BASHUNGWA AAGIZA UJENZI WA NJIA NNE BUKOBA KAZI IFANYIKE USIKU NA MCHANA
WAZIRI MKUU KUWA MGENI RASMI MKUTANO WA WADAU WA ANGA
Na Sophia Kingimali
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa anatarajia kuwa Mgeni rasmi kwenye mkutano mkubwa wa wadau wa Anga ambao watajadili mambo mbalimbali na
na namna walivyojipanga kuendeleza sekta ya anga na kuwa chachu ya uchumi wa Taifa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 20 ya mamlaka ya Usafiri wa Anga TCAA
Hayo yamebainishwa leo Oktoba 29, 2023 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA), Hamza Johari wakati akizungumzia miaka 20 ya mamlaka hiyo ambapo amesema waliamua kuandaa mbio za TCAA Fun Run 2023 katika mbio hizo ambazo wakinbiaji watashiriki katika mbio za kilomita 5 na 10.
Amesema Mamlaka hiyo ilianzishwa mwaka 2003 kufikia mwaka huu imetimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake hivyo wanaangalia miaka 20 walikotoka na 20 wanakokwenda.
“Kesho tunatarajia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kufungua mkutano wa wadau wa Anga na kusherekea miaka 20 ya TCAA na wadau wa anga kwa kutathimini mafanikio tuliyopata na changamoto zinazotukabili, “amesema Johari.
Amesema jukumu lao ni kuhakikisha wadau wa anga wanafanya shughuli kwa kufuata taratibu na sheria zilizowekwa.
Amesema watu walikuwa wanakimbia vizuri na walijiaanda na mbio hizo katika kuweka mwili vizuri na afya njema.
Ametoa wito kwa watanzania wote kujali sana afya zao kwa kula vizuri na kufanya mazoezi kwa sababu ni tiba na yawe sehemu ya maisha yetu.
“Tukiendelea kufanya mazoezi mara kwa mara tutaepukana na magonjwa nyemelezi ambayo yanaweza kuhatarisha afya zetu,” amesema .
Aidha amewashukuru wana TCAA na wadau wengine ambao wamewaunga mkono katika mbio hizo.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Ubungo, Hashim Komba amesema kuwa miaka 20 ya TCAA ni mageuzi ya Sekta ya anga.
“Leo tulikuwa tunasherekea miaka 20 ya TCAA kwa kukimbia mbio za TCAA Fun Run 2023 kufanya mazoezi ni kuimarisha afya ya akili zetu, “amesema Komba.
Amesema TCAA inatoa huduma kwenye viwanja vya ndege 15 nchi nzima na amempongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha viwanja vya ndege.
LAKE MANYARA MARATHON 2023 FURSA MPYA YA UTALII HIFADHI YA TAIFA ZIWA MANYARA
Na. Jacob Kasiri - Manyara.
Mkuu wa Wilaya ya Monduli Mhe.Joshua Nassari ameshiriki mbio za Lake Manyara Marathon 2023 na kusema kuwa ni fursa mpya ya utalii ndani ya Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara, hifadhi inayosifika kwa kuwa na Simba wengi wanaoparamia miti.
Mhe. Nassari alisema "kwa mara ya kwanza Wilaya ya Monduli imeandaa Marathon hii kwa lengo la kufungua fursa mpya ya utalii katika hifadhi yetu na kuongeza mzunguko wa fedha katika wilaya yetu".
"Kwakuwa eneo la Mto wa Mbu liko kimkakati wa kiutalii ndio imekuwa sababu kubwa ya kuvuta watu wengi kiasi hiki. Na tumeona kuanzia tarehe 27.10.2023 wakimbiaji walianza kuwasili hii yote imeongeza pato kwa taifa na mtu mmoja mmoja", aliongeza Mhe. Nassari.
Mbio hizi ndefu (Marathon) licha ya kuongeza fursa za kifedha kwa jamii pia, huimarisha afya na kuondoa magonjwa nyemelezi na kutoa mwanya kwa makampuni makubwa ikiwemo TANAPA kujitangaza na kupata wateja wanaowahitaji.
Afisa Mhifadhi Mkuu Kitengo cha Maendeleo ya Biashara Makao Makuu - TANAPA, Augustine Massesa alisema utalii huu wa michezo umeanza kushika kasi kwa miaka ya hivi karibuni. "Hivyo, niwaase na kuwashauri watanzania kujitokeza kwa wingi kushiriki, licha ya kuimarisha afya pia inakuza utalii".
Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Eva Mallya alisema mbio hizi ni fursa kwetu kwa sababu baadhi ya washiriki wamehamasika kuingia hifadhini na kuliingizia Taifa mapato.
"Kwa niaba ya hifadhi tunamshukuru Mkuu wa Wilaya yetu Mhe. Joshua Nassari na waandaaji wa Marathon hii, kwa kipindi chote cha uamasishaji kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii imeleta tija kwa hifadhi yetu.
Mbio hizo zenye lengo la kuhamasisha utalii zilizobeba kaulimbiu "Tukimbie Tukitalii" zimefanyika leo tarehe 29.10.2023 zikianzia katika Lango la Hifadhi ya Taifa Ziwa Manyara iliyopo Mto wa Mbu mkoani Manyara.
WAZIRI KAIRUKI AMUAPISHA CC MPYA WA NCAA NA KUSISITIZA USIMAMIZI WA SHERIA ZA UHIFADHI.
Kassim Nyaki, Karatu.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angellah Kairuki (Mb) leo tarehe 29 Oktoba, 2023 amemuapisha Bw. Richard Rwanyakaato Kiiza kuwa kamishna wa Uhifadhi wa mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) baada ya Uteuzi uliofanywa na mhe. Rais hivi karibuni.
Katika tukio hilo Mhe. Waziri amebainisha kuwa Uteuzi wa Kamishna huyo ni sehemu ya kuimarisha majukumu ya Uhifadhi, utalii na maendeleo ya Jamii na kuongeza kasi ya kutangaza utalii kwa njia mbalimbali za kisasa ili kuongeza idadi ya wageni wanaotembelea nchi yetu kama ilivyo adhima ya Mheshiwa Rais wetu.
Waziri Kairuki ameilekeza bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kusimamia sheria za uhifadhi ikiwemo kutoa mifugo yote iliyoingiza kinyemela katika maeneo yaliyohifadhiwa ikiwemo Pori tengefu la Loliondo.
“Pamoja na majukumu mengine mliyonayo nawaelekeza wahifadhi kusimamia sheria zilizopo na kuhakikisha mifugo iliyoangizwa kinyemelea katika maeneo ya Hifadhi iondolewe” amesisitiza mhe. Kairuki
Aidha Mhe. Kairuki amempongeza Kamishna wa Uhifadhi aliyemaliza muda wake, Dkt. Freddy Manongi kwa juhudi ambazo wamezifanya katika kutangaza Vivutio vya utalii tulivyonavyo ambapo juhudi hizo zimeiwezesha Hifadhi ya Ngorongoro (NCA) kuchaguliwa na mtandao wa “Word Travel Awards” kama kivutio bora cha Utalii barani Afrika “Africa Leading tourist Attractions” na mafanikio ya kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia wageni zaidi ya 752,000, kuongeza mapato hadi kufikia Bilioni 171 mwaka wa fedha 2022/2023
Vilevile Mhe. Kairuki amemuelekeza Kamishna wa Uhifadhi NCAA na wadau wengine wanaohusika na zoezi la zoezi la uelimishaji, uandikishaji, uthaminishaji na uhamishaji wa wananchi wa eneo la Hifadhi ya Ngorongoro wanaojiandikisha kuhama kwa hiari kuendelea kusimamia eneo hilo kwa kufuata sheria na misingi ya haki za binadamu.
“Serikali inaendelea kuwahakikishia Wadau mbalimbali, Wananchi wa Ngorongoro na Jumuiya za Kimataifa kuwa zoezi hili ni la hiari, shirikishi na linazingatia misingi ya haki za kibinadamu na utawala bora na kila mwananchi aliejiandikisha kuhama kwa hiari Serikali itampa fidia na gharama zote za kumhamisha hadi alipochagua kwenda zinabebwa na Serikali kwa asilimia 100” amesisitiza mhe Kairuki.
JUMUIYA YA WAZAZI (CCM) WILAYA YA TANGA WAMPONGEZA DKT TULIA
Na Oscar Assenga, TANGA
JUMUIYA ya Wazazi ya
Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga imepongeza Spika wa Bunge Dkt Tulia
Ackson kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) huku
wakihaidi kuendelea kumuunga mkono na kumuombea kwa Mwenyezi Mungu katika
majukumu yake hayo.
Pongezi hizo
zilitolewa leo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga Hamza Bwanga
wakati akizungumza na mtandao huo ambapo alisema kwamba wanaamini kwamba
kuchaguliwa kwake kumekuja wakati muafaka kutokana na utendaji wake mahiri
katika kuongoza Bunge la Tanzania.
Alisema kuchaguliwa
kwake ni kutokana na jitihada zake katika utendaji wake ambao umejengwa na
uchapakazi, uzoefu, uaminifu na uadilifu ambao umekuwa ni chachu kubwa kufikia
mafanikio hayo.
“Sisi kama Wazazi
wilaya ya Tanga tunakupongeza sana Spika wa Bunge kuwa kuchaguliwa kwake kuwa
Rais wa umoja huo na tunahaidi kumuunga mkono na nafasi hii imekuja wakati
muafaka kabisa kwa kuwa yeye ni spika na mchakapazi,mwerevu msikivu “Alisema
Hata hivyo alisema
kwamba wao wataendelea kumuunga mkono na kumuombe kwa mwenyezi mungu ili kutenda
vema majukumu yake kwa waledi mkubwa .
Kijani Bond ya Benki ya CRDB yaorodheshwa DSE baada ya kufanikiwa kukusanya Sh. 171.82 bilioni kufadhili miradi inayotunza mazingira
Akiwashukuru wawekezaji waliojitokeza kwa imani waliyonayo na ushirikiano walioutoa hata kuwezesha mauzo hayo kuvuka malengo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema kiasi kilichokusanywa kimeongeza mtaji mpya ndani ya taasisi hiyo kwa Shilingi bilioni 140 zitachochea utoaji wa mikopo kwenye miradi inayolenga kulinda mazingira nchini.