DC Mgaza awaasa vijana kupenda Michezo.

DC Mgaza awaasa vijana kupenda Michezo.

June 09, 2013

Na Oscar Assenga, Mkinga.
MKUU wa wilaya ya Mkinga, Mboni Mgaza amewataka vijana kupenda michezo na kuithamini kwa kuwa michezo ni ajira ambayo inaweza kuwainua kimaisha endapo wataizingatia na kucheza kwa umakini.

Mgaza alitoa wito huo jana wakati akifungua Mashindano ya Umoja wa Shule za Msingi wilayani humo (Umitashumta) ambapo alisema michezo pia huongeza upendo ushirikiano baina ya wachezaji wanaokuwa wakishiriki ikiwemo kujenga undugu miongoni mwao.

Amesema michezo pia inadumisha amani kwa kuwa watu wanaposhiriki katika michezo wanakuwa ndugu na kufikiria jinsi ya kupata mafanikio hivyo kupelekea kudumisha amani tulionayo.

Aidha amewataka washiriki kucheza vizuri ili kuweza kutengeneza timu nzuri ya wilaya ambayo itaanza kambi kwa ajili ya kuwakilisha wilaya hiyo katika mashindano hayo ngazi ya mkoa.

Awali akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano hayo, Afisa Elimu wilaya ya Mkinga Idara ya Elimu Msingi, Juma Mhina amesema mashindano hayo yanashirikisha timu kutoka tarafa mbili ambazo ni Mkinga na Maramba na inashirikisha idadi ya wanamichezo 190.

Mhina amesema michezo itakayochezwa ni Pete,Wavu, Mpira wa Miguu na Mpira wa mikono na kueleza kuwa lengo la serikali kurudisha michezo mashuleni ni kuibua vipaji vya wachezaji kuanzia mashuleni.

                        Mwisho.

Ufunguzi Umitashumta

June 09, 2013
WACHEZAJI kutoka Tarafa ya maramba na Mkinga wakiwania mpira wakati mchezo pete wa ufunguzi wa Mashindano ya Umitashumta ngazi ya wilaya ya Mkinga anayeshuhudia mwenye tishri nyeupe ni Mkuu wa wilaya ya Mkinga,Mboni Mgaza ambaye alikuwa mgeni rasmi.

Tunacheza hivi

June 09, 2013
MKUU wa wilaya ya Mkinga,Mboni Mgaza akishiriki katika mechi ya mpira wa pete ambayo ilichezwa mara baada ya kuifungua jana,picha kwa hisani ya blog hii.

DC Mgaza akizungumza na wanamichezo

June 09, 2013
MKUU wa wilaya ya Mkinga,Mboni Mgaza akisoma hotuba yake katika ufunguzi wa mashindano ya Umishumta ngazi ya wilaya ya Mkinga jana.

Mcheze kwa umakini.

June 09, 2013
Afisa Elimu wilaya ya Mkinga Idara ya Elimu Msingi, Juma Mhina mwenye suti akizungumza katika ufunguzi wa mashindano hayo,kulia kwake waliokaa ni Mkuu wa wilaya ya Mkinga,Mboni Mgaza na Afisa tarafa ya Mkinga,Picha kwa hisani ya blog hii

Wanafunzi wakiwa tayari kwa ajili ya kukaguliwa

June 09, 2013
MWANDISHI wa Shirika la Utangazaji la Taifa  (TBC)mkoa wa Tanga Bertha Mwambela naye alikuwepo katika ufunguzi wa Mashindano hayo,picha kwa hisani ya blog hii

Umitashumta yaiva Mkinga.

June 09, 2013
WANAFUNZI kutoka Tarafa za Mkinga na Maramba wilayani Mkinga wakiimba wimbo wa Taifa katika ufunguzi wa Mashindano ya Umoja wa shule za Msingi nchini Umitashumta ambayo yalifunguliwa jana na Mkuu wa wilaya ya Mkinga,Mboni Mgaza.
“Redd's Miss Tanga, kushiriki Kalembo Day”

“Redd's Miss Tanga, kushiriki Kalembo Day”

June 09, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
WAREMBO wanaowania umalkia wa Mkoa wa Tanga “Redd’s Miss Tanga 2013”wanatarajiwa kushiriki katika shughuli za usafi wa mazingira mkoani Tanga “Kalembo Day” June 15 mwaka huu na baadae kutembelea wagonjwa katika hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo kuwaona wagonjwa na kutoa zawadi.

Shughuli hizo za usafi watazifanya katika maeneo mbalimbali jijini Tanga siku hiyo ambayo ni siku maalumu ya usafi katika mkoa wa Tanga wakati wakiwa wanajiandaa na shindano hilo ambalo litafanyika June 22 mwaka huu kwenye uwanja wa Mkwakwani.

Siku mbili baada ya warembo hao kumaliza zoezi hilo watakwenda kutembelea vivutio vya utalii na maeneo ya kihistoria yaliyopo mkoani hapa June 17 mwaka huu lengo likiwa ni kujifunza utalii wa ndani ili kuweza kupata fuksa nzuri ya kuweza kuutangaza kwa wageni na wenyeji.

Vivutio ambavyo warembo hao wanatarajiwa kutembelea ni Mbuga ya Wanyama ya Sadani na Mapango ya kihistoria ya Amboni yaliyopo jijini Tanga ambapo watapata fursa ya kuona na kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu maeneo hayo.

Shindano hilo linatarajiwa kufanyika 22 kwenye Uwanja wa Mkwakwani mkoani hapa ambapo litapambwa na wasanii nguli wa muziki wa bongo fleva nchini ili kuweza kuwapa burudani wakazi wa mkoa huu ambao watajitokeza kushuhudia kinyang’anyiro hicho.

Mkurugezi wa Kampuni ya DATK Intertaimeint, Asha Kigundula, ambaye ndiye muandaaji wa shindano hilo alisema shindano hilo linatakuwa la aina yake kutokana na kuwa na warembo bomba.

Alisema kuwa warembo hao tayari wanaedelea na mazoezi kwenye Ukumbi wa Lavida uliopo jijini Tanga ambapo tayari wameshaanza kuwateka wadau wa tasnia hiyo ambao wamekuwa wakijitokeza kila siku kushuhudia mazoezi hayo.

   “Ninachoweza kusema shindano la mwaka huu litakuwa la aina yake kutokana na kusheheni warembo bomba wenye mvuto na hivyo kuonyesha kutakuwa na mchuano mkali miongoni mwao “Alisema Kigundul.

Shindano hilo litaanza saa 2, usiku na kueleza kuwa maandalizi ya shindano hilo yanaendelea vizuri na jumla ya warembo 12 watashindania taji hilo ambalo hivi sasa linashikiliwa na Miss Tanga 2012 Teresia Kimolo.

Warembo hao ni Hawa Ramadhan (18),Hazina Mbaga (19)Like Abdulraman (19), Jack Emannuel (18),Wahida Hashimu(20), Tatu Athumani (19), Mwanahamis Mashaka(20), Neema Abdallah (18), Winfrida Gutram (21)Lulu Mbonea (19) na Aisha Rashid (21),Azina Daniel (19),Lulu Matawalo(22),Judithi Moreli (21) na Hawa Twaybu(21)

Alisema kwamba shindano la mwaka huu litaandika historia mpya ya urembo mkoani humo kwa kuwa Kampuni DATK imejipanga, hivyo mashabiki wa mashindano ya urembo wa jijini hapo kwa ujumla wakae mkao wa kupata raha.

Redd's, Miss Tanga, imedhaminiwa na Dodoma Wine,CXC Africa,Executive Solutions,Busta General Supply, Mkwabi Interprises,Lusindic Investment LTD, Lavida Pub,Jambo Leo,Staa Spoti,Five Brothers Cloud's Media Group,  pamoja na Blog Michuzi Media Group,Bongostaz.com, Saluti5,Kajuna, JaneJohn, na Kidevu na assengaoscar.blogspot.com.

Mwisho.

Redd's Miss Tanga 2013usipime,Kufanyika June 22 Mkwakwani.

June 09, 2013
WAREMBO wanaowania taji la Redd's Miss Tanga,2013 wakiwa katika pozi mara baada ya kumaliza mazoezi yao yanayoendelea katika ukimbi wa Lavida Loca jijini Tanga ambapo shindano hilo linatarajiwa kufanyika June 22 mwaka huu katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga,Picha kwa hisani ya blogi hii.