TAARIFA KUTOKA SHIRIKISHO LA SOKA NCHINI TFF LEO

August 03, 2015
MALINZI AMSHUKURU TENGA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi amemshukuru Rais wa CECAFA, Leodgar Tenga kwa kuipa Tanzania uenyeji wa mashindano ya Vilabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup) iliyomalizika jana kwa klabu ya Azam FC kutawazwa Mabingwa wapya wa michuano hiyo.

Aidha Malinzi ameishukuru Kamati ya Ndani ya Uendeshaji ya Michuano hiyo (LOC) kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kuandaa na kuhakikisha michuano hiyo inafanyika na kumalizika katika hali ya usalama na amani.

Malinzi pia amewapongeza wapenzi, washabiki na wadau wa soka nchini waliojitokeza kushuhudia michezo ya michuano hiyo na kuonyesha nidhamu ya hali ya juu ndani nan je ya uwanja kipindi chote cha michuano.

Rais Malinzi ameipongeza klabu ya Azam FC kwa kutwaa Ubingwa Kagame, kwa kutwaa ubingwa huo imeweza kuweka historia ya kutwaa Ubingwa huo kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake na pia kuwa klabu iliyocheza michuano hiyo na kuwa Bingwa bila kuruhusu nyavu zake kutikisika.

Pia Malinzi amewashukuru waandishi wa habari/vyombo vya habari kwa sapoti yao wakati wa michuano hiyo. Shukrani hizo pia zimepelekwa kwa klabu za Yanga SC, KMKM kwa kushiriki mashindano hayo.

U-15 YAREJEA KUTOKA ZANZIBAR
Kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U-15), kimerejea leo asubuhi kutokea kisiwani Zanzibar kilipokwenda kucheza michezo ya kujipima nguvu na kombani ya U-15 ya kisiwani humo.

Katika michezo miwili iliyocheza kisiwani humo, iliweza kushinda michezo yote miwili, (4-0 ), (1-0), huku kocha Bakari Shime akiwapongeza vijana wake na kusema wanaendelea kuimarika kuelekea kujiandaa  na kuwania kufuzu kwa fianali za Mataifa Afrika chini ya miaka 17 mwakani.

Baada ya kurejea jijini Dar es salaam leo, kambi ya timu hiyo imevunjwa na vijana hao watakutana tena mwisho wa mwezi wa Agosti kama ilivyo katika program yao ya kukutana kila mwisho wa mwezi na kucheza michezo ya kirafiki.

Mwishoni mwa mwezi Agosti timu hiyo ya vijana inatarajiwa kuelekea mkoani Tanga kucheza michezo ya kirafiki na kombani ya mkoani humo, ambapo kocha wake Shime pia anatumia nafasi hiyo kutazama wachezaji wengine wenye uwezo mzuri katika timu za kombaini za mikoa kwa ajli ya kuwaongeza katika kikosi chake.

Mpaka sasa timu hiyo ya vijana chini ya miaka 15 (U15) imeshafanya ziara na kucheza michezo katika miji ya Mbeya na kisiwani Zanzibar.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


-
Best Regards,
 
Baraka Kizuguto
MEDIA & COMMUNICATION OFFICER
Tanzania Football Federation - TFF
A:I P.O.BOX 1574 Karume Memorial Stadium /Shaurimoyo/Uhuru Street I Dar es salaam I Tanzania 
WAKRISTO WA ITALIA WAWEZESHA ZAHANATI YA KISASA VIKAWE

WAKRISTO WA ITALIA WAWEZESHA ZAHANATI YA KISASA VIKAWE

August 03, 2015
IMG_0282
Mkuu wa Masista Waabuduo Damu ya Kristo, Euprasia Julius akimtambulisha mgeni rasmi na meza kuu kwa wageni waalikwa na wanakijiji wa Vikawe (hawapo pichani) katika hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa Maria De Mathias (MDM) Vikawe, Kibaha.
Na Mwandishi wetu, Kibaha
MGANGA Mkuu wa halmashauri ya Mji Kibaha, Dk. Happniness Ndosi amepongeza shirika la masisita wa Waabuduo Damu ya Kristo kwa kufanikisha ujenzi wa zahanati ya kisasa katika kijiji cha Vikawe wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Mganga huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa zahanati hiyo,pamoja na kuwapongeza amesema serikali itaendelea kushirikiana na mashirika yote kwa lengo la kuwezesha kila kijiji kiwe na zahanati na kila kata kituo na kila wilaya kuwa na hospitali.
Aliwapongeza masista hao kwa kuonesha upendo na huruma kama Biblia inavyomsimulia msamaria mwema ambaye alikuta mtu aliyepigwa na majambazi na kumsaidia.
Aliahidi ushirikiano wa serikali katika kufanikisha usajili wa zahanati hiyo na kuendelea kuisaidia hatua kwa hatua hadi inakuwa kituo mpaka watakapofanikisha safari yao ya kuwa hospitali kubwa ya kisasa.
Mganga huyo pamoja na kutoa ahadi hiyo aliwataka wananchi wa Vikawe kutumia huduma hiyo na kwamba zahanati hiyo itakapohitaji msaada wa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) wataletewa kuchukua mgonjwa na kumfikisha panapohusika.
Zahanati hiyo ya DA.MA Africa imejengwa kwa ufadhili wa wakristo wa Italia chini ya usimamizi wa Muitalia, Germano Frioni.
Akitoa salamu zake Muitalia huyo amesema kwamba anawashukuru wakazi wa Vikawe kwa kumpa nguvu ya kusonga mbele hasa kwa kutambua kwamba yeye na marafiki zake wamefanyakazi usiku na mchana kutafuta fedha kwa ajili ya kusaidia marafiki wa Afrika.
Alisema atajitahidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha changamoto za zahanati hiyo zinafanyiwa kazi.
Aliwaomba wananchi wa Tanzania kuendelea kumuombea yeye na wenzake kama Papa Francis anavyoagiza ili malengo ya safari ya kuwapo duniani yafanikiwe.
Alisema kwamba watoto wake Daniel na Marco (kwa sasa wote ni marehemu) ambao ndio kifupi cha zahanati hiyo DA.MA wamemfanya kujitambua na kusaidia wengine katika kuonesha upendo.
Aidha alisema kwamba ataendelea kukumbuka Vikawe kwani alifika mara ya kwanza mwaka 2005 na kuona hali ilivyokuwa ambapo sasa lipo jengo la zahanati hiyo likiwa limekamilika.
Wazo la ujenzi wa zahanati hiyo , lilitolewa na wananchi wa Vikawe kwa Masisita Waabuduo Damu ya Kristo mwaka 2004 wakati wakiwa katika eneo hilo baada ya kununua ekari 40 kwa ajili ya kilimo mwaka 1994.
Alisema pamoja na maombi hayo na wao wenyewe kutambua kwamba kuna mahitaji makubwa ya huduma ya afya japokuwa kuna zahanati ya serikali, hawakuweza kutekeleza maombi ya wanavijiji hadi mwaka 2011 walipofanikiwa kupata ufadhili kutoka Italia na kuanza ujenzi mwaka 2013.
Katika risala yao walisema kwa ushirikiano kati yao na wafadhili hao wamefanikiwa kuwapo kwa zahanati hiyo yenye mahitaji yote ya msingi kwa mujibu wa taratibu za serikali na kuzidi.
Msoma risala alisema kwamba wataendelea kupanua miundombinu mpaka zahanati hiyo ifikie ngazi ya cha afya na baadae hospitali.
Pamoja na ujenzi wa zahanati hiyo ya kisasa masisita hao wameanzisha shule ya awali kuwaandaa wanafunzi wa darasa la kwanza.
Wamesema kwamba wanaamini kwamba wataendelea kushirikiana na wananchi na wadau wengine wa afya katika kuimarisha huduma za hospitali hiyo.
Zahanati hiyo pamoja na vifaa tiba pia ina raslimali ya visima vya maji ya mvua ujazo zenye ujazo wa lita laki moja na kingine lita 49 elfu, wanatumia umeme wa sola na jenereta .
Walisema kwamba wanachangamoto ya kukosa umeme wa Tanesco, barabara nzuri na nyumba za wafanyakazi.
IMG_0289
Mwenyekiti wa kijiji cha Vikawe, Kibaha, Shabaan Mgini akiwasalimia wageni waalikwa wakati wa utambulisho.
IMG_0301
Sr. Theresia Rogatus akisoma risala katika hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa DMD iliyopo Vikawe, Kibaha.
IMG_0323
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa -DMD kijiji cha Vikawe, Kibaha. Kutoka kushoto ni Mdau wa Zahanati hiyo, Dr. Zuberi Mzige wa Hospitali ya Mwananyamala,
IMG_0335
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akimpa mkono wa shukrani Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Raia wa Italia, Germano Frioni kwa ujenzi wa Zahanati hiyo itakayohudumia wakazi wa kijiji cha Vikawe, Kibaha.
IMG_0341
Masista Waabuduo Damu ya Kristo wakielekea meza kuu kwa mwendo wa madaha huku wakiwa wamebeba zawadi kwa ajili ya kumkabidhi mgeni rasmi na wafadhili waliojitolea kujenga Zahanati hiyo.
IMG_0348
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi (kulia) akimkabidhi zawadi Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Raia wa Italia, Germano Frioni. Anaye shuhudia tukio hilo ni Baba Paroko wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeri Bunju...
IMG_0351
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akikabidhi zawadi kwa wadau waliombatana na Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Muitalia, Germano Frioni.
IMG_0354
IMG_0194
Mganga Mkuu wa halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dr. Happniness Ndosi (wa pili kulia) pamoja na Mfadhili wa ujenzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa ya kijiji cha Vikawe, Kibaha, Muitalia, Germano Frioni wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Zahanati hiyo inayosimamiwa na Masista Waabuduo Damu ya Kristo nchini.
IMG_0230
Muonekano wa ndani ya Zahanati ya Da. Ma Africa-DMD iliyop Vikawe, Kibaha mkoa wa Pwani.
IMG_0211
Mganga Mkuu wa halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dr. Happniness Ndosi akiangalia chumba cha dawa katika Zahanati hiyo mara baada ya kuzinduliwa.
IMG_0235
Wageni waalikwa wakijadiliana jambo mara baada ya kufungiliwa rasmi Zahanati hiyo nje ya moja ya chumba cha upasuaji mdogo.
IMG_0128
Baba Paroko wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeri Bunju akiendesha ibada takatifu ya misa maalum kabla ya ufunguzi rasmi wa Zahanati hiyo.
IMG_9973
IMG_0089
Wanakijiji wa Vikawe wakishiriki ibada maalum wakati wa uzinduzi wa Zahanati ya Da. Ma Africa.
IMG_0126
IMG_0086
IMG_0265
Kwaya ikitoa burudani.
IMG_0017
Wageni waalikwa na wanakijiji wakishiriki kuimba pamoja na kwaya.
IMG_0102
Pichani juu na chini ni baadhi ya wanakijiji na wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
IMG_0140
Umati wa wageni waalikwa na wanakijiji wa Vikawe.
IMG_0361
Mgeni rasmi Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi katika picha ya pamoja na wadau pamoja na wafadhili waliojenga Zahanati hiyo.
IMG_9898
Masista Waabuduo Damu ya Kristo wakifurahia taswira za picha za mnato kutoka kwenye kamera.
IMG_0224
Jenereta la Zahanati ya Da.Ma Africa linalotumika kutoa umeme katika Zahanati hiyo.
IMG_9881
Muonekano wa nje wa jengo la Zahanati ya Da.Ma Africa kabla ya kuzinduliwa rasmi.
IMG_0247
Wanakijiji wa Vikawe na wageni waalikwa wakiingia kukagua Zahanati hiyo mara baada ya kuzinduliwa.
MMLIKI WA ST. MATHEW AIHAMISHA MAHAKAMA KWA GHARAMA ZAKE

MMLIKI WA ST. MATHEW AIHAMISHA MAHAKAMA KWA GHARAMA ZAKE

August 03, 2015
court_gavel
Na Mwandishi Wetu, Singida
MDAI katika Kesi ya madai ya talaka Magreth Mwangu dhidi ya Mkurugenzi wa Shule ya St. Mathew, Thadei Mtembei amehoji uhalali wa mahakama kufikia kukagua mali zake siku ya Jumamosi bila kupitia mahakama yoyote hapa Singida.
Kesi hiyo ambayo inasikilizwa mahakama ya Mwanzo Kizuiani Mbagala Jijini Dar es Salaam, juzi (Jumamosi) ililazimika kuhamia mkoani Singida baada ya mdaiwa (Thadei Mtembei) kuitaka mahakama kuhamia mkoani Singida kwa gharama zake ili kuhakiki nyumba ambazo alidai alimjengea Mwangu.
Mtembei katika hoja yake ya kuitaka mahakama kuhamia Singida alisema yuko tayari kulipa gharama zote ikiwemo nauli na posho.
Hakimu anayesikiliza kesi hiyo Rajab Tamaambele, na wakili wa Mtembei ambaye ni mtoto wa mke mkubwa wa Mtembei (Peter Mtembei), karani na kesi na mtumishi wa mahakama ni miongoni mwa watu waliofika kwa ajili ya ukaguzi na uhakiki wa nyumba hizo.
Hata hivyo hakukuwepo na wazee wa baraza jmbo ambalo mwangu pia alililalamikia. Mwangu alidai kuwa licha ya kuwa hafahamu sheria kutokana na kutokuwa na elimu hata ya Sekondari lakini kitendo cha mahakama kufika Jumamosi kwa ajili ya kufanya uhakiki na ukaguzi haioni kama ni ha haki na pia kulikuwa hakuna afisa ustawi wa jamii.
Alidai hakimu kuongozana na wakili wa kesi hiyo na kuwa pamoja muda wote haoni kama atatendewa haki katika shauri hilo.
“Mimi nahoji ushirikiano huu kama utanitendea haki kwani watu wametoka pamoja Dar es Salaam wameongozana kwenye magari binafsi nafika eneo la tukio nakuta msafara wa hakimu, wakili wa mdaiwa, mwenyekiti wa kitongoji ukiwa umeshafika mbele ya nyumba ambayo walitaka kuanza kuihakiki” alidai.
Alidai hata Mwenyekiti wa Mtaa wa Sabasaba, Mahamoud alisema hajapewa taarifa yoyote ya maandishi kwani alishtukizwa na kupelekwa kwenye nyumba hiyo ambayo alisema hafahamu kama ni ya Mwangu.
Pia alihoji uhalali wa mtoto wa Mtembei ambaye ni wakili kusimamia shauri hilo katika mahakama ya Mwanzo huku mara kadhaa akimtolea maneno ya kashfa kama ni mfunga vidonda tu hawezi kujenga nyumba.
Mwangu alisema alishawahi kuiambia mahakama kuwa nyumba zake za Singida alizijenga na aliamua kuziuza kwa ajili ya elimu ya watoto wake ambao walitelekezwa na baba yao lakini cha kushangaza mahakama kwa amri ya Mtembei ikataka kufika Singida kuhakiki nyumba zake.
Hata hivyo mahakama ilikagua nyumba tatu ambapo moja ilikuwa imeshauzwa kwa Sh. Milioni 15 na nyingine iliuzwa ikiwa katika hatua ya msingi.
Baada ya kumalizika kwa uhakiki huo hakimu Tamaambele alimtaka Mwangu kuhakikisha anawasilisha mahakamani nyaraka zote za nyumba na kuwapeleka watoto mahakamani kabla ya kesi hiyo kutolewa hukumu Agosti 25, mwaka huu.
MTOTO WA MAMA NTILIE JUMAA AWESO ASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA NDANI CCM PANGANI

MTOTO WA MAMA NTILIE JUMAA AWESO ASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA NDANI CCM PANGANI

August 03, 2015
aweso
Ndugu Jumaa Aweso.
Na Mohammed Hammie, Pangani, Tanga
Mtoto wa mama ntilie mwenye uzao halisi kutoka wilayani Pangani mkoani Tanga, Ndugu Jumaa Aweso (pichani) ameibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa ndani wa chama cha mapinduzi CCM.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo katibu wa CCM wilayani Pangani Bi Zaina Mlawa amesema kuwa, katika uchaguzi huo uliowashirikisha wagombea wapatao kumi na moja, Ndugu Aweso amekuwa wa kwanza miongoni mwa wagombea hao.
Uchaguzi huo uliokuwa na ushindani wa aina yake kutokana na kuwepo kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Ndugu Salehe Pamba, uliwashirikisha wapiga kura wapatao 10376 wa chama cha mapunduzi.
Awali wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Bi Zania aliwataja wagombea hao kwa idadi ya kura walizopata na kusema kuwa "Ndugu Wahi Ibrahim amepata kura 87, ndugu Rosemary Luanda amepata kura 89, ndugu Elizabeth Alatanga amepataa kura 158, Halima Kimbau amepata kura 222, Ndugu Mohammed Rished amepata kura 442, Ndugu Ayubu Mswahili amepata kura 565"
Bi Zania ameongeza kwa kusema kuwa "Ndugu Omary Mwidadi amepata kura 587, ndugu Omary Chambega amepata kura 720, ndugu Salehe Pamba amepata kura 1567, ndugu Abdurahmani magati amepata 1956, na ndugu Jumaa Aweso 3983"
Ushindi huo kwa ndugu Jumaa Aweso unampa nafasi ya kuwa mgombea wa kwanza katika kuipeperusha bendera ya chama cha mapinduzi CCM wilayani Pangani endapo kamati kuu ya maamuzi itaridhia.
Mpaka sasa katika jimbo la Pangani kumepatikana wagombea wawili ambao wanaonekana kupendwa sana na wanancho ambao ni Amina Mwidau wa CUF pamoja na JUmaa Aweso wa CCM ambapo kwa mujibu wa wachambuzi wa masuala ya siasa, endapo watakutana katika nafasi ya ubunge upinzani utakuwa wa aina yake.