MAJINA YA WALIOTEULIWA UBUNGE, UWAKILISHI NA VITI MAALUM CCM YATANGAZWA RASMI

August 13, 2015
 Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akionyesha kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya 2015-2020 ya CCM wakati wa kufunga kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa mara baada ya kumaliza zoezi la kupitisha majina ya wagombea Ubunge na Uwakilishi mjini Dodoma.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar) Dk. Ali Mohamed Shein na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk.John Pombe Magufuli akipitia orodha ya majina ya waliopendekezwa kwenye nafasi za Ubunge na Uwakilishi,kulia ni Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Mizengo Pinda.

MNEC wa Wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete akipitia kitabu cha ilani ya Uchaguzi ya CCM kitakachotumika kwa mwaka 2015-2020.
 Dk. Salim Ahmed Salim akipitia majina ya walioteuliwa wakatia wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM mjini Dodoma.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma ambapo alitaja majina ya walioteuliwa na zile sehemu chache ambazo uchaguzi utarudiwa na sehemu zingine kufanyiwa uhakiki upya.
 Rais Kikwete Amzika Kisumo Mwanga

Rais Kikwete Amzika Kisumo Mwanga

August 13, 2015

2
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe mama Salma Kikwete wakitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza la Kada Mkongwe wa CCM  Marehemu Mzee Peter Kisumo wakati wa ibada ya mazishi iliyofanyika huko kijijini kwake Usangi- Mwanga Mkoani Kilimanjaro leo.
3
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Mama Hosiana Kisumo Mke wa Marehemu Peter Kisumo wakati wa mazishi yake huko Usangi Mwanga Mkoani Kilimanjaro.
5
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiweka udongo katika kaburi la Kada Mkongwe wa CCM Marehemu Peter Kisumo wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwake Usangi- Mwanga Mkoani Kilimanjaro.
6
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo kilichowekwa kanisani wakati wa mazishi ya kada mkongwe wa CCM Mzee Peter Kisumo yaliyofanyika kijijini kwake Usangi-Mwanga Mkoani Kilimnjaro.
(Picha na Freddy Maro)

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YATANGAZA MATOKEO YA TAKWIMU ZA PATO LA TAIFA KWA ROBO MWAKA YA KWANZA YA MWAKA 2015

August 13, 2015

Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Morrice Oyuke (Kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam wakati akitangaza matokeo ya takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka ya kwanza kuanzia mwezi Januari – Machi, 2015 ambayo yameonyesha kuwa thamani ya Pato la imekua na kufikia shilingi trilioni 21.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 18.6 ya robo mwaka ya kwanza ya mwaka 2014. Kushoto kwake ni Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa Daniel Masolwa wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Morrice Oyuke wakati akitangaza matokeo ya takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka ya kwanza kuanzia mwezi Januari – Machi, 2015 ambayo yameonyesha kuwa thamani ya Pato la imekua na kufikia shilingi trilioni 21.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 18.6 ya robo mwaka ya kwanza ya mwaka 2014. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO).

Na: Veronica Kazimoto
Matokeo ya takwimu za Pato la Taifa kwa robo mwaka ya kwanza yaani kuanzia mwezi Januari – Machi, 2015 yameonyesha kuwa thamani ya Pato la Taifa imekua na kufikia shilingi trilioni 21.9 ikilinganishwa na shilingi trilioni 18.6 ya robo mwaka ya kwanza ya mwaka 2014.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Morrice Oyuke amesema takwimu hizo zimetayarishwa kwa kuzingatia marekebisho ya Takwimu za Pato la Taifa kwa bei za mwaka 2007.
“Pato la Taifa kwa bei za mwaka 2007 katika kipindi cha robo mwaka ya kwanza linaonyesha kuwa na jumla ya thamani ya shilingi trilioni 10.6 kwa mwaka 2015 ikilinganishwa na shilingi trilioni 9.9 katika kipindi kama hicho mwaka 2014”, amefafanua Oyuke.
Oyuke amesema kuwa, Pato hili la Taifa limeongezeka kwa kasi ya asilimia 6.5 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 8.6 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.
Aidha, Oyuke amesisitiza kuwa utayarishaji wa takwimu za Pato la Taifa hujumuisha shughuli zote za kiuchumi na hivyo hutumika katika kutathmini, kupanga mipango na kutayarisha sera za kiuchumi.
Baadhi ya shughuli hizo za uchumi ni kilimo na mifugo ambazo zilikua kwa kasi ya asilimia 2.6 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 3.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.
Shughuli za Uvuvi ziliongezeka kwa asilimia 0.9 kwa robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na asilimia 2.3 kipindi kama hicho mwaka 2014. Ukuaji huu ulitokana na jitihada za Serikali kuwasaidia wakulima kwa kutoa ruzuku na maelekezo ya Ma-ofisa Ugani kwa wakulima kama vile kuchagua mbegu bora yaliyosaidia kuongeza uzalishaji.
Shughuli za Uchimbaji Madini, Mawe na Kokoto ziliongezeka kwa kasi ya asilimia 0.6 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya ukuaji wa asilimia 19.7 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.
Shughuli za Uzalishaji bidhaa Viwandani zilikua kwa  kasi ya asilimia 5.7  katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 8.2 kipindi kama hicho mwaka  mwaka 2014. Kasi ya ukuaji ilitokana na kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa za vyakula, vinywaji, tumbaku, nguo, simenti na bidhaa za kemikali na madawa.
Shughuli nyingine ni pamoja na Uzalishaji nishati ya umeme na maji ambazo zilikua kwa kasi ya asilimia 10.7 katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ikilinganishwa na kasi ya asilimia 10.1 katika kipindi kama hicho mwaka 2014. Kuongezeka kwa ukuaji wa nishati ya umeme kulitokana na kuongezeka kwa umeme uliozalishwa kutoka kwenye mitambo inayotumia, maji, mafuta na gesi asilia.
Shughuli za Fedha na Bima katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ziliongezeka kwa asilimia 9.1 ikilinganishwa na asilimia 11.2 kipindi kama hicho mwaka 2014.
Shughuli za Ujenzi (ambazo zinajumuisha ujenzi wa nyumba za makazi na zisizo za makazi; barabara na madaraja; na shughuli nyingine za uhandisi) katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2015 ziliongezeka  kwa asilimia 8.8 ikilinganishwa na asilimia 21.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2014.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu ina jukumu la kutayarisha na kusambaza takwimu rasmi nchini ikiwa ni pamoja na takwimu za Pato la Taifa kwa robo Mwaka ambazo hupimwa kwa kuangalia thamani ya bidhaa na huduma zilizozalishwa nchini katika vipindi vya miezi mitatu mitatu ambavyo ni Januari – Machi,  Aprili – Juni,  Julai – Septemba na Oktoba - Desemba.
UN CALLS FOR PATIENCE AND CALM AMIDST SUSPECTED DISEASE OUTBREAK

UN CALLS FOR PATIENCE AND CALM AMIDST SUSPECTED DISEASE OUTBREAK

August 13, 2015
IMG_0618
Ms. Joyce Mends-Cole, the UNHCR Representative in Tanzania.
src.adapt.960.high.burundi_tanzania_nyaragusu.1439212310200
Burundian families who fled their country wait to be registered as refugees at Nyarugusu camp in northwest Tanzania on June 11, 2015. (Aglietti / AFP / Getty Images).
The United Nations High Commissioner for Refugees (UNHCR) and the World Health Organization appeal for calm amid reports of the death of a Burundian refugee, suspected to have contracted the Ebola virus, in Kigoma region in North West Tanzania. The reports emanated following the death on 10th August in Maweni Hospital in the region. The deceased, had resided in Nyarugusu Camp for three years and was among refugees who were in the Resettlement program to United States of America.
On 9th August 2015, the refugee was sent to Kigoma Regional Hospital (Maweni) with bleeding gums, eyes and ears. He was fatigued and his body was itching. However, he had no fever. He was under treatment in the hospital when he passed away the following day (10th August 2015). Remains of the deceased were buried under close supervision by the Regional Medical Team and WHO staff. There is no evidence that the deceased had travelled outside of Kigoma region in the last three years, nor had he received visitors from any of the West African countries affected with Ebola, i.e. Liberia, Sierra Leone and Guinea. Therefore it is highly unlikely that he had Ebola, as a review of the case by WHO shows that it does not meet the standard case definition for the disease. However precautions have been taken and continue.
Two days after his death, his 14 year old daughter had a nose bleed. Standard care for nose bleeding was provided and it later emerged that she has a history of nose bleeding. The girl is now stable with no bleeding. “Blood samples of the deceased, wife, daughter, son and care taker were collected and sent to the National Laboratory for further investigation. Laboratory technicians have received them and preliminary results are now available.
WHO advises continued monitoring of all contacts, hand washing and maintenance of a high standard of personal hygiene as a precautionary measure. Laboratory tests done on samples collected from the suspected case and three close family members were negative for Chikungunya and Dengue. The blood picture does not show any of the features associated with viral infection. Specific test results for Rift Valley Fever, Ebola and Marburg will be shared when they become available. “However, there should be no disruption in day to day activities,” commented Dr. Chatora, WHO Representative in Tanzania.
Ms. Joyce Mends-Cole, the UNHCR Representative in Tanzania also spoke on the situation, saying, “UNHCR is aware that this situation has caused serious concern among refugees, the donor community and the Tanzanian public at large. However we ask for a calm approach to the situation, while we wait for the results of the tests and appeal to the media not to use alarmist language” All refugee movements have been halted and hygiene practices reviewed. In the meantime, as stated by the Government yesterday, all those in contact with the deceased have been isolated and none have shown similar symptoms to those of the deceased.
WHO has obtained information that the deceased took some traditional herbs. This is being investigated further and more information will be shared should there be any new developments.
UNITED BANK FOR AFRICA TANZANIA RECOGNIZES BEST EMPLOYEE OF THE SECOND QUARTER

UNITED BANK FOR AFRICA TANZANIA RECOGNIZES BEST EMPLOYEE OF THE SECOND QUARTER

August 13, 2015
EMPLOYEE OF THE QUARTER-3
Relationship Manager Nicholaus Shimba (right) receiving his certificate from the COO Mr. Chris Byaruhanga (left) in recognition of his significant performance in the second quarter.
EMPLOYEE OF THE QUARTER-2
Relationship Manager Nicholaus Shimba giving a word of thanks after receiving his certificate in recognition of his significant performance in the second quarter.
Pic 3
Fellow staffs look on in joy for the overwhelmed Relationship Manager Nicholaus Shimba (right) receiving his certificate from the COO Mr. Chris Byaruhanga (left).
Pic 2
One of the staff taking an autograph enjoying the moment with the winner of the employee of the quarter Nicholaus Shimba (right).
Pic 1
A cross section of employees enthusiastically listening to the speech of the MC of the day M/S Queen Odunga the Customer Service Quality Officer not in pictures as she announces the employee of the second quarter.
Recognizing staff performance is very important, United Bank for Africa Tanzania is making sure that employees have a very conducive and motivated working environment.
Following the employee’s recognition scheme that aims at recognizing and rewarding examples of high achievement and desirable behavior, encourage excellence and commitment from employees and raises the high morale of employees by showing appreciation of their efforts, Mr. Nicholaus Shimba was announced on Friday as the employee of the second quarter for April to June 2015.
“We take great pleasure in recognizing Nicholaus Shimba as the United Bank for Africa Tanzania employee of the quarter for the period of April through June 2015.” The Chief Operating Officer Mr. Chris Byaruhanga said when handing over the award to the winner. He continued to say “the selection was based on Nicholaus’s demonstrated, sustained, superior performance in the execution of his duties.”
“I am so overwhelmed; I thank you my fellow staff for this achievement, if it were not for the dedicated Wholesale Banking team that I work with, this wouldn’t have happened. He continued to commend the bank for recognizing his efforts “United Bank for Africa is a very good employer they motivate us to do better thus performing with great zeal. Let’s continue to support each other so that the time comes when we are all up to our game.” Advised the employee of the second quarter winner, Nicholaus Shimba, Relationship Manager Wholesale Banking…
This scheme is intended to create a positive working environment, show employees how much they are valued and appreciated, aid in retention and recruitment, and foster a spirit of healthy competition.
“Please join me in congratulating Mr. Nicholaus Shimba and be encouraged to be one of the employees of the next quarter, to get the sport award and be the team of the month in the coming awards. Let’s be recharged, work hard and deliver results. Together we can make things happen!” Urged Mr. Mathias Ninga the Head of Human Capital Management and Resources…
The rest of the staff were happy with the selection conveying that Nicholaus is a very hardworking and dedicated chap with a systematic way of handling his responsibilities, “you see him struggle with his team to retain our customers and making things happen in a timely manner. He really deserves the recognitions” they acknowledged.
The occasion ended with the motivated employees asking the winner to sign autographs in their notebooks as way of appreciating this achievement. Working hard comes with a reward and with United Bank for Africa it is an affirmative recognition.
MODEWJI BLOG YARUDI HEWANI BAADA YA KWIKWI YA MASAA 45

MODEWJI BLOG YARUDI HEWANI BAADA YA KWIKWI YA MASAA 45

August 13, 2015
modewjiblog logo
Baada ya kwikwi ya saa takribani 48 wataalamu wa Modewji blog wanakurejeshea hewani Blog yako pendwa.
Watundu wanaovuruga mambo mtandaoni (hackers) walijaribu kuimiliki blog hii kwa kufanya majaribio zaidi ya mara 300 yaliyosababisha mifumo ya kiusalama, kufanyakazi ya ziada kuihami Modewjiblog.
Hata hivyo wataalamu wetu wameziba mianya iliyokuwa imesababisha hali hiyo na sasa tupo pamoja nanyi.
Tunashukuru kwa uvumilivu wenu, tuko pamoja na endelea kuperuzi nasi.
Kwa mawasiliano zaidi tutumie email: info@modewjiblog.com
Imetolewa na Operation Manager, Zainul Mzige.

SIKU YA KIMATAIFA YA VIJANA DUNIANI YAADHIMISHWA KWENYE VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR

August 13, 2015


Maandamano  yakiongozwa na bendi ya jeshi la polisi
 
Baadhi ya vijana kutoka shule mbalimbali wakiandamana kuingia katika viwanja vya mnazi mmoja wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishw  jijini Dar es Salaam. Mashirika mbalimbali  ya mataifa yanayofanya shughuli za vijana ni kamaUNFPA, IYF, UNIC, ILO, RESTLESS DEVELOPMENT, YUNA, AMREF, MARIE STOPES, pamoja na PSI.(Picha zote na Geofrey Adroph)
 
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na viongozi wengine wakipokea maandamano ya vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja leo jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi na wapili kushoto ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bibi. Natalia Kanem.
 
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel pamoja viongozi wengine wakipokea maandamano ya vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja  jijini Dar es Salaam.
 Viongozi katika meza kuu wakiimba wimbo wa Taifa wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani iliyoadhimishwa katika Viwanja vya Mnazi Mmoja  jijini Dar es Salaam.
  Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem akizungumza na vijana wakati wa Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja. Katika hotuba yake aliweza kuzungumzia maswala ya watoto wa kike kubeba mimba wakiwa na umri mdogo ambao unapelekea kuacha masomo kutokana na ujauzito huo pia aliwasisitiza vijana kuwa na umoja kwani ndio nguvu kazi ya Taifa.
Mwendeshaji wa Sherehe hiyo Bi. Usia Nkhoma ambaye ni Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC)  akizungumza jambo na  vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi(wa nne kutoka kulia) akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza na vijana wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.Wa tatu kutoka Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel, Wa kwanza kulia ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa pili kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
 Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akitoa shukrani kwa wawakilishi wa Umoja wa Mataifa katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa pili kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwahutubia vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake aliwasisitiza vijana kujitokeza katika uchaguzi unaotegemea kufanyoka mwezi wa kumi mwaka huu ili kuchagua viongozi makini watakaoweza kutetea masuala ya vijana na pia aliwasisitiza vijana kufanya kazi za kujitolea.
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum akiwasalimia vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Bw. Hesein Melele(wa kwanza kuli) kijana ambaye ni mwakilishi wa asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA) akiwasilisha maazimio yaliyofikiwa na vijana wakati wa kongamano lililofanyika Agosti 10 mwaka huu kujadili ujumbe wa siku ya kimataifa ya vijana duniani na kuandaa maazimio yaliyowasilishwa kwa mgeni rasmi leo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani.
 Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Jangwani, Tatu Ahmed akitoa shukrani kwa wageni waalikwa waliofika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani.
Mratibu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutoka asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA), Rahim Nasser akiwatolea ufafanuzi vijana waliofika kwenye banda la Umoja wa Mataifa katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani  Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akimsikiliza kwa makini Mratibu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutoka asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA), Rahim Nasser alipotembelea kwenye banda la Umoja wa Mataifa
 Mkufunzi wa Ujasiriamali/Biashara wa Program ya anzisha na imarisha biashara yako (SIYB) iliyochini ya Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. MacDonald Lanzi (wa pili kutoka kulia) akimfafanulia jambo Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel. Wa pili kushoto ni Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum na wa kwanza kutoka kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem.
Mshauri na Mkufunzi wa Ujasiriamali/Biashara wa Program ya anzisha na imarisha biashara yako (SIYB) iliyochini ya Shirika la Kazi Duniani (ILO), Bw. Lawrence Ambokile(mwenye koti jeusi) akitoa ufafanuzi kwa Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel alipotembelea banda ilo
 Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum akisaini kitabu katika kwenye moja ya bada la PSI Tanzania katika Viwanja vya Mnazi Mmoja walipokua wakiadhimisha siku ya kimataifa ya vijana duniani. kushoto ni Dkt. Benedict Nyiro
Ofisa Habari wa Kituo cha Taarifa cha Umoja wa Mataifa Tanzania (UNIC), Stella Vuzo(wa kwanza kushoto), Meneja mradi wa ICS Bi. Imisa Masinjila(wa pili kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara hiyo Prof. Hermas Mwansoko(wapili kutoka kulia) pamoja na Imisa Masinjila wakizungumza jambo maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum(wa kwanza kushoto) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem(katikati) wakizungumza jambo na  Mkurugenzi Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. James Kajugusi  wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 Msaidizi wa Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini Tanzania Bi. Hashina Begum pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya vijana waliofika kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
  Bw. Hesein Melele(katikati) kijana ambaye ni mwanachama wa asasi ya vijana chini ya umoja wa mataifa (YUNA) akiwa kwenye picha ya pamoja na vijana wenzake ambao ni Rehema Pascal(kushoto) pamoja na Felister
  
 
 
 
 
 
 
 

 Vijana kutoka vikundi mbalimbali wakitoa burudani wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 
 
 
Vijana wakifuatilia kwa makini matukio mbalimbali yaliyokua yakiendelea wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya vijana duniani katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.