RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA KIKAO CHA MAAFISA WAANDAMIZI, MAKAMANDA WA MIKOA NA VIKOSI WA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

June 02, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka saini kitabu cha wageni alipowasili kufungua kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 2017. Kushoto ni Waziri wa mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Nchemba na Kulia ni Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Simon Sirro
Kwaya ya Polisi ikitumbuiza wakati wa kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 
Sehemu ya wajumbe katika  kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda akiongea machache wakati wa ufunguzi wa  kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 
Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Simon Sirro akitoa muhtasari wakati wa ufunguzi wa kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 2017
Police Brass band wakisiliza hotuba wakisubiri zamu ya kutumbuiza
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Nchemba akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kufungua kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifungua kikao cha Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi na Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi katika Bwalo la Maafisa wa polisi la Oysterbay jijini Dar es salaam leo Juni 2, 2017

CCBRT, TIGO TANZANIA WAUNGANA KUTIBU UGONJWA WA MIGUU PINDE KWA WATOTO

June 02, 2017
Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti na Mahusiano na Serikali wa Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Sylvia Balwire akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh 110 milioni kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa hospitali ya CCBRT Erwin Telemans, fedha hizo zimetolewa ili kusaidia matibabu kwa watoto wenye ugonjwa wa miguu pinde, hafla hiyo ilifanyika jana jijini Dar es Salaam.

 Afisa Mtendaji Mkuu wa hospitali ya CCBRT Erwin Telemans akifafanua jambo kwa wageni waalikwa wakati wa makabidhiano ya  hundi yenye thamani ya Sh 110 milioni kwa  hospitali ya CCBRT, fedha hizo zimetolewa ili kusaidia matibabu kwa watoto wenye ugonjwa wa miguu pinde, hafla hiyo ilifanyika  mapema leo jijini Dar es Salaam.



Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti na Mahusiano na Serikali wa Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Sylvia Balwire akihutubia wageni waalikwa wakati wa makabidhiano ya  hundi yenye thamani ya Sh 110 milioni kwa  hospitali ya CCBRT, fedha hizo zimetolewa ili kusaidia matibabu kwa watoto wenye ugonjwa wa miguu pinde, hafla hiyo ilifanyika  mapema leo jijini Dar es Salaam.



Mama mwenye mtoto  mwenye ugonjwa wa miguu pinde akizungumza na vyoombo vya habari mara baada ya makabidhiano ya  hundi yenye thamani ya Sh 110 milioni kwa  hospitali ya CCBRT, fedha hizo zimetolewa ili kusaidia matibabu kwa watoto wenye ugonjwa wa miguu pinde, hafla hiyo ilifanyika  mapema leo jijini Dar es Salaam.

JUMA NATURE, KHADIJA KOPA, NA TWANGA PEPETA WATUMBUIZA MKESHA WA MWENGE WA UHURU VIWANJA VYA BARAFU MANISPAA YA UBUNGO

June 02, 2017

Wasanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania akiwemo msanii mkongwe katika soko la muziki Juma Kasim maarufu kama Juma Nature, Msanii mkongwe wa Muziki wa taarabu Khadija Omar Abdallah Kopa maarufu kama Malkia wa Mipasho, Band ya Twanga Pepeta sambamba na wasanii wengine zaidi ya kumi wametumbuiza kwenye sherehe za Mkesha Wa Mwenge wa Uhuru 2017 zilizofanyika usiku wa kuamkia Leo Tarehe 1, Juni 2017 katika Viwanja Vya Barafu, Manispaaya Ubungo Jijini Dar es salaam.

Katika Sheree hizo zilizoratibiwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe Kisare Makori kwa ushirikiano Mkubwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo sambamba na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James Mkumbo wananchi waliitikia wito kwa kujitokeza kwa wingi Jambo ambalo limeimarisha umahiri wa Mwenge wa Uhuru ambao kwa mwaka huu una kauli mbiu isemayo Shiriki kukuza uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya nchi yetu.
Pamoja na kauli mbiu ya kutilia msisitizo kuhusu uchumi was viwanda pia Mwenge was Uhuru umebeba jumbe mbalimbali ikiwemo kupiga Vita Maambukizi mapya ya UKIMWI na Malaria sambamba na kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya.

Awali kabla ya mkesha wa Mwenge wa Uhuru katika Viwanja hivyo vya Barafu-Mburahati Mwenge huo ulizuru katika miradi mitano katika Manispaa hiyo Kama ifuatavyo;

1. Uzinduzi wa Jengo la Kituo Cha Huduma kwa wagonjwa wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) katika kituo Cha afya Mbezi. Jengo hilo limegharimu kiasi cha Tshs 125 milioni  ambazo zimetolewa na wafadhili ambao ni MDH (Management and Development for Health).

2. Kuweka Jiwe la Msingi wa Kituo Cha Polisi Cha Kati-Kata ya Kibamba ambapo wananchi wamekwisha changia jumla ya Tsh. 53,000,000/ = huku NSSF ikichangia Tsh. 50,000,000/= sawa na jumla ya Tsh. 103,000,000/=

3. Uzinduzi wa madarasa nane katika Shule ya Msingi Malambamawili Kata ya Msigani, Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es salaam. Jengo hilo lenye madarasa nane (8) yaliyozinduliwa yamejengwa kwa fedha kutoka Serikali kuu kwa  gharama ya Shilingi Milioni mia moja na thelethini na sita (Tshs 136,000,000/=)., madarasa hayo Yakikamilika shule itakuwa na vyumba vya madarasa 24.

4. Uzinduzi wa Mradi wa Mabasi SIMU 2000 Uliopo katika Kata ya Sinza. Kituo hicho kimejengwa kwa kutumia fedha zilizotokana na Mapato ya Ndani (Own Source)  Gharama yake ni Shilingi 2,376,647,991.89 chini ya Mkandarasi M/S DEL MONTE (T) LTD.

5. Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Zahanati ya Mburahati katika eneo la Mtaa wa NHC Kata ya Mburahati. Mradi huu wa ujenzi wa zahanati  ulianza kutekelezwa tangu Juni 2014 na kukamilika mnamo Oktoba 2016 chini ya Manispaa ya Ubungo, kwa gharama ya kiasi cha Tshs 84,000,000.00.
Tayari Mwenge wa Uhuru umekwisha ondoka Katika Mkoa wa Dar es sala ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo katika dhifa ya Makabidhiano iliyofanyika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J.K Nyerere Terminal 1 tayari kwa kuelekea Mafia Mkoani Pwani.

Imetolewa Na;
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ubungo

MAZISHI YA NDESAMBURO KUFANYIKA KWA SIKU MBILI MFULULIZO

June 02, 2017
Kikao cha Wanafamilia,Viongozi wa siasa na Viongozi wa Dini kikifanyika nyumbani kwa marehemu Ndesamburo kwa ajili ya maandalizi ya mazishi yake.
Ndugu na Baadhi ya watoto wa marehemu Philemoni Ndesamburo wakiwa katika kikao hicho.
Baadhi ya Viongozi wa Chadema wakishiriki katika kikao hicho.
Baadhi ya watoto wa marehemu Philemoni Ndesamburo.
Baadhi ya Wabunge wakishiriki katika kikao hicho.
Baadhi ya wanandugu wa familia ya marehemu Ndesamburo.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii ,Kanda ya Kaskazini

MAZISHI ya Mbunge mstaafu wa jmbo la Moshi mjini na Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro Philemon Ndesamburo Kiwelu (82) yanataraji kufanyika kwa siku mbili mfululilizo huku watu zaidi ya laki 2 wakitaraji kushiriki katika mazishi hayo.

Shughuli nzima za mazisihi zinataraji kufanyika June 5 na sita katika uwanja wa mashujaa mjini Moshi kabla ya kuhitimishwa siku ya Jumanne kwa ibada itakayoanzia kanisani na kumalizikia nyumbani kwa marehemu. 

Hatua ya maziko ya Ndesamburo kufanyika kwa siku mbili inatokana na uwepo wa idadi kubwa ya marafiki wa familia kushiriki katika maziko hayo ya kihistoria yatakayotanguliwa na kutoa heshima za mwisho ,shughuli zilizopangwa kufanyika katika uwanja wa mashujaa mjini Moshi.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa kikao kilichodumu kwa zaidi ya saa nne ,Msemaji wa Chadema katika maandalizi ya mazishi hayo Amani Golugwa amesema uamuzi huo unatokana na kutoa nafasi kwa watu mbalimbali kutoa heshima za mwisho kwa Ndesamburo.