BARRICK YASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA HEDHI SALAMA DUNIANI KWA VITENDO

May 28, 2024

 

Meneja Mawasiliano wa Barrick nchini, Georgia Mutagahywa (wa pili kushoto) akikabidhi taulo za kike kwa mwalimu mkuu wa shule ya msingi Mwananyamala B,Modeta Mushi, zilizotolewa na kampuni hiyo kwa ajili ya kuwasitiri watoto wa kike.Wengine pichani ni Afisa Mawasiliano wa Barrick, Neema Ndossi na Mkaguzi wa Polisi Kitengo cha Usalama barabarani Amina Said.

Na Mwandishi Wetu.

Katika dhamira yake ya kuhakikisha Watoto wa kike na wanawake wanapata elimu kuhusu umuhimu wa usafi katika kipindi vya hedhi, Barrick Tanzania imeshiriki maadhimisho ya siku hii ambayo⁹ huadhimishwa Mei 28 kila mwaka ambapo wafanyakazi wake walishiriki kugawa taulo za kike kwenye makundi mbalimbali yenye mahitaji ikiwemo kwa wanafunzi wa shule ya msingi zilizopo jirani na maeneo ya migodi yake ya North Mara, Bulyanhulu na ofisi ya Dar es Salaam.Vile vile imeshirikiana na Jeshi la Polisi Kitengo cha usalama barabarani kutoa elimu ya usalama kwa Wanafunzi.

Wanawake wengi na wasichana katika jamii zetu hupata changamoto kubwa katika kipindi cha mzunguko wao wa mwezi wa siku za hedhi, kutokana na kutoweza kumudu kununua pedi za kutumia,ukosefu wa elimu kuhusiana na hali hiyo.imani za mila ambazo zinawafanya wengi kuamini kuwa suala la hedhi halipaswi kuongelewa,ukosefu wa mazingira rafiki ya kujihifadhi mtu anapokuwa kwenye hali hiyo kama vile vyoo na maji safi ya kutumia. Changamoto hizo zote zinasababisha watumie vifaa vya kuwasitiri visivyofaa ambavyo vinaweza kuwasababishia kupata maradhi.
Wanafunzi wakipatiwa mafunza ya usafi katika hedhi na usalama kutoka kwa wafanyakazi wa Barrick na Jeshi la Polisi
---
Barrick inaamini Siku ya Usafi wa Hedhi Salama Duniani ni maalumu kwa ajili ya kuvunja ukimya na kujenga ufahamu kuhusu umuhimu mkubwa wa kutunza usafi wakati wa hedhi. Siku hii inaangazia changamoto mbalimbali ambazo wanawake na wasichana kote duniani wanakabiliana nazo kuhusiana na hedhi, ambazo zinaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa afya zao, elimu yao na hali yao ya maisha kwa ujumla.

Kwa kuunga mkono siku hii muhimu, Barrick inachangia katika kujenga jamii yenye usawa, afya, na ufahamu zaidi, ambapo kila mwanamke na msichana anaweza kujitunza kwa ujasiri na heshima wakati wa hedhi yake.
Wanafunzi wa shule ya msingi Mwananyamala B wakifurahia zawadi za taulo za kike walizopewa kwa ajili ya kuwasitiri.

NMB YATOA FURSA KWA VIJANA WENYE BUNIFU MBALIMBALI HAPA NCHINI

May 28, 2024

 

MENEJA wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka  Ladislaus akizungumza wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Elimu Profesa Adolf Mkenda ambapo alisema kwamba benki hiyo inatambua umuhimu wa ubunifu katika maendeleo ya nchi.
MENEJA wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini Baraka  Ladislaus kulia akifurahia Waziri wa Elimu Profesa Adolf Mkenda kushoto wakati alipotembelea banda lao wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo 



Na Oscar Assenga, Tanga.

BENKI ya NMB imeshiriki kwenye maadhimisho ya wiki ya elimu, ujuzi na ubunifu yanayoendelea kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlaly huku wakitoa fursa kwa vijana wenye bunifu mbalimbali kwenda kufanya majaribio kwenye benki hiyo.

Hayo yalisemwa leo na Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini wakati wa ufunguzi wa maadhimisho hayo ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Elimu Profesa Adolf Mkenda ambapo alisema kwamba benki hiyo inatambua umuhimu wa ubunifu katika maendeleo ya nchi.

Alisema kwamba wao kama benki pamoja na ufadhili wanatoa Jukwaa Maalumu (Platfom) kuwakaribisha vijana kufanya ubunifu, maendeleo ya kibunifu na miradi hiyo wamekuwa wakiifadhili.

“Kwa niaba ya Benki ya NMB niwaambie kwamba tunatambua umuhimu wa ubunifu na ndio maana tumeungana nanyi katika wiki hii kwa kuwa elimu ndio inachochea ubunifu sisi kama Benki pamoja na mfadhili tunatoa jukwaa maalumu kuwakaribishasha vijana kuja kufanya ubunifu kufanya maendeleo ya kibunifu na miradi hiyo tunaifadhili”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba na inasaidia kuleta chachu ya kuendelela kuleta mendeleo ya ubunifu Tanzania hivyo wataendelea kuwaunga mkono kuhakikisha maendeleo ya sekta hiyo yanapiga hatua kubwa.

“Mh Waziri niwakaribiha vijana wenye bunifu mbalimbali waje kufanya majaribio yao kwenye benki ya NMB tuna platfomu NMB Sign Box nzuri inatoa nafasi nzuri ya bunifu tupo tayari kushirikiana nao kama Wizara kuhakikisha ubunifu unaleta chachu ya maendeleo ya kiuchumi hapa nchini”Alisema

Awali akizungumza wakati akifungua maadhimisho hayo Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda Serikali imesema ipo katika mchakato wa kujenga shule 100 za mafunzo ya Amali nyanja ya ufundi nchi nzima ili kuwawezesha vijana wa kitanzania kuweza kujiajiri au kuajiriwa kupitia ujuzi watakaopata kupitia vyuo hivyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Pastrobas Katambi amesema dunia ya sasa ina mabadikiko makubwa hasa kwenye masuala ya sayansi na teknolojia ujuzi na ubunifu hivyo ni wakati wa vijana wa kitanzania kwenda sambamba na mabadiliko hayo.

Awali Katibu mkuu wizara ya elimu sayansi na teknolojia Profesa Carolyne Nombo alisema wanafunzi 27 walishinda shindano la ujuzi na ubunifu ngazi ya vyuo ambao watafanyiwa mchakato na kupatikana wanafunzi 3 wa fani tofauti ambao watakwenda kushiriki mashindano ya kikanda na kimataifa mapema mwaka 2025.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Elimu, Utamaduni na Michezo Mhe. Husna Sekiboko amesema bunifu zinazoibuliwa katika maeneo mbalimbali nchini zitengenezwe katika uhalisia ili kuleta tija kwa jamii na kiuchumi.

Mwenyeji wa maadhimisho hayo ambaye ni Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Buriani alisema mkoa wa Tanga umepokea trilioni 2 na milioni 600 kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya elimu ambapo shule mpya 27 zimejengwa pamoja na vyuo vya kati ambavyo vipo katika hatua mbalimbali.