RAILA ODINGA AMPONGEZA DKT MAGUFULI,AMSHAURI LOWASSA AENDE MAHAKAMANI KAMA HAJARIDHIKA

October 30, 2015
Waziri Mkuu wa zamani Kenya Raila Odinga amempongeza Dkt. John Pombe Joseph Magufuli baada yake kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa Urais Tanzania.

Akiongea katika mahojiano na BBC, Mhe Odinga amemshauri mgombea wa upinzani Mhe. Edward Lowassa Kuwa Kama Hajakubaliana na Matokeo basi Aende Mahakama kushtaki Kama yeye Alivyofanya wakati akigombea Urais Kenya na kushindwa na Rais Uhuru Kenyatta.

Ameeleza pia matumaini yake kwamba Dkt. Magufuli atahakikisha kuendelea kwa uhusiano mzuri uliopo katia ya Tanzania na Kenya, na kuimarisha Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuendeleza ndoto ya kuelekea kwenye Shirikisho la nchi hizo.

chanzo:Michuziblog

STEWART HALL: MBIO ZA UBNGWA SASA ZIMESHIKA KASI AZAM FC

October 30, 2015

MECHI ZIJAZO LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
Oktoba 31, 2015
Simba SC Vs Majimaji FC
Kagera Sugar Vs Yanga SC
Mtibwa Sugar Vs Mwadui FC
Prisons Vs Ndanda FC
Coastal Union Vs Mbeya City
Novemba 1, 2015
African Sports Vs JKT Ruvu
Azam FC Vs Toto Africans
Novemba 2, 2015
Mgambo Shooting Vs Stand United

Kocha Muingereza wa Azam FC, Stewart Hall amesema mbio za ubingwa sasa zimeshika kasi katika timu yake

Na Princess Asia,  DAR ES SALAAM
KOCHA Mkuu Azam FC, Muingereza Stewart John Hall amesema kwamba anataka kuendeleza wimbi la ushindi ili kuhakikisha anatimiza ndoto za kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Azam FC jana imepanda kileleni kwa Ligi Kuu kufuatia ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya JKT Ruvu, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, hivyo kufikisha pointi 22, mbili zaidi ya mabingwa watetezi, Yanga SC, baada ya timu zote hizo kucheza mechi nane.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE jana, kocha huyo aliyeipa Azam FC ubingwa wa Afrika Mashariki, Kombe la Kagame Agosti mwaka huu, amesema kwamba lengo si kuwa kileleni mwa Ligi Kuu kwa muda, bali kutwaa ubingwa.
“Si suala la kuwa juu tu, nataka kufikia malengo tuliyojiwekea, hivyo kazi kubwa iliyopo mbele yetu ni kuhakikisha tunapata pointi tatu za kila mechi tutakazocheza,” alisema.
John Bocco jana amefunga mabao mawili katika ushindi wa 4-2 wa Azam FC

Stewart amefurahishwa na safu yake ya ushambuliaji kwa kucheza kwa ‘njaa ya kufunga’ na kufuata maelekezo anayowapa kabla ya mchezo.
“Nina imani na safu yangu ya ushambuliaji, kama bao la nne lililofungwa na Kipre Tchetche ni la aina yake, ile ilikuwa moja ya maagizo niliyomuagiza na kufanyia kazi,” amesema.
Azam FC inatarajiwa kushuka tena dimbani Jumapili kumenyana na Toto Africans katika mfululizo wa ligi hiyo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Kwa ujumla Ligi Kuu inaendelea mwishoni mwa wiki, Jumamosi Simba SC ikimenyana na Majimaji FC Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga SC na Kagera Sugar Uwanja wa Mwinyi, Tabora, Mtibwa Sugar na Mwadui FC Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro, Prisons na Ndanda FC Uwanja wa Sokoine, Mbeya na Coastal Union na Mbeya City Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mechi nyingine zitachezwa Jumapili, na mbali ya Azam FC na Toto, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga African Sports itakuwa mwenyeji wa JKT Ruvu wakati Jumatatu, Mgambo Shooting itaikaribisha Stand United Uwanja wa Mkwakwani.
TANGAZO- NAFASI ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA- SHULE ZA SEKONDARI WAMA NAKAYAMA NA WAMA SHARAF

TANGAZO- NAFASI ZA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA- SHULE ZA SEKONDARI WAMA NAKAYAMA NA WAMA SHARAF

October 30, 2015

New Picture (6) 
Shule ya Sekondari ya WAMA- Nakayama, Nyamisati -Rufiji
New Picture (5)
Shule ya Sekondari ya WAMA- Sharaf, Mitwero Lindi
New Picture (7)
Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) inatangaza nafasi za kidato cha kwanza kwa wasichana katika Shule zake mbili za Sekondari:
(1) Shule ya Sekondari WAMA – Nakayama iliyopo Kijiji cha Nyamisati Wilaya ya Rufiji , Mkoa wa Pwani:
(2) Shule ya Sekondari ya WAMA- Sharaf iliyopo Mitwero katika Manispaa ya Lindi
WAMA ni Taasisi isiyo ya kiserikali iliyoanzishwa na Mhe. Mama Salma Kikwete ili kusaidia maendeleo ya wanawake na watoto. WAMA inaendesha shule hizi maalum kwa ajili ya watoto yatima na wanaotoka katika mazingira magumu. Hata hivyo, WAMA inatoa fursa chache kwa wanafunzi wengine ambao wazazi wao wana uwezo wa kulipia ili kuongeza uwezo wa kusaidia watoto wengi zaidi.
Tunafurahi kutoa fursa hii kwa wasichana ambao wataweza kulipia ada kwa kidato cha kwanza katika shule zote mbili kwa mwaka 2016.
Fomu za kujiunga zinapatikana katika ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Dar es Salaam zilizopo Kawe karibu na Hoteli ya Picolo Beach au katika Tovuti ya Taasisi: www.wamafoundation.or.tz
Kwa wakazi wa Lindi fomu zinapatikana katika Ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) tawi la Lindi zilizopo katika makutano ya Barabara ya Karume na Amani , Kiwanja no.11 kitalu B karibu na Ofisi za Magereza za Mkoa wa Lindi
Kwa Dar es Salaam mtihani wa kujiunga na shule zote mbili utakaotolewa na shule yetu utafanyika Alhamisi Novemba 12, 2015 katika Shule ya Sekondari Jangwani.
Kwa Lindi mtihani wa kujiunga na shule zote mbili utakaotolewa na shule yetu utafanyika Alhamisi Novemba 19 , 2015 katika Chuo cha VETA Lindi.
Mwanafunzi anatakiwa arudishe fomu pamoja na risiti ya malipo katika ofisi za Taasisi ya WAMA au kwa kutumia barua pepe: info@wamafoundation.or.tz, mbugunimwajuma@gmail.com na alimindria66@yahoo.com. Mwisho wa kurudisha fomu ni Jumatano tarehe 11 Novemba, 2015.
Shule zetu zina mazingira na huduma zote muhimu zinazowawezesha wanafunzi kufaulu vizuri yakiwemo mabweni ya kisasa, maabara za kisasa, maabara za computer, maktaba zenye vitabu vya kutosha na walimu wazuri na wakutosha.
Kwa Mawasiliano zaidi:
Piga Namba: 0685-651449, 0789-000341, 0754-439183,
Barua pepe: info@wamafoundation.or.tz
Tovuti: www.wamafoundation.or.tz

GLOBAL EDUCATION LINK (GEL) YAPELEKA WANAFUNZI 65 KUSOMA VYUO VIKUU NCHINI CHINA

October 30, 2015


 Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akiwa ameambatana na wafanyakazi wa kampuni hiyo kwa ajili ya kuwasindikiza wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu nchini China mapema jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Global education link (GEL) Abdulmalik Mollel akiwaita majina wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu nchini China mapema jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mfanyakazi wa Global link education (GEL) wakiwakagua wanafunzi viambatanisho vyao muhimu ikiwemo viza, vyeti, na passport.
 Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akibadilishana mawazo na wazazi mara baada ya kuwasili katika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Mwanafunzi akifurahia jambo na wazazi wake.
Wanafunzi wakiingia sehemu ya kwenda kukaguliwa tayari kwa safari.
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akiambatana na wanafunzi kuelekea sehemu ya ukaguzi.
Wanafunzi wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukamilisha zoezi muhimu