WAZIRI MAHUNDI AITAKA UCSAF KUTANGAZA SHUGHULI KUPITIA VYOMBO VYA HABARI

September 10, 2024

 

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) akizungumza wakati wa ziara yake katka Ofisi za Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Kanda ya Pwani ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo pamoja na taarifa ya kina ya mradi wa Tanzani ya Kidijitali wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano vijijini, Mikocheni jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Septemba, 2024.
Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) akipokea taarifa kutoka kwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Mhandisi Peter Mwasalyanda kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo pamoja na taarifa ya kina ya mradi wa Tanzani ya Kidijitali wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano vijijini wakati wa ziara yake katika ofisi hizo za Kanda ya Pwani zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Septemba, 2024.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) akizungumza wakati wa ziara yake katka Ofisi za Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Kanda ya Pwani ya shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo pamoja na taarifa ya kina ya mradi wa Tanzani ya Kidijitali wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano vijijini, Mikocheni jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Septemba, 2024.

Na Mwandishi Wetu.

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb), amewataka viongozi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) kutumia vyombo vya habari ili kutangaza shughuli mbalimbali zinazofanywa na mfuko huo.

Mhandisi Mahundi amesema hayo tarehe 10 Septemba, 2024, wakati wa ziara yake katika ofisi za UCSAF Kanda ya Pwani zilizopo Mikocheni, jijini Dar es Salaam, ambapo alikagua shughuli mbalimbali pamoja na mradi wa Tanzania ya Kidijitali wa ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano vijijini.

 “Mahusiano na vyombo vyetu vya habari ni muhimu, Ukifanya kazi ukikaa nayo, hakuna atakayejua umefanya hivyo. Ni muhimu kuvishirikisha katika utekelezaji wa shughuli zenu mbalimbali,” amesisitiza Mhandisi Mahundi.

Aidha, Naibu Waziri huyo amehimiza UCSAF kuwashirikisha viongozi mbalimbali, wakiwemo wabunge, wanapotoa huduma za mawasiliano katika maeneo yao. 
Amesema kuwa kufanya hivyo kutasaidia katika kupata taarifa sahihi za maendeleo katika maeneo husika.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Mahundi amesisitiza umuhimu wa kuongeza kasi katika ujenzi wa minara 758 ya mawasiliano vijijini, akieleza kuwa kumekuwa na mahitaji makubwa ya mawasiliano katika maeneo mengi.

Kwa upande wake, Kaimu Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Mhandisi Peter Mwasalyanda, amesema tayari wameshakaa kikao na kampuni za simu na kuweka utaratibu mzuri wa kukamilisha ujenzi wa minara hiyo, pamoja na kuongeza nguvu katika kutoa elimu kwa umma kuhusu shughuli zinazofanywa na mfuko huo.

FUNGUO na IMBEJU: Ushirikiano wa Kipekee Kukuza Ufadhili kwa Wajasiriamali Wabunifu wa Tanzania

September 10, 2024
Tanzania, 10 Septemba 2024. Mradi wa Ubunifu wa FUNGUO unaotekelezwa na UNDP hapa Tanzania kwa ufadhili wa na Umoja wa Ulaya na mfuko waIMBEJU wa CRDB Bank Foundation, imeamua kushirikiana ili kubadilisha mwenendo wa ufadhili wa wajasiriamali wabunifuhapa nchini. 
Ushirikiano huu wa kimkakati unalenga kutumiaruzuku inayotolewa na Umoja wa Ulaya kwa kampuni changa nakufungua fursa ya kupata mikopo ya riba na masharti nafuukutoka kwa CRDB Bank Foundation, ili kuongeza uwezo wakimtaji kuwawezesha wajasiriamali kukua kwa haraka zaidi. 

Tangu kuanziswa kwake mwaka 2022 kwa ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya kupitia mpango wa BEGIN unaoratibiwa na kitengacha mazingira ya biashara katika Ofisi ya Rais – Mipango naUwezeshaji, FUNGUO imewekeza zaidi ya TZS bilioni 3.8 katika kampuni changa 43, ikichangia katika kutengeneza nakuendeleza takribani ajira 4000 za moja kwa moja na zisizo za moja kwa kwa vijana wa Tanzania.
Dhamira ya mpango huu nikuongeza idadi ya kampuni za ubunifu zenye uwezo wa kustawiharaka ili kuharakisha kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevuya Tanzania. Wafadhili wengine wa mradi wa FUNGUO nipamoja na Serikali ya Uingereza kupitia mpango wa Africa Technology and Innovation Partnerships (ATIP) na UNDP katikamkakati wake wa kuwawezesha vijana kiuchumi.

Mwaka huu, FUNGUO imepanga kutoa hadi TZS bilioni 1.4, ikilenga kwa makusudi kuwawezesha wanawake walioanzishabiashara zenye ubunifu ndani yake. Angalau asilimia 40 yaufadhili uliopo umetengwa kwa ajili ya biashara zinazomilikiwa na kuongozwa na wanawake, ikiwa ni ongezeko la asilimia 30 ukilinganisha na mwaka jana, ili kutilia mkazodhamira ya ujumuishi wa kijinsia na kuunga mkono uongozi wawanawake katika ubunifu.

Ufadhili huu unalenga biashara changa bunifu zinazoongozwa na vijana ambazo zinamilikiwa kwa wingina raia wa Tanzania.

FUNGUO na IMBEJU hazitoi tu msaada wa kifedha, bali pia zinawawezesha wajasiriamali vijana, wanawake, na makundimaalum kwa kuwapa zana muhimu za kubadilisha mawazo yaoya biashara kuwa miradi yenye mafanikio na yenye athari kubwakwa jamii. 

Ufadhili wa mwaka huu kutoka FUNGUO naIMBEJU utawekeza katika kujenga mchakato unaovutia mifumomingine ya kifedha nchini, ikiwemo wawekezaji binafsi na taasisinyingine za kifedha.
Katika hotuba yake kama Mgeni Rasmi, Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo (MB), Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji, alieleza kuwa "Vijana wa Tanzania nirasilimali kubwa kwa taifa, wamejaa mawazo ya kibunifu namaarifa ya kutengeneza mustakabali ulio bora zaidi kwa taifaletu. 

Kwa kuwawezesha na mitaji ya kuanzisha na kuendelezabiashara zao, msaada wa kitaalamu, mafunzo, na kadhalika, vijana wetu wanakuwa wamepata zana wanazohitaji kujengabiashara zenye mafanikio na zinazoweza kukua kwa haraka nakuchangia uchumi. 

Hili ni muhimu tunapolenga kukuza sektabinafsi yenye nguvu inayoweza kutengeneza ajira nakuhamasisha ibunifu katika uchumi wetu. Ningependakuwashukuru washirika wetu wa maendeleo, Umoja wa Ulaya, Serikali ya Uingereza na UNDP kwa kuunga mkono miradi yaaina hii."
Bi. Christine Grau, Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Tanzania, amesisitiza dhamira ya Umoja wa Ulaya katika kukuza mazingiraya biashara yanayochochea ukuaji wa ubunifu nchini Tanzania. "Ni dhahiri ya kuwa Mpango wa FUNGUO ni ushahidi wakujitolea kwetu kusaidia wajasiriamali wa Kitanzania kufikiamafanikio. 

Tunaamini ushirikiano huu na IMBEJU utaimarishamfumo wa ujasiriamali nchini Tanzania, ukileta manufaa halisikwa wajasiriamali na uchumi kwa ujumla," alisema.
Kwa upande wake Bw. Muyeye Chambwera, Naibu Mwakilishi Mkazi wa UNDP Tanzania, alionyesha dhamira yaUNDP ya kuwawezesha vijana kupitia mipango mbalimbali. 

Bw. Chambwera alisema kuwa "UNDP imejitolea kusaidia vijanakutambua uwezo wao, na kufungua milango ya upatikanaji wafedha kupitia miradi yao. Tunaamini tunaweza kuleta atharikubwa kupitia ushirikiano huu na CRDB Bank Foundation ambaoni ushahidi wa juhudi nyingi tunazofanya kufungua milango zaidiya kufanya kazi pamoja na wadau mbalimbali."
Naye Bi Tully Esther Mwambapa, Mkurugenzi Mtendaji waCRDB Bank Foundation, alisisitiza uwezo wa mabadiliko waushirikiano huu kwa biashara za vijana. 

"Mpango wa IMBEJU umejizatiti kwa dhati kuwawezesha kizazi kijacho cha wajasiriamali wa Kitanzania. Kwa kuunganisha ujenzi wa uwezo, elimu ya kifedha, na maendeleo ya ujuzi wa ujasiriamali, IMBEJU haipatii msaada wa kifedha tu, bali tunatoa mfumokamili utakaokuza vipaji vya vijana. 
Ushirikiano huu na FUNGUO unaongeza juhudi zetu za kuboreasha mazingirayanayosaidia biashara zinazomilikiwa na vijana kufanikiwa.

Tunaamini kuwa kwa kuwapa wajasiriamali vijana zanawanazohitaji, tunajenga msingi wa mazingira thabiti na endelevuya ujasiriamali nchini Tanzania," alisema Bi. Mwambapa.

Wakati wa kutambulisha Mpango wa FUNGUO, Joseph Manirakiza, Meneja wa Mpango, alisisitiza njia jumuishi yakusaidia wajasiriamali. "FUNGUO haitoi ruzuku za mitaji, balitumewekeza pia kwenye mfumo mpana wa kustawishaujasiriamali na ubunifu, unaojumuisha usaidizi wa kiufundi, ushauri, na fursa za kujenga mitandao.
Lengo letu nikuwawezesha wajasiriamali wa Kitanzania kukabiliana nachangamoto huku tukitumia njia zote zinazowezekana ili biasharazao ziweze kufikia ukuaji endelevu. Ushirikiano wa kimkakatikama huu na CRDB Foundation unatufanya twende hatua mojambele zaidi ya kufungua uwezo kamili wa biashara za ubunifu nchini Tanzania," alielezea.

Bw. Richard Craig, Mkuu wa Idara ya Uchumi katika Ubalozi waUingereza, alisisitiza dhamira ya Uingereza ya kuendelea kushirikiana na Tanzania kwa ajili ya kuhakikisha Uchumi wanchi unakua. Akizungumza katika uzinduzi huo, alisema: "Programu ya FUNGUO ni sehemu ya ushirikiano mpana wakiuchumi kati ya Uingereza na Serikali ya Tanzania, kamailivyoainishwa katika Ushirikiano wetu katika Ufanisi waPamoja. Biashara changa bunifu ni muhimu katika njia ya ukuajiwa uchumi shirikishi. 
Tunaposaidia biashara hizi, tunaongezauwezo wa kutengeneza ajira na kuchochea suluhisho zilizo za kibunifu katika kukabiliana na changamoto zinazotucheleweshakufikia maendeleo maendeleo."

Dirisha la maombi ya ufadhili huu litafunguliwa rasmi kuanziatarehe 10 Septemba 2024 hadi tarehe 09 Oktoba 2024. Biasharazenye ubunifu (startups) na SMEs zinazostahiki zinahimizwakuomba na kutumia fursa hii kupata ufadhili na msaada wakukuza biashara zao zinazochochea mabadiliko katika jamii.






I VIVUTIO VYA UTALII 187 VYASAJILIWA KWENYE MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI (NaPA) VYOMBO VYA HABARI

September 10, 2024

 

Na Mwandishi Wetu, WHMTH, Arusha.

Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH) kwa kushirikiana na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, kupitia mradi wa Anwani za Makazi (NaPA) imefanikiwa kusajili anwani za makazi za vivutio vya utalii 187 na barabara zaidi ya 60 zinazopatikana ndani ya Hifadhi tatu zilizofanyiwa kazi.

Katika zoezi hilo lililoendeshwa katika Hifadhi za Taifa za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire, WHMTH imefanikiwa pia kusajili huduma 221 na kujenga uelewa wa Mfumo wa NaPA na umuhimu wake kwa Menejimenti zote za Hifadhi husika.

Hayo yamebainishwa tarehe 10 Septemba, 2024 na Mratibu wa kitaifa wa Mradi huo kutoka WHMTH, Mhandisi Jampyon Mbugi kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la usajili wa Vivutio vya Utalii katika Mfumo wa NaPA kwenye Hifadhi za Taifa.


Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakiwa kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.

Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakifuatilia wasilisho kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.



Viongozi na Wataalamu wa Mfumo wa Anwani za Makazi kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari (WHMTH), Wizara ya Maliasili na Utalii (WMU) na Wahifadhi na Viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania-TANAPA, wakifuatilia wasilisho kwenye kikao cha majumuisho ya zoezi la ukusanyaji wa taarifa za Anwani za Makazi lililofanyika awamu ya kwanza katika Hifadhi za Arusha, Ziwa Manyara na Tarangire tarehe 10 Septemba, 2024 mkoani Arusha.





Katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wataalamu wa Mfumo wa NaPA, baadhi ya Wahifadhi, Viongozi wa TANAPA na Wawakilishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mhandisi Mbugi amesema, ukamilishaji wa zoezi hilo utawezesha kuwa na taarifa nyingi za vivutio hivyo na kuzidi kuvitangaza ili kuwavutia watalii kufika na kuvitembelea.

Kuhusu uwekaji wa miundombinu katika maeneo ya Hifadhi, Mhandisi Mbugi amesema, kwa kuwa NaPA una sehemu mbili, yaani kidijitali (digital part) na miundombinu (Physical infrastructure), ni muhimu sehemu ya miundombinu ikafanyiwa kazi kwa kuweka kulingana na taarifa zilivyoingizwa kwenye Mfumo wa NaPA, kwani kwa sasa taarifa zimekusanywa kwenye mfumo wa kidigitali pekee.

Amesema, kuweka mfumo wa miundombinu kutamrahisishia mtalii au askari kutambua na kuona kwa urahisi eneo alilohitaji kulitembelea au kulifanyia kazi.

Aidha Mhandisi Mbugi amesema, ili kuhamasisha matumizi ya Mfumo wa NaPA kwa watalii, ni muhimu TANAPA ikashiriki kikamilifu kutangaza na kuhamasisha matumizi yake katika masuala ya utalii kuwezesha kufikiwa kwa malengo na kupata manufaa yanayokusudiwa.

Ameshauri picha za vivutio ziwekwe kwenye Mfumo wa NaPA ili kumvutia Mtalii anapotafuta taarifa za Hifadhi husika kama picha hizo zinavyowekwa kwenye Mitandao (Website) za Hifadhi, na kusisitiza kuwa, uwekaji wa Miundombinu ya Anwani za Makazi katika majengo ya Ofisi, mageti na hoteli, uzingatie Pia Makazi wa Mwaka 2016, isipokuwa kwa maeneo mengine, uzingatie Sheria, Kanuni na Miongozo ya uhifadhi.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Bw, Ignace Gara ameipongeza Wizara kwa utekezaji wa zoezi hilo na kwamba siyo tu ni msaada katika kutangaza utalii bali pia una faida katika ulinzi na uhifadhi wa wanyama adimu.

COSTECH WAZINDUA PROGRAM MBILI KUINUA WASICHANA NA WANAWAKE KIDIJITALI

September 10, 2024

 

KATIKA kuwasaidia Wasichana na Wanawake kumudu maisha na kuisaidia jamii Tume ya Sayansi na Teknolojia ( Costech), imezindua Program mbili kwa ajili ya kuwajengea uwezo kidijitali.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Septemba 10, 2025 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Costech, Dkt. Amos Nungu amesema kuwa Program hizo ni kwa ajili ya wasichana ambao hawakumaliza masomo yao na Wanawake wenye mawazo au biashara zinazohusiana na Teknolojia.

Lengo ni kuwapa ujuzi na taaluma ya kiteknolojia ili waweze kuja na biashara ambazo zinaweza zikasaidia waweze kumudu maisha yao, na wasaidie jamii.

Dkt. Nungu amesema Program ya kwanza inajulikana kama 'Future Femtech' inayowasaidia wanawake wenye kampuni changa au mawazo machanga ya kiteknolojia.

Amesema Program ya pili ijulikanayo kama 'Kuzatech' inaangalia mabinti ambao walikuwa shule lakini kwa namna moja au nyingine wakashindwa kuendelea na masomo hivyo wamewapa fursa ya kupata mafunzo kidijitali.

"Sasa hizi Program mbili tunazifanya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo,"amesema.

Nungu amesema Kuzatech wataunganika na Future Femtech ambao baadhi yao ni wahitimu wa vyuo vikuu wenye mawazo ya biashara ambapo wadogo wanapata fursa ya kuungana na hawa wakubwa ili waweze kupata mafunzo yatakayowasaidia kuwa nankitu cha kufanya.

Kwa upande wake Meneja Usimamizi na Uhaulishaji Teknolojia Costech, Dkt. Erasto Mlyuka amesema Program hiyo ya Future Femtech inawalenga wasichana ambao wamekuwa ni waanzilishi wa kampuni changa.

Amesema hupewa msaada wa kitaalam kwa maana ya mafunzo elekezi ya kujengewa uwezo pia kupewa fedha za kuwawezesha kufanya biashara zao.

Amesema program hizo zitatengeneza ajira kwa wanawake ili na wenyewe wapate nafasi ya kuchangia kwenye pato la nchi kwa kuwa na kipato halali.

Mbunifu kutoka Arusha, ambaye ni mnufaika wa Future Femtech, Pamela Chogo amesema mafunzo aliyoyapata ni chachu kubwa kwenye ubunifu wa biashara.

Amesema Program hizo ni muhimu kwa sababu zinasaidia kupata elimu ya ujasiriamali.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu mbili ambazo ni Femtech na Kuza femtech ambazo zitawasaidia wanawake. uzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam leeo Septemba 10, 2024.
Meneja Usimamizi na Uhaulishaji Teknolojia Costech, Dkt. Erasto Mlyuka akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu kwaajili ya wasichana na wanawake jijini Dar es Salaam leo Septemba 10, 2024.






Picha ya Pamoja

WAZIRI WA AFYA ATEMBELEA MUHIMBILI UPANGA NA MLOGANZILA, ASEMA SERIKALI KUENDELEA KUENDELEA KUBORESHA UBORA WA HUDUMA NCHINI

September 10, 2024


WAZIRI wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali itaendelea kusimamia ubora wa huduma zinazotolewa kwa wananchi ili kuhakikisha kuwa kila mtanzania anapata huduma bora za afya popote alipo na kwa wakati.

Mhe. Mhagama ametoa kauli hiyo mapema leo, alipofanya ziara katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila kwa lengo la kujionea namna hospitali hiyo inavyotoa huduma, ambapo ameupongeza uongozi na watumishi wa Muhimbili kwa namna wanavyotoa huduma za uchunguzi na matibabu kwa wananchi kwa kuzingatia weledi ubora unaotakiwa.

Mhe. Mhagama amesema kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa ndani ya miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ujenzi wa miundombinu, vifaa tiba vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu na kusomesha wataalam imewezesha wataalam hao hususani wa Muhimbili (Upanga &Mloganzila) kutoa huduma za ubingwa bobezi na kupunguza rufaa za kwenda nje ya nchi kwa matibabu.

“Sekta ya afya hapa Tanzania ndani ya miaka hii mitatu imekuwa kuliko kipindi chochote kwani katika hospitali zetu za Taifa na kipekee Muhimbili tunazo zaidi ya aina 35 za matibabu ya ubingwa bobezi ikiwemo upandikizaji wa uloto, upandikizaji wa figo, matibabu ya magonjwa ya moyo n.k, uwekezaji ambao unaacha deni kwetu la kutoa huduma bora kwa Watanzania wenzetu ili waweze kufurahia matunda ya uwekezaji huo” amebainisha Mhe. Mhagama

Aidha, Mhe. Mhagama ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutoa motisha na kuwajengea uwezo wataalam ili waweze kwenda sambamba na mabadiliko yanayotokea duniani kwa lengo la kuendelea kuimarisha utoaji wa matibabu hapa nchini kadiri mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanavyojitokeza duniani.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini MNH Dkt. Ellen Senkoro amemuhakikishia Mhe. Waziri kuwa bodi itashirikiana na menejimenti kuhakikisha kuwa wanatafsiri kwa vitendo maono ya Mhe. Rais na maelekezo ya wizara hatimaye watu wote wanaotibiwa Muhimbili wapate huduma bora na zenye kukidhi matarajio yao.

Mhe. Waziri katika ziara yake ameambatana na viongozi mbalimbali wa Wiraza ya Afya akiwemo Naibu Katibu Mkuu Bw. Ismail Rumatila pamoja na baadhi ya wakurugenzi wa wizara hiyo.






MAONESHO YA MIFUKO YA UWEZESHAJI FURSA KWA WANANCHI SINGIDA

September 10, 2024
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge na Uratibu) Mhe William Lukuvi akizingumza wakati akifungua maonyesho ya saba ya mifuko na programu za uwezeshaji wananchi kiuchumi mkoani Singida leo Septemba 10,2024

NA; MWANDISHI WETU – SINGIDA


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. William Lukuvi amefungua rasmi Maonesho ya Saba ya Mifuko na Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Mkoani Singida ambayo yanaratibiwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC)

Wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo, Mheshimiwa Lukuvi amesema kuwa maonesho hayo yatafungua fursa za Kiuchimi  kwa wafanyabiashara, wakulima na wafanyabiashara wa Singida na Mikoa ya Jirani. 

Waziri Lukuvi Aliongeza kuwa, Maonesho hayo yatawezesha wananchi kupata huduma za uwezeshaji ikiwemo mitaji, mikopo nafuu, dhamana za mikopo, vifaa, mashine au mitambo, urasimishaji ardhi,urasimishaji biashara, huduma za msimbomilia, ujuzi, ithibati ya bidhaa, huduma za sheria, huduma za ushirika, huduma za ushauri wa kitalaam, elimu rasmi na elimu ya ufundi stadi, kuunganisha wananchi na fursa,na ukaguzi wa bidhaa.

Mhe. Lukuvi alibainisha kuwa, Maonesho hayo ni muhimu kwa kuwa yanakutanisha wadau mbalimbali wa uwezeshaji wakiwemo, Wizara, Mikoa, Halmashauri; Taasisi zinazosimamia Mifuko na Programu za Uwezeshaji, Taasisi za Fedha, Wafanyabiashara, Kampuni, Taasisi za Elimu na Tafiti, Wakulima, Wafugaji,na Wajasiriamali.

Aliongeza kuwa, Maonesho hayo yana lengo la kuhakikisha kuwa washiriki wanabadilishana ujuzi, maarifa, uzoefu na teknolojia mbalimbali ambazo zinatumika katika kukuza ushiriki wa wananchi katika shughulli za kiuchumi.

 “Nina imani kuwa, Maonesho haya yatatoa fursa nyingi kwa wananchi wa Mkoa wa Singida na Mikoa mingine.” Alisisitiza 

Akiongea kwa Niaba  ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge naa Uratibu), Dkt. Jim Yonazi, Mkurugenzi wa Idara ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Maendeleo ya Sekta Binafsi, Bw. Condrad Milinga amesema kuwa pamoja na  maonesho hayo kutoa fursa mbalimbali kwa wajasailiamali, wananchi pia watapata mafunzo na ujuzi kuhusu masuala mbalimbali kutoka kwa Washiriki wa Maonesho na kutoa wito kwa wananchi kutembelea maonesho hayo.

Kwa Upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi (NEEC), Bi Beng’ Issa amesema kuwa kwa miaka mingi Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali za kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa lengo la kujenga uchumi na kuwaondoa wananchi katika umaskini.
“Juhudi hizo ni pamoja na kuanzisha mifuko na program za uwezeshaji mbalimbali kwa lengo la kutoa mikopo au dhamana ya mikopo kwa wananchi kwa masharti nafuu, kutoa ruzuku pamoja na kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi ili waweze kukopesheka au kuhudumiwa na wadau wengine.” Alibainisha

Aliendelea kufafanua kuwa, mpaka sasa Baraza linaratibu Jumla ya Mifuko ya Uwezeshaji na Programu 72 ambayo 62 ipo Serikalini na 10 ipo Sekta binafsi, hivyo Lengo kuu la Maonesho haya ni kutoa uelewa wa fursa za Mifuko kwa Wananchi ambapo ilionekana mifuko mingi haifahamiki kwa wananchi hivyo kuchelewesha kufikisha huduma za uwezeshaji kwa wananchi.

 Maonesho hayo ya siku Saba yaliyofunguliwa leo Mkoani Singida yana Kaulimbiu inayosema “Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Unufaike na Fursa za Uwezeshaji”