(KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Tanga,Constatine Massawe akizungumza na waandishi wa habari mapema leo ofisini kwake)
Na Oscar Assenga,Pangani.
JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga limefanikiwa kukamata kete 46 na misokoto 40 ya madawa ya kulevya aina ya Kokain na bangi baada ya kufanya msako maeneo ambayo yalikuwa yakisadikiwa wanakaa watumiaji wa madawa hayo wilayani hapa.
JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga limefanikiwa kukamata kete 46 na misokoto 40 ya madawa ya kulevya aina ya Kokain na bangi baada ya kufanya msako maeneo ambayo yalikuwa yakisadikiwa wanakaa watumiaji wa madawa hayo wilayani hapa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,Constatine Massawe alithibitisha kukamatwa madawa hayo ni kueleza tukio hilo lilitokea Julai 10 mwaka huu baada ya polisi kuvamia eneo hilo na kuwatuka watumiaji wanne ambapo walikuwa wakiyatumia huku
Amesema kukamatwa kwa madawa hayo kumetokana taarifa ambazo jeshi zililipata kutoka kwa wananchi wa maeneo hayo na kuitaka jamii kuwa inatoa taarifa pindi wanapoona vitendo viovu kwenye jamii zao vinafanyika.
Massawe aliwataja waliokamatwa katika tukio hilo ambao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani ni Shabani Ramadhani (20)mvuvi na mkazi wa Malindi wilayani Pangani,Mohamed Kijiba mvuvi na mkazi wa Fungoni na Iddi Hamdani (21)mvuvi mkazi wa Fungoni mjini Pangani.
Wakati huo huo,Kamanda Massawe alisema watu wawili walikamatwa na misokoto ya madawa ya kulevya aina ya bangi katika tukio hilo na kuwataja waliokamatwa ni Mohamed Kijiba ambaye alikutwa na bangi licha ya kukutwa pia na kokain na Rajabu Madaraka (28)wote wakazi wa Fungoni wilayani Pangani.
Kamanda Massawe ametoa wito kwa vijana kuacha kujihusisha na utumiaji na uuzaji wa madawa ya kulevya badala yake watafute kazi nyengine halali za kufanya ambazo zinaweza kuwaingizia kipato ili wapate maendeleo.
Mwisho.