WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI WAOMBWA KUZIPA KUPAUMBELE HABARI ZA UNYANYASAJI NA UKATILI.

January 08, 2014
Khadija Baragasha,Tanga.
WAMILIKI wa vyombo vya habari na Wahariri Nchini  wameombwa kuzipa kipaumbele  habari zinazohusu unyanyasaji na ukatili kwenye vyombo vyao  ili  jamii iweze kuelimika na kutambua athari  na kuepuka matendo hayo mabaya
Aidha waandishi  wa habari nchini wameshauriwa kutotangaza  habari za taasisi ama vikundi ambavyo shughuli zake zinamuelekeo wa  kuifanya jamii iende  kinyume na  maadili ya mtanzania.
Hayo yalielezwa na  mwanaharakati maarufu Jijini hapa  wa haki za binaadamu, Nuru Rajab  wakati akitoa maoni yake kuhusu matukio ya kinyama yanayotokea ndani ya jamii yanayokiuka mpaka  haki za binaadamu.
Akizungumzia  unyanyasaji huo aliyouelekeza hasa  kwa mtoto na wanawake, Rajab  alisema kuwa unyanyasaji ni kitendo  kisichokubalika ndani ya jamii na taifa kwa ujumla na kwamba elimu ya ubaya na athari zake ni vema ikatangazwa kwa upana zaidi na kupewa kipaumbele katika vyombo vya habari.

MWALALA:NILIWEKA HISTORIA YA MIAKA SABA YANGA KUIFUNGA SIMBA.

January 08, 2014
NAKUMBUKA bao ambalo nililifunga wakati nimesajiliwa na Yanga liliweka rekodi ya kufuta uteja wa timu hiyo kwa wapinzani wao Simba kwa kipindi cha miaka saba iliyopita kwa kufunga bao na hivyo kupelekea shangwe na nderemo katika mitaa ya Jangwani.

Kauli hii aliitoa mshambuliaji wa zamani wa Yanga,Benard Mwalala ambaye kwa sasa ni kocha mkuu wa timu ya Halmashauri FC ya Muheza anasema baada ya kufunga bao hilo alishangaa kuona uwanja mzima ukilipuka kwa kelele kitendo ambacho kilimfanya kuhisi upinzani wa timu hizo mbili ni mkubwa sana.

KIWANDA CHA UTENGENEZAJI WA BERI ZA MAGAIRI,BETRI ZA SIMU KUFUNGULIWA HANDENI.

January 08, 2014
UJENZI wa mradi wa kiwanda cha kwanza Nchini Tanzania Kilichopo katika kijiji cha Mkalamo Kata ya Kwamsisi Wilayani Handeni Mkoani Tanga kinachojishugulisha na maswala ya utengenezaji wa betri za magari, betri za simu pamoja na bidhaa mbalimbali kupitia madini ya Grafait (KINYWE) kipo mbioni kufunguliwa na kuanza shuguli za uzalishaji mwanzoni mwa mwaka ujao hali ambayo itakuza uchumi wa Nchi yetu na Taifa kwa ujumla.

 Mmoja wa wamiliki wa kiwanda hicho kijulikanacho kwa jina la SinoTan Minning Industry ltd Mussa Luhezi huku akishirikiana na wachina alisema kuwa wapo kwenye hatua za mwisho za kufunga mashine kubwa za uzalishaji na baada ya hapo wananchi wa eneo hilo watapewa kipaumbele ya kufanya kazi katika kiwanda hicho. 

Akifafanua juu ya mradi huo Mussa alisema kuwa kupitia madini hayo watatumia teknolojia ya kutumia betri hizo katika gari bila kutumia disel au petrol lakini kwa sasa hivi wameanza na kutengeneza tofali za kuzuia moto kwenye nyumba za makazi huku wakiendelea na juhudi za kuomba kibali serikalini cha kuzalisha betri hizo.