DR.Leader aipigia saluti Mganga.

July 04, 2013
 
IMEWEKWA saa 1:15 Mchana.
Na Oscar Assenga, Tanga.
 MSANII wa Muziki wa Bongo Fleva mkoa wa Tanga, Lucas Silas “Dr.Leader”ametamba wimbo wake wa “Mganga” aliouachia hivi karibuni kufanya vizuri kutokana na vionjo vikali ambavyo amevitumia kwenye wimbo huo.
 
Akizungumza blog hii, Dr.Leader ambaye ni msanii mahiri kutunga nyimbi zenye mahadhi ya kipwani alisema katika wimbo huo anaelezea jinsi watu wanaopenda kutamani wake za watu kwa hiyo alienda kwa mganga kumshtaki.
 
Alisema baada ya wimbo huo kuendelea kupigwa katika vituo mbalimbali vya radio hapa nchini lakini pia anatarajia kutoa video ya wimbo huo ambayo itatoka baada ya mwezi wa ramadhani na itakuwa imesheheni vitu mbalimbali.
 
Dr.Leader alisema mpango wake ni kutoa single moja moja kutokana na utoaji wake unakuwa ukilipa sana kuliko kusubiri kutoa album ambazo mara nyingi hushindwa kupata fedha nzuri kutokana na kupata mapato kiduchu.
 
Alisema wanaiomba serikali iangalie hatimiliki za wasanii ili waweze kufaidika na kazi zao ikiwemo kuwasaidia wasanii chipukizi kama zilivyo nchi nyengine duniani kutokana na kuwa na utaratibu mzuri wa kazi zao
 
Hata hivyo,Dr.Leader alitoa wito kwa wasanii wakubwa kuacha kuwabagua chipukizi kufanya nao kazi badala yake washirikiane pamoja lengo likiwa ni kusukuma gurudumu la maendeleo ya mziki huo hapa nchini.
 
Mwisho.
 
POOL Table Tanga kuanza kutimua vumbi leo.

POOL Table Tanga kuanza kutimua vumbi leo.

July 04, 2013
IMEWEKWA:1:12
Na Oscar Assenga, Tanga.
 MASHINDANO ya Pool Table ngazi ya Mkoa wa Tanga yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi leo kwenye ukumbi wa Fax Night Clabu na kushirikisha vilabu kumi kutoka maeneo mbalimbali mkoani hapa.
 
Akizungumza jana, Katibu wa Chama cha Pool Table Mkoa wa Tanga,(TARPA) Shabani Kibelo alisema msimu huu wamejipanga vema kuhakikisha mapungufu yaliyojitokeza mwaka jana hayajirudii katika mashindano hayo lengo likiwa ni kupata  wachezaji wazuri ambao wataunda timu mkoa huo.
 
Kibelo alivitaja vilabu hivyo kuwa ni Hai Pub Club,BP Muheza,Michael Pub,Tanga Beathing Club na Absam Pool Club ambapo vilabu hivyo vitakuwa katika kundi A huku kundi likiwa na High Way Club,Spaider Club,Carribean Club,Kijiti Club na Etu Bomba Fax Club.
 
Katibu huyo alisema mashindano hayo msimu huu yatafunguliwa na Afisa Utamaduni wa Halmashauri ya Jiji la Tanga,Peter Semfuko ambapo pia aliwataka chama hicho taifa kuhakikisha wanawaletea mapema vifaa vya muhimu ikiwemo meza za kuchezea.
 
Aidha aliwataka wadau mbalimbali wa mchezo huo kujitokeza kwa wingi ili kuweza kushuhudia mashindano hayo ambayo mwaka huu yanatarajiwa kuwa na upinzani mkubwa kutokana na timu shiriki kufanya maandalizi mapema.
 
Mwisho.