MATUKIO KATIKA PICHA MAHAFALI YA TATU YA KIDATO CHA NNE KWENYE SHULE YA SEKONDARI ELOHIMU JIJINI TANGA LEO

October 10, 2015
MGENI RAMSI  KWENYE MAHAFALI YA TATU YA SHULE YA SEKONDARI YA WAVULANA ELOHIMU ILIYOPO JIJINI TANGA,MOSES KISIBO KUSHOTO NI MKURUGENZI WA SHULE HIYO NA KULIA  NI MKUU WA SHULE HIYO AMATE RAPHAEL KIMARIO
MWALIMU MKUU WA SHULE HIYO AMATE RAPHAEL KIMARIO AKIZUNGUMZA KWENYE MAHAFALI HAYO KABLA YA KUMKARIBDISHA MGENI RAMSI























NEC:VIFAA VILIVYOKAMATWA SIO BVR, WALA HAVIHUSIANI VYOVYOTE NA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI

October 10, 2015

Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima.
Siku moja baada ya kunaswa mashine zilizosadikiwa kuwa ni za uandikishaji wapiga kura kwa njia ya kielektroniki (BVR), zilizokuwa zikiandikisha wafanyakazi wa Kiwanda cha MM Steel jijini Dar es Salaam, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeibuka na kueleza kuwa mashine hizo ni 'feki' na wala hazihusiani kwa namna yoyote na vifaa vyao.
 Jaji mstaafu Damian Lubuva akizungumza na viongozi wa Chadema. Kutoka kulia ni Wakili wa chama hicho, John Malya na Reginald Munisi
Jaji mstaafu Damian Lubuva akizungumza na viongozi wa Chadema. Kutoka kulia ni Wakili wa chama hicho, John Malya na Reginald Munisi.
Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima, ndiye aliyetoa ufafanuzi huo wakati akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na mashine hizo ambazo zilikamatwa juzi wakati zikiendelea kutumiwa kwa shughuli ya uandikishaji wa wafanyakazi wa kiwanda hicho kilichopo katika eneo la Mikocheni. 
 
Wakati Polisi wakizikamata jana kwa ushirikiano na maofisa kadhaa wa NEC, tayari mashine hizo zinavyofanana na BVR zilishaandikisha wafanyakazi zaidi ya 100 wa Kiwanda cha MM Steel.
 
Akielezea zaidi kuhusiana na tukio hilo, Kailima alisema kuwa, mara baada ya kupata taarifa za kuwapo kwa mashine hizo, walienda kuzikagua na kubaini kuwa hazina uhusiano na zile za Biometric Voter Registation (BVR), zilizotumiwa na wao (NEC) kuandikisha wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25.
 
“Hakuna ukweli wowote kuwa zile ni mashine za BVR na tumebaini ni feki, tena ni sawa na zile zinazotumika kwenye ofisi mbalimbali kuandikisha wafanyakazi wake... hawa waliosema ni mashine za kuandikishia wapiga kura hawako sahihi... si kweli,” alisema Kailima.
 
Alisema endapo watu wataendelea kuwa na shaka juu ya namna NEC inavyofanya kazi kwa sababu tu ya kuona mashine kama hizo, basi wanaweza pia kukamata mashine za ofisi nyingi zikiwamo za kwenye viwanja vya ndege, hospitali na hata manispaa kama ya Kinondoni ambayo hutumia mashine kama hizo kwa shughuli zake mbalimbali.
 
“Mashine tulizozikuta kwenye hiyo ofisi jana (juzi) ni computer mpakato (laptop) na mashine za kuchukua alama za vidole. Hata wale wafanyakazi tulipowahoji walibainisha kuwa wanazitumia kuorodhesha wafanyakazi wao kwa ajili ya usalama wa ofisi... na tena zipo ofisi nyingi zinatumia mashine hizo,” alisema Kailima.
 
Kailima alitoa tahadhari kwa wataalamu wanaovishauri vyama vya siasa kuwa makini na kuacha kupotosha kwa kuwaleza mambo yasiyo na ukweli, hasa kuhusiana na NEC kwani wao wanafanya kazi zao kisayansi zaidi na hakuna fursa ya kuwapo kwa ubabaishaji wa aina yoyote.
 
Aliongeza kuwa hawafanyi kazi zao kwa misikumo ya kisiasa, bali huzingatia utaalamu na hivyo wanaotumiwa kwa ushauri na vyama waache kuwadanganya wanasiasa.
 
“Hawa wanasiasa wanadanganywa na watu wanaojiita wataalamu... mashine hizi (zilizokamatwa) hazihusiani na BVR," alisisitiza.
 
CHADEMA WAHUSISHWA UCHUNGUZI
Akieleza zaidi juu ya hatua walizochukua baada ya tukio la juzi, Kailima alisema kuwa (jana) walifanya uchunguzi wa mashine hizo kwa kushirikiana na wawakilishi kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao ndiyo walitoa malalamiko kwao kuhusiana na madai ya kuwapo kwa mashine kama BVR zinazotumiwa kuandikisha watu.
 
“Wataalamu wao (Chadema) walikuja na tukathibitisha (wote) zile ni feki na hazihusiani kabisa na mashine zetu za BVR,” alisema Kailima.
 
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) John Mnyika, aliitaka NEC ivikabidhi vyama vya siasa nakala za daftari la kudumu la wapiga kura ili kuepukana na njama za wizi wa kura alizodai zinaweza kufanywa na chama tawala -- Chama Cha Mapinduzi (CCM).
 
Akizungumia tukio la juzi kuhusu kukamatwa kwa vifaa vinavyofanana na mashine za BVR, Mnyika alisema suala hilo walilikabidhi kwa maofisa wa NEC na Jeshi la Polisi ambao wanalichunguza kwa kushirikiana na maofisa wa Chadema ili kubaini ukweli.
 
Kadhalika, Mnyika aliitaka NEC kushughulikia suala hilo haraka na kutishia kuwa wasipotoa majibu ya kina ndani ya siku tatu, atashauri wanachama wenzake kuishinikiza ifanye hivyo ili kuondoa shaka iliyopo.
 
Hata hivyo, Mnyika aliyasema hayo kabla ya kutolewa kwa maelezo ya Kailima kuhusiana na uchunguzi walioufanya kwa mashine hizo zilizokamatwa Mikocheni. 
 
Juzi, Chadema walipata taarifa kutoka vyanzo vyao vyao kuwa kuna mashine zinazofanana na BVR zinaandikisha watu na hivyo wakashirikiana na Polisi na NEC kuvikamata kabla ya kwenda kuvichunguza. Meneja Mawasiliano wa MM Steel, Aboubakar Mlawa, alieleza kuwa kampuni yao imeamua kuandikisha wafanyakazi wao kwa nia ya kudhibiti usalama vitendo vya wizi, na kwamba tayari walishaandikisha wafanyakazi zaidi ya 100 kati ya 900 waliokuwa wakitarajiwa kutoka kwenye viwanda vyao saba.

BENKI YA CRDB YASAIDIA UJENZI VYUMBA VYA MADARASA GEITA

October 10, 2015

Benki ya CRDB kupitia tawi lake la mjini Geita imechangia ujenzi wa vyumba vya madarasa katika  Shule za Msingi Mwatulole na Shule ya Msingi Geita ambayo baadhi ya majengo yalibomolewa na mvua kubwa iliyoambata na upepo mkali mwanzoni mwa mwake huu mkoani Geita. 

Sambamba na kusaidia ujenzi na ukarabati wa madarasa Benki ya crdb ilichangia maadhimisho ya wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani yaliyofanyika mjini Geita kwa sababu benki hiyo inawajali wateja wake. Maadhimisho ya wiki Huduma kwa Wateja ilianza Oktoba 5 na kumalizika Oktoba 10 ambapo Benki ya CRDB ilishiriki kikamilifu katika kazi za kijamii. Benki ya CRDB imewashuru wateja wake kupitia tawi la Geita.
Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata (kushoto) akimkabidhi hundi ya shilingi milioni moja Mkuu wa Shule ya Msingi Mwatulole iliyopo Mkoani Geita, Catherine Mugusi  kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwatulole akipokea msaada wa vitabu vya ziada na kiada kutoka kwa Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata.
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwatulole akipokea msaada wa vitabu vya ziada na kiada kutoka kwa Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata.
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mwatulole akipokea msaada wa vitabu vya ziada na kiada kutoka kwa Meneja wa CRDB Geita, Amini Mwakang'ata.
Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Benki ya CRDB, Willy Kamwela (kushoto) akipokea maoni kutoka kwa mteja wa wa Benki ya CRDB tawi la Geita wakati wa Maadhiisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja mjini Geita.
Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Benki ya CRDB, Willy Kamwela akizungumza na wateja wa benki hiyo (hayupo pichani) katika maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja iliyofanyika katika tawi la Geita.

KINANA APIGA KAZI YA NGUVU MKOANI KIGOMA

October 10, 2015

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kwenye uwanja wa shule ya msingi Katanga,Kasulu mkoani Kigoma tayari kunadi sera za CCM kwa mwaka 2015-2020.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Kasulu Kusini Ndugu Agustino Zuma Ole kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika viwanja vya shule ya msingi Katanga, Kasulu,mkoani Kigoma.
Mgombea ubunge wa jimbo la Kasulu Kusini Ndugu Agustino Zuma Ole akiomba kura kwa wakazi wa Kasulu Kusini mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Katanga.
 Mgombea ubunge wa Jimbo la Kasulu mjini Ndugu Daniel Nswanzigwanko akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kabla ya kuhutubia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa CCM Kasulu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi
waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika
kwenye uwanja wa CCM Kasulu mjini.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi
Kasulu mjini na kuwaeleza kuwa CCM imeleta mgombea anayejali wananchi, mtendaji na mfuatiliaji asiyependa rushwa na anatanguliza maslahi ya nchi kwanza kwa manufaa ya wote.

LOWASA AAHIDI NEEMA KWA WAKULIMA WA ZAO LA KAHAWA KILIMANJARO

October 10, 2015
Kada mkongwe wa Chama cha Mapinduzi,aliyejiengua hivi karibuni ,Kingunge Ngombalemwiru akisalimia wakati wa mkutano wa kampeni za kumnadi mgombea Urais kupitia Chadema na Vyama vinavyounda Umoja wa katiba ya wananchi UKAWA uliofanyika katika viwanja vya mashujaa mjini Moshi.Picha zote na Dixon Busagaga wa Busagaga's Orijino Blog.
Kada mkongwe wa Chama cha Mapinduzi,aliyejiengua hivi karibuni ,Kingunge Ngombalemwiru akimkaribisha mgombea Urais kupitia Chadema na Vyama vinavyounda Umoja wa katiba ya wananchi UKAWA ,Edward Lowasa kuzungumza na wakazi wa mji wa Moshi katika viwanja vya Mashujaa mjini Moshi.
Mgombea Urais kupitia Chadema chini ya mwavuli wa vyama vinavyounda Umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) ,Edward Lowasa akizungumza na maelfu ya wakazi wa mji wa Moshi na Vitongoji vyake waliofika kumsikiliza katika mkutano uliofanyika viwanja vya Mashujaa mjini hapa.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo ,(Chadema) taifa ,Freeman Mbowe akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mashujaa Mjini Moshi.

Maelefu ya wananchi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni wa mgombea Urais kutia Chadema kwa mwavuli wa vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA,wakionesha ishara ya mabadiliko.
Mwenyekiti mwenza wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi,UKAWA,James Mbatia akizungumza katika mkutano wa kampeni wa kumnadi mgombea Urais ,Edward Lowasa uliofanyika katika uwanja wa Mashujaa mjini Moshi.

Mwenyekiti Mwenza wa vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA,James Mbatia akiwa amemnyanyua mkono na kumuombea kura mgombea Ubunge katika jimbo la Moshi mjini ,Jafary Michael
Mgombea Ubunge katika jimbo la Moshi mjini ,Jafary Michael (Chadema) akizungumza na maelefu ya wananchi waliofurika katika uwanja wa Mashujaa mjini Moshi katika mkutan wa kampeni wa kumnadi mgombea Urais kupitia UKAWA,Edward Lowasa.

BUZWAGI YAWAZAWADIA WAFANYAKAZI BORA WA MWAKA.

October 10, 2015
Meneja wa Idara ya Maboresho ya Biashara wa Mgodi wa Buzwagi Bwana Richard Ojendo wa kwanza kushoto akipokea tuzo ya heshima ya utumishi uliotukuka ya meneja wa mgodi, “General Manager Prestegious award” kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Bwana Benson Mpesya,(katikati) anaeshuhudia upande wa kulia ni Eng. Philbert Rweyemamu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi.Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kaskazini aliyekuwa Shinyanga.
Meneja wa Idara ya Maboresho ya Biashara wa Mgodi wa Buzwagi Bwana Richard Ojendo wa kwanza kushoto, mkuu wa wilaya ya Kahama bwana Benson Mpesya na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi wakiwa katika picha ya pamoja na Bwana Ojendo mara baada ya kutunukiwa uzo ya  akipokea tuzo ya heshima ya utumishi uliotukuka ya meneja wa mgodi, “General Manager Prestegious award”.
Meneja wa Idara ya Madini wa Mgodi wa Buzwagi Eng. Muganda Mutereko wa kwanza kushoto akipokea tuzo ya Meneja Bora wa Mwaka ”Best Manager of the year” kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Bwana Benson Mpesya,(katikati) anaeshuhudia upande wa kulia ni Eng. Philbert Rweyemamu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi.
Meneja wa Idara ya Ufanisi wa Kampuni wa Mgodi wa Buzwagi Bwana Saimon Sanga wa kwanza kushoto akipokea tuzo ya ya mshindi wa pili kwa nafasi ya Meneja Bora wa Mwaka ”Best Manager of the year” kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Bwana Benson Mpesya,(katikati) kulia ni Eng. Philbert Rweyemamu.
Mkuu wa kitengo cha Uchenjuaji wa Dhahabu wa Mgodi wa Buzwagi Bwana Festo akimpokelea Tuzo ya Mshindi wa tatu Bwana Karel Schultz ambaye ni meneja wa Kinu cha Uchenjuaji wa Mgodi wa Buzwagi mara baada ya kutangazwa mshindi wa tatu katika nafasi ya Meneja Bora wa Mwaka ”Best Manager of the year” tuzo hiyo ilikabidhiwa na mkuu wa wilaya ya Kahama Bwana Benson Mpesya.
Washindi wa Tuzo ya Meneja bora wa mwaka wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi na meneja mkuu wa mgodi wa Buzwagi.(kutoka kushoto ni Saimon Sanga Meneja wa Idara ya Ufanisi, wa pili ni Eng. Muganda Mutereko Meneja wa Madini, wa tatu ni Mkuu wa wilaya ya Kahama Bwana Benson Mpesya na wa nne ni Eng.Philbert Rweyemamu aliesimama upande wa kulia ni bwana Festo aliyepokea tuzo hiyo kwa niaba ya bwana Karel Schultez
Mkuu wa kitengo cha Load and Haul Bwana Marco Peter wa kwanza kushoto akipokea tuzo ya Mfanyakazi bora wa mwaka ”Best employee of the year” kutoka kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Bwana Benson Mpesya,(katikati) aliyesimama upande wa kulia ni Eng. Philbert Rweyemamu.
Bwana Gulam Fazal Mkuu wa kitengo cha Ghala(warehouse) wa kwanza kushoto akipokea tuzo ya mshindi wa pili wa nafasi ya Mfanyakazi bora wa Mwaka “Best employee of the year” anaekabidhi tuzo hiyo ni mkuu wa wilaya ya Kahama Bwana Benson Mpesya,(katikati) kulia ni Eng. Philbert Rweyemamu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi.
Waziri Selemani Mkuu wa kitengo cha Huduma za Nje (Outside Services) wa kwanza kushoto akipokea ngao ya mshindi wa yatu baada ya kuibuka mshindi wa nafasi hiyo katika kundi la wafanyakazi bora wa Mwaka anaemkabidhi tuzo hiyo ni mkuu wa wilaya ya Kahama bwana Benson Mpesya ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.
Washindi wa tuzo za mfanyakazi bora wa Mwaka “Best Employee of the Year” wakiwa katika picha ya pamoja na meneja mkuu wa mgodi wa Buzwagi Eng, Philbert Rweyemamu na Mgeni Rasmi mkuu wa wilaya ya Kahama Mh. Benson Mpesya.
Washindi wa tuzo za mfanyakazi bora wa Mwaka, meneja bora wa mwaka na mshindi wa tuzo ya heshima ya utumishi uliotukuka ya meneja mkuu wakiwa katika picha ya pamoja na meneja mkuu wa mgodi wa Buzwagi Eng, Philbert Rweyemamu na Mgeni Rasmi mkuu wa wilaya ya Kahama Mh. Benson Mpesya.
Bwana Amos John(Kushoto) ambaye ni Meneja wa Idara ya Biashara Mgodi wa Buzwagi akimkabidhi cheti Bwana James Jisena kama sehemu ya kutambua mchango wake kwa kampuni kwa utumishi wa muda mrefu.
Bwana Amos John(Kushoto) ambaye ni Meneja wa Idara ya Biashara Mgodi wa Buzwagi akimkabidhi cheti mmoja wa wafanyakazi wa Idara yake kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu.
Meneja wa Idara ya Uendelevu  wa Mgodi wa Buzwagi Bwana George Mkanza  akimkabidhi cheti Bwana Abdalah kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu.
Meneja wa Idara ya Madini wa Mgodi wa Buzwagi Eng. Muganda Mutereko  akimkabidhi cheti Wilbert Masawe kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu
Meneja wa Idara ya Huduma za kitaalamu za madini Bwana Sam Eshun akimkabidhi cheti mmoja wa watumishi katika idara yake kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu.
Meneja wa Idara ya Madini wa Mgodi wa Buzwagi Eng. Muganda Mutereko  akimkabidhi cheti Cosmas Joseph kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu.
Meneja Mkuu wa Idara ya Ufanisi wa Kampuni ya Acacia Bi. Janet Ruben akimkabidhi mmoja wa wafanyakazi cheti  kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu katika idara ya Ufanisi wa Kampuni katika Mgodi wa Buzwagi
Meneja Mkuu wa Idara ya Ufanisi wa Kampuni ya Acacia Bi. Janet Ruben akimkabidhi Victor Mtutwa kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu katika idara ya Ufanisi wa Kampuni katika Mgodi wa Buzwagi.

Meneja Mkuu wa Idara ya Ufanisi wa Kampuni ya Acacia Bi. Janet Ruben akimkabidhi Shamsa Mohamed kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu katika idara ya Ufanisi wa Kampuni katika Mgodi wa Buzwagi
Meneja wa Idara ya Assets Reliability Eng. Peter Mbawala akikabidhi cheti Agness Joseph kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi cha miaka mitano
Mkuu wa kitengo cha Idara ya Raslimali watu Bwana Ivocatus Masanja akitangaza majina ya washindi wa Tuzo mbalimbali ambazo zilitolewa wakati wa halfa ya siku ya familia ya Mgodi wa Buzwagi.
Mshauri Mkuu wa Idara ya Uendelevu wa kampuni ya Acacia Steve Kisyaki (kushoto) akimkabidhi cheti Bwana Franco Eliya Mwakalinga kwa kuitumikia kampuni kwa kipindi kirefu.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Eng.Philbert Rweyemamu akizungumza na wafanyakazi wa Mgodi wa Buzwagi pamoja na familia zao mara baada ya kuwatunuku tuzo mbalimbali na vyeti baadhi ya wafanyakazi waliofanya vizuri katika kipindi cha mwaka 2015
Kutoka kulia ni Mkuu wa Idara ya Mawasiliano wa Mgodi wa Buzwagi Bi Blandina Munghezi na Magesa Magesa Afisa Mawasiliano wa Mgodi wa Buzwagi (Kulia) wakifafanua jambo kwa mshereheshaji wa shughuli hiyo MC kalinga. (katikati)
Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kahama Benson Mpesya (wa kwanza Kulia) akifurahia jambo na meneja mkuu wa Mgodi wa Buzwagi Eng.Philbert Rweyemamu (katikati) wakati wa hafla ya kutoa tuzo kwa wafanyakazi bora pamoja na kuadhimisha siku ya familia ya wafanyakazi wa Buzwagi.
BURUDANI YA KUKATA NA SHOKA NAYO HAIKUKOSEKANA VIJANA WA JJ BAND KUTOKA MWANZA WAKAUFANYA USIKU WA FAMILIA YA BUZWAGI KUWA WA AINA YAKE.