MATUKIO YA PICHA YA MECHI YA SIMBA NA COASTAL UNION MKWAKWANI LEO

February 07, 2015
KIKOSI CHA COASTAL UNION KILICHOANZA

KIKOSI CHA SIMBA KILICHOANZA LEO

MBUNGE WA JIMBO LA TANGA,OMARI NUNDU AKISALIMIA NA WAAMUZI KABLA YA KUANZA MECHI HIYO LEO KUSHOTO NI NAHODHA WA COASTAL UNION MBWANA HAMISI


MASHABKI WA COASTAL UNION WAKISHANGILIA MECHI YA LEO

SPLM YAANZA UTEKELEZAJI WA MAKUBALIANO YA ARUSHA

February 07, 2015

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (wa tatu kutoka kushoto) akiwa kwenye mazungumzo na Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (wa tatu kutoka kushoto) akiwa kwenye picha ya na Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini 

Ujumbe wa Viongozi wa Makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan ya Kusini yalifanya mazungumzo  na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mjini Dar es Salaam jana.
Mazungumzo haya yalilenga kuandaa utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa mjini Arusha  mwezi wa januari tarehe 21 ambayo yanalenga kuyaunganisha makundi matatu katika chama cha SPLM kurudisha Amani na kuunda Serikali itakayowajumuisha viongozi kutoka makundi yote.
Katika mazungumzo ya jana makundi haya yamekubaliana kuendelea na mkakati  wa utekelezaji wa makubaliano ya Arusha kwa lengo la kuandaa utaratibu wa viongozi  wa makundi yote kurudi Sudan ya Kusini mapema iwezekanavyo.
Mizengo Pinda aimiza Wabunge kushiriki mazoezi na michezo kulinda afya zao

Mizengo Pinda aimiza Wabunge kushiriki mazoezi na michezo kulinda afya zao

February 07, 2015
553
Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akiwapongeza wachezaji wa timu za Bunge la Jamuhuri kwenye tafrija ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2015 katika majengo ya Bunge hilo Mjini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Peter Pinda aliwapongeza wanamichezo wa Timu za Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuliletea sifa kubwa Bunge hilo kwenye mashindano ya michezo mbali mbali ya Kitaifa na Kimataifa.
Mh. Pinda alitoa pongezi hizo katika Tafrija maalum ya kuukaribisha mwaka mpya zilizofanyika katika majengo ya Bunge la Jamuhuri Mjini Dodoma hafla iliyokwenda sambamba na kuwapongeza wanamichezo wa Bunge hilo baada ya kushinda michezo tofauti katika mashindano ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Mjini Arusha Tanzania.
Waziri Mkuu Pinda alisema kwamba michezo inatoa nafasi kubwa ya ushirikiano ambayo ni kielelezo cha msingi kinachozaa Viongozi bora wanaotokana na sekta ya michezo.
528
Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda akiwa pamoja na Spika wa Bunge Mh. Anna Makinda na Baadhi ya Wabunge wakifurahia vikombe mbali mbali vilivyoibuliwa na Timu za Bunge la Jamuhuri katika Mashindano ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Aliishauri Kamati ya Uongozi wa Michezo ya Bunge hilo kufikiria umuhimu wa kuwashirikisha wawakilishi wa wanamichezo wa mabunge wanachama kwenye tafrija kama hizo kwa lengo la kusherehekea nao pamoja ili kudumisha ushirikiano pamoja na ujirani mwema.
Alieleza kwamba michezo ina nafasi pana ya kupunguza joto la kisiasa, hitilafu au ugomvi unaotokea baina ya nchi na nchi na kupelekea watu wa pande zinazohitilafiana kurejea kwenye ushirikiano na mafungamano baina yao.
Mh. Pinda alifahamisha kwamba kwa kuwa mabunge mengi yana utaratibu mzuri wa kuandaa mashindano ni vyema kwa waheshimiwa wabunge kuzitumia fursa kama hizo katika kushiriki kwenye mazoezi na hatimae mashindano kwa lengo la kudumisha afya zao.
550
Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wakiwa kwenye tafrija ya kuupokea mwaka mpya wa 2015 iliyofanyika katika majengo ya Bunge Mjini Dodoma sambamba na kuzipongeza Timu za Bunge hilo zilizoshinda kwenye mashindano ya Mabunge ya Afrika Mashariki.
Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania aliwatakia mwaka mwema wa 2015 Waheshimiwa wote wa Bunge la Jamuhuri hasa mwezi Oktoba mwaka huu ambao kama wamefanya vyema majimboni mwao utawarejesha tena kwenye wadhifa wao.
Alisema kurejea kwa Wabunge hao kwa kiasi kikubwa kunaweza kuleta faraja kubwa kwa vile tayari wameshazoeana kutokana na kushirikiana pamoja katika vikao vya Bunge hilo kwa takriban miaka mitano.
Mapema Mwenyekiti wa Bunge Sports Club Iddi Azan alisema ongezeko la michezo mbali mbali kwenye mashindano ya Timu za Mabunge ya Afrika ya Mashariki linatokana na azimio la Mabunge ya Jumuiya hiyo la kuzitaka Nchi Wanachama kuongeza michezo mengine kwenye mashindano hayo.
560
Waziri Mkuu akiwaongoza waheshimiwa wenzake kwenye mduara ulioporomoshwa na bendi ya Utalii katika tafrija ya kuukaribisha mwaka mpya wa 2015 Mjini Dodoma.(Picha na – OMPR – ZNZ).
Mwenyekiti Azan alisema mshindano ya Mabunge hayo yalikuwa yakishirikisha michezo miwili tuu ile ya Kandanda na Pete ambapo kwa sasa ipo riadha, mbio za vijiti, kuvuta kamba, kufukuza kuku ikiwemo pia ile ya watu wenye mahitaji maalum { Walemavu }.
Mwenyekiti huyo wa Bunge Sports Club alielezea faraja yake kutokana na ushiriki mzuri wa wanamichezo wa Timu za Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye mashindano mbali mbali ya Mabunge na kuleta ushindi katika michezo tofauti.
Katika mashindano hayo ya mwaka 2014 ya Timu za Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyoshirikisha wachezaji 150 Timu ya Mpira wa Pete Wanawake ya Bunge la Tanzania ilitokea mshindi wa kwanza, Riadha wanawake washindi wa kwanza, riadha wanaume washindi wa Tatu, mpira wa miguu washindi wa Pili na kuvuta kamba Timu za wanawake na wanaume Tanzania zimeshika nafasi ya kwanza.

Penzi la Wema Sepetu na Ommy Dimpoz Lawekwa Hadharani.......Wapiga Picha wakiwa bafuni Usiku

February 07, 2015


Hatimaye zile tetesi  kwamba mwigizaji Wema Sepetu na msanii wa muziki Ommy Dimpoz wanatoka kimapenzi  zimekuwa kweli kwa zaidi ya asilimia 200....
 
Tetesi  hizo  zimethibitishwa na picha waliyopiga jana usiku wakiwa bafuni huku Wema akiwa amevaa taulo tu na  Ommy Dimpoz akionekana kwa mbali kama ananawa mikono. 
 
Picha hii iliamsha watu kibao usiku wa jana hasa wale Team Wema, kwani comments na likes zilivyo tiririka utadhani  picha imewekwa saa sita mchana, kumbe ni usiku wa manane.

Baadhi ya picha zao 
 

“SUMATRA TANGA WAWATANGAZIA KIAMA WAMILIKI WA MABASI MKOANI TANGA”

February 07, 2015



MAMLAKA ya Usimamizi wa Usafiri nchi Kavu na Majini Mkoani Tanga (Sumatra) umewapa muda wa siku mbili wamiliki wa mabasi mkoani hapa kuhakikisha wanahamia kwenye kituo kipya cha mabasi kilichopo kange jijini Tanga ndani ya siku mbili zijazo la sivyo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Agizo la hilo lilitolewa na Ofisa Mfawizi wa Sumatra Mkoa wa Tanga, Walukani Luhamba wakati alipofanya ziara ya kutembea kituo hicho kuangali namna ya agizo la Mkuu wa mkoa wa Tanga, Said Magalula namna linavyokwenda.


Alisema kuwa kimsingi wamiliki hao kuendelea kubaki kwenye stendi ya zamani ikiwemo wengine kupaki magari pembezoni mwa ofisi zao zilizopo karibu na maeneo hayo ni kukiuka amri iliyotolewa na mamlaka hiyo hivyo watakaobainika kufanya hivyo baada ya muda uliotolewa watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Aidha alisema licha ya kuchukuliwa sheria kali kwa watakaobainika kukaidi agizo hilo lakini pia watawatoza faini ya sh.lakini mbili (200,000) pamoja na kuvutiwa leseni ili kuweza kuwa fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo.


Ofisa huyo alisema kuwa serikali imetumia fedha nyingi kuhakikisha stendi hiyo inakuwa katika kiwango kizuri kwa ajili ya kupunguza msongamano eneo la mjini kwa kuijenga lakini wao wameshindwa kufikiria suala hilo na kuendelea kubaki mjini.

Awali akizungumza ,Mwenyekiti wa Muungano wa Wasafirishaji wa Daladala  Jijini Tanga,Atwabi Shabani aliwataka wamiliki hao kuhakikisha wanazingatia agizo hilo ili kuweza kuepukana na adhabu wanazoweza kukumbana nazo.

Kwa upande wao baadhi ya madereva wanaofanya safari zao kati ya Tanga na mikoa mengine waliotii agizo hilo waitaka mamlaka hiyo kwa kushiriki Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama barabarani kuhakikisha wanasimamia suala hilo ipasavyo ili kuepusha malalamiko.

Mmoja kati ya madereva hao,Omary Chuchuli alisema kuwa utaratibu huo ni nzuro kwa sababu unaondoa manung;uniko kwa baadhi ya wasafirishaji wengine ambao walikwisha kutii agizo la kuhamia kwenye kituo hicho cha mabasi.


Naye Fadhili Jumanne alisema lazima vyombo vinavyohusika na jambo hilo kuhakikisha vinashirikiana kwa pamoja ili kuweza kuondoa changamoto hiyo iliyopo.