HAIJAWAHI KUTOKEA: MAZISHI YA BILIONEA WA MAPENZI GARINI BUKOBA HISTORIA!
Msafara
wa magari kuelekea kwenye mazishi. Tukio hilo la mazishi lilijiri
Jumamosi iliyopita katika Kijiji cha Kyaikailabwa, nje kidogo ya mji wa
Bukoba ambapo siku hiyo, shughuli zote zilisimama kwa siku nzima kupisha
tukio hilo lililogusa hisia za watu wengi.
ACHANA
na mazingira ya kifo cha Bilionea maarufu wa Bukoba, Leonard Mtensa
aliyefariki saa chache baada ya kufanya mapenzi ndani ya gari kuacha
gumzo, gumzo lingine lilitokea wakati wa mazishi yake ambayo
yalihudhuriwa na wananchi wengi kutoka ndani na nje ya mkoa, mkanda
kamili huu hapa.
Kwa mujibu wa chanzo kilichoshuhudia mazishi hayo mwanzo mwisho,
msiba huo ulikuwa wa pekee kwani haijawahi kutokea kwa yeyote kuzikwa na
umati mkubwa kiasi hicho na kusababisha watu wote wasimame kiasi cha
kuwafanya askari wa usalama barabarani kufanya kazi ya ziada kuhakikisha
mambo yanakwenda sawa.
Wananchi
wakiwa barabarani kushuhudia msafara huo ukipita. “Msafara ulianzia
mochwari ya Hospitali ya Bukoba, ukapita katika klabu yake ya Lina’s
kisha ukapitia mtaa wa Jamhuri lilipo Soko Kuu la Bukoba kisha kuelekea
kijiji cha Kyaikailabwa.
“Ilikuwa si mchezo, hii ni historia kwa Bukoba. Haijawahi kutokea
msiba wa mtu wa kawaida ukawasababisha watu kujipanga barabarani,
trafiki kuongoza harakati utafikiri mapokezi ya rais,” kilisema chanzo.
Inadaiwa kuwa msafara wa magari ulivunja rekodi kwani wakati magari
mengine yalikuwa yameshafika makaburini, mengine yalikuwa bado kwenye
foleni nyumbani.
Jeneza likibebwa kuelekea makabulini.
Chanzo hicho kilizidi kupasha habari kuwa, msafara wa kutoka nyumbani
kwa marehemu, Bukoba mjini hadi katika Kijiji cha Kyaikalabwa ambacho
kipo umbali wa kilomita 3, ulikuwa mrefu kiasi ambacho magari
yalijipanga kuanzia mjini hadi kaburini.
RAIS KIKWETE APOKEA SALAMU ZA KHERI TOKA KWA RAIS BARACK OBAMA WA MAREKANI
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiongea kwa furaha na ujumbe kutoka Ubalozi wa
Tanzania ulioko jijini Washington DC uliomtembelea kumjulia hali na
kwasilisha salamu maalumu za pole za Rais Barack Obama jijini
Baltimore, Maryland.
|
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi Liberata Mulamula na
ujumbe wake wa maafisa waandamizi wa ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
baada ya kupokea salamu maalumu za kumtakia kheri na afya njema kutoka
kwa Rais Barack Obama wa Marekani leo jijini Baltimore, Maryland,
Marekani.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi Liberata Mulamula na
ujumbe wake wa maafisa waandamizi wa ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
baada ya kupokea salamu maalumu za kumtakia kheri na afya njema kutoka
kwa Rais Barack Obama wa Marekani leo jijini Baltimore, Maryland,
Marekani.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na maafisa waandamizi wa Ubalozi wa
Tanzania nchini Marekani uliopo Washington D.C. wakati walipomtembelea
mjini Baltimore Maryland ambapo balozi Liberata Mulamula aliwasilisha
kwa Rais Kikwete Salamu maalum za kumtakia kheri na afya njema kutoka
kwa Rais Barack Obama leo jijini Baltimore, Maryland, Marekani. Picha na
Freddy Maro
DC,GAMBO AWATAKA WAUGUZI KUKOMESHA VIFO VYA MAMA NA MTOTO WAKATI WA KUJIFUNGUA
NA SALUM MOHAMED,KOROGWE
MKUU wa Wilaya ya Korogwe, Mrisho
Gambo, amewataka wauguzi Wilayani humo kutoa elimu kwa wazazi majumbani
kujifungulia katika vituo vya afya lengo likiwa ni kupunguza vifo vya mama na
mtoto wakati wa kujifungua.
Akifungua kongamano la Chama Cha Wauguzi Tanzania (TAMA) hivi karibuni
Wilayani humo, Gambo alisema kuongezeka kwa vifo vya mama na mtoto ni kutokana
na wazazi wengi kutokuwa na elimu ya kuhudhuria vituo vya afya kutambua
mwenendo wa mtoto tumboni.
Alisema hali hiyo imekuwa ikiwalazimu kujifungulia katika
sehemu ambazo sio za kutolea huduma na hivyo kuwataka kutoa elimu nyumba kwa
nyumba jambo ambalo litasaidia kuwa na ada ya kuhudhuria vituo vya afya kila
baada ya muda.
“Nashukuru kwa kupata nafasi hii adhimu ya kuzungumza nanyi
natambua kuwa ni watu muhimu sana hasa suala zima la vifo vya mama na
mtoto-----tutambue kuwa muko na nafasi ya kuelimisha jamii” alisema Gambo
“Wilayani kwetu hapa munatambua kuwa vifo vya mama na mtoto
vimepungua kiasi ila tusibweteke kwani kuna kundi kubwa halina elimu ya
kuhudhuria vituo vya afya wakati wa ujauzito na mwisho hujifungulia sehemu
zisizo salama” alisema
Gambo aliwataka wauguzi hao kuwa na mkakati wa kupita nyumba
kwa nyumba kutoa elimu hiyo kwa wanawake ili wakati wa ujauzito kuwa na utaratibu wa
kuhudhuria vituo vya afya na madhara ya kujifungulia sehemu ambazo sio za
kutolea huduma.
Akizungumza katika kongamano hilo, Mkunga na mwalimu chuo
kikuu cha Canada, Angella Spencer, aliwataka wauguzi kuwa na kauli nzuri kwa
wajawazito hasa wakati wa kujifungua.
Alisema wauguzi wako na nafasi kubwa ya kumfanya mzazi
kujifungua kwa hali ya furaha baada ya kupata faraja na hivyo kuwataka
kuzitumilia nafasi zao lengo likiwa ni kuwaweza wazazi katika mazingira ya kujifungua salama.
“Ili kutokomeza vifo vya mama na mtoto kwanza ni muuguzi
kuhakikisha anampokea mzazi kwa furaha-----hii itamfanya kujisikia furaha hadi
muda wa kujifungua” alisema Spencer
Alisema kama wauguzi wataifuata taaluma yao ni wazi kuwa vifo
vya watoto wakati wa kujifungua vitapungua Tanzania sambamba na utoaji wa elimu
ya kila mjamzito kuhudhuria kituo cha afya kwa utaratibu.
HIVI NDIVYO COASTAL UNION U-20 LEO WALIVYOIKALISHA MONGA STARS YA VYERU WILAYANI MKINGA,YAIPIGA 1-0
KIKOSI CHA U-20 CHA COASTAL UNION KIKIPASHA KABLA YA KUANZA MECHI HIYO DHIDI YA MONGA STARS AMBAPO COASTAL UNION U-20 ILIIBUKA NA USHINDI WA BAO 1-0 BAO HILO LILIFUNGWA NA ZAMIRU ISSA DAKIKA YA 36 |
MAKIPA YA KIKOSI CHA U-20 COASTAL UNION WAKIPASHA KABLA YA KUANZA MECHI HIYO LEO |
KOCHA WA KIKOSI CHA U-20 YA COASTAL UNION,JOSEPH LAZARO AKISISITIZA JAMBO KWA WACHEZAJI WA TIMU HIYO KABLA YA KUANZA MECHI HIYO LEO |
KIKOSI CHA COASTAL UNION U-20 AMBACHO KILICHEZA NA MONGA STARS LEO NA KUWAFUNGA BAO 1-0 |
MWAMUZI WA MECHI HIYO,KASID KITENDO AKIWA NA WACHEZAJI WA TIMU ZOTE MBILI KABLA YA KUANZA MPAMBANO HUO |
KIKOSI CHA MONGA STARS KILICHOPIGWA KIMOJA NA COASTAL UNION U-20 LEO |
KOCHA WA TIMU YA VIJANA YA COASTAL UNION U-20 JOSEPH LAZARO AKISISITIZA JAMBO KWA WACHEZAJI WA TIMU HIYO LEO WAKATI WA MAPUMZIKO |
SHUHUDIA AJALI YA TOYOTA HAICE ILIYOUWA WATU TISA NA KUJERUHI WENGINE TISA SHINYANGA
Toyota
haice yenye namba za usajili T761 CKD iliyokuwa ikitoka wilayani Kahama
kuelekea mjni Shinyanga ikiwa imepinduka katika eneo la Buhangija
manispaa ya Shinyanga na kuuwa watu tisa na kujeruhi wengine tisa,baada
ya kupinduka mara tatu baada ya kuvuka tuta kisha kugonga daraja na
kuangukia mtaroni,chanzo chake ni mwendo kasi ambapo dereva wa gari hilo
Anwar Awadhi mkazi wa Lubaga Shinyanga aliruka na kukimbia.
Gari likitolewa kwenye mtaro ni baada ya kuuwa watu tisa ambapo watano walikufa papo hapo .
Wananchi wakiwa eneo la tukio
WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI KUTOKA UBELGIJI WATEMBELEA MAENEO YA UWEKEZAJI BAGAMOYO
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza akiukaribisha ujumbe wa
Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ubelgiji ambao wametembelea mkoa wa
Pwani kujionea fursa za uwekezaji.
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza akiongozana na ujumbe wa
Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ubelgiji ambao wametembelea mkoa wa
Pwani kujionea fursa za uwekezaji.
Katibu Tawala Mkoa wa Pwani, Mgeni Baruani akizungumza akizungumza
wakati wa mkutano uliowakutanisha Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka
nchini Ubelgiji na Uongozi wa Mkaoa wa Pwani.
Ujumbe wa Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ubelgiji ukiwa katika mkutano wa pamoja na viongozi wa Mkoa wa Pwani.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara kati ya Tanzania na Ubelgiji, Otieno Igogo.
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza akizungumza wakati wa Mkutano
uliowakutanisha viongozi wa mkoa huo na ujumbe wa wafanyabiashara na
wawekezaji kutoka Ubelgiji.
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza akizungumza wakati wa Mkutano
uliowakutanisha viongozi wa mkoa huo na ujumbe wa wafanyabiashara na
wawekezaji kutoka Ubelgiji.
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza akizungumza wakati wa Mkutano
uliowakutanisha viongozi wa mkoa huo na ujumbe wa wafanyabiashara na
wawekezaji kutoka Ubelgiji.
Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dk. Diodorus Buberwa Kamala akizungumza katika mkutano huo.
Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dk. Diodorus Buberwa Kamala akizungumza katika mkutano huo.
Ujumbwa wa Tanzania ukiwa katika mkutano huo.
Kamishina wa Biashara kutoka Ubalozi wa Ubelgiji nchini, Ivan Korsak akizungumza katika mkutano huo.
Kamishina
wa Biashara kutoka Ubalozi wa Ubelgiji nchini Tanzania, Ivan Korsak
akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wafanyabiashara na wawekezaji
kutoka Ubelgiji na uongozi wa Mkoa wa Pwani waliofika kuangalia fursa
za uwekezaji mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza (kushoto) akifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa katika mkutano huo.
Shangwe Tamala akitoa mada kuhusu vivutio vya kitalii na maeneo ya uwekezaji katika mkoa wa Pwani.
Ujembe wa Tanzania na Ubelgiji ukiwa katika mkutano huo.
Mmoja wa wawekezaji kutoka Ubelgiji, Jean-Christophe Van Acker akizungumza wakati wa mkutano huo.
Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ubelgiji wakiwa mjini Bagamoyo wakiangalia maeneo ya uwekezaji.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza akimkabidhi zawadi, mmoja wa wawekezaji kutoka Ubelgiji, Yvan De Coninck.
Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Dk. Diodorus Buberwa Kamala.
Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Dk. Diodorus Buberwa Kamala.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza (wa tatu kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wawekezaji kutoka Ubelgiji.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA), Clara Ibinya akizungumza katika mkutano huo.
Mmoja wa wawekezaji kutoka Ubelgiji, Jean-Christophe Van Acker akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja kati ya viongozi wa Mkoa wa Pwani na ujumbe wa wafanyabiashara na wawekezaji waliotembelea maeneo ya uwekezaji Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamishina wa Biashara kutoka Ubalozi wa Ubelgiji nchini, Ivan Korsak akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
Jean-Christophe Van Acker akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.
Nikki Martine Fedorowicz akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mko wa Pwani.
Jacques Delaunoit akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.
Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Dk. Diodorus Buberwa Kamala akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara kati ya Tanzania na Ubelgiji, Otieno Igogo akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza (katikati) akiwaongoza wafanyabiashara
na wawekezaji kutoka Ubelgiji waliotembelea eneo la ujenzi wa Bandari
ya Bagamoyo.
Eneo la ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani akito ufafanuzi kwa wawekezaji waliotembelea eneo litakalojengwa Bandari ya Bagamoyo. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Dk. Diodorus Buberwa Kamala.
Eneo itakayojengwa Bandari Mpya ya Bagamoyo katika eneo la Mbegani.
Ujumbe wa Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ubelgiji wakitembelea eneo la Mamlaka ya Ukanda Maalum ya Uwekezaji (EPZA) eneo la ekari 300 la Kamal Industrial Estate mjini Bagamoyo ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kuangalia maeneo ya uwekezaji.
Mmoja wa wawekezaji kutoka Ubelgiji, Jean-Christophe Van Acker akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja kati ya viongozi wa Mkoa wa Pwani na ujumbe wa wafanyabiashara na wawekezaji waliotembelea maeneo ya uwekezaji Bagamoyo mkoani Pwani.
Kamishina wa Biashara kutoka Ubalozi wa Ubelgiji nchini, Ivan Korsak akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
Nikki Martine Fedorowicz akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mko wa Pwani.
Jacques Delaunoit akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.
Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Dk. Diodorus Buberwa Kamala akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara kati ya Tanzania na Ubelgiji, Otieno Igogo akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.
Eneo la ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo.
Mkuu wa Mkoa wa Pwani akito ufafanuzi kwa wawekezaji waliotembelea eneo litakalojengwa Bandari ya Bagamoyo. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Dk. Diodorus Buberwa Kamala.
Eneo itakayojengwa Bandari Mpya ya Bagamoyo katika eneo la Mbegani.
Ujumbe wa Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka Ubelgiji wakitembelea eneo la Mamlaka ya Ukanda Maalum ya Uwekezaji (EPZA) eneo la ekari 300 la Kamal Industrial Estate mjini Bagamoyo ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kuangalia maeneo ya uwekezaji.
Subscribe to:
Posts (Atom)