March 29, 2014

BUNGE MAALUM LAPITISHA AZIMIO LA KURA YA MSETO

1900159_602127046540927_77902724_n 
Na Magreth Kinabo – MAELEZO, Dodoma
Hatimaye baada ya mvutano wa baadhi wa wajumbe wa Bunge la  Maalum la Katiba kuhusu upigaji wa kura ya siri na ya wazi kuendelea  leo  Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge Maalum, Mhe . Pandu Ameir Kificho amewasilisha  azimio la mapendekezo ya  ya upigaji kura wa wazi na siri  kutumika kwa pamoja katika kaununi ya 37 na 38, ambalo limetipitishwa na Bunge hilo kwa  matokeo ya  jumla kwa kura  ya ndiyo 376 na hapana 133 .