Simba na Mgambo kupambana leo uwanja wa Taifa kuwania pointi tatu.
Kikosi cha timu ya Mgambo Shooting ambacho kitapambana na Simba katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam.
KOCHA Mkuu wa timu ya Mgambo Shooting ya Tanga,Mohamed Kampira amesema timu yao imapania kupata matokeo mazuri katika mechi yao ya Ligi kuu Tanzania Bara dhidi yao na Simba itakayochezwa leo saa kumi jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kampira alisema kikosi ambacho kitashuka kwenye dimba hilo hii leo kitakuwa chenye upinzani mkubwa kutokana na maandalizi ambayo wameyafanya kuelekea mechi hiyo .
Alisema licha ya kujiandaa kwa mechi hiyo lakini pia wao wamejiandaa katika mechi zao zilizosalia ili kuhakikisha wanachukua pointi tatu muhimu kwani lengo lao ni kumaliza ligi hiyo wakiwa kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo.
Blog hii inaitakia kilala heri Mgambo shooting kwenye mechi hiyo ili iweza kufanya vizuri kwani tunaamini uwezo wanao na nia pia wanayo hivyo wachezaji wahakikisha wanacheza kwa umakini mkubwa sana.
Mwisho.
Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam.
KOCHA Mkuu wa timu ya Mgambo Shooting ya Tanga,Mohamed Kampira amesema timu yao imapania kupata matokeo mazuri katika mechi yao ya Ligi kuu Tanzania Bara dhidi yao na Simba itakayochezwa leo saa kumi jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kampira alisema kikosi ambacho kitashuka kwenye dimba hilo hii leo kitakuwa chenye upinzani mkubwa kutokana na maandalizi ambayo wameyafanya kuelekea mechi hiyo .
Alisema licha ya kujiandaa kwa mechi hiyo lakini pia wao wamejiandaa katika mechi zao zilizosalia ili kuhakikisha wanachukua pointi tatu muhimu kwani lengo lao ni kumaliza ligi hiyo wakiwa kwenye nafasi nzuri kwenye msimamo.
Blog hii inaitakia kilala heri Mgambo shooting kwenye mechi hiyo ili iweza kufanya vizuri kwani tunaamini uwezo wanao na nia pia wanayo hivyo wachezaji wahakikisha wanacheza kwa umakini mkubwa sana.
Mwisho.
African Sports mabingwa wa soka Tanga.
Na Mwandishi Wetu,Tanga.
Akizungumza mara baada ya kumalizika mchezo huo,Kocha Mkuu wa timu ya African Sports "Wanakimanumanu"Edmund Nyoni alisema wanamshukuru mungu kwa kuweza kuwa mabingwa na kuhaidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyopo kwenye kikosi chake kabla ya kuanza mashindano ya mabingwa wa mikoa.
TIMU ya African Sports
"Wanakimanumanu" mwishoni iliweza kufanikiwa kuwa
mabingwa wa wapya wa mkoa wa Tanga baada ya kuibamiza Makorora Star mabao 5-0
ikiwa ni ligi ya mkoa wa Tanga mchezo uliochezwa uwanja wa soka
Mkwakwani.
Licha ya African Sports kuwa mabingwa lakini bado wamesalia na
michezo michache kwenye ligi hiyo kutokana na kuwa na wingi wa pointi ambazo
haziwezi kufikiwa na timu yoyote kwenye ligi hiyo ambapo mpaka sasa wamekwisha
kujikusanyia pointi 54.
Furaha ya wanakimanumanu hao ilianza baada ya mchezaji wao
James Mendy kupachika bao katika dakika ya 5 ambaye alitumia uzembe wa mabeki wa
makorora waliokuwa wamezubaa langoni mwao wakishindwa kujua nini cha
kufanya.
Bao hilo lilidumu mpaka timu zote zinakwenda mapumziko ambapo
kipindi cha pili kilianza kwa kasi kutokana na kila timu kuonekana kujipanga kwa
ngwe hiyo ya mwisho kwa kufanya mashambulizi kwa zamu langoni mwa timu
pinzani.
Wakionekana kujipanga na kupanga mashambulizi langoni mwa
Makorora Star,African Sports waliweza kucheza kwa umakini na kucheza pasi
fupifupi na ndefu na kuweza kukitawala kipindi hicho na kupelekea kuandika bao
la pili dakika ya 47 kupitia Thabiti Mgoha ambaye alimalizia kazi iliyofanywa na
Pera Ramadhani.
Baada ya kuingia mabao hayo langoni mwa Makorora Star nao
waliweza kucharuka na kucheza kwa umakini huku wakifanya mashambulizi ya
kushtukiza lakini mlinda mlango wa African Sports Omari Jengo aliweza kupanchi
mashuti yaliyokuwa yakielekezwa kwenye lango lao.
Wakiendeleza wimbi la
mashambulizi ,African Sports waliweza kuongeza mabao mengine mawili kupitia
dakika za 67 likifungwa na Shekue Salehe na bao la nne likifungwa na Mohamed
Issa kwenye dakika ya 75 ambapo zilipoingia bao hizo ziliwafanya wapinzani wao
kukata tamaa mapema na kucheza ilimradi mchezo umalizike.
Katika dakika ya 88 ya mchezo huo mchezaji Gidatu Akudae
aliweza kuwainua mashabiki wa timu hiyo baada ya kuhitimisha karamu ya mabao
langoni mwa Makorora kwa kupachika bao la tano ambapo alitumia uzembe wa mlinda
mlango wa timu hiyo,Ally Salim kufunga bao hilo.
Akizungumza mara baada ya kumalizika mchezo huo,Kocha Mkuu wa timu ya African Sports "Wanakimanumanu"Edmund Nyoni alisema wanamshukuru mungu kwa kuweza kuwa mabingwa na kuhaidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyopo kwenye kikosi chake kabla ya kuanza mashindano ya mabingwa wa mikoa.
Mwisho.
MIKOA YATAKIWA KUCHEZESHA COPA COCA-COLA WILAYANI
Na Boniface Wambura,Dar es Salaam.
Vyama vya Mpira wa Miguu vya mikoa vinatakiwa kuendelea
na mashindano ya Copa Coca-Cola yanayoshirikisha watoto wenye umri chini ya
miaka 15 katika ngazi ya wilaya wakati vikisubiriwa vifaa na fedha za uendeshaji
kutoka kwa mdhamini.
Kwa mujibu wa kalenda ya mashindano (roadmap),
mashindano ya Copa Coca-Cola ngazi ya wilaya yanatakiwa kufanyika na kukamilika
ndani ya mwezi Mei mwaka huu ili baadaye kuendelea na hatua inayofuata.
Hivyo, Shirikisho la
Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawataka wanachama wake (vyama vya mpira wa
miguu vya mikoa) ambao wamejipanga kuendelea na mashindano wakati suala la vifaa
na fedha likiendelea kufuatiliwa kwa mdhamini wa mashindano.
Vifaa na fedha zitapatikana wakati wowote baada ya
taratibu husika kukamilika. Vifaa kwa ajili ya mashindano hayo vimeagizwa kutoka
nje ya Tanzania.
Ni matumaini yetu kuwa tutakuwa na mashindano mazuri
mwaka huu kulinganisha na msimu uliopita. Kampuni ya Coca Cola ilianza kudhamini
mashindano hayo mwaka 2007, na tangu mwaka huo yamekuwa yakifanyika kila
mwaka.
Mwisho.
Subscribe to:
Posts (Atom)