BOBBI Kristina Brown - mtoto pekee wa mwimbaji nyota wa Marekani Whitney Houston amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 22 baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi sita.
Familia
yake imesema: "Bobbi Kristina (pichani juu) amefariki dunia Julai 26,
2015 akiwa amezungukwa na familia yake. Hatimaye amepumzika kwa amani
kwenye mikono ya Mungu. "Kwa mara nyingine tena tungependa kuwashukuru
nyote kwa upendo na mshikamano wenu katika kipindi chote cha kuugua
kwake".