Idara ya Elimu ikitoa maelezo katika sherehe hizo

July 01, 2013
Afisa Elimu Msingi katika Halmashauri ya Jiji la Tanga,Damasi Kifanya akitoa maeleo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji hilo ambaye hakuwepo pichani juu ya idara hiyo mapema leo.

Naibu Meya Shemdoe akipata maelezo.

July 01, 2013
Naibu Meya wa Jiji la Tanga,Mdamiru Shemdoe akipata maelezo kwenye banda la Idara ya afya wakati wa maadhimisho ya serikali za mitaa leo yaliyofanyika viwanja vya Tangamano.

Mkuu hapa ni

July 01, 2013
NAIBU Meya wa Halmashauri ya Jiji la Tanga,Mdhamiru Shemdoe akipata maelekezo toka kwa wa mtaalamu wa Idara ya Elimu leo katika sherehe za serikali za mitaa ambapo kiwilyani ziliazimishwa katika viwanja vya Tangamano jijini Tanga.

COASTAL Union yawatimua wajumbe wawili wa Kamati ya Utendaji.

July 01, 2013

 Na Oscar Assenga, Tanga.
UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umetimua rasmi wajumbe wa kamati ya utendaji wa timu hiyo ambao walichaguliwa katika uchaguzi mkuu mwaka uliopita kutokana na kushindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo.

Akitangaza uamuzi wa kuwafukuza katika mkutano mkuu wa wanachama mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Hemed Aurora alisema hatua hiyo inatokana na wajumbe hao kuwa mzigo katika nafasi zao ikiwemo kushindwa kuhudhuria vikao vya kamati tendaji tokea walipochaguliwa.


Kauli ya Aurora inafuatia na swali aliliulizwa na Mwanachama wa Klabu hiyo, Miraji Wandi aliyetaka kujua uongozi wa timu hiyo umewachukuliwa hatua gani viongozi ambao wanashindwa kutimiza wajibu wao hali ambayo inapelekea kuwa mzigo kwa klabu hiyo?

Aurora alisema tayari wameandaa utaratibu wa kuandika barua kwa ajili ya kuwatimua rasmi katika nafasi zao hizo pamoja na kutangaza nafasi za hizo katika uchaguzi mdogo ambao utafanyika hivi karibuni kuziba mapengo hayo.

Aidha mwenyekiti huyo aliwataka viongozi waliopo katika klabu hiyo na wanachama kila mmoja kutimiza majukumu yake ili kuweza kusukuma gurudumu la maendeleo ya timu hiyo ambayo imedhamiria msimu ujao kuchukua ubingwa.

Mwenyekiti huyo aliwataja wajumbe wa kamati ya utendaji ambao wamewatimuliwa ni Julius Benjamini na Nashoni Kweli ambao tokea wachaguliwe katika nafasi zao wamekuwa wakishindwa kutekeleza majukumu yao.

Mwisho.

Coastal haina mpango wa kumsajili mlinda mlango mwengine-Binslum

July 01, 2013

Na Oscar Assenga,Tanga.
 
MKURUGENZI wa Ufundi wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga,Nassoro Hemed “Binslum amesema timu hiyo haina mpango wa kumsajili mlinda mlango mwengine isipokuwa waliopo wakishirikiana na Shabani Kado.
 
Kauli hiyo ya Binslum inafuatia taarifa ambazo zimekuwa zikieleza kuwa uongozi wa klabu hiyo wana mpango wa kumsajili aliyekuwa mlinda mlango wa Simba Juma Kaseja katika kipindi hiki na kusema taarifa hizo hazina ukweli wowote ule.
 
Binsulum alisema wanachokifanya hivi sasa ni kuangalia wachezaji wenye uwezo wa kuweza kuiletea mafanikio timu hiyo na sio majina kwani wapo wachezaji wa aina hiyo ambao hawaweze kuwa msaada katika timu.
 
Alisema kuelekea msimu mpya wameimarisha safu ya walinda milango ambapo Shabani Kado atasaidiana na Said Rubawa aliyesajiliwa kutoka Oljoro JKT na Mansour A.Mansour ambaye walimpandisha kutoka katika kikosi chao cha pili chini ya umri wa miaka 20.
 
Mkurugenzi huyo aliendelea kusisitiza kuwa hawajafanya mazungumzo yoyote na Juma Kaseja pia hawana mpango nae ambapo wao wanasajili kwa mipango lengo lao likiwa ni kupata mafanikio kwenye msimu mpya wa Ligi kuu Tanzania bara.
 
Alisema kabla ya kufanya usajili huo walimu walitoa mipango yao nao kama uongozi wakaona watekeleze na kueleza kuwa katika kikosi chao mchezaji huyo hana nafasi kutokana na kuwa na walinda milango mahiri.
 
Wakati huo huo uongozi klabu hiyo umemteua Hafidhi Kido kuwa mwandishi wa klabu hiyo ambaye atakuwa na jumuku la kuhakikisha taarifa za klabu hiyo zinafika kwa wakati katika vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini nafasi ambayo aliteuliwa leo(jana).