WAZIRI MWAKYEMBE APOKELEWA OFISINI KWAKE DODOMA

March 29, 2017



 Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof Elisante ole Gabriel akiteta jambo na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe na wakati waziri huyo alipowasili Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe akisalimiana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Anastazia Wambura wakati alipowasili Ofisini kwake Mjini Dodoma.
  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe akisalimiana na baadhi ya wakurugenzi na wakuu wa Taaisi zilizo chini ya Wizara yake wakati alipowasili Ofisini kwake Mjini Dodoma.
  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe akitia saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ofisini kwake Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura akitia saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ofisini za Wizara Mjini Dodoma.
 Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel (aliyesimama) akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe (katikati) kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari kushoto ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Anastazia Wambura.
 Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura(kushoto) akimkaribisha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe (katikati) kuzungumza na waandishi wa habari Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof Elisante Ole Gabriel.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu mikakati yake katika kuiongoza Wizara.
 Baadhi ya wakurugenzi wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt.Harrison Mwakyembe(hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza nao alipowasilikatika Ofisi za Wizara Mjini Dodoma.

Picha zote na Raymond Mushumbusi WHUSM Dodoma.

WADAIWA SUGU NA TANESCO WAONJA JOTO YA JIWE MKOAN KIGOMA

March 29, 2017
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

SHIRIKA la umeme Tanzania TANESCO Mkoani Kigoma imesitisha huduma za umeme kwa Mamlaka ya Maji safi na Mazingira KUWASA, kufuatia deni la umeme la shilingi bilioni 1.3 ambalo halijalipwa tangu mwaka 2013 hadi sasa hali inayopelekea kukosekana kwa Maji Manispaa ya Kigoma na kupelekea dumu moja la maji kuuzwa shilingi 1000.

Akizungumza na Globu ya Jamii,Kaimu Mkurugenzi wa KUWASA, Muhandisi Mbike Jones alisema Mamlaka ya Maji ilikatiwa umeme wiki iliyopita kufuatia deni lililokuwa linadaiwa tangu mwaka 2013 na limeshindwa kulipwa kutokana na Mamlaka hiyo kutegemea fedha hizo kulipwa na Wizara ya maji.

Jones alisema KUWASA ilijitahidi kufanya mazungumzo na TANESCO waweze kurudisha umeme na kudai kuwa ni maelekezo kutoka Makao makuu, mpaka sasa Wizara imejitahidi kufanya mzungumzo na Wizara ya fedha na kudai kuwa watalitatua tatizo hilo baada ya mazungumzo na Shirika la umeme waweze kulipa kidogo kidogo.

Alisema Mpaka sasa KUWASA inadai taasisi za serikali milioni 380 na Wananchi milioni 330, hali inayopelekea kukwamisha zoezi la ulipwaji wa deni hilo kushindwa kulipwa, na aliwaomba Wananchi na Taasisi zinazo daiwa kulipia madeni hayo ili maji yaweze kurudishwa na kuepukana na kero hiyo.

" niwaombe wananchi wawe wavumilivu na waendelee kuchemsha maji wanayo yachota kwenye vyanzo vya maji, ili kuepukana na magonjwa ya milipuko na wawe wavumilivu jitihada zinaemdelea za kuhakikisha tatizo hilo linakwisha na kuendelea kupata maji kama mwanzoni", alisema Jones.

Nao Baadhi ya Wakazi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji , Athumani Rashidi na Destina Paulo walisema kumekuwa na tatizo la maji hali inayopelekea Dumu moja la maji kuuzwa shilingi 1000 hali niyopelekea Wananchi wenye kipato kidogo kushindwa kumudu gharama hizo na kushindwa kununua.

Paulo alisema kwasasa wanalazimika kwenda kuchota maji kwenye mito na Visima vilivyoko mbali na mji kilomita nane kutokea Mjini hali hiyo inawapelekea kushindwa kukabiliana na kero hiyo, na waliiomba serikali na mamlaka inayo husika kuliahughurikia suala hilo ilikuepukana na kero hiyo.


Baadhi ya wakazi kutoka maeneo mbalimbali wakichota maji kwenye vyanzo vya maji vinavyopatikana mjini humo.

REA YAMWONDOA MKANDARASI MZEMBE

March 29, 2017


Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (mwenye kipaza sauti) akiwatambulisha wafanyakazi wa Kampuni ya Nakuroi Investment Co. Ltd (waliochuchumaa), ambao watatekeleza Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijini Awamu ya Tatu mkoani Singida.
Sehemu ya umati wa wananchi waliohudhuria katika hafla ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Singida. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni katika Kijiji cha Mkwese, wilayani Manyoni.
Moja ya vikundi vya ngoma kutoka Manyoni, kikitumbuiza katika hafla ya uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Singida. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni katika Kijiji cha Mkwese, wilayani Manyoni.


Na Veronica Simba – Dodoma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), umesitisha mkataba wa Mkandarasi Spencorn Services, aliyekuwa akitekeleza mradi wa kusambaza umeme vijijini awamu ya pili kwa Mkoa wa Singida.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga aliyasema hayo hivi karibuni katika hafla ya uzinduzi wa mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini awamu ya Tatu katika Mkoa wa Singida, uliofanyika kijijini Mkwese, wilayani Manyoni.

Mhandisi Nyamo-Hanga alimweleza Mgeni Rasmi katika uzinduzi wa Mradi huo, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kuwa, ufanisi wa kazi wa Mkandarasi husika haukuwa mzuri hivyo kusababisha baadhi ya vijiji ambavyo vilipangwa kupelekewa umeme katika REA II, kutofikiwa na huduma hiyo.

“Tumechukua hatua za kinidhamu. Tumemsimamisha kazi na tutaleta wakandarasi wapya ambao wataendelea na kazi ya kusambaza umeme pale alipoishia.”

Aidha, Mkurugenzi Nyamo-Hanga alitoa shukrani kwa Serikali kwa ushirikiano na msaada ambao imekuwa ikitoa, ulioiwezesha REA kuendelea na zoezi la kuwafikishia umeme wananchi wa vijijini kwa mafanikio makubwa.

Alisema kuwa, gharama ya utekelezaji wa REA III Mkoa wa Singida ni shilingi bilioni 47.36 ambapo jumla ya vijiji vitakavyonufaika ni 267. Aliongeza kuwa, Mkandarasi atakayetekeleza Mradi huo ni Nakuroi Investment Co. Ltd.

“Tutaanza na kuunganisha umeme katika vijiji 185 na baadaye tutamalizia vijiji 82 vitakavyokuwa vimebaki, na kuwezesha vijiji vyote vya Mkoa wa Iringa kuwa na umeme kwa asilimia 100.”

Idadi ya vijiji vilivyo na umeme hadi sasa kwa Mkoa wa Singida ni 196, sawa na asilimia 42.

Mhandisi Nyamo-Hanga, amewataka wananchi watakaounganishiwa umeme katika Mradi wa Kusambaza Umeme Awamu ya Tatu, kama ilivyokuwa kwa Mradi wa Awamu ya Pili; kukamilisha utandazaji wa nyaya katika nyumba zao mapema ili wakati mkandarasi atakapofika katika maeneo yao, wawe tayari kulipia na kuunganishiwa umeme.

Vilevile, ameomba Serikali za Kata na Vijiji kubainisha maeneo maalum ya viwanda ambayo katika mradi huu, yatafikishiwa miundombinu ya umeme mkubwa ili kuwezesha wajasiriamali vijijini kupatiwa umeme utakaowezesha kuanzishwa kwa viwanda vidogo vidogo na vikubwa vijijini kwa gharama nafuu.

Uzinduzi wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu, unaendelea katika Mikoa mbalimbali nchini. Mpaka sasa, uzinduzi umekwishafanyika katika Mikoa ya Tanga, Pwani, Dodoma, Iringa, Mbeya, Songwe, Mara na Singida. Kwa Mkoa wa Shinyanga, uzinduzi utafanyika tarehe 1 Aprili, mwaka huu.

MKUU WA WILAYA YA CHEMBA AZINDUA ZOEZI LA UTHAMINI

March 29, 2017
Mkuu wa Wilaya ya Chemba Ndugu Simon Ezekiel Odunga akizungumza na wananchi wa kata ya Farkwa wakati wa uzinduzi wa zoezi la uthamini mali ili kupisha ujenzi wa bwawa la Farkwa.
Mkuu wa Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma akiongozana na baadhi wa Viongozi wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Wataalamu wa Halmashauri, Wataalamu kutoka Wizara ya Maji, Uvuvi na umwaguliaji, Wataalamu wa Bonde la Kati na Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wamezindua zoezi la uthamini wa mali za wananchi wa vijiji viwili vya Mombose na Bubutole watakaohama kupisha mradi mkubwa wa Ujenzi wa bwawa la Farkwa mkoani hapa.

Mradi wa bwawa la Farkwa ni mradi mkubwa ambao huenda ukawa ni mkubwa katika Ujenzi wa mabwawa makubwa kuliko yote barani Afrika. Mradi huu uliasisiwa na baba wa Taifa tangu mwaka 1970 utazinufaisha Wilaya za Bahi, Chemba, Chamwino na Dodoma Manispaa na utegemea kutumia pesa za Tanzania zaidi ya Tilioni 2.

Kufuatia umuhimu wa mradi huu na uwijio wa makao makuu ya nchi mkoani Dodoma, serikali imezamilia ifikapo mei mwaka huu zoezi la Uthamini wa mali za wananchi wanaohama kupisha mradi huu mkubwa katika Vijijini vya Mombose na Bubutole vilivyopo Wilayani Chemba pamoja na vijiji vinavyopitiwa na njia Kuu ya bomba linalopeleka Maji eneo la Kilimani mjini Dodoma liwe limekamilika tayari kwa kuwalipa wananchi ili Ujenzi wa bwawa uanze.

Ujenzi wa mradi huu unategemea kuchukua miaka mitatu 2017-2021 mpaka kukamilika kwake. Hivyo wananchi wametakiwa kutoa ushirikiano kwa Wataalamu wa uthamini kwa kuwa wameusubiri mradi huu kwa zaidi ya miaka 47 na leo serikali imepata fedha ya kuutekeleza.

Mhe Mkuu wa Wilaya ya Chemba Ndugu Simon Odunga wamewataka wananchi hao kujiepusha na watu wasiopenda maendeleo yao na nchi yetu kwa ujumla wa anaopita pita huko na kujifanya watetezi wa haki za wananchi. Swali hao watetezi walikuwa wapi tangu 1970 waje leo ambapo mradi unaanza kutekelezwa.? 

Aidha, amesisitiza wananchi ambao ni wamiliki halali wa maeneo husika ndio wajitokeze kwenye uthamini huo ili kuepusha udanganyifu na migogoro isiyo ya lazima wakati wa malipo yatakopoanza. Kwani kuna baadhi ya wananchi zi waaminifu na atakayefanya hivyo akibaini sheria kali dhidi yake zitachukua mkondo.

Kwa upande wa Wataalamu Mkuu huyo wa Wilaya amewataka kutumia akili, uweledi na taaluma zao katika kuhakikisha kila mwananchi wa maeneo hayo anapata haki yake stahiki kwa mujibu wa sheria za uthamini.

Katika Mkutano huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Mhe Rajabu Muheshimwa ameongea kwa kupongeza juhudi za Serikali kwa kuamua kuanza mradi huu na zaidi kusihi wananchi kutoa ushirikiano kwa Wataalamu, hali kadhalika Mhe Diwani wa Kata ya Farkwa Ndugu, Suleiman Gawa amesisitiza kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu pia Wataalamu wahakikishe wanaorodhesha mali zote za wananchi zinazotambulika kisheria ili kuepusha migongano hapo baadae.

Naye Katibu Tawala wa Wilaya amewataka Viongozi wa Vijiji na vitongoji kusimamia zoezi hili kikamilifu kwani wao ndio wanaowafahamu wananchi wao pia watoto ambao wanamiliki mali lakini hawatambuliwi kisheria kutokana na umri wao.

WAKURUGENZI NCHINI WACHAGUA VIONGOZI WAO MD KAYOMBO JOHN AWA MUWEKA HAZINA

March 29, 2017
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo ambaye kachaguliwa kuwa MUWEKA HAZINA wa Wakurugenzi nchini
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba, ambaye kachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Wakurugenzi nchini
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Ndg Anne Claire Shija (Kushoto) ambaye kachaguliwa kuwa katibu wa Wakurugenzi nchini

Na Mathias Canal, Dodoma

Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na Manispaa kote nchini kwa kauli moja wameridhia na kuwachagua viongozi watakaowawakilisha katika kufikisha changamoto zao mbalimbali katika ngazi za juu ili kupungunza uwasilishaji wa kila Mkurugenzi kufikisha changamoto zake ngazi za juu.

Uchaguzi huo umefanyika hii Leo katika ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma kwa maridhiano ya Wakurugenzi wote kwa asilimia 100% ya kura zote.

Uchaguzi huo umejili Mara baada ya kumalizika kikao cha kazi kilichoongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Eng Musa Iyombe kilichohudhuriwa na Wakurugenzi wote 185.

Wakurugenzi hao wamefanya uchaguzi kwa nafasi nne ambazo ni Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti sambamba na Katibu pamoja na Muweka Hazina.

Wakurugenzi waliochaguliwa katika nafasi hizo ni

1. Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba, ambaye kachaguliwa kuwa Mwenyekiti

2. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Ndg Rachel Chuwa ambaye kachaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti.

3. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Ndg Anne Claire Shija, ambaye kachaguliwa kuwa katibu. Na

4. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo
Ndg John Lipesi Kayombo ambaye kachaguliwa kuwa MUWEKA HAZINA

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Mara baada ya uchaguzi huo kumalizika Viongozi hao waliochaguliwa wameeleza namna bora ya kuhumiza uwajibikaji kwa Wakurugenzi wote sambamba na kuwawakilisha vyema kufikisha changamoto zao kwa ngazi za juu.

Wameueleza mtandao wa www.wazo-huru.blogspotm.com kuwa imani kubwa waliyopatiwa na Wakurugenzi wote nchini ya kuwachagua kuwa wawakilishi wao ni kubwa hivyo wana kila sababu ya kuitumikia kwa weledi na usawa.

"Kupitia Wawakilishi hao waliochaguliwa Wakurugenzi nchini wataraji utendaji uliotukuka na uwakilishi unaostahili kulingana na changamoto zinazowakabili katika maeneo yao" Alisema MD Kayombo John L.

SHIRIKA LA EfG LAPUNGUZA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA SOKO LA MCHIKICHINI NA KISUTU JIJINI DAR ES SALAAM

March 29, 2017
 Mwenyekiti wa Soko la Ilala Mchikichini, Jumanne Kongogo, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu kupungua vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo baada ya kufanyika kampeni mbalimbali za kupinga ukatili huo zilizofanywa na Shirika la Equality for Growth (EfG) kwa kipindi cha miaka mitatu.