Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Profesa Simon Msanjila akikabidhi
zawadi kwa Prosper Gasper na Erick Simon kutoka Shule ya Sekondari St.
Jude's jijini Arusha baada ya kuibuka washindi wa jumla wa Mashindano ya
Wanasayansi Chipukizi (YST) yaliyofanyika leo yaliyofanyika katika
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar
es Salaam.
Na Daniel Mbega, MaendeleoVijijini Blog
SHULE
za Sekondari nchini Tanzania zimetakiwa kuanza kutuma maombi sasa ili
kupata fursa ya kushiriki katika Maonyesho ya 8 ya Sayansi kwa wanafunzi
yanayoandaliwa na Shirika la Young Scientists Tanzania (YST) kila mwaka.
Taarifa
kutoka YST zimeeleza kwamba, maonyesho hayo ni kwa wanafunzi wa kuanzia
kidato za kwanza hadi cha sita kwa shule zote za sekondari – za umma na
binafsi – zilizoko nchini.
“Mwisho
wa kutuma maombi ni Machi 31, 2018 na maonyesho hayo yatafanyika jijini
Dar es Salaam mwezi Agosti,” imesema taarifa hiyo.
Taarifa
hiyo imeeleza kwamba, kutuma mapema maombi kutasaidia hata zoezi la
mchujo ili kuwapata washiriki wenye mawazo yatakayoleta ushindani pamoja
na ubunifu kwa maendeleo ya sayansi na teknolojia nchini Tanzania.
Jumla
ya mawazo 100 yanatarajiwa kushindanishwa mwaka huu ambapo washindi
katika vitengo mbalimbali watapatiwa zawadi za fedha pamoja na ufadhili
wa masomo ya chuo kikuu.
MaendeleoVijijini inafahamu
kwamba, wanafunzi Prosper Gasper na Erick Simon wa shule ya Sekondari
ya St. Jude’s kutoka Arusha, ndio walioibuka mabingwa wa jumla wa
sayansi katika Maonyesho ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania 2017 kutokana na wazo lao la “Kutumia Simu za Mkononi kama Mfumo wa Kubaini Ajali za Moto” (The Use of Mobile Network as a Fire Alert System).
Kwa
ushindi huo, mbali ya kutunukiwa medali na tuzo, pia walipata kitita
cha Shs. 1,800,000 pamoja na udhamini wa masomo yao hadi elimu ya juu.
Aidha,
walipata nafasi kwa mara ya kwanza ya kushiriki mashindano ya ubunifu
wa sayansi na teknolojia yaliyofanyika jijini Johannesburg, Afrika
Kusini mwezi Oktoba 2017 na mwaka huu 2018 watashiriki maonyesho ya
kimataifa ya sayansi na teknolojia jijini Dublin, Ireland.
Kumekuwepo
na ongezeko kubwa la ushiriki wa shule za sekondari kutoka shule 4
mwaka 2011 hadi 100, hatua ambayo imetokana na hamasa ya kuendeleza
masomo ya sayansi kwa shule mbalimbali za sekondari nchini.
MaendeleoVijijini inafahamu
kwamba, uwepo wa maonyesho hayo ya sayansi kwa wanafunzi usaidia ufaulu
wa masomo ya sayansi kwa shule nyingi za sekondari nchini, mfano
mmojawapo ukiwa ni Shule ya Sekondari ya Wasichana Mtwara.
Katika matokeo ya kidato cha sita mwaka 2017,
kwa mara ya kwanza shule hiyo ilipata daraja kwa kwanza (Division One)
kwa wanafunzi wa masomo ya sayansi, jambo ambalo lilikuwa adimu.
Uchunguzi wa MaendeleoVijijini umebaini
kwamba, kwa miaka takriban 10 mchepuo wa masomo ya sayansi, Kemia,
Baolojia na Jiografia (CBG), haujawahi kutoa hata mwanafunzi mmoja
aliyepata daraja la kwanza katika matokeo ya kidato cha sita.
MaendeleoVijijini imegundua
kwamba, miaka yote ufaulu mkubwa wa masomo ya sayansi shuleni hapo
umekuwa daraja la pili (division two) ambao nao haukuwa wa kuridhisha
ikilinganishwa na masomo ya sanaa na uchumi, huku wanaochukua mchepuo wa
sayansi ‘wakiongoza’ kwa kupata daraja la nne pamoja na kupata sufuri.
Kati
ya wanafunzi nane waliopata Daraja la Kwanza mwaka 2017 shuleni hapo,
wawili walikuwa wanachukua mchepuo wa sayansi na kati ya wanafunzi 57
waliopata daraja la pili, 17 wanatoka mchepuo wa sayansi pia.
Wanafunzi wawili waliopata daraja la pili shuleni hapo Diana Sosoka na Nadhra Mresa, ambao walikuwa washindi wa jumla mwaka 2016 katika maonyesho hayo ya sayansi ya YST nao walionyesha kushangazwa na matokeo hayo.
“Kweli
ni maajabu kwa mara ya kwanza kuna Division One kwenye CBG pale shuleni
kwetu, ni mafanikio ambayo yametokana na hamasa ya kuwepo kwa
mashindano haya ya sayansi na sisi tunashukuru kuwa sehemu ya
mafanikio,” anasema Diana.
Diana
na Nadhra ambao walipata ushindi kwa kubuni mashine ya kienyeji ya
kutotoresha mayai, pia walipata udhamini wa masomo ya chuo kikuu kutoka
taasisi ya Karimjee Jivanjee Foundation.
Wote
kwa pamoja walikuwa wanachukua mchepuo wa Kemia, Baolojia na Jiographia
(CBG) na kwa bahati nzuri, wote wawili wamepata Division Two ya alama
12.
Imeandaliwa na www.maendeleovijijini.
|
MWENYEKITI WA UVCCM KHERI D JAMES AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI MBALI MBALI WA UVCCM MKOA WA DAR ES SALAAM.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg.Kheri Denis James(MCC) akizungumza kwa Msisistizo wakati wa kikao na Wajumbe wa kamati ya Utekelezaji ya mkoa wa dar esa salaam pamoja na Baraza kuu la Vijana Wilaya ya Kinondoni, kulia ni Kaimu Katibu mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar Es Salaam Mussa Kilakala,Katika Ofisi ndogo ya Makao makuu ya UVCCM Upanga Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg.Kheri Denis James(MCC) akizungumza wakati wa kikao na Wajumbe wa kamati ya Utekelezaji ya mkoa wa dar esa salaam pamoja na Baraza kuu la Vijana Wilaya ya Kinondoni ,Katika Ofisi ndogo ya Makao makuu ya UVCCM Upanga Dar es Salaam.
Kaimu Katibu mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akizungumza wakati wa kikao na Wajumbe wa kamati ya Utekelezaji ya mkoa
wa dar esa salaam pamoja na Baraza kuu la Vijana Wilaya ya Kinondoni
,Katika Ofisi ndogo ya Makao makuu ya UVCCM Upanga Dar es Salaam.
Baadhi ya Wajumbe wakifuatilia kwa Umakini kikao hicho.
kikao kikiendelea.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg.Kheri Denis
James(MCC) akizungumza kwa Msisistizo wakati wa kikao cha Viongozi wa Seneti Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na Viongozi wa Matawi yote ya Vyuo na vyuo vikuu mkoa wa Dar es Salaam , kulia ni Kaimu Katibu mkuu wa UVCCM Taifa
Shaka Hamdu Shaka na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar Es Salaam Mussa
Kilakala,Katika Ofisi ndogo ya Makao makuu ya UVCCM Upanga Dar es
Salaam.
Sehemu ya Wajumbe wa Vyuo na Vyuo Vikuu wakifurahia jambo(PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)
....................................................................................................................................................................
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Cha
Mapinduzi Ndugu Kheri Denis James (MCC) leo amekutana na kufanya mazungumzo na
kamati ya Utekelezaji ya Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na wajumbe wa Baraza la
Vijana (UVCCM) Wilaya ya Kinondoni kuzungumzia maandalizi ya Uchaguzi wa
marudio utakaofanyika tarehe 17 Februari, 2018.
Pamoja na mambo mengine Mwenyekiti
amesisitiza kuwa nguvu ya Vijana wa CCM itumike vizuri katika kuhakikisha
CCM inashinda kwa kishindo Uchanguzi huo.
''Suala la ushindi wa CCM katika
uchaguzi huu wa marudio halina mjadala tutashinda kwa heshima, Amani na demokrasia vijana wa CCM tumejipanga vyema
kufanikisha hilo ngazi zote" Alisisitiza Mwenyekiti Kheri
Wakati huo amekutana na kufanya
mazungumzo na Viongozi wa Seneti ya Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Dar es Salaam
pamoja na Viongozi wa Matawi yote ya Vyuo na Vyuo Vikuu vilivyopo Mkoa wa Dar
es Salaam. ''Tunatambua na kuthamini
mchango wa Vijana wenzetu wote katika jamii mkiwemo ninyi wa Vyuo na Vyuo Vikuu
tunawategemea sana hivyo tutaendelea kufanya kazi nanyi katika maeneo yote
katika kutimiza wajibu wetu wa msingi” Alibainisha Mwenyekiti Kheir.
Mazungumzo
hayo yamehudhuriwa na Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka,
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam Mussa Kilakala, Mwenyekiti wa Seneti
Mkoa wa Dar es Salaam Asha Feruzi pamoja na Mjumbe wa Baraza kuu Taifa Alex
Gwantwa.
MAKAMU WA RAIS AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MIRADI YA UKUTA WA BAHARI KATIKA ENEO LA KIGAMBONI NA OCEAN ROAD
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati
alipokagua maendeleo ya ujenzi wa ukuta wa bahari Kigamboni wenye urefu
wa mita 500. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongozana na Meneja wa
Mradi na Miundo Mbinu wa UNOPS Bw. Bernard Odhuno wakati wa ukaguzi wa
maendeleo ya ujenzi wa ukuta wa bahari Kigamboni wenye urefu wa mita
500. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ameketi kwenye moja
ya sehemu za kupumzikia pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais
Muungano na Mazingira Mhe.January Makamba(kulia) pamoja na Mkuu wa Mkoa
wa dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa
maendeleo ya ujenzi wa ukuta wa bahari Kigamboni wenye urefu wa mita
500. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Waziri nchi Ofisi ya Makamu wa
Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akifafanua jambo mbele
ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu
Hassan pamoja na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda wakati
wa ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa ukuta wa bahari Ocean Road. (Picha
na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akipokewa na Mkuu wa Mkoa wa
Dar es Salaam Paul Makonda mara baada ya kuwasili katika Chuo cha
Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara
yake ya kukagua maendeleo ya mradi wa Uimarishaji wa Kingo za Bahari
ambao mradi unatekelezwa katika eneo la Kingo ya Bahari iliyopo Chuoni
hapo yenye urefu takribani mita 400. Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Makamu wa Rais Mazingira a Muungano January Makamba.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akizungumza wakati wa ziara
yake ya kukagua maendeleo ya mradi wa Uimarishaji wa Kingo za Bahari,
mradi unatekelezwa katika eneo la Kingo ya Bahari iliyopo Chuo Kikuu
cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) yenye urefu takribani mita
400. Katikati ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira a
Muungano January Makamba.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu
wa Rais Mazingira na Muungano January Makamba akizungumza wakati wa
ziara ya Makamu wa Rais ya kukagua maendeleo ya mradi wa Uimarishaji wa
Kingo za Bahari katika eneo la Kingo ya Bahari iliyopo Chuo Kikuu cha
Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) yenye urefu takribani mita 400 leo
jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Paul Makonda akielezea jambo wakati wa ziara ya Makamu wa Rais ya
kukagua maendeleo ya mradi wa Uimarishaji wa Kingo za Bahari, mradi
ambao unatekelezwa katika eneo la Kingo ya Bahari iliyopo Chuo Kikuu
cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA) yenye urefu takribani mita
400.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kuhusu
maendeleo ya ujenzi wa mradi wa Uimarishaji wa Kingo za Bahari kutoka
kwa mmoja wa wakandarasi wa mradi huo wakati wa ziara yake ya kukagua
maendeleo ya mradi huo leo Jijini Dar es Salaam. Mradi huo wa Kuimarisha
Kingo za Bahari unatekelezwa katika kingo za Chuo Kikuu cha Kumbukumbu
ya Mwalimu Nyerere(MNMA) Kigamboni yenye urefu wa mita 400, Sea View
yenye urefu wa mita 900 na Pangani Tanga.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akipita juu ya Kingo ya Bahari
iliyojengwa kupitia mradi wa uimarishaji wa Kingo za Bahari
alipotembelea Fukwe ya Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere
(MNMA) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam leo. Fukwe hiyo
imefanyiwa maboresho ambapo kingo yake imejengewa njia ya wapita kwa
miguu na sehemu za kupumzikia.
Sehemu ya Kingo iliyojengwa
katika fukwe ya bahari ya hindi eneo la Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya
Mwalimu Nyerere (MNMA) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa akiwa katika picha ya
pamoja na wajumbe wa Kamati ya Siasa wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya
Kigamboni alipokutana nao wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya
mradi wa Uimarishaji wa Kingo za Bahari, mradi unaotekelezwa katika eneo
la Kingo ya Bahari iliyopo Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu
Nyerere (MNMA) yenye urefu takribani mita 400. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam Paul Makonda na Kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar
es Salaam Kate Mfutakamba. (Picha na Frank Shija – MAELEZO)
Ujenzi wa Ukuta wa bahari katika eneo la umekamilika kwa zaidi ya asilimia 90. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
MKAZI WA DAR NA KIGOMA WAJISHINDIA KITITA CHA MILIONI 10 KILA MMOJA
.Akizungumza na waandishi habari wakati wa kukabidhi hundi hizo kwa washindi hao , mapema leo mbelee ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani),Mmoja wa Maofisa Habari wa Tatu Mzuka, Millard Ayo alisema droo hiyo inachezwa kila siku,huku wenye bahati zao wakiendelea kujinyakulia vitita vyao vya Tatumzuka.Milard amewaasa Watanzania waendelee kucheza kwa wingi na mara kwa mara mchezo huo,kwani ukiibuka mshindi maisha yake huinuka na kuwa bora zaidi tofauti na alivyokuwa hapo awali.Mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka umetoa washindi wawili wa sh.
Milioni 10 katika droo inayochezwa kila siku,mmoja akitokea jijini Dar
na mwingine akitokea mkoani Kigoma
Mmoja wa Maofisa habari wa mchezo wa Kubahatisha wa Tatumzuka,Millard Ayo akimkabidhi mfano wa hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka inayofanyika kila siku ,Harieth Steven (21) mkazi wa Kigoma ambaye anajishugulisha na kazi za ndani (housegirl),mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .
Mmoja wa Maofisa habari wa mchezo wa Kubahatisha wa Tatumzuka,Millard Ayo akimkabidhi mfano wa hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka inayofanyika kila siku ,Harieth Steven (21) mkazi wa Kigoma ambaye anajishugulisha na kazi za ndani (housegirl),mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .
Harieth Mwenye mtoto mmoja alifurahia kujishindia donge hilo kupitia mchezo wa kubahatisha wa Tatumzuka,kwani baada ya kutaarifiwa kuwa amejishindia kiasi hicho cha fedha,akajipa matumaini ya kuwa ndoto yake ya kufanya biashara ya vitenge sasa inakwenda kutimia rasmi,na kuacha kufanya kazi za ndani.
Mmoja wa Maofisa habari wa mchezo wa Kubahatisha wa Tatumzuka,Millard Ayo akimkabidhi mfano wa hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Ally Rashid (26) mkazi wa Yombo Buza ambaye anajishugulisha na biashara ya kuuza Mboga mboga jijini Dar,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .
--
Ahmad Issa Michuzi
Editorial Director
P.O BOX 9033,
DAR ES SALAAM.
issamichuzi.blogspot.com
www.michuzijr.blogspot.com
othmanmichuzi.blogspot.com
Phone:0713 422 313/ 0783 422 313
Tanzania- East Africa.Mmoja wa Maofisa habari wa mchezo wa Kubahatisha wa Tatumzuka,Millard Ayo akimkabidhi mfano wa hundi ya sh.milioni 10 kwa mshindi wa droo ya Tatu Mzuka ,Ally Rashid (26) mkazi wa Yombo Buza ambaye anajishugulisha na biashara ya kuuza Mboga mboga jijini Dar,mapema leo kwenye mkutano na Wanahabari (hawapo pichani),uliofanyika leo jijini Dar .
WCF YAWANOA WAAMUZI, WASULUHISHI NA MAKATIBU MUHTASI KUTOKA TUME YA USULUHISHI NA UAMUZI (CMA)
Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw.Peter Kalonga, (kushboto), akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, (wkawanza kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw.Shanes Nungu, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa Waamuzi, Wasuluhishi na
Makatibu Muhtasi kutoka Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) mjini Morogoro leo Januari 17, 2018. Bw. Kalonga alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw. Eric Shitindi.
Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw.Peter Kalonga,kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Eric Shitindi, akifungua mafunzo hayo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akitoa hotuba yake. |
NA
K-VIS BLOG/Khalfan Said, Morogoro
MFUKO
wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), umejipanga vema kuendelea kutoa huduma bora
kwa wadau, hususan katika kipindi hiki ambacho Mfuko unategemea ongezeko kubwa
la waajiri na wafanyakazi, kutokana na mkakati wa Serikali ya awamu ya tano wa
kujenga uchumi wa viwanda, ambao utaongeza ajira.
Hayo
yamesemwa leo Januari 17, 2018 mjini Morogoro na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia
kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku
tatu kwa Waamuzi, Wasuluhishi na Makatibu Muhtasi kutoka Tume ya Usuluhishi na
Uamuzi (CMA), ili kuongeza ujuzi kwenye utekelezaji wa majukumu ya Tume.
“Katika
jambo hili la kujenga uchumi wa viwanda, makampuni mengi yataanzishwa, kutakuwa na
waajiri wengi, ongezeko la wafanyakazi, kwa hivyo unategemea kwamba hitajio la
utoaji huduma za Mfuko kwa wadau litaongezeka
na Mfuko umekuja wakati muafaka na tupo kwa ajili ya kuwahudumia wale wote
watakaopatwa na majanga mahala pa kazi lakini pia kuelimisha.” Alisema Bw. Mshomba.
Bw.
Mshomba alisema, kuanzia Julai, 2016 Mfuko
ulianza kupokea madai ya Fidia yanayotokana na kuumia au kuugua mahali pa kazi.
“Jambo
hili si rahisi kwa sababu ndio linaanza kwa hivyo tunahitaji ushirikiano wa
karibu sana kutoka kwa wadau mbalimbali mkiwemo ninyi CMA, na katika hilo
ushirikiano tu hautoshi Mfuko umekuwa ukitoa elimu ili kuwawezesha watu wajue Mfuko umeanzishwa kwa sababu gani, kazi
zake, lakini pia kujua taratibu za kudai fidia pale mfanyakazi anapopatwa na
majanga ya kuumia au kuugua wakati akitekeleza wajibu wake wa kikazi.” Aliongeza
Bw. Mshomba.
“Ndio
maana leo hii tunao wataalamu wetu watakaotoa mada mbalimbali zikiwemo, Sheria
za Fidia, Namna Fidia inavyolipwa lakini shughuli za Mfuko.” Alibainisha
Mkurugenzi Mkuu Bw. Mshomba.
Aidha
aliishukuru Tume kwa kuwashirikisha WCF ili kuwaelimisha wafanyakazi wake kutoka
mikoa yote ya Tanzania bara.
“Ni
muhimu kwetu sisi kuwaelimisha wadau kuhusu shughulim zetu na ndio maana huwa
tuko tayari wadau wetu wanapotualika ili kutoa elimu hiyo.” Alisema.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa ……..kwa niaba ya Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu,
Kazi, Vijana, Ajira, na Wenye Ulemavu, Bw. Eric F. Shitindi amewahimiza
washiriki wa kuzingatia elimu watakayoipata kwenye mafunzo hayo ili hatimaye
watekeleze ipasavyo malengo ya serikali ya awamu ya nne ya kujenga uchumi wa kati
ifikapo mwak 2025.
“Ni
matarajio yetu kwamba Tume na Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, mnao wajibu
mkubwa sana katika kufanikisha azma hiyo ya serikali kama nyinyi mtatekeleza
wajibu wenu.” Alisema.
Baadhi ya washiriki.
Baadhi ya washiriki.
Mwenyekiti wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw.Edrisa Mavura, akitoa hotuba yake.
Maafisa wa CMA wakiteta jambo.
Bw. Mshomba, (kulia), na Bw.Nungu, wakijadili jambo.
Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Bw.Peter Kalonga, akikaribishwa na Wakurugenzi wa WCF, Bw. Masha Mshomba, (kulia) na wa CMA, Bw.Shanes Nungu, alipofika kufungua mafunzo hayo
Bw. Mshomba akijibu baadhi ya maswali ya washiriki kuhusu shughuli za Mfuko.
Baadhi ya washirtiki wakifuatilia mafunzo.
Kamishna wa Tume, Bi.Suzanne Ndomba, (kulia), akizungumza kwenye mafunzo hayo. Wengine ni Makamishna wenzake, kutoka kushoto, Bw.Kibwana Njaa, Bw.Jones Majura na Bw.Jaffary Ally Omar.
Picha ya pamoja.
Bw. Mashomba akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Sheria wa WCF, Bw. Abraham Siyovelwa, (katikati) na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulsalam Omar.
Washiriki wakipitia vipeperushi vya WCF.
WATOTO YATIMA 150 WAPATIWA MSADA WA VIFAA VYA SHULE
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akiwaasa watoto yatima wa kituo cha Bethel Wilayani Gairo. Kulia kwake ni baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama walioambatana naye.
Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo, Mhe. Andrea Sendeha akitoa salamu kwa watoto yatima.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe akigawa zawadi kwa watoto yatima wa kituo cha Bethel kilichopo wilayani humo.
Watoto wa kituo cha Bethel Wilayani Gairo wakiwa wamejipanga mstari kupokea zawadi.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo, Mhe. Siriel Mchembe (mwenye nguo ya njano), Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mji Mdogo Gairo, Mhe. Andrea Sendeha (wa tatu toka kulia) pamoja na kamati ya ulinzi na usalama wakiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wa kituo cha Bethel wa Gairo.
MPINA AKAMATA MAROBOTA 1152 YA NYAVU HARAMU MWANZA NA SINGIDA ZENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 894.
Waziri
wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina (mwenye miwani na kofia )akisikiliza
jambo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Ukerewe, Frank
Bahati (kushoto) wakiwa kwenye boti ya doria kutoka katika kijiji Kakukuru
wakielekea kwenye kambi ya uvuvi ya Kisiwa cha Galinzila ambapo
Mhe.Waziri alifanya mkutano na wavuvi . Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe
Estomiah Chang’a. (Na John Mapepele)
Mmliki wa ghala lenye shehena ya marobota 600 ya nyavu haramu
za kuvulia samaki zisizoruhusiwa kisheria zenye thamani ya shilingi
milioni mia tano, Meshaki Chacha akihojiwa na Mwandishi
wa Habari wa ITV baada kikosi kazi kilichoundwa na Waziri wa Mifugo
na Uvuvi, Mhe. Luhaga Mpina(mwenye kofia) kuvamia ghala lake lililopo
jijini Mwanza leo. Ametakiwa kulipa faini ya shilingi milioni
50 ndani ya masaa 24 leo. (Na John Mapepele)
- Aapa kutokomeza uvuvi haramu nchini
- Asema imebaki 3% tu ya Sangara wanaokubalika kuvuliwa katika ziwa Victoria
Na
John Mapepele
Waziri wa Mifugo na
Uvuvi, Mhe Luhaga Joelson Mpina amekamata marobota 1152
ya aina mbalimbali za nyavu haramu zisizoruhusiwa kisheria
kutumika kuvulia samaki zenye thamani ya shilingi milioni 894
jijini Mwanza na Singida ambapo baadhi ya nyavu hizo zimetaifishwa
na nyingine kuteketezwa na wamiliki wakitakiwa kulipa faini ya
shilingi milioni 120 ndani ya masaa 24 kwa makosa ya kufanya biashara
ya nyavu hizo kinyume cha sheria.
Akiongea na Vyombo
vya Habari jijini Mwanza katika ghala la nyavu la Meshack Chacha
mara baada ya kukamata shehena ya marobota 600 ya nyavu haramu
kwenye ghala lake, Mhe. Mpina alisema nyavu haramu 294 kati ya 894 zilikamatwa
na kikosi kazi maalum cha kudhibiti uvuvi haramu katika kanda ya Ziwa
Victoria alichokiunda hivi karibuni wakati mmoja wa wafanyabiashara
hao Masagati Majani alijaribu kutorosha vyavu hizo kwa kutumia gari
aina ya Scania lenye namba za usajili T.452 BBS kutoka Mwanza kuelekea
Dar es Salaam.
Gari hilo lipo katika
kituo cha polisi cha Singida kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria ambapo
kulingana na sheria ya Uvuvi namba 22 ya mwaka 2003, imetoa
mamlaka kwa watendaji wa Serikali kutaifisha mali zote zilitumika katika
uvuvi haramu kupitia kifungu cha 37(a) (ii) na (iii)
Aliwataja wamiliki wengine
ambao walikamatwa kutokana na kujihusisha na biashara haramu ya
uagizaji na uuzaji wa vyavu zisizoruhusiwa kisheria kuwa ni Josia Jonam
Obielo, Jeremiah Asam na Dastun Venant ambapo alisema Serikali imejipanga
kuhakikisha kwamba wafanyabiashara wote wanao agiza
na kuuza zana haramu za uvuvi wanakamatwa na sheria kali zinachukuliwa
ili kudhibiti uvuvi haramu nchini.
“Niliapa kusimamia
ulinzi wa raslimali za uvuvi nchini hivyo nitahakikisha operesheni
hii inakuwa ya kudumu katika kupambana na uvuvi haramu hadi uvuvi
haramu utakapokwisha” alisisitiza Mpina
Katika hatua nyingine
Waziri Mpina amelaani kitendo Kiwanda cha Sunflag cha mkoani
Arusha kwa kuendelea kufadhili uvuvi haramu nchini kutengeneza na kuuza
vyavu za kuvulia samaki zisizoruhusiwa kisheria wakati Serikali imekuwa
ikisisitiza viwanda vyote nchini kuacha tabia ya kufadhili uvuvi haramu
kwa kutengeneza zana haramu za uvuvi.
Waziri Mpina ameagiza
watalam kwenda mara moja katika kiwanda hicho kuchunguza ukweli
wa jambo hilo ili sheria zichukue mkondo wake.
Hivi karibuni Waziri
Mpina aliunda Kikosi maalum cha kupambana na uvuvi haramu ambapo katika
kipindi kisichozidi siku kumi na nne zaidi ya zana haramu za uvuvi ikiwa
ni pamoja na nyavu zenye jumla ya bilioni tatu zimeteketezwa katika
kanda ya ziwa Victoria peke yake huku viwanda vitano vya kusindika
samaki vilivyopo jijini Mwanza vikitakiwa kulipa jumla ya shilingi milioni
180 ndani ya masaa 24.
Viwanda hivyo vilitozwa
faini hiyo kutokana na kuendelea kuwa wafadhili wakuu wa uvuvi haramu
kwa kununua na kuchakata samaki aina Sangara wachanga na wazazi kinyume
cha Sheria ya Uvuvi.
Waziri Mpina alisema
Sheria ya Uvuvi namba 22 ya Mwaka 2003 na Kanuni zake za mwaka
2009 kifungu cha 90(1) inataka samaki wanaovuliwa waandaliwe katika
mazingira yanayokidhi vigezo vya usalama kwa mlaji na kwamba
ni kosa kisheria kuwavua au kuchakata samaki aina ya Sangara walio chini
ya sentimeta 50 kwa kuwa ni wachanga na sentimita 25kwa Samaki aina
ya Sato. Pia sentimita 85 kwa Sangara kwa kuwa ni wazazi wanaotakiwa
kundelea kuzaa.
Waziri Mpina alisema samaki aina ya Sangara kwenye
Ziwa Victoria wapo katika hatari ya kutoweka kabisa katika kipindi cha
miaka miwili endapo hali ya uvuvi haramu ukiachwa uendelee bila
kuchukua hatua za haraka na madhubuti kudhibiti janga hili.
Alisema kulingana na utafiti uliofanywa na
Taasisi ya Utafiti wa Samaki Tanzania (TAFIRI) 2017 unaonesha kuwa samaki
wachanga waliochini ya sentimita 50 wasioruhusiwa kuvuliwa ni asilimia
96.6 , samaki wazazi walio zaidi ya sentimita 85 ambao pia hawarusiwi
kuvuliwa ni asilimia 0.4 na samaki wa sentimita 50 mpaka 85 ambao ndio
wanafaa kuvuliwa ni asilimia 3 tu hivyo juhudi za pamoja za wadau wote
wa sekta ya uvuvi zinahitajika ili kurejesha raslimali ya uvuvi katika
Ziwa Victoria kwa faida ya vizazi vya sasa na baadaye.
Subscribe to:
Posts (Atom)