BARAZA LA HALAMSHAURI YA WILAYA YA MOSHI LAMCHAGUA MICHAEL KILAWILA KUWA MWENYEKITI WA HALMASHAURI.

December 09, 2015
Wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,wakiwa ukumbini hapo kabla ya kuapishwa.
Wagombea waliopitishwa na Chadema kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Halmashauri na Makamu Mwenyekiti wakiwa katika ukumbi wa halmashauri hiyo.
Baadhi ya wajumbe wa baraza hilo kabla ya kuapishwa.
Wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,wakiapishwa kuwa madiwani rasmi.
Mwenyekiti mstaafu wa Halmashauri hiyo,Moris Makoyi akiwa katika kikao cha kwanza cha baraza hilo.
Katibu tawala wilaya ya Moshi,Remida Ibrahim akiongoza zoezi la upigaji kura kwa ajili yakumpata Mwenyekiti na Makamu wake wa Halmashauri hiyo.
Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akiteta jambo na Diwani wa kata ya Kahe ,Rodrick Mmanyi wakati wa kikao cha baraza hilo.
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) Joseph Chata akiomba kura mbele ya wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Moshi.
Mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti kupitia chama cha Demokasia na Maendeleo (Chadema)  Michael Kilawila akijinadi mbele ya wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Moshi akiomba kuchaguliwa kuogoza baraza hilo.
Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) Sephen Charles akiomba kura mbele ya wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Moshi.
Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti kupitia chama cha Demokasia na Maendeleo (Chadema)  Exaud Mamuya akijinadi mbele ya wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Moshi akiomba kuchaguliwa kuogoza baraza hilo.
Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti kupitia chama cha NCCR -Mageuzi Gibrata Riwa akijinadi mbele ya wajumbe wa baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Moshi akiomba kuchaguliwa kuogoza baraza hilo.
Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akipiga kura wakazi wa zoezi hilo.
Wajumbe wakishiriki zoezi la upigaji kura.
Diwani wa kata ya Mabogini Emanuel Mzava akimpongeza Diwani wa kata ya Kindi,Michael Kilawila baada ya kutangazwa mshindi kwa kupigiwa kura 36 .
Madiwani wakifurahia mara baada ya kuvaa joho rasmi kwa ajili ya uzinduzi wa baraza hilo.
Mwenyekiti mpya wa baraza la Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Michael Kilawila akiongozana na Makamu wake ,Exaud Mamuya wakati wakiingia katika ukumbi wa baraza hilo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Fulgence Mponji akitoa muongozo wakati wa uzinduzi rasmi wa baraza hilo.
Mwenyekiti wa baraza la Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Michael Kilawila akitoa hotuba yake ya kwanza wakati wa uzinduzi rasmi wa baraza hilo.
Mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga akizungumza wakati wa uzinduzi wa baraza la Halmashauri ya wilaya ya Moshi.
Mwenyekiti wa Halamshauri ,Michael Kilawila na Makamu wake ,Exaud Mamuya wakifuatilia hotuba ya mkuu wa wilaya (hayupo pichani).
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro ,Severine Kahitwa akitoa maelekezo mbalimbali ya uendeshaji wa baraza hilo kwa Madiwani na uongozi mpya wa baraza hilo.
Mbunge wa jimbo la Vunjo,James Mbatia akifuatilia .
Menyekiti wa Chadema wilaya ya Moshi vijijini Ekarist Kiwia pia alikuwa ni miongoni mwa mashuhuda wa mchakato wa kumpata Mwenyekiti wa Halmashauri.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Moshi ,Michael Kilawila.
Makamu Mwenyekiti wa baraza la Halmashauri ya wilaya ya Moshi,Exaud Mamuya.
Ndugu wa madiwani wakifurahia nje ya ukumbi wa Hlamshauri ya wilaya ya Moshi mara baada ya Madiwani kuapishwa.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kakskazini (0755659929).

WAFANYAKAZI WA NURU FM 93.5 IRINGA WAFANYA USAFI HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA IRINGA KUMUUNGA MKONO RAIS DR JOHN POMBE MAGUFULI

December 09, 2015
Fredy mgunda ambaye ni chief repoter wa radio nuru fm 
 hawa muhamed na devota romanus wakiwa eneo la tukio wakifanya usafi 
 shauri mkwawa a.k.a mama la mama na wafanyakazi wenzake wakifanya usafi
  shauri mkwawa a.k.a mama la mama na wafanyakazi wenzake wakifanya usafi



Wafanyakazi wa kituo cha redio nuru fm 93.5 iringa wamejitokeza kufanya usafi katika hospital ya rufaa ya iringa kwa lengo la kumuunga mkono rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania dr john pombe magufuli.

Wakizungumza wakati wakiwa wanafanya usafi katika eneo hilo wamesemakuwa wameamua kufanya usafi katika hospital hiyo kwa kuwa ndio hospital inayohudumia wananchi wengi kuliko hospitali nyingine zilizopo mkoani hapa.
Denis nyali ni mhariri wa habari wa radio hiyo amesema kuwa wameamua kufanya usafi kwa lengo la kuwaonyesha wananchi na wafanyakazi wa hospital hiyo kuwa iringa kuwa safi inawezekana kutokana na kauli moja tu aliyoitoa rais imekuwa gumzo kila kona hivyo wananchi wanatakiwa kufanya usafi kila mara na usafi uwe jadi yao.

“Angalia hapa leo hospitali kama hii ya rufaa uchafu wote huu unatoka hapa kama wanagekuwa wanafanya usafi kila siku na kuona usafi ni sehemu ya maisha yao tusingeona hali hii na pia tusinge pata wagonjwa wa magonjwa ya milipuko naomba wananchi wezangu zoezi hili liwe endelevu”alisema denis nyali.
Hawa muhamed na grace michaeli wamesema ni aibu wananchi kukumbushwa kufanya usafi na rais wakati huo ni wajibu wa kila mwananchi na kuongeza kuwa wanampongeza rais wa awamu ya tano  kwa kasi yake anayoendana nayo sasa kwa inawafanya watanzania waanze kuiamini serikali yao tofauti na ilivyo kuwa hapo awali.

Fredy mgunda ambaye ni chief repoter wa radio nuru fm amewataka wananchi kuendeleza juhudi za rais kwa kuwa wasafi kila siku na kuafanya usafi kila mara ili nchi hii isikumbwe na magonjwa ya milipuko na kuongeza kuwa serikali ya manispaa ya iringa inatakiwa kutunga sheria ndogondogo za usafi.

“Hapa iringa hatuna kabisa sheria za usafi kwa utaona wananchi wanatupa takataka hovyo huku viongozi wa mji huu wakiwa kimya kwa namna hiyo hatuwezi kuwa na mji msafi hata siku moj,ukienda pale stand watu wanakojoa na kujisaidia hovyo lakini hawachukuliwi hatua yoyote ile “alisema fredy  mgunda

Hussein faraha ni mtangazaji wa radio hiyo amewaomba wananchi kuendeleza kufanya usafi kwa kuwa ndio jadi ya mtazania hata ukikumbuka hapo zamani wakati mwalimu nyerere akiwa hai alikuwa akisisitiza usafi hivyo ujio wa rais huyu wa awamu ya tano john magufuli naanza kufananisha na marehem waziri mkuu Edward molinge sokoine  kwa uchapaji kazi wake.

“Leo nimemuana rais huyu akizama kwenye matope kufanya usafi huku akiwa na sura ya furaha kujumuika na wananchi wakati wa kufanya kazi hiyo ni ishara tosha kumlinganisha na marehemu mwalimu nyerere kwani alikuwa anafanya kazi pamoja na wananchi wake”. alisema husien farahani

Naye jeni kalinga amesema kwa anamkubali sana rais kwa kasi yake na kuwaomba wananchi kumuombea awe na uhai kwa kuwa sasa anatimiza matakwa ya watanzania wengi waliokuwa wamekata tamaa na nchi yao

“Daa jamaa yangu magufuli jembe kinoma si unaona linavyolima kila kona ni gumzo hivyo lazima tumpe nguvu na serikali imuongezee ulinzi tuiseje tukalipoteza jembe letu lilorudisha matumaini ya watanznia”alisema jeni kalinga.

Kwa upande wao baadhi ya wafanyakazi wa hospitali hiyo wamekipongeza kituo hicho cha radio kwa kuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa wamejituma kufanya usafi kwenye mahodi na nje ya hodi hasa wanaume walikuwa wanadeki huku kwenye mahodi hicho ni kitendo cha kujivunia kutoka kwako.



KIPINDI CHA 'TUWALINDE WATOTO WETU' KURUKA TENA ALHAMISI HII, CLOUDS TV

KIPINDI CHA 'TUWALINDE WATOTO WETU' KURUKA TENA ALHAMISI HII, CLOUDS TV

December 09, 2015
janeth 2
Mmiliki na mwendeshaji wa kipindi cha Tuwalinde Watoto Wetu, Janet Mwenda.
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Kipindi cha Tuwalinde Watoto Wetu kilichokuwa kikirushwa na Clouds TV, Alhamisi ya wiki hii kinatarajiwa kuanza tena kuonekana kupitia Clouds TV Alhamisi ya Disemba 10, saa tatu kamili usiku.
Akizungumza na Dewjiblog, Mmiliki na mwendeshaji wa kipindi hicho, Janet Mwenda amesema kuwa kipindi cha Alhamisi hii kinatarajiwa kuja na kitu kipya tofauti na vile walivyokizoea kuonekana hapo awali na hivyo kuwataka watazamaji kukaa tayari kuona kipindi bora kuhusu watoto na changamoto wanazokutana nazo.
Amesema lengo la kipindi hicho ni kuwakumbusha wazazi na walezi majukumu yao kwa watoto wao na hatari wanazoweza kukutana nazo pindi wasiposimamiwa vizuri na watu wanaoishi nao na kupitia kipindi hicho wanaweza kuona maisha wanayokutana nayo watoto hao pindi wanapokuwa nje ya familia zinazowalea.
“Kuna mambo jamii inakuwa haiyaamini kama yanatokea na tunachofanya ni kujaribu kuionesha jamii ni mambo gani yanawatokea watoto wanapokuwa mtaani na tunachotaka ni wazazi watambue hatari hiyo na waweze kuwalea vizuri watoto awe wa kwako au wa mwenzako,” amesema Janet.
Akizungumzia kipindi cha Alhamisi hii, Janet amesema kipindi cha wiki hii kitakuwa kinamuhusu kijana wa miaka 16 aliyekuja Dar es Salaam kutafuta maisha baada ya kutoroka nyumbani kwao na kujiunga na makundi mabaya ya vijana ambayo yalipelekea kuanza kujiingiza katika vitendo vya kimapenzi na wanawake wanaofanya biashara ya kuuza mwili na kuwa katika hali ya hatari ya kupata magonjwa ya zinaa.
Kujua kilichofuata baada ya kujiingiza katika vitendo hivyo na hali aliyonayo sasa kijana huyo usikose kutazama kipindi hicho alhamisi hii, Disemba 10 kupitia Clouds Tv!!!
USIKOSEEE!!
MeTL GROUP YASHEREKEA SIKU YA UHURU KWA KUFANYA USAFI COCO BEACH

MeTL GROUP YASHEREKEA SIKU YA UHURU KWA KUFANYA USAFI COCO BEACH

December 09, 2015
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) imesherekea sherehe za Uhuru wa Tanganyika, Disemba 9 kwa kufanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach kama jinsi alivyoagiza rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuagiza kuwa siku ya Uhuru itumike kufanya usafi kutokana na kushamiri kwa uchafu katika mazingira yanayotuzunguka.
Kwa kufata agizo hilo la Dkt. Magufuli, MeTL Group kwa kujumuisha viongozi wa kampuni na wafanyakazi wake imefanya usafi kwa pamoja katika ufukwe wa Coco Beach ili kusafisha eneo hilo ambalo linatumiwa na watu wa aina mbalimbali kwenda kujipumzisha pamoja ndugu na familia siku za mapumziko.
Hizi ni baadhi ya picha wakati wafanyakazi wa MeTL Group wakifanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach;
IMG_7859
Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya MeTL Group, Bi. Fatema Dewji-Jaffer (kulia) akiongoza na Afisa Afya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Kijumbe kuelekea kwenye eneo la usafi mara baada ya kuwasili kwenye fukwe za Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote Dec 9, 2015.
IMG_7779
Baadhi ya wafanyakazi wa makampuni ya MeTL Group wakiwasili kwenye fukwe za Coco Beach kushiriki zoezi la usafi.
IMG_7812
#HapaKaziTu........Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya MeTL Group, Bi. Fatema Dewji-Jaffer (kulia) akisaidiana na Kiongozi Mahusiano ya Kazi wa MeTL Group, Subrina Gulamali Bhatti kubeba moja ya gogo lililokuwa linazagaa kwenye fukwe hizo.
IMG_7815
IMG_7820
Wafanyakazi wa makampuni ya MeTL Group wakiendelea na zoezi la usafi katika fukwe za Coco Beach ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 54 ya Uhuru wa Tanzania kama alivyoagiza Mhe Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambapo zoezi hilo limefanyika nchini kote Dec 9, 2015.
IMG_7739
Zoezi la kukusanya takataka na kuchoma mifuko ya nailoni iliyokuwa imezagaa kwenye fukwe za Coco Beach likiendelea.
IMG_7733
IMG_7739
IMG_7765
Wengine wakiendelea kufyeka vichaka vya majani katika fukwe za Coco Beach.
IMG_7717
Zoezi likiendelea.
IMG_7704
Takataka zikiendelea kukusanywa na kuchomwa moto.
IMG_7746
Takataka zikikusanywa kwenye viroba.
IMG_7832
Zoezi likiendelea kwa ushirikiano wa hali ya juu.
IMG_7879
IMG_7881
#HapaKaziTu ndio maneno waliyokuwa wakisema wafanyakazi wa MeTL Group wakiendelea na zoezi la kusafisha fukwe za Coco Beach jijini Dar.
IMG_7809
IMG_7847
Baadhi ya wafanyakazi wa MeTL Group katika picha ya pamoja.
IMG_7662
Picha za kumbukumbu baada ya kazi zilipigwa.
IMG_7955
Mkuu kitengo cha Rasimali watu anayeshughulikia wafanyakazi wa ndani (Local) kampuni ya MeTL Group, Masuma Mushtak (waliosimama wa pili kushoto) katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Makao Makuu ya Ofisi za MeTL Group.
IMG_7964
IMG_7971