Na Mwandishi Wetu, Handeni
BAADHI ya vyakula vya asili ya Handeni, vinatarajiwa
kuwapo katika Tamasha la Utamaduni la Handeni Kwetu 2013 linalotarajiwa
kufanyika Jumamosi hii katika Viwanja vya Azimio, wilayani Handeni, mkoani
Tanga.
Akizungumza jana mjini Handeni, Mratibu wa
Tamasha hilo, Kambi Mbwana, alisema kuwa tayari wametoa nafasi kwa wanaoweza kazi
hiyo kwa umakini na usafi wa aina yake ili kuliweka tamasha hilo kwenye mguso
wa aina yake.