NYOTA WATATU COASTAL UNION WAPATA ULAJI OMAN, NI NYOSSO, SANTO NA DANNY LYANGA
WACHEZAJI
watatu wa timu ya soka ya Coastal Union ya Tanga, beki Juma Nyosso,
kiungo Jerry Santo na mshambuliaji Danny Lyanga wanatakiwa na klabu ya
Al Musannaa ya Ligi Kuu ya Oman, imefahamika.
Habari ambazo BIN ZUBEIRimezipata mjini hapa zimesema kwamba klabu hiyo imekwishakutana na
Habari ambazo BIN ZUBEIRimezipata mjini hapa zimesema kwamba klabu hiyo imekwishakutana na
Jerry Santo kulia akiwa na Salum Esry jana kabla ya chakula cha usiku |
Mwenyekiti wa Coastal Union, Hemed Hilal ‘Aurora’ kwa mazungumzo juu ya nyota hao.
Hata
hivyo, habari zaidi zinasema makubaliano hayajafikiwa kutokana na
Coastal kusema Musannaa imetoa ofa ndogo ya kuwanunua nyota wake hao.
Inaelezwa, kiungo Mkenya, Jerry Santo anatakiwa pia klabu ya Fanja,
ambayo hadi sasa ina mgeni mmoja tu kikosini mwake, Cisse wa Senegal.
Jana tena Aurora alikuwa ana kikao na uongozi wa Musannaa hata akashindwa kuhudhuria mwaliko wa chakula cha usiku, ambao Coastal walipewa na mwanachama wa timu hiyo anayeishi hapa, Salum Esry.
Aurora hakuwa wazi sana alipoulizwa leo asubuhi kuhusu maendeleo ya mazungumzo hayo, lakini Ofisa Habari wa Coastal, Hafidh Kido alisema dili hilo bao halijaiva.
Jana tena Aurora alikuwa ana kikao na uongozi wa Musannaa hata akashindwa kuhudhuria mwaliko wa chakula cha usiku, ambao Coastal walipewa na mwanachama wa timu hiyo anayeishi hapa, Salum Esry.
Aurora hakuwa wazi sana alipoulizwa leo asubuhi kuhusu maendeleo ya mazungumzo hayo, lakini Ofisa Habari wa Coastal, Hafidh Kido alisema dili hilo bao halijaiva.