SERIKALI YATOA ONYO URAIS 2015.
Suala la baadhi ya viongozi nchini kuanza kampeni za kuwania urais mwaka 2015 kwa kumwaga fedha ili kujijengea mazingira ya ushindi, limechukua sura mpya baada ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kuanza kuwabana.
Habari zilizolifikia gazeti hili na baadaye kuthibitishwa na Kamishna wa Sekretarieti hiyo, Jaji Mstaafu Salome Kaganda, zinaeleza kuwa chombo hicho cha Serikali tayari kimewaita watu hao na kuwapa onyo baadhi yao wakiwamo mawaziri na wabunge walioanza kufanya kampeni.