RC MAGALULA AWASIMAMISHA KAZI WAKUU WA IDARA SABA WILAYANI MKINGA.

January 09, 2015

MKUU wa Mkoa wa Tanga, Magalula Saidi Magalula amewasimamisha kazi vigogo saba Halamshauri ya wilaya ya Mkinga pamoja na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Amina Kiwanuka kuwachukuliwa hatua watumishi wengine 74 walipo chini ya mamlaka yake,

Agizo la Mkuu huyo wa Mkoa linafuatia ziara yake aliyotembelea wilaya hiyo hivi karibuni wakati akijimbulisha kwa wananchi ambapo alibaini tatizo kubwa lilikuwa ni watumishi wa Halmashauri hiyo kukataa kuhamia wilayani humo na kuendelea kubaki kuishi Tanga mjini.

Kutokana na hali hiyo Mkuu huyo wa Mkoa alitoa agizo la siku saba watumishi hao wawe wamekwisha kuhamia kwenye wilaya hiyo jambo ambalo lilishindwa kufanyika kutokana na watumishi hao kuendelea kubaki mjini.

Alisema kuwa jana alikwenda wilayani humo kuangalia namna gani agizo hilo limekwenda bado akakuta watumishi wakiwa wanaendelea na utaratibu wao wa kawaida wa kuendelea kufanya kazi wilayani humo na kuandoka jioni kurejea Tanga mjini.

Waliosimamishwa kazi na mkuu huyo wa mkoa ni Afisa Ardhi,Afisa Mifugo,Afisa Kilimo,Mkaguzi wa Ndani,Afisa Uchaguzi,Afisa Manunuzi na Afisa Tehama kutokana na kukiuka taratibu za utumishi.

   “Mh Rais na Mh Waziri Mkuu waliagiza watumishi hawa kuhamia wilayani humo lakini cha kushangaza mpaka leo hii wameshindwa kufanya hivyo jambo ambalo linapelekea kudodora maendeleo kwenye wilaya hiyo ambayo ilianzishwa miaka saba iliyopita “Alisema Magalula.

‘”Kutokana na watumishi hao kuishi mbali na wilaya hiyo kumepelekea kukwamisha shughuli mbalimbali za kimaendeleo na kuwafanya wananchi kushindwa kupata mafanikio..hata ukiangalia ujenzi wa maabara bado upo kwenye hali ya chini sana “Alisema RC Magalula.

 Alisema kuwa kabla ya kufanya maamuzi hayo alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kumpatia orodha ya watumishi wa Halmashauri wanaotaka kuishi wilayani humo lakini walikataa kufanya hivyo.

Aidha alisema kuwa amewasimamisha kazi ili kuona serikali ilivyokuwa makini  katika masuala ya utendaji ikiwemo kuwataka watumishi wenye tabia kama hizo kuacha mara moja kwani wakibainika wahawatumiliwa.

Hata hiyo alisema kuwa maamuzi hayo sio nguvu za soda kwa kuhakikisha analishughulikia suala hilo ipasavyo kwa sababu lazima ufike wakati watumishi watende haki kwa kuwahudumia wananchi ipasavyo.

  “Halmashauri ya Mkinga imeanzishwa miaka saba iliyopita mpaka sasa bado maendeleo yameendelea kusuasua kutokana na watumishi waliopenda kuwa karibu na kuwatumikia wananchi hii sio sawa hata kidogo.


WAZIRI WA NISHATI NA MADINI AZINDUA MRADI MKUBWA WA REA WA SHILINGI BILIONI 25.7 MKOANI SIMIYU

January 09, 2015
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo leo amezindua mradi wa umeme vijijini uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili, mkoani Simiyu ambapo vijiji 170 vimeunganishwa na mradi huo. Ninawasilisha picha za matukio pamoja na captions kwa ajili ya kuchapishwa kwenye vyombo vyenu vya habari ili kuhabarisha umma. Aidha, captions zinapatikana mwishoni mwa email hii.
Mwananchi kutoka katika kijiji cha Nyanguge kilichopo wilayani Bariadi mkoani Simiyu akiwasilisha hoja mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo ( wa kwanza kulia) mara Waziri alipotembelea kijiji hicho wakati akielekea kwenye uzinduzi wa mradi wa umeme vijijini uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili wenye thamani ya shilingi bilioni 25.7.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Erasto Sima akizungumza na wanakijiji wa Nyanguge wilayani Bariadi juu ya utunzaji wa miundombinu ya umeme iliyowekwa na REA. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Sehemu ya umati wa watu waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa mradi wa umeme vijijini katika kijiji cha Shishiyu kilichopo wilayani Maswa mkoani Simiyu.
Sehemu ya watoto kutoka katika kijiji cha Shishiyu kilichopo wilayani Maswa mkoani Simiyu waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa mradi wa umeme uliotekelezwa na REA Awamu ya Pili.
Wananchi wa kata ya Shishiyu wakinyanyua mikono juu kama ishara ya kuridhishwa na utekelezaji wa mradi wa umeme vijijini uliotekelezwa na REA kabla ya kuzinduliwa rasmi kwa mradi huo na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akihutubia wananchi wa kata ya Shishiyu (hawapo pichani) kabla ya kuzindua rasmi mradi wa umeme.
Mtaalamu kutoka kampuni ya LTL (PVT) LTD Michael Marenye akitaja orodha ya vijiji vilivyonufaika na mradi wa umeme vijijini uliotekelezwa na REA Awamu ya Pili. Kulia ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Mbunge wa Maswa Magharibi John Magale Shibuda akimpongeza Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kusambaza umeme katika jimbo lake.
Mbunge wa Maswa Magharibi John Magale Shibuda (kushoto) akitafsiri hotuba ya shukrani iliyotolewa kwa lugha ya kisukuma na mmoja wa wakazi wa kijiji cha Shishiyu mbele ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kabla ya kuzinduliwa rasmi kwa mradi huo.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa umeme vijijini uliotekelezwa na REA Awamu ya Pili.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (mwenye tisheti ya kijani) akisoma maandishi kwenye jiwe la msingi mara baada kukata utepe kama ishara ya uzinduzi wa mradi huo.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati) Mbunge wa Maswa Magharibi John Magale Shibuda (kushoto mwa Waziri) na mmoja wa wakazi wa Shishiyu wakibonyeza kitufe kama ishara ya uzinduzi wa mradi huo.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (katikati aliyeshika mtoto); Mbunge wa Maswa Magharibi John Magale Shibuda (wa pili kutoka kulia waliokaa mbele) na Diwani wa Kata ya Shishiyu wilayani Maswa Pili Kidesela (wa kwanza kulia waliokaa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) mara baada ya kumalizika rasmi kwa uzinduzi wa mradi huo.
KENGE 140 WANASWA UWANJA WA NDEGE DAR WAKITOROSHWA NJE YA NCHI

KENGE 140 WANASWA UWANJA WA NDEGE DAR WAKITOROSHWA NJE YA NCHI

January 09, 2015

Jeshi la Polisi la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)linamshikilia raia wa Kuwait kwa tuhuma za kukutwa na viumbe hai aina ya Kenge 149 wenye thamani ya Sh 6.3 milioni.
Kamanda wa Polisi wa JNIA, Khamis Suleiman alimtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Hussain Ahmed Ally Mansour(34), raia wa Kuwait ambaye alikamatwa uwanjani hapo jana majira ya saa 5 usiku wakati akijiandaa na safari ya kuelekea nchini Kuwait kupitia Dubai na Shirika la Ndege la Emirates .
Kamanda Selemani alisema Mansour alikamatwa na wanyama hao ambao aliwahifadhi kwenye mifuko midogo midogo ilivyowekwa katika begi kubwa lenye rangi nyeusi.
“Kenge waliwekwa kwenye mifuko midogo midogo 15 na kila mmoja kuna kenge 15 na mifuko mingine walikaa wawili,”alisema kamanda Selemani.

Alisema kati ya Kenge hao, 15 walikufa na walio hai walikuwa 134 ambao walikuwa wamefichwa kwenye mifuko hiyo.
Seleman alisema wakati wanafanyiwa upekuzi ndipo walipogundua kuna vitu ambavyo vinafanana na nyoka na kuamua kuwashirikisha wataalamu wa maliasili ambao walibaini kuwa begi hilo lilikuwa na Kenge.


“Huyu mtuhumiwa alikuja nchini Januari 6,alitiliwa mashaka na polisi wa JNIA na tulimuamuru akae pembeni kwa upekuzi zaidi na kugundua anasafirisha kenge bila Kibali,”alisema Selemani. Selemani alisema walipoendelea kumuhoji mtuhumiwa huyo alidai kuwa alikuja nchini kwa ajili ya kuchukua viumbe aina ya ndege lakini baada ya kuwakosa aliamua kubeba Kenge hao. Kamanda Selemani aliwaomba wananchi kuwa na uzalendo wa nchi yao wanapoona mtu anasafirisha rasilimali za nchi watoe taarifa katika jeshi la polisi. Alisema polisi wataendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo ya mipakani na viwanja vya ndege ili kudhibiti aina hiyo ya utoroshaji wa nyara. Julai 31, mwaka jana raia wa Vietnam, Dong Van (47) naye alikamatwa uwanjani hapo akiwa na meno 65 na kucha 447 za simba zenye thamani ya Sh189.4 milioni.

Tanesco Sacos yafanya mkutano wa mwaka na kuchagua viongozi

January 09, 2015

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),Mhandisi Felchesmi Mramba akipitia hutuba kabla ya kufungua mkutano akiwa mgeni rasmi.
  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),Mhandisi Felchesmi Mramba akiwasalimia wajumbe wa mkutano wakati akiingia.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),Mhandisi Felchesmi Mramba akiwasalimia wajumbe wa mkutano wakati akiingia.
 Wajumbe wakiwa katika mkutano.
 Wajumbe wakifuatilia wakati wa mkutano.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),Mhandisi Felchesmi Mramba,akifungua mkutano.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),Mhandisi Felchesmi Mramba akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano kutoka nchi nzima.
 Viongozi katika picha ya pamoja.
  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco),Mhandisi Felchesmi Mramba akizungumza na waandishi.
 Baadhi ya viongozi na wajumbe katika picha ya pamoja.
Sehemu ya viongozi na wajumbe katika picha ya pamoja.

WAZIRI WA VIWANDA ATEMBELEA MACHIMKBO YA CHUMA LIGANGA NA MAKAA YA MAWE MCHUCHUMA

January 09, 2015
Waziri wa Viwanda na Biashara akutana na wafanyabiashara wa Mkoani Njombe na kuzungumza nao fursa mbalimbali zilizopo katika mkoa huo mara baada ya kupokewa na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi.

 wafanyabiashara wa Mkoani Njombe
Mlima wa Liganga uliopo mkoani njombe wilaya ya Ludewa ambapo kampuni ya Tanzania China International Mineral Resources Ltd.
 Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kiogoda (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Tanzania China International Mineral Resources Ltd, Erick Mwingira juu ya miradi hiyo ya makaa ya mawe, alipotembelea miradi ya Chuma cha Liganga na Makaa ya mawe ya Mchuchuma. Kulia ni  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Mligi Mkucha.
 Picha ya pamoja ya Mh. Waziri wa Viwanda na Biashara pamoja na watafiti na Viongozi wa serikali.

Waziri wa Viwanda na Biashara katika mlima wa liganga.
TAMKO LA POLISI KUHUSU ZOEZI LA KUAPISHWA SERIKALI ZA MITAA

TAMKO LA POLISI KUHUSU ZOEZI LA KUAPISHWA SERIKALI ZA MITAA

January 09, 2015

Advera-Senso
Kufuatia kukamilika kwa mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji na hivi sasa kuendelea kwa zoezi la kuapishwa kwa viongozi hao katika maeneo mbalimbali hapa nchini, kumejitokeza tabia ya baadhi ya wananchi kufanya vurugu na fujo katika zoezi hilo.
Baadhi ya wananchi wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya kihalifu kwa kufanya fujo na vitendo vya vurugu ikiwemo kuwapiga baadhi ya watendaji wanaosimamia zoezi la kuapisha na kuwapiga viongozi wateule waliochaguliwa kihalali na wananchi kwa madai kuwa hawakushinda kihalali katika uchaguzi huo jambo ambalo ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za nchi.
Kufuatia hali hiyo, Jeshi la Polisi nchini, linatoa onyo kwa wananchi wenye tabia hiyo kuacha mara moja na badala yake kama mtu hakuridhika na matokeo ya uchaguzi huo, afuate utaratibu wa kuwasilisha malalamiko yake kwenye ngazi husika ili yaweze kufanyiwa kazi kwa mujibu wa sheria.
Aidha, Jeshi la Polisi linawata Wakurugenzi na Maafisa watendaji wenye dhamana ya kusimamia mchakato wa kuwaapisha wenyeviti waliochaguliwa, kufuatilia kwa karibu migogoro inayojitokeza na kuitatua migogoro hiyo mapema ili kuepusha migongano inayoweza kusababisha uvunjifu wa amani.
Jeshi la Polisi halitamvumilia mtu ama kikundi chochote kitakachofanya vurugu ama fujo kwa kisingizio cha ushabiki wa siasa na badala yake atakayebainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Imetolewa na: Advera J. Bulimba – SSP Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya DAWASA) wafanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji.

Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya DAWASA) wafanya ziara ya kukagua mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji.

January 09, 2015


unnamed1d 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) Didas Mwilawi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fedha akisalimiana na Mwenyekiti wa wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya DAWASA Christine Kilindu alipowasili eneo zinapojengwa ofisi za mradi wa bomba kuu la maji kutoka Ruvu Juu zilizopo Kibaha.
unnamed2d 
Meneja wa Mradi wa upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu Pintu Dutta kwa kampuni ya VA TECH WABAG kutoka India akifafanua jambo kwa Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) walipotembelea huo eneo la upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu wakati wa ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.
3d
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) wakiangalia maungio ya mradi wa bomba jipya kutoka mtambo wa Ruvu Chini yaliyopo eneo la Mpiji wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani
unnamed4d.
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) kukagua mabomba yaliyohifadhiwa eneo la Kibaha Mwendapole wakati wa ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo. unnamed6d 
Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) wakitembelea sehemu unapofanyika upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu wakati wa ziara yao ya siku moja katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo.
Sehemu ya mtambo wa Ruvu Juu kabla ya upanuzi. unnamed8d 
Moja ya hatua ya kusafisha maji katika mtambo wa Ruvu Juu kabla ya kusafirishwa tayari kwa matumizi kwa wakazi wa mikoa ya Dar es salaasm na Pwani
(Picha zote na Eleuteri Mangi- MAELEZO)
……………………………………………………………………………….
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO Wajumbe wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) wamefanya ziara ya siku moja katika mikoa ya Dar es salaam na Pwani kukagua na kujionea hatua iliyofikiwa katika mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji kutoka Ruvu Chini na Ruvu Juu ili kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji kwa wananchi katika mikoa hiyo. Ziara ya wajumbe hao wa kamati Ufundi ilianza kwa kukagua kazi ya ukarabati wa kituo yalipo matangi ya maji eneo la Chuo Kiukuu cha Dar es salaam, maungio ya mradi wa bomba jipya yaliyopo eneo la Mpiji, ujenzi wa ofisi ya mradi wa bomba kuu la maji kutoka Ruvu Juu zilizopo Kibaha, kukagua mabomba yaliyohifadhiwa eneo la Kibaha Mwendapole na upanuzi wa mtambo wa Ruvu Juu Mladizi na Ruvu darajani. Akifanya majumuisho ya ziara hiyo Mwenyekiti wa wa Kamati ya Ufundi ya Bodi ya DAWASA Christine Kilindu amesema kuwa wajumbe wameridhishwa na kasi ya ujenzi wa miundo mbimu hiyo ambapo matarajio mradi huo utakamilika kwa wakati kama ilivyopangwa mwishoni mwa mwaka huu. Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa wananchi wa mikoa ya Dar es salaam na Pwani watarajie kupata huduma ya maji iliyo bora mara miradi ya Ruvu Juu Chini itakapokamilika. Aidha, Christine amewaasa wananchi wa maeneo yanapopita mabomba wa miradi hiyo kuyatunza vizuri kuanzia wakati huu yalipohifadhiwa na yatakapokuwa yameanza kutumika ili yawanufaishe wananchi wote wa mikoa hiyo. Naye Kaimu Mkurugenzi DAWASA Romanus Mwang’ingo alisema kuwa pamoja na kuboresha huduma kwa maeneo yaliyo pembezoni mwa barabara ya Morogoro yaani Kimara, Mbezi, Kiluvya, Kibaha, Visiga, Mlandizi na Kibamba, utekelezaji huo pia utawanufaisha wakazi wa Ubungo, Vingunguti, Kimara, Tabata na Kinyerezi ambao nao wanahudumiwa na mtambo unaotoa maji kutoka Ruvu Juu. Mradi wa upanuzi wa mtambo wa Ruvu Chini unalenga kuongeza uzalishaji maji na kuwahudumia wakazi wa maeneo ya uwekezaji (EPZ), Chasimba, Buma, Zinga, Kerege, Mpiji, Bunju, Wazo, Salasala, Madale, Kinzudi, Mbezi Juu, Goba, Kawe, Makongo, Mwenge, Msasani, Mikocheni, Mlalakua, Masaki, Sinza, kijitonyama, Manzese, Konondoni, Magomeni, Kigogo, Vingunguti, Buguruni, Kariakoo na Ilala. Kazi hiyo ya maboresho inafanyika chini ya mpango maalumu wa kuboresha huduma ya upatikanaji wa Maji Safi na Maji Taka jijini Dar es salaam na maeneo mengine yanayohudumiwa na DAWASA unaohususha ujenzi wa miradi mipya na pamoja na kukarabati miundombinu iliyopo.

UELEWA MDOGO BAADHI YA WAJUMBE SERIKALI ZA MITAA WAWAKWAMISHA WENGINE KULA KIAPO

January 09, 2015
HAFLA ya kuapishwa wenyeviti wateule wa serikali za mitaa wa Halmashauri ya jijini Tanga, imefanyika leo na kukamilika kwa kiwango kikubwa kwenye Ukumbi wa Shule ya ufudi Tanga, iliyopo kata ya Mzingani.
 
Hata hivyo uelewa mdogo miongoni mwa wajumbe hao wa serikali za mitaa, waliopatikana katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni umezua changamoto wakati wa zoezi hilo la kula kiapo hivyo italazimu kurudiwa kwa baadhi yao.
 
Akitangaza utaratibu wa kiapo Hakimu Mkazi Mfawidhi wilaya ya Tanga Aziza Lutalla alisisitiza kuwa kiapo ni kifungo ambacho hakitakiwi kiwe kimefutwafutwa iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya, kauli hiyo ilizua minong’ono kwa baadhi yao hadi pale  alipotangaza kwamba kwa waliokosea kujaza fomu zao za kiapo itawalazimu kurudia kuzijaza upya kisha zitawekwa sahihi nayeye kwa utaratibu utakaopangwa.
 
“Kiapo ni ushahidi wa kukubaliana na masharti ya utumishi wa Umaa katika nafasi yako na kukiuka ni kosa la jinai na kuna adhabu yake kwa mujibu wa sheria za nchi... haitakiwi kiwe kimefutwafutwa, kwahiyo kama kuna mjumbe aliyefanya hivyo awasiliane na mratibu wa zoezi upewe fomu nyingine,” aliwasisitizia viongozi hao
 
Baada ya zoezi la Kuapishwa kwa Wenyeviti 181, wajumbe mchanganyiko 543 na wajumbe 362 wa viti maalumu, Mstaiki Meya wa Jiji la Tanga, Omari Guledi aliwasisitizia viongozi hao kuachana na itikadi za vyama vyao lakini wawe wamoja kwa kufanya vikao kwa mujibu wa taratbu kwa maslahi ya nchi.
 
Nao wajumbe hao walizungumza na Mwanamke Makini walibainishwa kuwa licha ya zoezi hilo kukamilika lakini lilikuwa na dosari ambazo hazina budi kufanyiwa kazi kwa wakati mwengine kwavile sasa limeshapita salama.
 
“Sina hakika kama wajumbe wote wanajua kusoma na kuandika, kama ulifuatilia kwa makini mwandishi wengine hawakuwa wakijaza wala kusema yale maneno ya kuapa, sasa kwasababu tuliapishwa jumla angalau imewabeba," alisema Hussein Abasi  mwenyekiti mtaa wa New Hotel kata ya central
 
CHANZO:MWANAMKEMAKINIBLOG
DE GEA KUFUNGA 'NDOA' NYINGINE OLD TRAFFORD

DE GEA KUFUNGA 'NDOA' NYINGINE OLD TRAFFORD

January 09, 2015


Manchester United goalkeeper David de Gea is close to extending his current deal at Old Trafford 
 David de Gea mbioni kusaini mkataba mpya

Manchester United wanakaribia kumbakisa David de Gea kwa kumuongeza mkataba mpya muda mfupi baada ya kipa mpya namba mbili, Victor Valdes kutua Old Trafford.
United imempa Valdes mkataba wa miezi 18 huku wakiweka kipengele cha kuongeza mwaka mwingine na tayari kocha wa Old Trafford Louis van Gaal amethibitisha kuwa kipa huyo atakuwa chaguo la pili.
MBWANA SAMATTA ATOWEKA NYUMBANI

MBWANA SAMATTA ATOWEKA NYUMBANI

January 09, 2015


KATIKA hali isiyo ya kawaida,  staa  wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mtanzania Mbwana Samatta, amelazimika kuyakimbia kwa muda makazi ya familia yaliyopo jijini Dar es Salaam.
Samatta ambaye yupo nchini kwa mapumziko, amelazimika kufanya hivyo kupisha mkusanyiko wa mashabiki unaokesha nyumbani kwao kwa ajili ya kuomba msaada na wengine wakitaka kumshuhudia tu.
Mwanaspoti ilifika nyumbani kwao na Samatta, Mbagala Rangitatu na kukutana na baba mzazi wa mwanasoka huyo, Ally Samatta aliyeweka wazi kuwa mwanaye yupo jijini, lakini amejificha mahali na huwa anafika nyumbani hapo kwa kuvizia.
Baba huyo alisema awali  mwanaye alikuwa akifikia hapo kila alipokuwa anakuja mapumzikoni, lakini hali haikuwa shwari kutokana na watu kujaa hapo mchana na usiku.
“Kila mmoja huja na sababu yake, wengine walikuwa na hamu tu ya kumshuhudia staa huyo na wengine walifika hapo kwa ajili ya kuomba msaada wakijua jamaa amekuja na pesa nyingi kutoka kwa mmiliki wa TP mazembe, Moise Katumbi,” Baba huyo alisema.
“Chumba chake hiko hapo (anakionyesha), lakini sasa hivi hafikii hapa, anafikia huko mbali na anakuja hapa kwa kuvizia tu. Tunawasiliana na akijua nipo anaweza kuja usiku na kukaa masaa mawili matatu na baada ya hapo anaondoka, hata hivyo kwa sababu anatumia gari yake, wanapoiona tu hapo nje ni tabu, wanajaa.
“Kutokana na hali hiyo inanibidi nizoee tu ndiyo hivyo tena, lakini huwa nakosa raha kwa sababu nakosa muda wa kutosha wa kukaa kuzungumza na kufurahia na mwanangu.”
Hata hivyo mchezaji huyo amekiri kuwa anaiheshimu jamii aliyokuwa nayo wakae wazungumze, lakini kutokana na majukumu mengi anayokuwa nayo inambidi afanye hivyo kwa sababu lengo la kuja nyumbani Dar es Salaam ni kupumzisha akili yake.
“Nathamini mchango wa jamii, tukae tuzungumze kama zamani, lakini sasa hivi ni tofauti nina majukumu mengi, hivyo kuna wakati natakiwa nipumzike na ndiyo maana huwa sipatikani kwa urahisi,” alisema Samatta.
Mchezaji huyo pia anaichezea timu ya taifa, Taifa Stars.
Source: Mwanaspoti

COASTALA UNIONI KUKIPIGA NA MOMBASA COMBAINI KESHO

January 09, 2015



TIMU ya Coastal Union “Wagosi wa Kaya”kesho wanatarajia kucheza mechi ya kirafiki na timu ya Mombasa Combain ikiwa ni kukipa makali kikosi hicho kabla ya kucheza mechi zake zinazofuata za Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.

Mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani kuanzia saa kumi jioni ikiwemo wadau mbalimbali wa soka kutakiwa kujitokeza ili kuweza kushuhudia mchezo huo.

Ofisa Habari wa Coastal Union, Oscar Assenga amesema kuwa mechi hiyo ni sehemu ya kuhakikisha kikosi hicho kinajiimarisha zaidi kila idara kabla ya mchezo wake na Polisi Morogoro.

Assenga amesema kuwa maandalizi ya kuelekea mchezo huo yamekamilika kwa asilimia kubwa na Mombasa Combain wanatarajiwa kutua leo jijini hapa tayari kwa ajili ya mechi hiyo itayochezwa kesho kuanzia saa kumi
jioni.

Hata hivyo aliwataka wapenzi wanachama na mashabiki wa soka kuhakikisha hawakosi fursa hii adimu kuja kuishuhudia timu yao ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani kabla ya kuanza mechi za Ligi kuu zinazofuata.

Wakati huo huo,Kikosi cha timu ya Coastal Union kinaendelea na mazoezi kila siku kwenye viwanja vya shule ya sekondari Popatlaly na sasa kipo tayari kuweza kuikabili timu yoyote ile itakayokutana nayo na kuweza kupata matokeo mazuri.

KILUVYA UTD, NJOMBE BADO ZAKIMBIZA SDL

January 09, 2015
Kiluvya United ya Pwani na Njombe Mji ya mkoani Njombe ndizo timu pekee zilizomaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa kushinda mechi zote katika makundi yao, hivyo kujipatia pointi 15 kila moja.

Njombe Mji imeongoza kundi D lenye timu za Mkamba Rangers ya Morogoro iliyofikisha pointi nane, Wenda ya Mbeya pointi sita, Volcano FC ya Morogoro pointi sita, Town Small Boys ya Ruvuma pointi tano na Magereza ya Iringa yenye pointi moja.

Katika kundi C, Kiluvya United inafuatiwa na Mshikamano ya Dar es Salaam yenye pointi kumi, Abajalo pia ya Dar es Salaam pointi saba, Cosmopolitan na Transit Camp za Dar es Salaam ambazo kila moja imemaliza mzunguko huo ikiwa na pointi tano. Kariakoo ya Lindi haina pointi.

Mji Mkuu (CDA) ya Dodoma na Singida United ya Singida ndizo zinazochuana katika kundi A kila moja ikiwa na pointi nane. Mvuvuma FC ya Kigoma yenye pointi tano ndiyo inayofuatia, wakati Milambo ya Tabora ina pointi nne huku Ujenzi Rukwa ikikamata mkia kwa pointi moja.

Pia mchuano mkali uko katika kundi B ambapo JKT Rwamkoma ya Mara na Mbao FC ya Mwanza ziko kileleni kila moja ikiwa na pointi tisa. AFC ya Arusha inafuatia kwa pointi sita, Bulyanhulu FC ya Shinyanga ina pointi nne wakati Pamba FC ya Mwanza iko mkiani kwa pointi moja.

Mzunguko wa pili wa ligi hiyo itakayotoa timu nne zitakazopanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao (2015/2016) utaanza kutimua vumbi Januari 24 mwaka huu.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

POLISI YATINGA HATUA YA NUSU FAINALI KWA KUIFUNGA KCC YA UGANDA KWA PENATI 5-4, MAPINDUZI CUP

January 09, 2015



Wachezaji wa timu ya Polisi wakifurahia ushindi wao dhidi ya timu ya KCC ya Uganda, baada ya kushinda kwa mikwaju ya peneti baada ya mchezo kutoka sare na kupigiana peneti Polisi imeshinda 5 na KCC imepata peneti 4,
Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Makame, akiwa na Viongozi wa timu ya Polisi akitowa zawadi kwa wachezaji wa timu ya Polisi kwa ushindi wao akitoa Dola Mia. ikiwa furaha yake kwa kufanikiwa kuingia Nusu Fainali na kucheza na Timu ya Simba.

Kamishna wa Polisi Zanzibar Hamdani Makame akiwa na Viongozi wa timu ya Polisi baada ya kuwakabidhi Dola mia ikiwa ni Asante yake kwa kuweza kufuzu kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi itakutana na Timu ya Simba baada ya kufuzu kwa kuifunga Timu ya Taifa ya Jangombe.