Benki ya Watu iwa Zanzibar PBZ Yaibuka Kidedea Katika Mwajiri Bora Katika Ushirikishwaji na Chama cha Wafanyakazi ZAFICOW

July 30, 2017
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi ZAFICAW Bi. Rihii Haji Ali, akimkabidhi Cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh cha Mwajiri Bora Katika Ushirikiano na ZAFICOW kwa mwaka 2017. wakati wa hafla ya Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi ZAFICAW Bi. Rihii Haji Ali, akimkabidhi Cheti Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh cha Mwajiri Bora Katika Ushirikiano na ZAFICOW, wakati wa hafla ya Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
 Viongozi wa PBZ na wa ZAFICOW wakiimbi wimbo wa ushirikiano wa Wafanyakazi wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa Cheti zilizofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Zanzibar. 
Wafanyakazi wa Benki ya Watu wa Zanzibar wakiimbi wimbo wa Wafanyakazi wa Mshikamano wakati wa mkutano wao na Mwenyekiti wa ZAFICOW wakati wa hafla ya bonaza la Michezo lililowashirikisha Wafanyakazi wa PBZ, 
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Bi. Rihii Haji Ali akitzungumza wakati wa mkutano huo na wafanyakazi wa PBZ kujuwa wajibu wao katika kazi na kuwataka kujiunga na Chama hicho kwa faida yao na maslahi kwa muajiri wao.Pia alikabidhi Kadi kwa Wanachama wapya ya PBZ 10 waliojiunga na kuwakabidhi Kadi za Uwanachama. 
Watendaji wa PBZ wakifuatilia mkutano huo na Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar Bi Rihii Haji Ali alipokuwa akizungumza na wafanyakazi hao wakati wa Tamasha la Bonaza la Wafanyakazi wa PBZ lililofanyika katika viwanja vya Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Wafanyakazi wa PBZ wakifuatilia mkutano huo na Uongozi wa PBZ na ZAFICOW uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Visiter Inn Jambiani.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Ndg. Suleiman Abdi, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Ndg. Bakari Hussein, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Bi. Fatima Ali Denge, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Juma Ameir Khafidh akimkabidhi Kadi ya Mwanachama mpya wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar ZAFICOW Bi. Mkunga Mohammed Saleh, baada ya kujiunga na Chama hicho wakati wa hafla hiyo iliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.
Mkurugenzi Mtendajio wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ngd Juma Ameir Khafidh akimkabidhi zawada ya fedha shilingi miliono moja kwa kuibuka Mfanyakazi Bora wa Benki ya Watu wa Zanzibar kwa mwaka 2017  Ndg. Juma Ameir Makame (kulia) akishuhudia Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar (ZAFICOW) Bi. Rihii Haji Ali hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mfanyakazi wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ndg.Haji Masoud, akikisoma Cheti cha Mwajiri Bora Katika Ushirikishwaji katika Chama  cha Wafanyakazi cha ZAFICOW, wakati wa kukabidhi na Uongozi wa ZAFICOW.  
Afisa Muandamizi Masoko wa Benki ya Watu wa Zanzibar PBZ Ndg. Anasi Rashid akizungumza na kutowa maelekezo wakati wa Mkutano huo wa Wafanyakazi na Uongozi wa Chama cha Wafanyakazi Zanzibar Wafanyakazi Zanzibar (ZAFICOW)  
Mkurugenzi Rasilimali Watu PBZ Ndg. Mohammed Omar (kulia) akimkabidhi zawadi maalum iliyotolewa na Wafanyakazi wa PBZ kwa Boss wao wakati wa Mkutano huo na Wafanyakazi wa PBZ Zanzibar hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Zanzibar. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Ndg Juma Ameir Khafidh akitowa nasaha zake kwa Wafanyakazi wakati wa mkutano huo ulioambatana na michezo mbalimbali iliowashirikishwa Wafanyakazi kujumuika pamoja na kubadilishana mawazo Bonaza hilo limefanyika katika ufukwe wa Hoteli ya Visiter Inn Jambani.Mkoa wa Kusini Unguja.  
Mkurugenzi Mtendaji wa PBZ Ndg. Juma Ameir Khafidh akisisitiza jambo wakati wa mkutano huo na Wafanyakazi uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Visiter Inn Jambiani Zanzibar.


Wafanyakazi wa PBZ wakipata viburudisho ya maji ya madafu baada ya mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Visiter Inn Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja.

Imeandaliwa na Othmanmapara.blog.
Zanzinews.com
othmanmaulid@gmail.com
Mobile.0777424152.

MBUNGE ROSE TWEVE WATENDAJI FANYENI KAZI ACHENI MAJUNGU

July 30, 2017
Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Rose Tweve akizungumza na madiwani na wananchi wa halmashauri ya Mafinga Mjini wakati wa baraza la madiwani
Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga akizungumza wakati wa baraza la madiwani lilofanyika katika ukumbi wa halmashauri hiyo
Baadhi ya madiwani,viongozi pamoja na wananchi waliohudhuria baraza la madiwani lilofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya Mafinga Mjini.

Na fredy Mgunda, Mafinga.

Mbunge wa viti Maalum mkoa wa Iringa kupitia chama cha mapinduzi CCM Rose Tweve amewata watendaji wa halmashauri ya Mafinga Mjini kufanya kazi kwa kujituma na kuwa tumikia wananchi wa Jimbo la Mafinga Mjini ambalo linaongozwa na mbunge Cosato Chumi.

Akizungumza wakati wa baraza la madiwani wa halmashauri ya Mafinga Mjini alisema kuwa watendaji wengi wamekuwa wakilalamikiwa kutokana na kufanya kazi chini ya kiwango na kuwapelekea wananchi kuwa na changamoto ambazo hazina sababu.

"Hivi watendaji kitu gani kinachosababisha msifanye kazi kwa weledi kama ambavyo mlivyokuwa mnaomba kazi,jamani serikali ya awamu ya tano haitaki mfanye kazi kwa mazoea kama zamani saizi mnatakiwa kufanya kazi kutokana na kasi ya kimaendeleo ya serikali ya awamu ya tano"alisema Tweve

Tweve alisema kuwa watendaji wanaohusika na sekta ya maji katika halmashauri ya Mafinga Mjini wamekuwa hawafanyi kazi kwa weledi kwani tatizo kuwabambikia bili wananchi limekuwa Sugu na kuongeza malalamiko mengi huko mitaani hivyo lazima mbadilike maana swala la bili limekuwa kero sana hapa Mafinga Mjini lazima mlitafutie ufumbuzi.

"Toka nimerudi nimekuwa nikipokea malalamiko mengi yanayohusu bili za maji naombeni tembeleeni nyumba kwa nyumba kuandika bili sahihi na sio kutoa bili kwa kukisia hii inaalibu sura nzima ya viongozi wa halmashauri ya Mafinga Mjini, narudia tena watendaji fanyeni kazi kwa kujituma acheni mazoea kazini"alisema Tweve

Aidha Tweve alimuomba Mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuhakikisha wanafanya kazi za wananchi na sio kukaa tu ofisini kitu kinachosababisha kuongezeka kwa matatizo kwa wananchi, hivyo mtalazimika kuwafuata wananchi kujua changamoto zinazowakabili wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Mafinga Mjini Charles Makoga alisema kuwa ahakikisha watendaji wote wanaenda kufanya kazi kwa wananchi na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kama ilivyokuwa miaka ya huko nyuma na kuendelea kutekeleza Sera za chama cha mapinduzi CCM na kuendena na kasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John pombe Magufuli na kuwaletea maendeleo wananchi.

"Watendaji wangu mmekisikia alichosema mbunge Rose Tweve kuhusu wajibu kwa kweli hii ni aibu kubwa inatupaswa kujilekebisha ili kuendelea kutekeleza Sera za serikali ya awamu ya tano la sivyo nitaanza kuwatumbua mmoja baada ya mmoja ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wa halmashauri ya Mafinga Mjini"alisema Makoga

Lakini Makoga aliwasifu wabunge Wawili ambao ni mbunge Cosato Chumi na Rose Tweve kwa kufanya kazi kwa nguvu na kuleta maendeleo ya wananchi wa wilaya ya Mufindi kwa ujumla maana kila siku tunapata mambo mapya ya kimaendeleo kupitia migongo yao na kuwaomba waendelee kutafuta njia nyingine za kuiletea maendeleo Mufindi.

"Miaka yote tungekuwa na wabunge kama hawa wawili leo hii Mufindi ingekuwa mbali sana kimaendeleo kutokana na Juhudi zao tunaziona maana saizi kila secta wameigusa kwa kuleta maendeleo au mikakati ya kutatua changamoto za maeneo husika" alisema Makoga

Nao baadhi ya watendaji wa halmashauri hiyo wasema kuwa bado wazitafutia ufumbuzi changamoto za Mji wa Mafinga licha ya kuwa na ufinyu wa bajeti za kimaendeleo kwenye miradi waliyoiomba hivyo wakipewa bajeti na kuajiri baadhi ya watumishi kila kitu kitaenda vizuri na changamoto za wananchi zitatuliwa kwa wakati.