Khadija Baragasha,Tanga.
WAMILIKI wa vyombo vya habari na Wahariri Nchini
wameombwa kuzipa kipaumbele habari
zinazohusu unyanyasaji na ukatili kwenye vyombo vyao ili
jamii iweze kuelimika na kutambua athari
na kuepuka matendo hayo mabaya
Aidha waandishi wa habari nchini wameshauriwa
kutotangaza habari za taasisi ama
vikundi ambavyo shughuli zake zinamuelekeo wa
kuifanya jamii iende kinyume
na maadili ya mtanzania.
Hayo yalielezwa na mwanaharakati maarufu Jijini hapa wa haki za binaadamu, Nuru Rajab wakati akitoa maoni yake kuhusu matukio ya
kinyama yanayotokea ndani ya jamii yanayokiuka mpaka haki za binaadamu.
Akizungumzia unyanyasaji huo aliyouelekeza hasa kwa mtoto na wanawake, Rajab alisema kuwa unyanyasaji ni kitendo kisichokubalika ndani ya jamii na taifa kwa
ujumla na kwamba elimu ya ubaya na athari zake ni vema ikatangazwa kwa upana
zaidi na kupewa kipaumbele katika vyombo vya habari.