleta madhara kwa binadamu kama vile ukeketaji.
Akitoa
salamu za shukurani mara baada ya hotuba ya mgeni huyo,Mkurugenzi
Mtendaji wa TAMWA,Edda Sanga aliweka wazi kwamba suala la harakati za
ukeketaji ni harakati ambazo zimeweza kuleta machungu mengi katika
jamii,jambo ambalo linahitaji msukumu mkubwa wa serikali.
Kwa
mujibu wa Mkurugenzi huyo licha ya machungu yanayotokana na vitendo vya
ukeketaji kunakosababisha vilio vya watu kutoka sehemu
mbalimbali,lakini vilio peke yake havitasaidia chochote na kwamba ni
wakati muafaka sasa wa kuchukua hatua za kuhakikisha mila na desturi
zilizopitwa na wakati zinatoweka kabisa nchini.
“Mheshimiwa
Naibu waziri tulilia hapa machozi jana lakini kama unavyojua mheshimiwa
waziri machozi hayatoshi ni lazima tuchukua hatua na hatua ndizo hizo
ambazo umetuahidi hapa,jamani naomba tumpigie makofi mheshimiwa
waziri”alisisitiza Sanga.
baadhi
ya wanaharakati wa mapambano dhidi ya kupinga vitndo vya ukeketaji
kutoka katika mikoa mitano ya Tanzania Bara waliohudhuria kongamano la
siku mbili lililofaanyika mjini Singida.
ASILIMIA 10 YA WATANZANIA WANAMILIKI UCHUMI WA NCHI’
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akifungua Mkutano wa Wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwenye
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam
Februari 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akifungua Mkutano wa Wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwenye
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam
Februari 9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
kaipata maelezo kutoka kwa Bi Fatuma Kango kuhusu Msimbomilia au
Barcode baada ya kufungua Mkutano wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwenye
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar
es slaam Februari 9, 216. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akiagana na Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP na Mwenyekiti wa
Taasisi ya Sekta Binafisi nchini, Reginald Mengi baada ya kufungua
mkutano wa Wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwenye Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari
9, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akimsikiliza Rais wa VICOBA, Devota Likokola (wapili kulia ) wakati
alipotembelea banda la Benki ya Posta Tanzania katika Mkutano wa Wadau
wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi alioufungua kwenye Kituo cha Kimataifa
cha Mikutano cha walimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam Februari 9,
2016. (Picha na Ofisi yaWaziri Mkuu)
…………………………………………………………………………………………………………
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa
amesema Serikali imebuni na kuanza kutekeleza Sera ya Uwekezaji ili
kufikia lengo la kuwawezesha wananchi kiuchumi.
“Taarifa zilizopo zinaonyesha ni
asilimia 10 tu ya Watanzania ndio wanaomiliki uchumi wa nchi na sera
hiyo ndiyo inatoa mwongozo wa jumla unaohakikisha kwamba wananchi
wanapata fursa mbalimbali za kiuchumi ambazo zitawawezesha kujenga na
kufaidika na uchumi wa mchi yao,” alisema.
Waziri Mkuu amesema maeneo
yanayolengwa na sera hiyo ni yale yenye kuleta matokeo ya haraka na
yanayogusa maisha ya wananchi hasa katika sekta za kilimo, ufugaji,
uvuvi, misitu, ujenzi, biashara, utalii, madini, viwanda na
usafirishaji.
Ametoa kauli hiyo leo mchana
(Jumanne, Februari 7, 2016) wakati akizungumza na washiriki wa Mkutano
wa Kwanza wa Wadau wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi nchini uliofanyika
kwenye ukumbi wa kituo cha kimataifa cha mikutano cha mwalimu Nyerere,
jijini Dar es Salaam.
Alisema Dira ya Taifa ya
Maendeleo 2025 inalenga kuhakikisha kuwa sehemu kubwa ya uchumi wa nchi
yetu inamilikiwa na Watanzania wenyewe. Waziri Mkuu pia alizindua
Mwongozo wa Utekelezaji Mkakati wa Taifa wa Uwezeshaji Wananchi
Kiuchumi.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu
kufungua mkutano huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera,
Bunge, Ajira na Walemavu, Bibi Jenista Mhagama alisema hadi sasa mikoa
20 imekwishatenga maeneo ya uwekezaji kwenye halamhashauri zake na
imeanza kuweka miundombinu ya kuvutia wawekezaji.
Naye Mweyekiti wa Baraza la Taifa
la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Prof. Omari Issa alisema katika dunia
ya sasa imebainika kuwa haina maana kumpatia mtu mkopo bila kumtafutia
masoko au kumuunganisha wadau wa masoko. Kwa hiyo wamejipanga kuwasaidia
Watanzania kwa kuwaunganisha na masoko.
WAFANYABIASHARA WAASWA KULIPA KODI.
WAFANYABIASHARA waasa kulipa kodi kwa kuto kulipa kodi ni kinyume
cha sheria kwani huleta kuleta msukumo kwa Mamlaka ya Mapato kukusanya
wa mapato ya serikali ili fedha hizo zitumike kwa matumizi
yaliyokusudiwa.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango wakati akizungumza na wafanyabiashara jijini Dar es Salaam leo.
Pia amesema kuwa wafanyabiashara wanatakiwa kushirikiana na
serikali ya awamu ya tano katika ukusanyaji mapato ili kujenga mazingira
bora ya wafanyabiashara.
Mpango amewaomba wafanyabiashara kutumia mashine za EFD ili
kuongeza mapamo ya serikali wanampango wa kununua Mashine za EFD ili
kuwapa wananchi ambao hawajaanza kuzitumia kwaajili ya kukusanya mapato
ya serikali.
Waziri
wa Fedha na Mipango, Philip Mpango akizungumza na wafanyabiashara leo
katika ofisi za wizara ya Fesha jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni
Makamu Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF), Salum Shamte.
Kutoka kulia ni Naibu waziri wa Fedha na Mipango, Ashantu Kijaji,
katika ni Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo
Kidata na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servacius
Likwelile wakiwa kwenye mkutano wa waziri wa Fedha na Mipango leo jijini
Dar es Salaam.
Makamu
Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF), Salum Shamte akizungumza
na wafanyabiashara waliokusanyika leo katika ofisi za Wizara ya Fedha
na Mipango jijini Dar es Salaam leo.
Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF), Felix Mosha na Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya sekta binafsi (TPSF) wakiwa kwenye mkutano wa wafanyabiashara leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wafabiashara wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mwakilishi wa sekta ya Kilimo Sinari Sinari akizungumzia kuhusiana na sekta ya Kilimo jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugugenzi
wa Bravo Logistics, Angelina Ngalula akizungumza na wafanyabiashara
katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam leo, kuhusiana na
usafilishaji wa mizigo kwa kutumia magari na jinsi adha ya usafari
katika sekta ya usafirishaji hapa nchini.
Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii.
TIGO YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA CHAMA CHA WAANDISHI DODOMA
Meneja Mawasiliano wa Tigo John Wanyancha (Kushoto) akikabidhi vifaa mbalimbali vifaa vya mawasiliano na michezo vyenye thamani ya shilingi milioni nane kwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Dodoma (CPC) Habel Chidawali, ili kufanikisha bonanza la wanahabari la kufunga mwaka 2015 lililopangwa kufanyika baadaye mwezi huu. Makabidhiano hayo yalifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Dodoma.
|
Subscribe to:
Posts (Atom)