BREAKING NEWS: WAZIRI MKUU MSTAAFU FREDRECK SUMAYE AONDOKA CCM NA KUJIUNGA NA CHADEMA

August 22, 2015

 Waziri Mkuu mstaafu, Fredreck Sumaye (kushoto), akizungumza na wanahabari wakati akitangaza kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo mchana.
 Waziri Mkuu mstaafu, Fredreck Sumaye (kulia), akipeana mkono na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe Dar es Salaam leo mchana, baada ya kujiunga na chama hicho. Anayeshuhudia katikati ni Mgombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
 Sumaye akisisitiza jambo
Sumaye (wa tatu kulia), akiwa na viongozi wanaunda Umoja wa Katiba (UKAWA) baada ya kuondoka CCM na kujiunga na Chadema.

MTOTO WA MAMA NTILIE PANGANI ACHUKUA FOMU ZA KUWANIA UBUNGE,AHAIDI UJENZI WA BARABARA YA TANGA-PANGANI-SADANI

August 22, 2015


MSIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA PANGANI,ZABIBU SHABANI AKIMKABIDHI FOMU ZA KUWANIA UBUNGE KUPITIA CCM JUMAA AWESO JUZI WILAYANI PANGANI
















JEMBE FM MWANZA YAFUNGUA MILANGO KWA VYAMA VYA SIASA KUTANGAZA MIKUTANO LIVE

August 22, 2015

 Mbio za kampeni ya uchaguzi mkuu 2015 tayari zimeanza. Ni wasaa sasa kwa wagombea wa vyama mbalimbali kupishana huku na kule vijiji kwa vijiji, kata kwa kata, wilaya kwa wilaya, mkoa kwa mkoa wakifanya mkutano ya kampeni za siasa kutambulisha wagombea wao na kuzinadi sera zao al-muradi wapate ridhaa ya wananchi. 
 
Zoezi hilo ni gumu ila sisi kama jEMBe fM tunalirahisisha!! Sasa ili upate kuwafikia wananchi wengi ndani ya muda mfupi jEMBe fM imefungua milango kwa kutoa huduma ya matangazo ya moja kwa moja yaani LIVE toka viwanja vya mikutano tena full kiwango (HATUBAHATISHI) kwa maelezo zaidi piga simu kitengo cha masoko katika namba ±255282506068 au fika katika ofisi zetu zilizopo jengo la PPF ghorofa ya 6.

YANGA SC 'WAWANYWA' AZAM FC KWA MATUTA, WABEBA NGAO MARA YA TATU MFULULIZO

August 22, 2015


Kocha wa Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm akimpongeza kipa Ally Mustafa 'Barthez' baada ya mechi jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam 
Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
MLINDA mlango Ally Mustafa ‘Barthez’ amepangua penalti mbili na kuiwezesha Yanga SC kutwaa Ngao ya Jamii baada ya kuifunga Azam FC kwa penalti 8-7 kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Barthez alipangua penalti za beki raia wa Ivory Coast, Serge Wawa Pascal na mshambuliaji Ame Ali ‘Zungu’, wakati kipa wa Azam FC, Aishi Manula naye alicheza penalti ya Nahodha wa Yanga SC, Nadir Haroub Ali ‘Cannavaro’ ikapanguliwa.
Penalti za Yanga SC zilifungwa na Haruna Niyonzima, Deus Kaseke, Amissi Tambwe, Andrey Coutinho, Godfrey Mwashiuya, Thabani Kamusoko, Mbuyu Twite na Kelvin Yondan aliyepiga ya mwisho.
Wachezaji wa Yanga SC wakishangilia na Ngao yao baada ya mechi

Penalti za Azam FC zilifungwa na Kipre Herman Tchetche, Nahodha John Raphael Bocco, Himid Mao Mkami, Aggrey Morris, Jean Baptiste Mugiraneza, Erasto Nyoni na Shomary Kapombe. 
Ushindi huo ni sawa na kisasi baada ya Yanga SC kufungwa kwa penalti 5-3 katika Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame Julai 29, mwaka huu Uwanja wa Taifa, baada ya sare ya 0-0. 
Katika dakika 90 za mchezo wa leo, timu zote zilishambuliana kwa zamu na kosakosa zilikuwa za pande zote mbili, lakini dakika za mwishoni, Yanga SC walikuwa wakali zaidi.
Kipa wa Azam FC, Aishi Manula alionekana kabisa akijiangusha kupoteza muda ili kupunguza kasi ya Yanga SC dakika za mwishoni.
Kevin Yondan alicheza kwa kiwango kikubwa leo na dakika ya 37 aliitokea vizuri pasi ndefu ya Mzimbabwe Thabani Kamusoko na kumchambua vizuri kipa Aishi Manula, lakini beki Shomary Kapombe akabinuka ‘tik tak’ kuuokoa mpira uliokuwa unaelekea nyavuni.  
Nahodha wa Azam FC, John Bocco (kushoto) akimuacha chini beki wa Yanga SC, Kevin Yondan 

Almanusra Bocco aifungie Azam FC dakika ya 86 baada ya pasi nzuri ya Mugiraneza, lakini shuti lake likaokolewa na kipa Barthez aliyekuwa katika ubora wake siku ya leo.
Hii inakuwa mara ya tano Yanga SC kutwaa Ngao ya Jamii ikiwa ni rekodi, baada ya kuifunga Simba SC mara mbili, mwaka 2001 mabao 2-1 na 2010 kwa penalti 3-1 baada ya sare ya 0-0 ndani ya dakika ya 90, kabla ya kuifunga Azam FC miaka mitatu mfululizo, 2013 bao 1-0 na 2014 mabao 3-0.
Inafuatia Simba SC iliyotwaa Ngao mara mbili, mwaka 2011 wakiifunga Yanga SC 2-0 na 2012 wakiifunga Azam FC 3-2, wakati Mtibwa Sugar ni timu nyingine iliyowahi kutwaa Ngao mwaka 2009 ikiifunga 1-0 Yanga SC.
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Mwinyi Mngwali, Kevin Yondani, Nadir Haroub, Said Juma/Haruna Miyonzima dk57, Simon Msuva, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma/Deus Kaseke dk85, Amisi Tambwe na Godfrey Mwashiuya.
Azam FC: Aishi Manula, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Agrey Morris, Paschal Wawa, Mudathir Yahya/Jean Mugiraneza dk68, Himid Mao, Frank Domayo/Ame Ally dk82, Farid Mussa, John Bocco na Kipre Tchetche.

MAANDALIZI YA UZINDUZI WA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU CCM YAKAMILIKA, MAGUFULI, SAMIA KUUNGURUMA JANGWANI KESHO

August 22, 2015

 Katibu Muenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Juma ‘Gadafi’ akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisi kwake leo asubuhi, kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya uzinduzi wa mkutano wa kampeni za uchaguzi mkuu wa chama hicho utaofanyika kesho viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Picha zikichukuliwa.
……………………………………………
Na Dotto Mwaibale
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dar es Salaam kimetangaza ratiba ya uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa chama hicho utakaofanyika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam.
Katibu Muenezi wa chama hicho Mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Juma ‘Gadafi’ akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake Dar es Salaam leo asubuhi, alisema maandalizi yote ya uzinduzi huo tayari yamekamilika.
“Maandalizi yote tayari yamekamilika na leo jukwaa kubwa la kukaa viongozi linafungwa na tunategemea kuwa na watu wengi katika uzinduzi huo” alisema Gadafi.
Gadafi alisema kuanzia saa tatu asubuhi watu kutoka sehemu mbalimbali na wapenzi wa chama hicho wataanza kuwasili katika viwanja hivyo ambapo viongozi wastaafu wa chama na serikali na wale waliopo kazini watafuatia na kisha watawasili mgombea nafasi ya urais kupitia CCM Dk.John Magufuli na mgombea mwenza wake Samia Hassan Suluhu na baadae Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
Alisema katika uzinduzi huo wageni mbalimbali wamealikwa kutoka mikoa ya jirani na mabalozi kadhaa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.
Gadafi alisema kuwa wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo viongozi wa chama hicho wakiwemo mgombea urais Dk.Magufuli na mgombea mwenza wake watahutubia wanachama kuelezea sera za chama hicho na utekelezaji wa ilani ya CCM kuelekea uchaguzi mkuu.
Gadafi alitumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi, wanaccm na makundi mengine kufika katika uzinduzi huo ambapo kutakuwepo na vikundi mbalimbali vya burudani na kufanyika kwa dua za madhehebu yote za kukiombea chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu kama inavyofanyika vipindi vyote wanapo zindua kampeni za uchaguzi mkuu.
Katika hatua nyingine Gadafi amekemea vikali vitendo vya udhalilishaji kwa wanachama wake vya kuzomewa na kuchaniwa nguzo zao wanapopita maeneo ya Kariakoo na Mwenge.
Alisema kila mwana chama yeyote wa chama cha siasa ana haki ya kuvaa nguo za chama chake hivyo kuwazomea wanachama wao ni kukiuka sheria ya nchi na inaweza kuleta ugomvi pale upande wa pili utakapoamua nao kujibu mapigo.
“Napenda kuiomba serikali ya mkoa wa Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Suleiman Kova kukomesha vitendo hivyo dhidi ya wanachama wetu na kama wanaona tunawakera wasubiri majibu yao baada ya uchaguzi kwani CCM itachukua ushindi mapema huku wakibaki wakishangaa” alisema Gadafi.

MSHINDI WA SHINDANO LA MAMA SHUJAA WA CHAKULA CAROLINA CHILELE AIBUKA NA MILIONI 20

August 22, 2015
Mshindi wa Shindano lala Mama Shujaa wa Chakula Msimu wa Nne mwaka 2015 Calorina Chilele Muda mchache Baada ya kutangazwa kuwa mshindi.
Afisa Kilimo Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Dkt. Kissa Kajigili , akiwapongeza Oxfam kwa kuandaa shindano la Mama Shujaa wa Chakula na washiriki wote kwa ujumla walioshiriki katika Shindano hilo, Pia alimpongeza Mshindi wa Mama Shujaa wa Chakula 2015 Carolina Chilele na kumtaka awe mfano bora pia akawe chachu ya kuinua kilimo na kuwasaidia wenye uhitaji yaani wakulima wanawake wadogo wadogo, Mwisho aliwaomba Oxfam waendelee na Shindano hili muhimu.
Jackson Yusuph Mzumba Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kibweni akitoa neno la Shukurani kwa niaba ya Serikali ya Kijiji cha Kisanga
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kisarawe Bw. Ellioth Phillemon Mwasambwite akiwashukuru Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 , na kuwaaaga rasmi, pia kumpongeza Mshindi wa Shindano hilo msimu wa Nne Bi. Carolina Chilele , Mwisho aliwapongeza Oxfam kwa kuanzisha shindano endelevu kwa Maendeleo ya wakulima hasa wanawake.
Mmoja wa akina mama ambao walikuwa wanakaa na Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula katika Kijiji cha Kisanga Bi. Sophia Shomvi akitoa neno la Shukurani kwa washiriki hao kwa  jinsi walivyo kaa vizuri pamoja na pia kuwaachia elimu kubwa wanakijiji hao. Mwisho alitoa neno la Kuwaaga Rasmi
VYAMA 8 VYAPITISHWA KUWANIA NAFASI YA URAIS BARA

VYAMA 8 VYAPITISHWA KUWANIA NAFASI YA URAIS BARA

August 22, 2015

New Picture (1)
Mgombea Urais KupitiaChama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Jaji Mstaafu na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa Uchaguzi Damian Lubuva wakati wa kurejesha Fomu za kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mapema leo kwenye ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jijini Dar es Salaam.
New Picture (2) New Picture (3)
Mgombea Kupitia Chama cha Mapinduzi Dkt. John Pombe Magufuli akipokea nyaraka mbalimbali ikiwemo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria ya Taifa ya Uchaguzi,Maelekezo kwa wagombea wa vyama vya siasa, Maadili ya Uchaguzi toleo la mwka 2015 na sheria na kanuni za gharama za uchaguzi kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa Uchaguzi Damian Lubuva, mapema leo kwenye ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jijini Dar es Salaam.
New Picture
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Mstaafu Damian Lubuva akijadili Jambo na Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Hamid Mahmoud Hamid wakati wa urudishaji wa fomu za kugombea nafasi ya Urais Kuelekea Katika Uchaguzi Mkuu wa Octoba 25, 2015.
New Picture (4)
Mgombea Urais kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akipokea nyaraka mbalimbali toka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa Uchaguzi Damian Lubuva, mapema leo kwenye ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jijini Dar es Salaam.
New Picture (5)
Mgombea Urais Kupitia chama cha TLP Bw. Macmillan Elifatio
Lyimo (Kushoto) akipokea nyaraka mbalimbali toka kwa Mwenyekiti wa Tume ya
Taifa Uchaguzi Damian Lubuva, mapema leo kwenye ofisi za Tume ya Taifa ya
Uchaguzi Jijini Dar es Salaam.
 RAIS KIKWETE AMUAPISHA BALOZI MPYA WA TANZANIA NCHINI ZIMBABWE LEO IKULU

RAIS KIKWETE AMUAPISHA BALOZI MPYA WA TANZANIA NCHINI ZIMBABWE LEO IKULU

August 22, 2015
1
Rais Jakaya Kikwete akimuapisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala katika hafla iliyofanyika leo Ijumaa Agosti 21, 2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
2
 Rais Jakayta Kikwete akimkabidhi nyaraka za kazi Balozi Mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala katika hafla iliyofanyika leo Ijumaa Agosti 21, 2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
7
Viongozi waandamizi wa Vyombo vya Ulinzi wakibadilishana mawazo wakati wa hafla ya kumuapisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Luteni Jerenali Charles Lawrence Makakala, leo Ijumaa Agosti 21, 2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
3 Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala mara baada ya kumuapisha leo Ijumaa Agosti 21, 2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
4
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala (wa tatu kushoto) pamoja na familia yake mara baada ya baada ya kumuapisha leo Ijumaa Agosti 21, 2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
5
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi Waandamizi wa Vyombo vya Ulinzi pamoja na Balozi Mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala mara baada ya kumuapisha iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Agosti 21, 2015.
6
  Rais Jakaya Kikwete akibadilisha mawazo na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zimbabwe, Luteni Jenerali Charles Lawrence Makakala mara baada ya baada ya kumuapisha leo Ijumaa Agosti 21, 2015 Ikulu Jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.
PICHA NA ISMAIL NGAYONGA.

OFISA MTENDAJI MKUU DAWASCO,MHANDISI CYPRIAN LUHEMEJA AAGA RASMI MUWSA.

August 22, 2015
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,( MUWSA ) ambaye kwa sasa ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco,Mhandisi Cyprian Luhemeja akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa MUWSA,Mhandisi Patrick Kibasa ,karatasi zenye ndoto za wafanyakazi wa Mamlaka hiyo hukuakimtaka kuzifanyia kazi.
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,wakiwa katika kikao maalumu kwa ajili ya kuagana na aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo.
Ofisa Mtendaji mkuu wa DAWASCO ,Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWASA pindi alipokutana nao kwa ajili ya kuaga rasmi katika ofsi yake hiyo ya zamani aliyokuwa Mkurugenzi.
Meneja rasilimali watu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi ,Michael Konyaki (kushoto) akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa MUWSA,Mhandisi Patrick Kibasa wakati wa kikao cha kuagana na aliyekuwa mkurugenzi wa Mamlaka hiyo,Mhandisi Cyprian Luhemeja.
Meneja Fedha wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi ,Joyce Msiru (kulia) akiwa na Meneja Biashara  wa MUWSA,John Ndetiko wakati wa kikao cha kuagana na aliyekuwa mkurugenzi wa Mamlaka hiyo,Mhandisi Cyprian Luhemeja
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Mhandisi ,Patrick Kibasa akizungumza katika kikao hicho.
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na uSAFI WA Mazingira mjini Moshi,MUWSA.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi TUICO tawi la Muwsa,Maulid Barie akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wakati wa kikao cha kuagana na aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo,Mhandisi ,Cyprian Luhemeja aliyehamishiwa Dar es Salaam kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO.


Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,wakiwa katika kikao hicho.
Meneja Biashara wa MUWSA,John Ndetiko akitoa neon la shukrani katika kikao hicho.
Wafanyakazi wa MUWSA.
Mhandisi Luhemeja akiagana na wafanyakazi wa MUWSA.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.