Wasanii watembelea Duka la Tigo mjini Mtwara

November 11, 2017
Wasanii Stamina na Chege wakiwa na mtoa huduma ya mauzo wa duka la Tigo Mtwara, Farida Salum wakiangalia simu zinazouzwa, mara baada ya wasanii wa Tigo Fiesta walipotembelea duka hilo leo.
Wafanyakazi wa duka la Tigo mjini Mtwara wakipiga picha ya pamoja na msanii Janjaroo.
Wateja wakipata huduma leo.
Mashabiki wa muziki wa bongo fleva wakishuhudia wasanii waliotembelea duka la Tigo mtaa wa stand kuu mjini Mtwara.

WANAFUNZI 250 WAPATA MAFUNZO YA GIRL GUIDES TEMEKE

November 11, 2017
 Baadhi ya  Girl Guides ambao ni wanafunzi kutoka Shule mbalimbali za Manispaa ya Temeke wakionesha moja ya alama muhimu za Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA), baada ya kupata mafunzo ya awali  katika Shule ya Msingi Mbagala, Dar es Salaam leo. Wanafunzi wa kike 250 walishiriki mafunzo hayo yaliyoendeshwa na Kamishna wa TGGA Mkoa wa Temeke,  Leonida Komba ( wa tatu kushoto waliosimama)

Girl Guides hao walipata mafunzo kuhusu historia ya Girl Guides duniani, kanuni, malengo na madhumuni ya kuanzishwa kwake.

Pia hufundishwa ujasiri, ukakamavu, mambo ya uongozi, maadili, kujitolea pamoja na uzalendo.
(PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Kamishna wa TGGA Mkoa wa Temeke, Leonida Komba (kushoto) akiwahamasisha Girl Guides wakati wa mafunzo hayo




 Girl Guides wakiwa na furaha baada ya kupata mafunzo ya chama hicho kuhusu kanuni, historia ya Girl Guides Duniani, malengo na madhumuni yake.
Kamishna wa TGGA Mkoa wa Temeke, Leonida Komba (wa pili kulia waliosimama) akiwa na walimu ambao ni walezi wa Girl Guides wa shule walikotoka wanafunzi hao.
RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AREJEA NCHINI MARA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE NCHINI UGANDA

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AREJEA NCHINI MARA BAADA YA KUMALIZA ZIARA YAKE NCHINI UGANDA

November 11, 2017

1
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipita kwenye gwaride la Kimya lililoandaliwa kwa heshma na Jeshi la Uganda mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tatu nchini Uganda na kurejea nchini.
3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakifurahia ngoma ya asili iliyokuwa ikipigwa na watoto wa nchini Uganda katika eneo la mpakani la Mutukula kabla ya kurejea nchini.
4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa mpakani Mutukula upande wa Tanzania mara baada ya kuwasili akitokea Uganda.
5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mpakani mwa Tanzania na Uganda (Mutukula) kuhusu  ujenzi wa barabara ya Kutoka Miziro hadi Mutukula bila kupitia wilayani Misenyi. Pembeni yake ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akisikiliza.
8
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na viongozi wakuu wa Majeshi ya Uganda mara baada ya kumaliza ziara yake nchini Uganda.
10
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wananchi wa mpakani  Mutukula upande wa Uganda mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku tau nchini Uganda.
PICHA NA IKULU

MAHAFALI YA TISA YA KIDATO CHA NNE KOM SEKONDARI 2017 YAFANA

November 11, 2017
Shule ya Sekondari Kom iliyopo mjini Shinyanga leo Jumamosi Novemba 11,2017 imefanya mahafali ya 9 ya kidato cha nne tangu kuanzishwa kwa shule hiyo mwaka 2006.

Alpha Abdul ashinda kinyang'anyiro cha Tigo Fiesta Supa Nyota 2017 Mtwara

November 11, 2017

Mshindi wa Tigo Fiesta Supa Nyota toka mkoa Mtwara, Alpha Abdul akionesha umahiri wake wa kufokafoka kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka mshindi wa shindano hilo la kusaka vipaji leo.
Tano bora walioingia kwenye mchujo wa Tigo Fiesta Supa Nyota 2017 mkoani Mtwara.

MHANDISI MTIGUMWE ATOA MWEZI MMOJA KWA MRATIBU OFISI YA UKAGUZI KANDA YA KASKAZINI KUBAINI WALA RUSHWA

November 11, 2017
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew John Mtigumwe (Kushoto) akisalimiana na Mratibu wa Ofisi ya Ukaguzi Kanda ya Kaskazini Ndg Juma Mwinyimkuu mara baada ya kuwasili kwa ziara ya kikazi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew John Mtigumwe akizungumza na wafanyakazi wa Ofisi ya Ukaguzi Kanda ya Kaskazini mara baada ya kuwasili kwa ziara ya kikazi.

Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala wa Wizara ya Kilimo Bi Hilda Kinanga akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ofisi ya Ukaguzi Kanda ya Kaskazini kwa ziara ya kikazi.

Baadhi ya wafanyakazi Ofisi ya Ukaguzi Kanda ya Kaskazini-Arusha wakifatilia kikao cha kazi kilichoongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew John Mtigumwe.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew John Mtigumwe akisisitiza jambo kwa njia ya simu kwa watumishi waliopo Mjini Dodoma kuongeza ufanisi katika kazi.

YALIYOSEMWA NA DK. HASSAN ABBAS KATIKA KIPINDI CHA VIJANA TZ JUU YA MAFANIKIO /UTENDAJI WA SERIKALI NA CHANGAMOTO KATIKA TASNIA YA HABARI

November 11, 2017
"Ofisi yangu ina jukumu la kutoa taarifa sahihi na kwa wakati ya Serikali; Kusajili na kufungua Magazeti; Kusaidia Watu wa mifumo mingine ya Serikali kusema" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Uhuru wa vyombo vya habari upo wa kutosha. Serikali imeruhusu uhuru wa Vyombo vya habari. Kuna Redio zaidi ya 150, tuna redio zaidi ya 30, kuna Magazeti zaidi ya 110 yanayotoka nchini" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Serikali ina simamia Wananchi wapate habari sahihi na si kulishwa habari mbovu. Serikali tunalisimamia hili" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Changamoto iliyopo ni kuhakikisha habari zsahihi zinawafikia Watu wote kwa wakati" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Rais @MagufuliJP amefanikiwa sana kuleta mageuzi ya kifikra. Kujenga hari ya Uzalendo, nidhamu, uwajibikaji kwa Watu wake wakiwemo Watumishi wa Umma na Wananchi" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Rais @MagufuliJP ameleta nidhamu kubwa ya matumizi ya fedha za umma. Mathalani amefanikiwa kudhibiti safari za nje zisizo na tija" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Hapo nyuma zilitumika bilioni zaidi ya 200 kwa safari tu wakati hivi sasa zimetumika bilioni 25 tu kwa safari tumeokoa pesa nyingi"@TZ_MsemajiMkuu
"Rais @MagufuliJP ameleta mageuzi ya kudhibiti Wafanyakazi hewa zaidi ya 20,000 na kuokoa zaidi ya Tsh. Bilioni 238. Ni mageuzi makubwa" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Tumeondoa wafanyakazi hewa takribani elfu 20 kwa zoezi hilo tumeokoa bilioni 238" @TZ_MsemajiMkuu
"Hawa wanaopiga kelele juu ya mageuzi ya rasilimali za madini. Ipo siku watanyamaza wakiona manufaa ya wazi. Serikali ya @MagufuliJP imeonyesha uzalendo kwenye madini" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Zipo nchi kubwa duniani awapati 50/50 kwenye Madini sisi tumeweza @TZ_MsemajiMkuu
"Serikali itaendelea kuhakikisha kila kilicho chetu tunakipata"@TZ_MsemajiMkuu
"Kwenye vyeti feki Serikali ya Rais @MagufuliJP imeokoa zaidi ya Tsh. Bilioni 148 ambazo zinaenda kwenye shughuli za kimaendeleo." - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Sekta ya habari ni sekta nyeti na Sheria hii ya habari tuliyo nayo sasa imeleta maboresho na ubora kwenye sekta ya habari nchini" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Huwezi kutoa habari kwa kuingilia faragha ya mtu" @TZ_MsemajiMkuu
"Huwezi ukakiacha kituo cha radio kinawachochea wakulima wakawaue wafugaji arafu ukasema wana haki ya habari "@TZ_MsemajiMkuu
"Sheria mpya ya huduma ya habari vimeweka ustawi wa vyombo vya habari na si kweli ipo kwa ajili ya kufungia habari." - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Popote duniani hakuna nchi yenye sheria inayosema andika chochote" @TZ_MsemajiMkuu
"Hakuna nchi yeyote Duniani inayotoa Uhuru kwa vyombo vyao vya habari kuwa na uhuru wa kuandika chochote kile wanachojisikia" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Uandishi wa habari ni taaluma sasa ukikiuka sisi kama serikali hatuwezi kukuacha"@TZ_MsemajiMkuu
"Sisi tunailea sekta yote ya habari"@TZ_MsemajiMkuu
"Wananchi wapuuze habari kuwa Serikali inafungia vyombo vya habari inapojisikia bali ina zingatia sheria" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Chombo cha habari kinatakiwa kifuate miiko"@TZ_MsemajiMkuu
"Vijana waamue kufanya kazi, wawe Wazalendo, wamwogope Mungu. Safari ya Mabadiliko ni ngumu lakini inahitaji uvumilivu" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Watanzania wamuunge mkono Rais @MagufuliJP atimize utekelezaji wa ilani ya uchaguzi" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Mwakani 2018 mwezi Julai Serikali italeta ndege kubwa ya kisasa itakayokuwa inakwenda popote pale Duniani" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
Mheshimiwa Rais @MagufuliJP alikuta mikopo inatolewa kiasi cha bilioni 48 kwa mwaka Lakini sasa hivi tumefikia bilioni 472 @TZ_MsemajiMkuu
"Fedha zipo na watapata kila mwanafunzi mwenye haki ya kupata"@TZ_MsemajiMkuu
"Serikali ya Rais @MagufuliJP inatoa Tsh. Bilioni zaidi ya 400 kwa Wanafunzi. Kwa mara ya kwanza fedha imetangulia vyuoni kabla ya Wanafunzi kuanza masomo" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Serikali imeboresha makusanyo kutoka Tsh. Trilioni 9.9 mpaka Tsh. Trilioni 14 kwa mwaka" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
Mheshimiwa @MagufuliJP alipoingia madarakani tulikuwa tunakusanya kodi kwa kiasi cha "Trilioni 9.9.Leo hii tunakusanya trilioni 14 kwa mwaka haya ni mafanikio makubwa"@TZ_MsemajiMkuu
"Serikali imeleta miradi ya kihistoria nchini ya kuzalisha umeme kupitia miradi ya Kinyerezi 1 & 2" - Dk. H.A @TZ_MsemajiMkuu
"Hivi tunapozungumza kuna watu hawalali kuna watu wanajenga reli Usiku na mchana"@TZ_MsemajiMkuu
Dk. Hassan Abbas ni Mkurugenzi Mkuu Idara ya Habari na Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali aliyasema hayo katika kipindi cha VijanaTz kilichorushwa Mubashara siku ya Ijumaa Novemba 10, 2017 kupitia mitandao ya kijamii ya UVCCM ya Twitter, Facebook na Instagram
IMEANDALIWA NA;
Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi
UVCCM Taifa