HOTUBA YA BAJETI WIZARA YA MALIASILI NA UTALII-2023/2024 JUNE 2.

May 24, 2023

 


ZAIDI BILIONI 126 HUPATIKANI KUTOKANA NA ZAO LA UFUTA MKOA WA LINDI

May 24, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Lindi na Kamishina wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania, Mhe. Zainab Telack akizingua gari kwa Mrajis Msaidizi wa Mkoa wa Lindi ambapo gari hilo limetolewa na  Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) limekabidhiwa wakati wa Jukwaa la Ushirika la Mkoa wa Lindi lililofanyika Mjini Lindi likiwa na kauli mbinu "Ushirika ni Biashara". Kwenye jukwaa hilo Mkuu wa Mkoa,ametoa rai kwa wana Lindi wanaojishugulisha na masuala ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji kujiunga na Vyama vya Ushirika ili waweze kuuza kwa  pamoja kwenye soko.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi na Kamishina wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania Zainab Telack akikagua bada la mjasiliamali anayeuza bidhaa za asili Kwenye Jukwaa la Ushirika la Mkoa wa Lindi,ametoa rai kwa wana Lindi wanaojishugulisha na masuala ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji kujiunga na Vyama vya Ushirika ili waweze kuuza kwa  pamoja kwenye soko.
Washiriki mbalimbali walioshiliki Jukwaa la Ushirika la Mkoa wa Lindi
Jukwaa la Ushirika la Mkoa wa Lindi


Na Fredy Mgunda,Iringa.



Mkoa wa Lindi umekuwa unapata Zaidi ya bilioni 126 kutokana na uuzaji wa zao la ufuta kutoka wilaya zote za mkoa huo kutokana na zao hilo kuuzwa kwa mfumo wa stakhabadhi gharani.

Akizungumza wakati wa jukwaa la maendeleo ya ushirika mkoa wa Lindi 2023, mkuu wa mkoa wa Lindi Zainab Taleck alisema kuwa wamekuwa wakipata kiasi cha fedha kutokana na mazao ambayo yamekuwa yanahifadhiwa kwa mfumo wa stakhabadhi gharani.


Taleck alisema kuwa shilingi billion 126 zimepatikana kwenye zao la ufuta kutoka na kuuza zao hilo kwa njia ya stakhabadhi gharani ambapo wakulima wamekuwa wakipangia bei tofauti na zamani wakulima walikuwa wanapangiwa bei.

Telack amewataka wakulima na wavuvi kuingia katika vyama mbalimbali vya ushirika kwa lengo la kujenga umoja,kuongeza vipato vyao na kupata uongozi utakaoenda kutetea haki na maslahi ya shughuli zao wanazozifanya

"Uaminifu na Uadilifu tu ndio unaowaweka salama viongozi wa ushirika na wakulima salama hivyo amewataka kuacha vitendo viovu vinavyodhorotesha Maendeleo ya Ushirika ndani ya Mkoa wa Lindi"

Alimalizia kwa kuwataka wakulima kuuza mazao mbalimbali kwa njia ya stakhabadhi gharani ili wapate faidi ya kilimo wanacholima.

Kwa mwenyekiti wa vyama vya ushirika Odasi Mpunga alisema kuwa wakulima wanatakiwa kuuza mazao kwa mfumo wa stakhabadhi gharani ili wapate faida kulingana na thamani ya mazao yao.

Mpunga  aliwaomba wakulima wa zao la mbazi kuanza kuuza zao hilo kwa njia ya stakhabadhi gharani ili nao wapate faida kama wakulima wengine ambavyo

Naye naibu Mrajis Uhamasishaji, Consolata Kiluma, amevitaka Vyama vya Ushirika Mkoani Lindi kushirikiana na Maafisa Ushirika na ofisi ya Mrajis Mkoa kujibu  hoja za wakulima kwa wakati. 

Naibu Mrajis amesema kuwa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Lindi vimefanikiwa kusajili  vyama ila idadi ya wakulima na wanachama wamewasajili  wachache hivyo wamalizie kusajili wakulima wao wote wanaowahudumia.

WAZIRI MKUU AONGOZA KIKAO KAZI CHA MAWAZIRI

May 24, 2023

 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiongoza Kikao Kazi cha Mawaziri kilichofanyika kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 23, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 Baadhi ya washiriki wa Kikao Kazi cha Mawaziri wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipofungua kikao hicho kwenye ukumbi wa Hazina jijini Dodoma, Mei 23, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

HISTORIA MPYA MIUNDOMBINU YA KIMKAKATI KUANDIKWA

May 24, 2023

 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kauli moja limeridhia na kuidhinisha zaidi ya shilingi trilioni 3.5 kwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa mwaka wa fedha 2023/24.

Bajeti hiyo pamoja na mambo mengine inatarajiwa kuweka historia nchini ambapo barabara kuu na za mikoa zenye urefu wa kilometa 2,035 zinatarajiwa kujengwa kwa kiwango cha Lami na kuchochea ukuaji wa uchumi katika maeneo mbalimbali.

Akijibu hoja za wabunge wakati wa majumuisho ya bajeti ya Wizara hiyo Bungeni jijini Dodoma Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kwa dhati kuifungua nchi kiuchumi kupitia miundombinu ya kimkakati inayosimamiwa na Wizara kwa upande wa Sekta ya Ujenzi na Uchukuzi.

Prof. Mbarawa amezitaja barabara 7 zenye urefu wa kilometa 2,035 zitakazojengwa kwa utaratibu wa EPC + F kuwa ni barabara ya Kidatu – Ifakara – Lupiro – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo   – Londo – Lumecha/Songea (km 435), barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti River – Lalago – Maswa (Simiyu) (km 339) na barabara ya Handeni – Kibirashi – Kijungu – Kibaya – Njoro – Olboroti – Mrijochini – Dalai – Chambalo – Chemba – Kwa Mtoro – Singida (km 460).

Miradi mingine ni barabara ya Arusha – Kibaya – Kongwa Junction (km 453.42), barabara ya Masasi – Nachingwea – Liwale (km 175), barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (km 218), barabara ya mchepuo ya Uyole – Songwe yenye urefu wa kilometa 48.9 pamoja na barabara ya Mafinga – Mtwango – Mgololo (km 81).

Aidha, barabara ya Express way kutoka Kibaha-Chalinze-Morogoro ambayo ujenzi wake unashirikisha sekta binafsi  itajengwa huku miradi ya mabasi ya mwendo kasi ya DART na daraja la Jangwani vikitengewa Bilioni 2.2.`

Kwa upande wa Sekta ya Uchukuzi shilingi Trilioni 1.13 zinatarajiwa kutekeleza miradi ya ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), ikiwemo vipande vipya vya Dodoma hadi Kigoma, Uvinza hadi Burundi na DRC.

Ununuzi na utengenezaji wa ndege nne utakaogharimu takriban shilingi bilioni 300 utatekelezwa ukiwa ni mkakati wa kuendelea kuifufua ATCL ili kulifanya shirika hilo kuwa na tija na kuchagiza uchumi nchini.

Profesa Mbarawa amesema Serikali imejipanga kuhakikisha huduma za usafiri wa anga, utabiri wa hali ya hewa na usafiri kwa njia ya maji zinakuwa salama na za uhakika.

Jumla ya wabunge 75 wamechangia katika bajeti hiyo ambapo kati ya hao 67 kwa kuongea na nane kwa maandishi. Na hatimaye bunge kupitisha kifungu kwa kifungu Bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.


SAMIA LEGAL AID YAZINDULIWA MANYARA, HUDUMA ITATOLEWA SIKU KUMI.

May 24, 2023

 Na John Walter-Manyara


Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Paulina Gekul amewataka wananchi kutumia Huduma ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid Campaign), kupata haki zao na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Naibu Waziri Gekul ametoa wito huo leo mei 23,2023 mjini Babati wakati akizindua kampeni hiyo kwa Mkoa wa Manyara, itakayotolewa bure kwa wananchi wote kwa siku kumi katika wilaya tano za mkoa huo.

Amesema kampeni hiyo inayosimamiwa na serikali kupitia wizara ya Katiba na Sheria, itasadia kuimarisha mfumo wa utoaji Huduma za msaada wa kisheria kuanzia Serikali Kuu Hadi Serikali za Mitaa.

Pia, Gekul amewaagiza viongozi wote kuanzia ngazi ya Vijiji, kuweka mfumo mzuri wa kushighilikia changamoto za kisheria zitakazoibuliwa wakati wa kampeni hiyo.

Aidha amesema wataalamu wa sheria kutoka wizara ya Katiba na Sheria watakuwepo katika wilaya zote tano za mkoa wa Manyara kwenye majimbo Saba kuwasikiliza wananchi kuanzia ngazi ya kata na kutoa elimu ya masuala mbalimbali yanayohusu Sheria.

Kampeni hiyo inayotekelezwa chini ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Shirika la Legal Services Facility (LSF) na mashirika mengine, imepewa jina la Samia, ili kuenzi mchango wa Rais Dr. Samia Suluhu Hassan katika kutokomeza vitendo vya ukatili hasa kwa kina mama, watoto na makundi Maalum na kutoa nafasi ya msaada wa kisheria bure kwa wananchi wote.
 

Mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Manyara Kheri James ambaye ni mkuu wa wilaya ya Mbulu, amesema mkoa upo tayari kutoa ushirikiano ili wananchi waweze kupata huduma hiyo muhimu. Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Pater Toima amempongeza na kumshukuru Rais kwa kuwakumbuka wanyonge wanaokosa haki zao kwa kutokujua sheria.

 



NAIBU WAZIRI PINDA ATAKA UWAJIBAKAJI UNAOZINGATIA SHERIA SEKTA YA ARDHI

May 24, 2023

 Na Munir Shemweta, WANMM

 

Naibu waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda amesema watumishi wa sekta ya ardhi nchini wanao wajibu katika utendaji kazi na dhana nzima ya kuongeza ufanisi na tija kwa kuzingatia sheria.

 

"Tunahitaji nidhamu na miongozo mbalimbali ili kutoa hiduma stahiki kwa watanzania.

 

Pinda aliyekuwa akimuwakilisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleio ya Makazi Dkt Angeline Mabula alisema hayo tarehe 22 Mei 2023 jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendekeo ya Makazi.

 

Aidha, amesema mwajiri naye anao wajibu wa kuweka mazingira mazuri mahali pa kazi sambamba na kuwaheshimu watumishi na kuwaendeleza ili kuwezesha kutekeleza majukumu yao  ipasavyo.

 

Akigeukia suala la urasimishaji makazi holela, Naibu Waziri Pinda alisema mpango wa urasimishaji unafikia kikomo mwaka huu wa 2023 na makazi holela yanaendelea kushamiri huku miji ikikua kwa kasi.

 

Kwa mujibu wa Pinda aliyekuwa akimuwakilisha Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula, kazi ya Baraza la Wafanyakazi ni kutumia mkutano huo wa Baraza kuishauri serikali juu ya mkakati mpya wa kuondoa makazi holela.

 

Amelitaka Baraza la Wafanyakazi kujadili kwa kina makadirio ya mipango ya matumizi  kwa mwaka 2023/2024  na kuweka mipango inayotekelezeka.

 

Pamoja na mambo mengine ametaka kuwekwa mikakati madhubuti kwenye masuala ya makusanyo ya kodi ya ardhi ambapo amesema wizara imekusanya bil 129 sawa asilimia 51.6 ya lengo jambo alilolieleza  halikubalikia.

 

Ameelekeza kila mkoa kuongeza kasi ya makusanyo ili kutimiza lengo lililowekwa na kuchukua hatua kwa wadaiwa wote sugu kutokana na muda wa msamaha wa rais kupita.

 

 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Geophrey Pinda akizungumza katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara yake tarehe 22 Mei 2023 jijini Dodoma.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga akizungumza wakati wa kikoa cha Baraza la Wafanyakazi wa wizara yake tarehe 22 Mei 2023 mkoani Dodoma (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

 

Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiwa katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi kilichofanyika tarehe 22 Mei 2023 mkoani Dodoma.
RAIS  DKT. SAMIA AMWAPISHA JAJI (Mst.) TEEMBA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAADILI.

RAIS DKT. SAMIA AMWAPISHA JAJI (Mst.) TEEMBA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAADILI.

May 24, 2023

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, (Kushoto) akimwapisha Mhe. Jaji (Mst.) Rose Teemba (Mwenye suti ya kijivu) kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino jijini Dodoma tarehe 23.5.2023.

 Kamishna wa Maadili Mhe. Jaji (Mst.) Sivangilwa Mwangesi,(hayuko pichani) akiongoza kiapo cha Ahadi ya Uadilifu kwa waheshimiwa majaji wa Rufani na Mwenyekiti wa Baraza la Maadili katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu chamwino, jijini Dodoma tarehe 23. 5.2023.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,(wa pili kushoto), Mhe. Kassim Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (wa kwanza kushoto), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Jamhuri (wa tatu kushoto) na Jaji. Sivangilwa Mwangesi, Kamishna wa Maadili wakiwa katika picha ya pamoja na waheshimiwa majaji wa Rufani, Mwenyekiti wa Baraza la Maadili na watendaji wa Wizara ya Katiba na Sheria Ikulu, Chamwino jijini Dodoma tarehe 23.5.2023.

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amemwapisha Jaji (Mst.) Rose Teemba kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino jijini Dodoma tarehe 23.5.2023.

Mhe. Rais alimteua Jaji Teemba tangu tarehe 24.4.2023 kwa mujibu wa kifungu cha 26(1) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya 1995 kinachoeleza kuwa Baraza la Maadili litakuwa na wajumbe watatu watakaoteuliwa na Rais, miongoni mwao akiwemo aliyeteuliwa kutoka miongoni mwa watu wenye wadhifa au wamewahi kuwa na wadhifa wa Jaji wa Mahakama Kuu.

Aidha, kifungu hicho cha 26(3) kinasema kuwa Rais, atateua mmojawapo wa Wajumbe wa Baraza kuwa Mwenyekiti.

Katika hafla hiyo, Mhe. Rais ameeleza kuwa hana mashaka na uzoefu katika utendaji kazi wa Jaji Teemba.

“Jaji Sivangilwa Mwangesi, Kamishna wa Maadili akisha maliza kazi yake anakuleteeni nyinyi Baraza la maadili, ichambueni vizuri na kutuletea mapendekezo yenu,” amesema na kuongeza kuwa, “Tuna matatizo makubwa kwenyey eneo la uadilifu katika utawala, shughulikieni.”

Kazi kubwa ya Baraza la Maadili ni kufanya uchunguzi wa kina wa malalamiko yanayohusu ukiukwaji wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma dhidi ya viongozi wa umma waliotajwa katika kifungu cha 4 cha Sheria hiyo.

Aidha, uchunguzi huo hutanguliwa na uchunguzi wa awali ambao kwa mujibu wa kifungu cha 18(2)(c) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, hufanywa na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Jaji mstaafu Teemba anachukua nafasi ya Jaji mstaafu Ibrahim Mipawa aliyemaliza muda wake, akiongoza Baraza hilo tangu Agosti 16, 2019 alipoteuliwa kushika wadhifa huo.

Jaji mstaafu Teemba anakuwa Mwenyekiti wa tano wa Baraza la Maadili toka kuanzishwa kwake akitanguliwa na Jaji mstaafu Damian Lubuva, Jaji mstaafu Hamis Msumi, Jaji mstaafu Januari Msofe na Jaji mstaafu Ibrahim Mipawa.
ELIMU YA UFUNDI NA MAFUNZO YA STADI ZA KAZI NI MUHIMU KWA KUANDAA NGUVU KAZI YENYE UJUZI – MHE. KATAMBI

ELIMU YA UFUNDI NA MAFUNZO YA STADI ZA KAZI NI MUHIMU KWA KUANDAA NGUVU KAZI YENYE UJUZI – MHE. KATAMBI

May 24, 2023

 

 

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi akihutubia washiriki wakati wa hafla ya kufunga maonesho ya pili ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Jijini Arusha tarehe 22 Mei, 2023.

 

Sehemu ya washiriki wakifuatailia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi (hayupo pichani) wakati wa hafla ya kufunga maonesho ya pili ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Jijini Arusha tarehe 22 Mei, 2023.


Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi (katikati) akiwa aomeongozana na viongozi Baraza La Taifa La Elimu Ya Ufundi Na Mafunzo Ya Ufundi Stadi (NACTVET) na Mkoa wa Arusha alipokuwa akitembelea mabanda ya washiriki katika maonesho ya pili ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Jijini Arusha.



Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi akizungumza na wanafunzi wenye Ulemavu alipotembelea banda la Arusha City Council Special Education Need na kujionea bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wanafunzi hao.




Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi akipata maelezo kutoka kwa washiriki alipotembelea mabanda katika maonesho ya pili ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) yaliyofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Jijini Arusha tarehe 22 Mei, 2023.

PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)

Na: OWM (KVAU) - ARUSHA

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi amesema kuwa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi ni muhimu sana katika kuandaa nguvukazi yenye ujuzi unaohitajika katika kuendeleza uchumi wa taifa.

Amebainisha hayo wakati akifunga maonesho ya pili ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi (TVET) katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Jijini Arusha.

Aidha, Naibu Waziri Katambi ameeleza kuwa elimu hiyo itasaidia kuwajenga vijana kuwa na uwezo na ujuzi wa kufanya kazi mbalimbali za kiufundi, kuunda bidhaa na hata kuwa wajasariamali wakubwa.

“Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) ni chombo muhimu katika kusimamia vyuo na kuvifanyia kazi ili viweze kuinua ubora wa elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi,” amesema.

Ameongeza kuwa, Serikali inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Saluhu Hassan imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha kuboresha elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi.

“Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeanza kupitia sera ya elimu ili kuifanya elimu yetu kuwa na tija zaidi na katika mapitio hayo, tunatarajia kuona mapinduzi makubwa katika sekta ya elimu hapa nchini kwa kuweza kukidhi mahitaji ya soko la ajira na kuwezesha vijana wetu kuwa na ujuzi unaohitajika,” amesema.

Kwa upande mwingine, Naibu Waziri Katambi ametoa wito kwa Waajiri na Wadau wote wa Elimu kushirikiana kwa karibu na Vyuo vya Mafunzo ili viandae Wahitimu wanaohitajika katika soko la ajira.


Naye, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu Ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), Dkt. Adolf Rutayuga, amesema kuwa taasisi hiyo itahakikisha inaendelea kutekeleza dhima iliyojiwekea kwa mwaka 2023 ambayo imelenga kuimarisha elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi kwa nguvukazi yenye ujuzi nchini.

MCHENGERWA AWAASA WANANCHI KUTOSHIRIKI UHALIFU, AWAPONGEZA ASKARI WA UHIFADHI WA MANYARA KUZINGATIA WELEDI

May 24, 2023

Na John Mapepele

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mohamed Mchengerwa amewaasa wananchi kuacha tabia ya kuwashambulia Askari wa Uhifadhi pindi wanapokamata wahalifu huku akiwapongeza Askari wa Uhifadhi wa Manyara kwa kuzingatia maelekezo aliyoyatoa kwa askari wote wa uhifadhi nchi nzima ya kuwataka kutumia busara , weledi na kuzingatia sheria wakiwa kwenye doria badala ya kutumia nguvu zisizohitajika.

Mhe. Mchengerwa ametoa kauli hiyo leo Mei 23, 2023 wakati alipoongea na Vyombo vya Habari kuhusu tukio la uvamizi wa majangili katika eneo la Hifadhi la Ziwa Manyara waliokamatwa na Askari wa uhifadhi bila kutumia nguvu wala silaha ambapo baada ya kukamatwa wakiwa ndani ya ziwa hilo, majangili walio karibu na boti ya doria waliwasaidia watuhumiwa na kutaka kuzamisha boti hiyo.

Amesema baada ya purukushani hiyo majangili wenzao wapatao 40 waliokuwa karibu na tukio walikuja na kuanza kuwashambulia Askari wanne waliokuwa kwenye boti na kuharibu mashine ambapo askari hao walijipa ujasiri wakapiga makasia na hatimaye kutia nanga katika eneo la Nyati.

Ameongeza kuwa baada ya kuweka nanga katika eneo la Nyati, eneo ambalo askari mmoja wa uhifadhi aliuawa kwa kushambuliwa na Nyati katika siku za hivi karibuni, majangili hao waliendelea kuwashambulia lakini askari hao waliendelea kutumia busara na hawakuweza kutumia silaha walizonazo.“Kwa kuwa nilishatoa maelekezo kwa askari wote wa uhifadhi nchi nzima kutotumia nguvu wakati wa ukamataji wahalifu hata inapokuwa ndani ya hifadhi, watumie busara na weledi na pamoja kwamba askari hawa walikuwa na silaha hawakutumia nguvu wala silaha hali hii ilipelekea majangili hao kushirikiana na wenzao kuwavamia na kuwateka askari na wale watuhumiwa ambao walikuwa wamekamatwa na kutiwa pingu.” Amefafanua 

Ameeleza kuwa majangili hao walifanikiwa kuwatorosha watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi na wakiwa na pingu ambapo askari wa uhifadhi waliomba msaada mara moja kwa askari wenzao na wakatoa taarifa kwa jeshi la polisi na polisi walipofika walifanikiwa kuwaokoa askari wa uhifadhi waliokuwa wakishambuliwa na kutaka kuuawa na majangili hao.

Amesema baada ya tukio hilo majangili walikusanyika tena na kuanza kuvamia kwenye Ofisi ya vijiji na kutaka kuingia kwenye lango la Ofisi za Hifadhi ya Manyara ambapo amesema Jeshi la Polisi walitumia takribani masaa manne kuzuia vurugu hizo ili wasiingie ndani ya Hifadhi kufanya uhalibifu au matukio mengine ya kiuhalifu ambapo pia walitumia mabomu ya machozi.

Amesema hata baada ya kutumia mabomu ya machozi bado vurugu ziliendelea na kupelekea mtu moja kufariki.

Akisimulia kwa uchungu Waziri Mchengerwa amesisitiza kuwa tukio hilo ni la kusikitisha kwa kuwa haya yote yasingeweza kutokea kama wananchi wangetii sheria, aidha askari wote wa hifadhi wangeweza kuzama kwenye maji baada ya kushambuliwa na majangili na wananchi kuanza kuchukua sheria mkononi kwa kuwashambulia wahifadhi bila kuogopa na kuwatorosha watuhumiwa waliokamatwa kwa kufuata taratibu bila kuwapiga wala kutumia silaha walizokuwa nazo.

Amesema Serikali imeandaa maeneo mengi kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwa ni pamoja na shughuli za uhifadhi, kilimo, ufugaji na uvuvi ambapo wananchi wangeweza kuyatumia kwa kuzingatia sheria ambazo zimetungwa na wawakilishi wao bungeni kwa miaka mingi kwa faida ya vizazi vya sasa na baadaye badala ya kuwa sehemu ya uhalifu.
“Sisi kama Serikali tunatamani kuona kila mwananchi awe na furaha lakini tunawaomba watanzania, hatupaswi kugombana kwa kuwa maeneo ni mengi, naomba sana wananchi wafuate sheria, iwapo kila mtanzania akitii sheria ambazo tumezitunga sisi wenyewe hakutakuwa na mivutano yoyote baina ya wananchi na wahifadhi, na sisis tumejitahidi katika kipindi hiki kifupi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi wetu, tunaendelea kuwahamasisha wananchi kushiriki katika uhifadhi kwa kuwa wananchi ndiyo wahifadhi namba moja” Amesisitiza

Aidha amewataka wahalifu wote walioshiriki katika tukio hili kujitokeza mara moja kwenye jeshi la polisi kwa kuwa tayari taarifa ilifatolewa kabla ya tukio hilo kuwa kubwa ambapo amelishukuru jeshi la polisi kwa kuokoa askari wa uhifadhi ambao ni watoto wa watanzania ambao wanafanya kazi kubwa ya uhifadhi wa raslimali kwa faida ya taifa zima.

Kufuatia vurugu hizo Jeshi la Polisi mkoani Arusha linawashikilia watu 12 wanaodaiwa kufanya uhalifu na uchunguzi wa tukio hilo unaendelea ikiwa ni pamoja na kuwasaka vinara wa vurugu hizo ambapo pia amesisitiza kwa wananchi kuzingatia sheria za nchi na kuacha tabia za uvuvi haramu.