BREAKIN NEWZZZZ!!:- EXCLUSIVE PICHA ZA HOTEL YA NAURA SPRING IKUNGUA SASA HIVI LIVE ARUSHA HABARI ZAIDI ZINAKUJA SOON STAY TUNED!!

July 18, 2014



MTOTO AUAWA KIKATILI NA MUUAJI AJIKATA UUME WAKE NA KUULA KAMA KITOWEO

July 18, 2014

KILIMANJARO mtoto mmoja aliyefahamika kwa jina la Francis Fortunatus  mwenye umri wa miaka (9) ameuwawa kikatili kwa kukatwakatwa na mapanga kichwani huku mtuhumiwa aliyetenda kosa hilo akijikata uume wake na kisha kufariki dunia. Tukio hilo la kusikitisha limetokea  wilaya ya Moshi vijijini Mkoani Kilimanjaro.


Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Robert Boaz, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 1:00 asubuhi julai 18 mwaka huu katika eneo la marangu kata ya marangu mashariki, jimbo la Vunjo wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akielezea mazingira ya tukio hilo la kusikitisha kamanda Boaz, alisema kuwa mtoto huyo akiwa njiani akielekea shuleni gafla alivamiwa na mtu aliyejulikana kwa jina la Laurance Flavian (20) na kuanza kumkatakata kwa mapanga kichwa bila sababu yeyote na kusababisha kifo cha mtoto huyo papohapo.

Boaz alisema mara baada ya mtuhumiwa huyo kuona kuwa amesababisha mauaji alichukua panga alilo tumia kumkatakata mtoto huyo na kuamua kujikata uume wake mwenyewe.

MANGULA AKUTANA NA KATIBU MKUU WA CAPP JIJINI DAR ES SALAAM

July 18, 2014


Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip Mangula akimkaribisha Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan kwenye ofisi Ndogo za CCM Lumumba.
Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip akiwa kwenye mazungumzo na Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan kwenye ofisi ndogo za CCM Lumumba jijini Dar es Salaam,Julai 18,2014.
 Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip Mangula akiagana na Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan
Makamu Mwenyekiti wa CCM(Bara) Ndugu Philip Mangula akiagana na Balozi wa Sudani nchini Tanzania Dk.Yassir Mohamed Ali nje ya Ofisi Ndogo za CCM Lumumba ambapo Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) alikuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa CAPP Dk. Nafie Ali Nafie kutoka Khartoum Sudan.
(Picha na Adam Mzee wa CCM Blog)
WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS-MAZINGIRA AFANYA ZIARA KIWANDA CHA NIDA

WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA RAIS-MAZINGIRA AFANYA ZIARA KIWANDA CHA NIDA

July 18, 2014


DSC_0039 
Picha ikionyesha jinsi maj i yenye kemikali  yanavyotiririshwa toka katika kiwanda cha kutengeneza nguo cha NIDA kilichopo barabara ya Mandela.
DSC_0046 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Injinia Dkt Binilith Mahenge akiangalia uharibifu wa mazingira  uliosababishwa na maji yenye kemikali yanayotiririshwa na kiwanda cha NIDA. Anayemfuatia ni Mkurugenzi Mtendaji wa NEMC Bonaventura Baya, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Eng. Angelina Madete.
DSC_0054 
Jengo la kiwanda cha NIDA likionekana kwa nje
DSC_0064 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Injinia Dkt Binilith Mahenge akiongea na Menejimenti ya kiwanda cha kutengeneza nguo cha NIDA Textiles kuhu kiwanda hicho kinavyoharibu mazingira kwa kutiririsha maji yenye kemikali katika mto kibangu.
DSC_0073 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira Injinia Dkt Binilith Mahenge, akiongea na Vyombo vya habari kuhusu ziara yake aliyoifanya katika kiwanda cha NIDA textiles jijini Dar es Salaam
…………………………………………………
Rai imetolewa kwa wawekezaji wote Nchini kuhakikisha wanajali na kutunza Mazingira.Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt Binilith Mahenge wakati  alipofanya ziara ya kutembelea kiwanda cha kutengeneza nguo cha NIDA kilichopo barabara ya Mandela katika kata ya Kigogo jijini Dar es Saalam.
Kiwanda hicho ambacho kinalalamikiwa na wananchi kuwa kinatiririsha maji machafu yenye kemikali katika mto kibangu uliopo pembeni ya kiwanda hiko ambako wananchi wanalima mbogamboga kando yamto huo na wanatumia kula pia  wanauza ili kujipatia kipato pasipo kujali athari zilizopo kwenye maji hayo yenye kemikali.
Akiongea na Menejimenti ya kiwanda hiko Dkt. Mahenge baada ya kutemebelea mto huo na kujionea maji yalivyoathiriwa na kemikali zitokazo kiwandani, aliitaka Menejimenti ya kiwanda hiko kuacha mara moja kutiririsha maji yenye kemikali katika mto kibangu na hivyo basi kuchukua hatua za kitaalamu ili kuondoa kemikali zilizopo kwenye maji hayo.
Akiongea kwa niaba ya Menejimenti ya Kiwanda Afisa Utawala Mohammed Olewo aliahidi kwamba watafanyia kazi maagizo ya Waziri kwa ufasaha na wanaahidi watarekebisha makosa yote yaliyotokea pia watadumisha na kutunza  mazingira.
Ziara hiyo ni moja ya ziara za Waziri anazofanya kutembelea  maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kukagua utunzaji wa mazingira. 
RAIS AFUTARISHA WANANCHI MKOA WA KUSINI UNGUJA

RAIS AFUTARISHA WANANCHI MKOA WA KUSINI UNGUJA

July 18, 2014
IMG_6807 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (wa nne kulia) akijumuika na waislamu na Viongozi katika swala ya Magharibi katika viwanja vya Ofisi ya Uhamiaji Tunguu kabla ya  futari aliyowaandalia wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja jana.
IMG_6811 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akijumuika na Viongozi  katika futari aliyowaandalia wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja jana katika viwanja vya  Ofisi ya Uhamiaji Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.
IMG_6816 
Wananchi wa Mkoa wa Kusini  Unguja   kwa pamoja  wakijumuika katika fuitari iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein jana katika viwanja vya  Ofisi ya Uhamiaji Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.
IMG_6824 
Naibu Waziri wa Habari,Utalii,Utamaduni na MIchezo Bihindi Hamadi Khamis (wa pili kulia) akijumuika na Viongozi wengine katika futari iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein kwa wananchi wa Mkoa wa Kusini Unguja katika Ukumbi wa Ofisi ya Uhamiaji Tunguu Mkoa wa Kusini jana.
IMG_6831 Akinamama wa Mkoa wa Kusini Unguja wakijumuika katika futari iliyoandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Ali Mohamed Shein katika Ukumbi wa Ofisi ya Uhamiaji Tunguu Mkoa wa Kusini jana.
 [PICHA ZOTE NA RAMADHAN OTHMAN<IKULU]
NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ANGELLAH KAIRUKI AKIFANYA MAJUMUISHO YA WIZARA YAKE ALIYOIFANYA WIKI HII

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ANGELLAH KAIRUKI AKIFANYA MAJUMUISHO YA WIZARA YAKE ALIYOIFANYA WIKI HII

July 18, 2014


PIX 1 (1)Mkurugenzi mkuu wa kituo cha haki za binadamu  Hellen Kijo Bi. Simba(LHRC) (kulia) akimshukuru Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria baada ya kutembelea Taasisi zinazoshughulikia msaada wa kisheria jijini Dar es Salaam.
PIX5 
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angellah Kairuki akiongea na wanahabari(hawapo pichani) kutoa maelezo ya majumisho ya ziara yake ya siku tano ya kuzitembelea Taasisi zinazotoa Huduma ya Msaada wa Kishria Mkoani Dar es Salaam.
Picha na Rose Masaka-MAELEZO.
WAZIRI CHIKAWE ASHIRIKI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU JIMBONI KWAKE NACHINGWEA LEO

WAZIRI CHIKAWE ASHIRIKI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU JIMBONI KWAKE NACHINGWEA LEO

July 18, 2014

PIX 1 (2) 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe  (kushoto), akipokea Mwenge wa Uhuru katika Kijiji cha Chiola, Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi baada ya Mwenge huo kumaliza kukimbizwa katika Wilaya Ruangwa. Mwenge huo wa Uhuru ambao mwaka huu 2014 umebeba ujumbe usemao “Katiba ni Sheria Kuu ya Nchi, Jitokeze Kupiga Kura ya Maoni tupate Katiba mpya” utakimbizwa katika Wilaya ya Nachingwea ambapo miradi mbalimbali ya maendeleo itafunguliwa pamoja na kuzinduliwa. Picha zote na Felix Mwagara.
PIX 2 (1) 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto), akisalimiana na Kiongozi wa Mbio za Mwenge Mwaka 2014, Rachel Kassanda baada ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru uliotoka Wilaya ya Ruangwa na kuingia Wilaya ya Nachingwea. Wapili Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo ambaye ndio aliyekabidhiwa rasmi Mwenge huo kutoka Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi. Picha na Felix Mwagara.
PIX 3 (1) 
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Mwaka 2014, Rachel Kassanda (kulia) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chiola (hawapo pichani) baada ya kufungua Mradi wa Nyumba ya Mganga katika  Kijiji hicho kilichopo Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi. Katikati ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe. Mwenge huo wa Uhuru ambao mwaka huu 2014 umebeba ujumbe usemao “Katiba ni Sheria Kuu ya Nchi, Jitokeze Kupiga Kura ya Maoni tupate Katiba mpya” utakimbizwa katika Wilaya ya Nachingwea ambapo miradi mbalimbali ya maendeleo itafunguliwa pamoja na kuzinduliwa. Picha na Felix Mwagara.
PIX 4 (1) 
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Mwaka 2014, Rachel Kassanda (aliyebeba ndoo ya maji) akishangiliwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (wapili kulia), Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Regina Chonjo pamoja na wananchi baada ya kubeba ndoo ya maji baada ya kufungua mradi wa maji katika Kijiji cha Mituguru, Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi. Wapili kulia ni  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe akiwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Regina Chonjo. Mwenge wa Uhuru ambao mwaka huu 2014 umebeba ujumbe usemao “Katiba ni Sheria Kuu ya Nchi, Jitokeze Kupiga Kura ya Maoni tupate Katiba mpya” umengia katika wilaya hiyo ambapo unatarajiwa kufungua na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo. Picha na Felix Mwagara.
PIX 5 (1) 
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Mwaka 2014, Rachel Kassanda akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ikungu, Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi baada ya kukabidhi Bajaj kwa walemavu na Pikipiki kwa watendaji wa Wilaya na Kata mbalimbali katika wilaaya hiyo zikiwa ni kwa shughuli za maendeleo katika Halmashauri hiyo. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe. Mwenge huo wa Uhuru ambao mwaka huu 2014 umebeba ujumbe usemao “Katiba ni Sheria Kuu ya Nchi, Jitokeze Kupiga Kura ya Maoni tupate Katiba mpya” utakimbizwa katika Wilaya ya Nachingwea ambapo miradi mbalimbali ya maendeleo itafunguliwa pamoja na kuzinduliwa. Picha na Felix Mwagara.
PIX 6 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (kushoto), akiwasalimia wapiga kura wake wa Kijiji cha Ikungu wakati wa ukimbizaji wa Mwenge wa Uhuru katika Jimbo lake la Nachingwea.  Waziri Chikawe alimshukuru Kiongozi wa Mbio za Mwenge Mwaka 2014, Rachel Kassanda pamoja na timu yake kwa kuzindua na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo jimboni kwake. Picha na zote na Felix Mwagara.
*MBUNGE RIDHIWANI KIKWETE AENDELEA KUTIMIZA AHADI ZAKE JIMBO LA CHALINZE, SASA NI ZAMU YA JESHI LA POLISI

*MBUNGE RIDHIWANI KIKWETE AENDELEA KUTIMIZA AHADI ZAKE JIMBO LA CHALINZE, SASA NI ZAMU YA JESHI LA POLISI

July 18, 2014

1A
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akizungumza na uongozi wa polisi Mkoa wa Pwani na Wilaya ya Kipolisi ya Chalinze pamoja na wananchi waliojitokeza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa mbalimbali kwa jeshi hilo zikiwemo kompyuta, mifuko ya Saruji pamoja na fedha vilivyotolewa na mbunge huyo, Kwa ajili ya kutatua matatizo mbalimbali yanayolikabili jeshi la polisi katika utekelezaji wa majukumu yake ya ulizni na usalama wa raia na mali zao. 
Pamoja na kukabidhi kompyuta hizo zitakazosaidia katika utunzaji wa kumbukumbu pia mbunge huyo ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi vya Mbwewe na Kiwangwa ambavyo thamani inafikia zaidi ya shilingi milioni 11, Kushoto kwake ni Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei, hafla ya makabidhiano hayo imefanyika jana kwenye kituo kikuu cha polisi Chalinze.
1
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete kompyuta Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Kamanda ACP Ulrich Onesphory Matei zilizokabidhiwa na mbunge huyo kwa ajili ya kuboresha shughuli za jeshi hilo jimbo la Chalinze katikati ni Mkuu wa kituo cha polisi Chalinze Afande J. S. Magomi.
2
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akikata utepe kufungua ili kuonyesha kompyuta hizo huku viongozi wa jeshi hilo mkoani Pwani na jimbo la Chalinze wakishiriki shghuli hiyo.
3
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimuonyesha moja ya kompyuta Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei.
4
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei wakati alipokuwa akitoa shukurani zake kwa niaba ya jeshi la polisi mkoani Pwani mara baada ya kukabidhiwa kompyuta hizo , katikati ni mkuu wa ituo cha polisi cha Chalinze Afande J.S Magomi.
5
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Chalinze Mzee Bw. Kamis Kameza wakati alipokuwa akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa shule hiyo ambayo inajengwa na jeshi la kujenga taifa JKT kambi ya Ruvu.
6
Baadhi ya wanajeshi wa kambi ya JKT Ruvu wanaoshiriki katika ujenzi wa shule hiyo.
7
Moja ya madarasa ya shule hiyo ambayo yako katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wake.
8
Baadhi ya madarasa na maktaba ya shule hiyo yakiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi wake.
9
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na wanafunzi wa darasa la saba wa shule ya msingi ya Chalinze Mzee wakati alipokagua ujenzi wa shule hiyo.
10
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akiendelea kufanya ukaguzi wa ujenzi shuleni hapo kushoto ni Diwania wa kata ya Bwilingu Chalinze Bw. Ahmed Nasser.
11
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikweteakikagua ujenzi wa Maktaba ya shule hiyo akiwa ameongozana na Diwani wa kata ya Bwilingu Ahmed Nasser mbele na Mwalimu mkuu wa shule hiyo Khamis Kameza.
12
Baadhi ya wananchi waliohudhuria wakati wa hafla kukabidhi kompyuta kituo cha polisi Chalinze.
13
Diwani wa kata ya Bwilingu Chalinze Bw. Ahmed Nasser akizungumza wakati mbune wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete alipolokabidhi jeshi la polisi kompyuta kwa ajili ya kuboresha shughuli za jeshi hilo.
MKUU WA WILAYA JORDAN RUGIMBANA VITAMBULISHO KINONDONI

MKUU WA WILAYA JORDAN RUGIMBANA VITAMBULISHO KINONDONI

July 18, 2014

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana leo amezindua rasmi utoaji wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi Wilaya ya Kinondoni, na kuwa mtu wa kwanza kupokea kitambulisho chake mbali na kuwakabidhi wananchi 22 Vitambulisho vyao kutoka Kata ya Saranga mtaa wa Matangini.
1
Hapa anamkabidhi mmoja wa wananchi Bi. Chiku Issa Waziri kitambulisho cha Taifa, akishuhudiwa na Maafisa Usajili katika Wilaya Bw. Dickson Mbanga Weiss na Bw. Abdulrahman Muya (1505)
3
Mkuu wa Wilala ya Kinondoni akiwasili leo katika Kata ya Saranga Mbezi tayari kuzindua zoezi la utoaji Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wa Kata ya Saranga, Mbezi Dar-es-salaam (1462)
2
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana akikabidhiwa Kitambulisho chake na Afisa Usajili Wilaya ya Kinondoni Ndugu Abdulrahman Muya baada ya kukamilisha hatua za mwisho za uhakiki leo Kata ya Saranga Mbezi Dar-es-salaam. Kushoto ni Bw. Dickson Mbanga Weiss Afisa Usajili Kinondoni. (1470)
4
Mmoja wa wananchi wa Kata ya Saranga akiongozwa na Afisa Usajili wa NIDA kukamilisha hatua za mwisho za kuhakiki taarifa zake kabla ya kukabidhiwa kitambulisho chake leo, Kata ya Saranga Mbezi.(1505)
ZIARA YA WAZIRI WA FEDHA, MHE. SAADA MKUYA KATIKA MANISPAA ZA ILALA, KINONDONI NA TEMEKE.

ZIARA YA WAZIRI WA FEDHA, MHE. SAADA MKUYA KATIKA MANISPAA ZA ILALA, KINONDONI NA TEMEKE.

July 18, 2014


PIX 1
Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Bw. Stima Kabikile (katikati) akimkaribisha rasmi Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kulia) wakati alipofanya ziara yake ya siku moja katika Manispaa za Ilala, Kinondoni na Temeke kwaajili ya kupata taarifa kuhusu kodi za majengo na utendaji kazi wa wataalam wanaoshughulikia masuala hayo na mbinu za kuboresha namna ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia walipaji kodi.
PIX 3.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya (kulia) Ilala akimsomea taarifa ya makusanyo ya kodi za majengo na mikakati yake ya kufikia malengo waliojipangia ili kuongeza mapato Mhe. Waziri wa Fedha Bi. Saada Mkuya wakati wa ziara ya siku moja katika Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni.
PIX 7.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw. Yusuph Mwenda (kulia) akitoa maelezo yake kwa Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kushoto) wakati wa mkutano na viongzoi wa Manispaa ya Kinondoni jana jijini Dar es Salaam.
PIX 8.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw. Yusuph Mwenda (kulia) akitoa maelezo yake kwa Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kushoto) wakati wa mkutano na viongzoi wa Manispaa ya Kinondoni jana jijini Dar es Salaam.
PIX 10.
Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kulia) akiongozana na viongozi wa Manispaa ya Kinondoni wakati alipofanya ziara ya kikazi katika ofisi ya Manispaa hiyo jana kwaajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu makusanyo ya kodi za majengo pamoja kupeana mikakati mizuri ya kuboresha mifumo ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia kazi walipaji kodi ambao ni wananchi. katikati ni Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo Bw. Yusuph Mwenda na kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mwandisi Mussa Natty.
PIX 11.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw. Photidas Kagimbo (kulia) akisalimiana na Waziri waFedha, Mhe. Saada Mkuya (kushoto) mara alipowasili katika ofisi za Manispaa hiyo kwa ziara ya kikazi katika jana kwaajili ya kupata taarifa mbalimbali kuhusu makusanyo zikiwemo njia wanazotumia kukusanya kodi za majengo pamoja kupeana mikakati mizuri ya kuboresha mifumo ya ukusanyaji kodi hizo ili kuwarahisishia kazi walipaji kodi ambao ni wananchi.
PIX 12.
Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya (kulia) akihutubia mkutano huku akisisitiza juu ya kujikita zaidi katika kutumia TEHAMA katika kukusanya kodi za majengo kama njia rahisi inayomrahisishia mlipaji kodi kuweza kulipa kodi zake katika vituo vya huduma.
PIX 14.
Waziri wa Fedha, Mhe. Saada Mkuya akipitia moja ya taarifa alizopewa na uongozi wa Halmashauri wilaya ya Kiondoni wakati alipofanya ziara yake ya siku moja ofisi hapo.
……………………………………………………………………….
Na Rose Masaka.
 
WAZIRI wa Fedha Bi. Saada Mkuya amefanya ziara yake ya kikazi katika Wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam ili  kupata taarifa za makusanyo ya kodi za majengo ikiwa ni eneo moja kati ya maeneo sita ambayo yamepewa kipaumbele katika suala la ukusanyaji wa kodi kama vile eneo la kilimo na miundombinu.
 
Bi. Saada Mkuya amesema kuwa aliahidi kufanya ziara hiyo katika kikao kilichofanyika wiki iliyopita baada ya kurudisha zoezi la ukusanyaji wa kodi za majengo katika Serikali za Mitaa ili kuona kinachoendelea, kupata uhalisia na changamoto zinazowakabili watendaji wote wa Manispaa ya Ilala, Kinondoni naTemeke.
 
“Tumerudisha makusanyo ya kodi za majengo kwenye mitaa kwasababu ni rahisi na wanajua nyumba zote” alisema Bi. Mkuya.
 
Kodi ya majengo imekuwa ni moja ya chanzo kikubwa kinachotegemewa na Halmashauri za wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam. Serikali iliona hili mnamo mwaka 2013 na kuteua chanzo hiki kuwa mfano katika mpango wake wa matokeo Makubwa Sasa (BRN).
 
Kwa upande wake Mweka hazina wa Wilaya ya Ilala Bw. Stima Kabikile amesema kuwa Halmashauri ya Illala kupitia kitengo chake cha uthamini kwa kushirikiana na viongozi wa kata na mitaa wamejiwekea malengo ya kuyatambua majengo 10,000 ambayo hayakuwepo katika jedwali la awali kwa kutumia njia rahisi ya haraka ya uthamini.
 
“Tumeweza kubaini na kuongeza idadi ya majengo 6,820 kati ya 10,000 tuliyokadiria yenye thamani ya Shilingi bilioni 989.6 yenye tozo ya kiasi cha shilingi trilioni 1.5 na kuweka kwenye mfumo tayari kwa malipo”. Alisema Bw. kabikile.
 
Mtaalamu wa kodi za majengo Wilaya ya Ilala Bw. Joseph Kawiche amesema kuwa kila mmiliki wa nyumba hulipa kutokana na asilimia zake ingawa kuna baadhi ya watu ambao hawajaona umuhimu wa suala hili na kuwa wanafichiana majina,kwa hiyo wameona ni vizuri kutumia njia mbadala ya picha ili kuwabaibni wanaokwepa kulipa kodi.
 
Kwa upande wa Manispaa ya Kinondoni, Mstahiki Meya wa Wilaya hiyo Bw. Yusuph Mwenda amesema kuwa ameona umuhimu mkubwa wa kutumia Serikali za Mitaa na kutoa matangazo kwenye vyombo vya habari na vipaza sauti ili kujenga  uelewa kwa wananchi kuhusu kulipa kodi za majengo.
 
“Wenyeviti wa mitaa 171,watendaji wa Kata 34 na Watendaji wa Mitaa 171 wanashiriki na kuainisha majengo yaliyoachwa wakati wa uthamini”. Alisema Mwenda.
 
Mkurugenzi wa wilaya ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty amesema kuwa jumla ya Shilingi bilioni 1.1 zimekwishakusanywa katika majengo 3123,aidha majengo 3120 yaliyobakia yenye wigo wa kodi bilioni 1.4 yao katika hatua nzuri ya ulipaji.
 
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke amesema kuwa Halmashauri imekusanya kiasi cha shilingi milioni 165.7 kutokana na majengo ambayo awali hayakuwepo katika daftari la majengo ambapo mapato yanatarajiwa kuongezeka kwa hali ya juu katika mwaka huu wa fedha baada ya majengo yote 10,000 kuthaminiwa.
 
Baadhi ya changamoto zinazozikabili Wilaya hizo ni pamoja na waraka wa msamaha wa kulipa kodi ya majengo wakati sheria ipo kimya wakati wanamiliki majengo ya makazi,kupangishana biashara  ambao raia na wanajeshi wastaafu wanao,pia shule binafsi kudai kutoa huduma wakati ada zao zipo juu, hivyo Manispaa zote tatu zimetoa wito kwa wananchi wa Tanzania kulipa kodi kwa hiari na Serikali iweke wazi sheria za misamaha kama zipo.