Mweyekiti wa Chama cha Maafisa
Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki wa Serikali (TAGCO) Paschal
Shelutete akizungumza kuhusu Mkutano mkuu wa 13 wa mwaka wa chama hicho
leo Jijini Dar es Salaam. Mkutano huo unatarjiwa kufanyika kuanzia
tarehe 13 Machi Jijini Arusha. Kutoka kushoto ni Kaimu Katibu Mwenezi wa
TAGCO Dkt. Cosmas Mwaisobwa, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari
(MAELEZO) Rodney Thadeus na Katibu Mkuu wa TAGCO Abdul Njaidi.
Mkurugenzi Msaidizi Idara ya
Habari (MAELEZO) Rodney Thadeus akifafanua jambo wakati wa Mkutano wa
uongozi wa Chama cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki
Serikalini (TAGCO) na waandishi wa habari kuhusu Mkutano mkuu wa 13 wa
mwaka wa chama hicho leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia Katibu Mkuu
wa TAGCO Abdul Njaidi na Mweyekiti wa Chama hicho Paschal Shelutete
Kaimu Katibu Mwenezi wa Chama cha
Maafisa Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki wa Serikali (TAGCO)
Dkt. Cosmas Mwaisobwa akisistiza jambo wakati wa mkutano wa uongozi wa
Chama cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki Serikalini
(TAGCO) na waandishi wa habari kuhusu Mkutano mkuu wa 13 wa mwaka wa
chama hicho leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia Katibu Mkuu wa TAGCO,
Abdul Njaidi, Mweyekiti wa Chama hicho Paschal Shelutete na Mkurugenzi
Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Rodney Thadeus
Baadhi ya waandishi wa habari
wakifuatilia mada wakati wa mkutano wa viongozi wa Chama cha Maafisa
Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki wa Serikali (TAGCO) leo Jijini
Dar es Salaam.
Picha na MELEZO
……………………………………………………………………
Na Florah Raphael-Fullshangwe-Dar es Salaam
Mkutano Mkuu wa
Chama Cha Maafisa Habari na Mawasliano Serikalini (TAGCO) kwa
kushirikiana na Idara ya Habari Maelezo , unatarajiwa kufanyika mnamo
tarehe 12-16 Machi mwaka huu mkoani Arusha ambapo jumla ya maofisa 300
wanatarajiwa kishiriki katika mkutano huo.
Akiongea Na vyombo
vya habari leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa chama hicho Paschal
Shelutete amesema kuwa lengo kuu kuelekea mkutano huo ni kukumbushana
wajibu na majukumu yao serikalini.
Aidha amesema kuwa
kikao hicho kina kazi ya kuwajengea washiriki uwezo wa namna ya
kutangaza shughuli za serikali na kuhakikisha idara ya mawasikiano na
uhusiano serikalini vinaimarishwa ili kuendana na kasi ya utendaji wa
serikali ya awamu ya tano.
Pia ameongeza na
kusema kuwa katika mkutano huo jumla ya mada 14 zitaongelewa ambazo
zitajikita zaidi kwenye masuala mbalimbali yahusuyo habari, mawasiliano
na itifaki.
Pia amesema kuwa
mada hizo zitawasilishwa na wataalam watakaoleta uzoefu mpana katika
mawasiliano na kuongeza kuwa kutakuwepo mijadala na fursa ya
kubadilishana uzoefu kati ya maaafisa mawasiliano na wadau wengine wa
habari.
Mwisho kabisa
amewaasa Maafisa Uabari, mawasiliano, uhusiano na Itifaki kuthibitisha
ushiriki wao kabla ya tarehe 7 machi mwaka huu.