PINDA AKUTANA NA MAMEYA NA WENYEVITI WA HALMASHAURI MJINI TANGA
WAZIRI MKUU: OMBEENI TAIFA NA UCHAGUZI MKUU UJAO
*Askofu Niwemugizi ataka UKAWA warudi bungeni mwezi ujao, asema siyo ombi
……………………………………………………………
WAZIRI MKUU
Mizengo Pinda amewaomba viongozi wa dini kote nchini na wananchi
waungane pamoja ili kuombea uchaguzi mkuu wa viongozi wakuu wa Rais,
wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Ametoa wito huo leo mchana
(Jumanne, Julai mosi, 2014) wakati akizungumza na maelfu ya waumini na
viongozi mbalimbali waliohudhuria ibada ya Jubilei ya miaka 25 ya Askofu
Mkuu wa Jimbo Katoliki la Iringa, Mhashamu Tarsicius Ngalalekumtwa
katika uwanja wa Kichangani wa Kanisa Kuu la Kihesa.
“Maaskofu wote mliopo hapa, najua
mnavyoipenda Tanzania… kila kanisa lina sala maalum ya kuliombea Taifa
na viongozi wake, ninawaomba viongozi wetu mliombee Taifa letu ili mambo
yaende salama na hasa uchaguzi wa mwakani,” alisema.
Akirejea mahubiri yaliyotolewa
kwenye ibada hiyo na Mhashamu Askofu Mkuu Paulo Ruzoka wa Jimbo Katoliki
la Tabora ambaye alitoa mfano wa Daudi na Goliathi, Waziri Mkuu
alimfananisha Goliathi na masuala ya rushwa, ubinafsi na tabia ya
viongozi kutojali wananchi wa hali ya chini.
“Viongozi tusipokuwa waadilifu,
tukawa wala rushwa na hatujali wananchi wa hali ya chini tutakuwa sawa
na Goliathi. Nawasihi sana ombeeni Taifa hili na uchaguzi mkuu ujao ili
Mungu atupe Daudi atakayeweza kuliongoza Taifa hili na kulipeleka
kunakostahili,” alisema huku akishangiliwa.
MMILIKI WA MICHUZI BLOG, MUHIDIN ISSA MICHUZI AFURAHISHWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA MFUKO WA PPF KATIKA MAONYESHO YA SABASABA
Afisa
Kanda Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Monica Mbogoni
akimuhudumia mmiliki wa Mtandao wa Michuzi Blog, Ndg Muhidin Issa
Michuzi wakati alipotembelea banda la PPF katika maonyesho ya Sabasaba.
Afisa
Kanda Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Monica Mbogoni
akimuhudumia mmiliki wa Mtandao wa Michuzi Blog, Ndg Muhidin Issa
Michuzi wakati alipotembelea banda la PPF katika maonyesho ya Sabasaba.
Afisa
Kanda Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Monica Mbogoni
akimkabidhi taarifa ya michango mmiliki wa Mtandao wa Michuzi Blog,
Muhidin Issa Michuzi wakati alipotembelea banda la PPF kwenye maonyesho
ya 38 ya Sabasaba. Pembeni wanaoshuhudia ni wafanyakazi wa mfuko wa
Pensheni wa PPF.
Meneja
Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Bi Lulu Mengele (Kulia)
akimkabidhi zawadi Mmiliki wa Mtandao wa Michuzi, Ndg Muhidin Issa
Michuzi wakati alipotembelea banda la PPF katika Viwanja vya maonyesho
ya 38 ya biashara yanayoendelea kufanyika Jijini Dar Es Salaam.Picha
Zote na Josephat Lukaza- Lukaza Blog
COUTINHO AJIPIGA KITANZI MIAKA MIWILI YANGA SC
Kiungo mshamabuliaji Andrey Marcel Ferreira Coutinho raia wa Brazil leo amesaini mkataba wa miwili kuitumikia timu ya Young Africans kwa ajili ya michuano mbalimbali ikiwemo ya Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Tovuti
ya Yanga imemnukuu Katibu Mkuu wa klabui hiyo, Beno Njovu akisema
usajli wa mchezaji Coutinho ni sehemu ya muendelezo wa maandalizi ya
msimu mpya wa Ligi Kuu na kama ilivyokawaida wao mambo yao ni
kimyakimya.
Coutinho ambaye alizaliwa tarehe 12 Januari 1990 amekulia kwenye mji wa Berem ambapo alianza kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Paysandu Sports Club kabla ya kwenda nchini Asia katika nchi ya Myanmar katika klabu ya Rukhapura United.
Mpaka anajiunga na klabu ya Young Africans Andrey Coutinho alikuwa akichezea timu ya Castanhal EC iliyopo kwenye Ligi Daraja la pili ambao aliweza kuichezea kwa michezo yote ya mzunguko wa pili mwaka 2014.
Katika hatua nyingine kikosi cha Young Africans kinatarajia kuendelea na mazoezi kesho chini ya kocha Marcio Maximo katika ufuke wa Coco Beach ikiwa ni siku yake ya kwanza na jioni katika Uwanja wa Bandari Tandika kuanza kazi baada ya leo kuwa na mkutano wa ndani na wachezaji wake pamoja na benchi la ufundi.
Coutinho akisani mbele ya Katibu wa Yanga SC, Beno Njovu |
Coutinho ambaye alizaliwa tarehe 12 Januari 1990 amekulia kwenye mji wa Berem ambapo alianza kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Paysandu Sports Club kabla ya kwenda nchini Asia katika nchi ya Myanmar katika klabu ya Rukhapura United.
Mpaka anajiunga na klabu ya Young Africans Andrey Coutinho alikuwa akichezea timu ya Castanhal EC iliyopo kwenye Ligi Daraja la pili ambao aliweza kuichezea kwa michezo yote ya mzunguko wa pili mwaka 2014.
Katika hatua nyingine kikosi cha Young Africans kinatarajia kuendelea na mazoezi kesho chini ya kocha Marcio Maximo katika ufuke wa Coco Beach ikiwa ni siku yake ya kwanza na jioni katika Uwanja wa Bandari Tandika kuanza kazi baada ya leo kuwa na mkutano wa ndani na wachezaji wake pamoja na benchi la ufundi.
STARS YAJIPIMA KWA BOTSWANA
Timu ya Taifa (Taifa Stars) inacheza mechi ya kirafiki
na Botswana leo (Julai Mosi mwaka huu) kuanzia saa 9 alasiri kwa saa za huko.
Mechi itakayofanyika Uwanja wa Taifa jijini Gaborone
ni sehemu ya maandalizi ya Taifa Stars kwa ajili ya mechi ya michuano ya Afrika
dhidi ya Msumbiji (Mambas) itakayochezwa Julai 20 mwaka huu Uwanja wa Taifa,
Dar es Salaam.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager
inatarajiwa kurejea nchini Julai 6 mwaka huu kuendelea na programu nyingine kwa
ajili ya mechi dhidi ya Msumbiji.
Wakati huo huo, kutakuwa na
utaratibu maalumu kwa waandishi wa habari za michezo kwa ajili ya kuripoti
mechi ya Stars dhidi ya Msumbiji. Hivyo, vyombo vya habari vinatakiwa kutuma
majina mawili ya waandishi watakaoripoti mechi hiyo. Mwisho wa kupokea majina
hayo ni Julai 8 mwaka huu.
WACHEZAJI WATANO WAOMBEWA ITC
Wachezaji
watano wameombewa Hati ya Uhamisho ya Kimataifa (ITC) ili waweze kucheza mpira
wa miguu nchini na nje ya Tanzania.
Abdulhalim
Humoud kutoka Simba, Crispine Odulla (Coastal Union) na Haji Ugando (Mbagala
Market FC) wameombewa ITC na Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kenya (FKF) ili wakacheze
nchini humo katika klabu za Sofapaka, Bandari FC na Nakuru All Stars.
Vilevile TFF
imemuombea ITC mchezaji Ismaila Diarra kutoka nchini Mali ili aweze kujiunga na
timu ya Azam FC. TFF inafanyia kazi maombi hayo, na mara taratibu zote
zitakapokamilika itatoa ITC hizo kwa wachezaji wanaokwenda nje ya Tanzania.
SERENGETI BOYS
YAJINOA KUIKABILI AFRIKA KUSINI
Timu
ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) inaendelea
vizuri na mazoezi kujiandaa kwa mechi ya mashindano dhidi ya Afrika Kusini
(Amajimbos).
Mechi
hiyo ya kwanza ya raundi ya pili itachezwa Ijumaa ya Julai 18 mwaka huu Uwanja
wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili
jioni.
Kocha
Mkuu wa Serengeti Boys, Hababuu Ali Omari ameshafanya mchujo wa awali wa
wachezaji wa timu hiyo kutoka 39 na kubaki na 31. Timu hiyo imepiga kambi
kwenye hosteli ya TFF iliyopo Uwanja wa Karume.
MBEYA CITY,
PRISONS KUJARIBU TIKETI ZA ELEKTRONIKI
Timu
za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) za Mbeya City na Tanzania Prisons zinacheza mechi
ya kirafiki Jumamosi (Julai 5 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine
jijini Mbeya.
Mechi
hiyo ambayo itakuwa ya kwanza kuchezwa jijini Mbeya katika mfumo wa matumizi ya
tiketi za elektroniki kwa washabiki wanaoingia uwanjani itaanza saa 10 kamili
jioni.
Kiingilio
ni sh. 3,000 kwa majukwaa yote ambapo tiketi zimeanza kuuzwa leo (Julai Mosi mwaka
huu).
Wakati
huo huo, keshokutwa (Julai 3 mwaka huu) kutakuwa na mafunzo ya matumizi ya
tiketi za elektroniki yatakayofanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini
Mbeya kuanzia saa 3 asubuhi.
Washiriki
wa mafunzo hayo ni wasimamizi wa mechi katika uwanja huo, viongozi wa Chama cha
Mpira wa Miguu Mkoa wa Mbeya (MREFA), meneja wa Uwanja wa Sokoine na msaidizi
wake, makatibu wa Tanzania Prisons na Mbeya City, maofisa habari wa Mbeya City
na Tanzania Prisons, Ofisa Usalama wa MREFA na wasimamizi wa milangoni
(stewards).
BONIFACE WAMBURA MGOYO
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Subscribe to:
Posts (Atom)