SSRA YASHIRIKI MAONYESHO YA MAADHIMISHO YA SIKU YA USALAMA NA AFYA MAHALA PA KAZI MJINI MOSHI MKOANI KILIMANJARO

April 29, 2017
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi, na Watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama, akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Meneja wa Rasilimali watu na Utawala wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Bi Amina Ally aliotembelea banda la SSRA wakati wa Maonyesho ya Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa kazi (OSHA) yanayoendelea mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama akiatoa maelekezo wakati alipotembelea banda la Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kwenye Maonyesho ya Maadhimisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa kazi (OSHA) yanayoendelea mjini Moshi mkoani Kilimanjaro. 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu, Mh. Jenista Mhagama, akimkabidhi cheti cha Ushiriki Kaimu Meneja wa Rasilimali watu na Utawala wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA). Bi. Amina Ally wakati wa kilele cha maonesho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayoendelea Mjini Moshi, mkoani, Kilimanjaro.   
Afisa Matekelezo wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), akigawa vipeperushi kwa wananchi waliotembelea banda la SSRA wakati wa Maonesho ya OSHA yanayondelea Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro. 
Afisa Uhusiano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Ally Masaninga akitoa maelezo kwa wananchi waliotembelea banda la SSRA, wakati wa Maonesho ya OSHA yanayondelea Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro. 
Maafisa wa SSRA, wakitoa ufafanuzi juu ya Masuala yanayohusu Sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa wadau waliotembelea banda la mamlaka hiyo, wakati wa Maonesho ya OSHA, yanayoendelea Mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Wananchi wakisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa wa SSRA, wakati wa maonesho ya OSHA, yanayofanyika mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro. 
Wadau waliotembelea banda la SSRA, wakijipatia vipeperushi wakati wa maonesho ya Maadhmisho ya Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi yanayofanyika Mkoani Kilimanjaro.

RAIS DKT MAGUFULI APOKELEWA KWA SHANGWE NA NDEREMO MKOAN KILIMANJARO

April 29, 2017




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Kamnda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Hamisi Issa alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongiozana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Rais wa TUCTA Bw. Tumaini Nyamhokwa alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aiiongiozana na Waziri Mkuu Mhe. Kassim majaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Said Meck Sadick alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wanahabari alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017




  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wana UVCCM alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo leo Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Bomang'ombe Wilaya ya Hai waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Bomang'ombe Wilaya ya Hai waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza changamioto za wananchi wa Kwa Sadala Wilaya ya Hai waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


 Kijana akiwa kabebwa mgongoni akirekodi wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017








 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiagana na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiongea na wananchi wa Karanga Wilaya ya Moshi mjini waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017








  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maagizo wa kutotoza ushuru wachuuzi kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Hai Bw. Yohana Sintoo wakati akiongea na wananchi wa Kwa Sadala waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017


    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maagizo wa kutotoza ushuru wachuuzi kwa Mkurugenzi wa Wilaya ya Hai Bw. Yohana Sintoo wakati akiongea na wananchi wa Kwa Sadala waliomsimamisha kwa muda wakati akitokea uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro alipowsili tayari kwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani humo Kilimanjaro Jumamosi Aprili 29, 2017





  Mbunge Mstaafu na aliyekuwa Mkuu wa Sekondari ya Weruweru, Dk Maria Kamm akimshangilia Rais Magufuli alipoongea na wananchi wa Karanga

MPINA AWATAKA WAKAZI WA MOROGORO KUTUNZA VYANZO VYA MAJI NA MAZINGIRA

April 29, 2017
Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi muungano na Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina, amewataka wakazi wa Mkoa wa Morogoro kutunza Vyanzo vya maji na Mazingira kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wameokoa maisha ya binadamu na viumbe hai wengine.
Naibu Waziri Mpina ameyasema hayo leo alipikuwa katika zoezi la usafi kitaifa Mjini Morogoro ambapo amesisitiza kwa kufanya hivyo wakazi wa mkoa huo watakuwa wamesaidia wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam Pamoja na pwani ambao vyanzo vyao vyingi vya maji vimetokea mkoani Morogoro.
 Kulia Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwna Kebwe Steven Kebwe akimkabirisha Naibu Waziri Mpina kabla a kuanza kwa zoezi la Usafi kitaifa Mjini Morogoro siku ya Jumamosi ya Mwisho wa mwezi wa nne.
(Habari na Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akitoa Mchanga katika moja ya Mtaro Mijini Morogoro wakati wa kufanya usafi, Leo.
Moja ya Mtaro Uliosafishwa katika zoezi la usafi wa mazingira leo Mjini Morogoro
Mpina pia aliweka msisitizo katika zoezi zima la upandaji miti ambapo kila wilaya inatakiwa kupanda miti milioni moja na nusu, "kutakuwa na ufuatiliaji wa hali ya katika utekelezaji wa zoezi hiyo katika ngazi ya Wilaya." Alisisitiza Mpina.
Aidha Mpina aliunga Mkono Jitihada za Mkuu wa Mkoa wa Morogoro katika suala zima la utunzani na usafi  wa mazingira , "Mnae Mkuu wa Mkoa anaetosha, anaujua mkoa vizuri na hwa ndiyo viongozi wa mkoa tunaowataka, wachapakazi na wenyekujituma. Alisema Mpina."
Akiongelea suala la kuhamishwa wananchi katika milima na vyanzo vya maji, NW Mpina Alisema kuwa  " Tunapowaondoa wananchi katika maeneo hayo aimaaninishi kwamba tunawatesa. tunawapenda ndo maana tunawahamishia katika maeneo salama na rafiki kwa mazingira, RC watoeni wananchi wanaokaa katika maweneo Hatarishi." Alisema.
Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bwana Kebwe Steven Kebwe, akizungumzia hali ya mazingira ya mkoa huo, alisema kuwa mkoa utajitahidi kupambana na hali ya uharibifu wa mazingira, pamoja na changamoto mkoa unazokumbana nazo akitolea mfano upungu wa vifaa vya kuzolea taka.

Jumamosi ya usafi wa Mazingira Mkoani Morogoro kwa Jumamosi ya Mwishho wa mwezi wa nne ni utegelezaji wa Agizo la Mhe. Rais la Usafi wa Mazingira.

UHARIBIFU WA VYANZO VYA MAJI VYAIGIZA HASARA TANGA UWASA YA MILIONI 13 KWA SIKU.

April 29, 2017
 Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusiana na mikakati waliochukua kukabiliana na kuondoa tatizo la maji machafu yanayotoka jijini Tanga ili kuhakikisha maji yanarudi kwenye hali yake ya kawaida  lakini kulia ni Meneja wa Ufundi wa Mamlaka hiyo,Farles Aram
 Kushoto mwenye tisheti ya njano ni Mwandishi wa Gazeti la Majira Mkoani Tanga,Mashaka Mhando akiuliza swali katikati ni Joachim Kapembe kutoka Shirika la Utangazaji la TBC na kulia ni Mwandishi wa ITV na Radio One Mkoani Tanga,Wiliam Mngazija.
 Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Citizeni Mkoani Tanga, George Sembony kulia akiuliza swali kwenye mkutano huo kushoto ni Mwandishi Zawadi Kika wa Clous TV
 Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo kulia ni Mwandishi wa Gazeti la Citizeni George Sembony

Mratibu wa shughuli za Mazingira wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa,Ramadhani Nyambukah akizungumza jambo kwenye mkutano huo
 Baadhi ya watumishi wa mamlaka hiyo wakifuatilia mkutano huo na waandishi wa habari leo
 Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakichukua habari
 Joachim Kapembe kutoka Shirika la Utangazaji la TBCkushoto akiwa sambamba na mtumishi wa mamlaka ya Maji Tanga Uwasa wakiingia kwenye kituo cha kusafishia Maji cha Moye
 Waandishi wa habari wakitazama namna maji yaliyohifadhiwa kwenye kituo cha kusafishia maji cha Mowe kabla ya kufika kwa walaji wa kwanza ni Sophia Wakati wa Gazeti la Uhuru wa pili ni Mbaruku Yusuph wa gazeti la Tanzania Daima
 Mwandishi wa Gazeti la Mtanzania,Sussan Uhinga naye akiangalia namna maji yanavyosafishwa kabla ya kuwafikia walaji
 Waandishi wa Habari wakiongozwa na Amina Omari wa Gazeti la Mtanzania wakitembelea eneo la kusafishia maji kabla ya kufika kwa watumiaji la



 Eneo la Mowe ambalo maji huchujwa kabla ya kuwafikia walaji
 Mwandishi wa gazeti la Mtanzania,Sussan Uhinga na Frank wa TK wakiwa kwenye eneo hilo kujionea
 Mratibu wa shughuli za Mazingira wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa,Ramadhani Nyambukah akizungumza jambo kwa waandishi wa habari kuhusu dawa ambazo zinatumika kuwekwa kwenye maji
 Mratibu wa shughuli za Mazingira wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Tanga Uwasa,Ramadhani Nyambukah akiwaonyesha mitambo iliyopo kwenye kituo hicho wakati walipoitembelea kujionea

 Waandishi wakitoka kulia ni Mashaka Mhando wa gazeti la Majira Mkoani Tanga kushoto ni William Mngazija wa ITV na Radio One Mkoani Tanga 


 William Mngazija wa ITV na Radio One Mkoani Tanga akiwa ongoza waandishi wengine kuingia kwenye vyanzo vya maji kuona namna hali ilivyo
 Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Citizeni Mkoani Tanga, George Sembony akiwa kwenye vyanzo hivyo vya maji
 Muonekano wa Maji kwenye chanzo cha Maji cha Mto Zigi
MAMLAKA ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga
Uwasa)inapoteza kiasi cha shilingi milioni 13 kila siku kutokana na kuongezeka kwa za shughuli za kibinaadamu zinazofanywa katika vyanzo vya maji vilivyopo katika Mto zigi na Muzii Wilayani Muheza.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea kwenye vyanzo vya maji,Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa alikiri kuwepo kwa uharibifu mkubwa katika vyanzo hivyo unaosababishwa na wananchi katika maeneo hayo.

Mhandisi Mgeyekwa alisema shughuli za uchimbaji wa dhahabu,kilimo na maogesho ya mifugo katika vyanzo hivyo vimekuwa vikichangia kwa kiasi kikubwa kuongeza matope kwenye bwawa la Mabayani linalosambaza maji Mjini hasa kipindi hiki cha mvua za masika.

Aidha alisema kuwa awali mamalaka hiyo ilikuwa inazalisha maji kiwango cha ujazo km 29,000 na kupungua hadi kufikia ujazo wa km 20,000 kwa sasa jambo lililopelekea kuanza kutoa huduma hiyo kwa mgao ndani ya Jiji la Tanga.

Alisema wao kama mamlaka baada ya kugundua kuwepo kwa tatizo hilo walianza kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuvitembelea vyanzo vyote vya maji ili kubaini uhalisi uliopo na namna ya kuanza kulishughulikia jambo hilo kwa haraka zaidi ili lisiweze kuleta madhara kwa wananchi.

“Ki ukweli tatizo hili la katizo la maji na maji kutoka machafu
haliwaathiri wananchi peke yake hata sisi kwenye maeneo yetu tunayokaa limekuwa likijitokeza hivyo tunaangalia namna ya kupambana nalo usiku na mchana kwa lengo la kutatua shida hiyo”Alisema.

Mkurugenzi huyo alisema tayari mamlaka hiyo imekwisha kuanza kuchukua jitihada za haraka ikiwemo kutumia maji ya kisima cha mwakileo ambacho kina uwezo wa kutoa maji kwa ujazo wa km 30,000 hadi 35,000 ambayo yanaweza kukidhi mahitaji ya zaidi wananchi 47,000 kwa wakati mmoja sambamba na kuzibua mabomba ambayo yamekuwa na tope iliyosababishwa na mvua zinazoendelea sasa.

Hata hivyo aliwataka wananchi kuacha kufanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji kwani kufanya hivyo kunasababisha madhara makubwa kwa watumiaji wake ikiwemo kupungua kina cha maji na maji kutoka machafu jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

Akizungumza wakati wa ziara ya waandishi wa habari walio tembelea vyanzo vya maji vya Mto Muzii,Zigi,Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumiaji wa Maji Zigi Juu,Philipo Mdoe alisema hali ya uchafuzi wa maji na kupungua kina kumechangiwa kwa asilimia kubwa na shughuli za kibinadamu zinazofanywa karibu na vyanzo hivyo jambo ambalo jitihada za haraka zisipochukuliwa kunaweza kukaleta athari zaidi kwa wananchi.

 “Tunaiomba mamlaka kwa kushirikiana na serikali kupitia vyombo vya dola vifanye operesheni za kushtukiza mara kwa mara kwani hii itasaidia kupunguza ama kuondokana na uchafuzi wa mazingira unaofanywa na watu kwenye nyanzo hivyo “Alisema.

Awali akizungumza katika mkutano huo,Mratibu wa Mazingira Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Nyambuka Ramadhani alisema suala la utunzaji wa vyanzo vya maji ni wajibu kwa jamii kuhakikisha wanakuwa mabalozi wazuri wa kuona namna ya kuvilinda ili visiweza kuharibiwa.

“Lazima jamii itambua umuhimu wa kuvitunza na kuvilinda vyanzo vya maji kwani bila hivyo wanaweza kukumbwa na athari za kukosekana kwa maji au kupatikana kwa maji yasiyokuwa safi na salama hivyo tushirikiana kupambana na waharibifu wa mazingira “Alisema.